RC Adam Malima ashauri Serikali kuwa makini kwenye Mkataba wa DP World, ili tusipigwe kama kwenye Mikataba ya Madini

RC Adam Malima ashauri Serikali kuwa makini kwenye Mkataba wa DP World, ili tusipigwe kama kwenye Mikataba ya Madini

Nimemsikia ila hakuna popote aliposema mkataba wa DPW ni mkataba mbovu!.

Alichosema ni tuwe makini ili tusipigwe, kwasababu huko nyuma, tulipigwa!.

Msimchonganishe Malima na Samia!. Serikali yetu inafanya kazi kwa mtindo wa a collective responsibility, serikali ikiisha sema ndio, Bunge likasema ndio, chama tawala, chama cha Mapinduzi, CCM, kikasema ndio, hawezi tena kuibuka mserikali yeyote akasema sio, huko kutakuwa ni kwenda kinyume cha kanuni ya collective responsibility.

Kwenye kanuni hiyo ya a collective responsibility, ukiamua kutofautiana na uwajibikaji wa pamoja ni unajinyamazia kimya!. Ukijiona huwezi kunyamaza, kwanza ana resigns ndipo unapinga!.

Hivyo mleta mada umepotosha!, usimlishe maneno Adam Malima.

P
Hapa kwenye suala la DPW hakuna cha collective responsibility bali kuna kuburuzana! Serikali haikutoa muda wa kutosha kujadili makubaliano hayo kama inavyoyaita ingawa sisi tunajua ni mkataba.
 
Kaongea vizuri kabisa. "Tutazame tutakapoingia ubia hili linafaa hili halifai...".


Na hayo ndiyo serikali yoe inasema hivyo, kila mtu kinamna ya kuongea kwake".


Ubia bado, mkataba bado. ndiyo yote hayo yanapitiwa kwa kina kwa sasa na wataalaam wetu. Heko Malima.
Wewe kilikuzuia nini kutoa maoni kama ya Malima hapo mwanzo?
 
Ila kwenye hii issue ya bandari NIMEGUNDUA maafsa habari wa SERIKALI na taasis zake zikiwamo wizara, wanatakiwa wajitafakari sana sana... Hawakutoa elimu ya kutosha na kutoa taarifa sahihi kwa WANANCHI na ndo MAANA Kuna mkanganyiko namna hii

Sent from my TECNO CI6 using JamiiForums mobile app
Waandishi wa habari siku hizi wamekuwa ni mawakala wa matangazo, kwenye "bahasha" kubwa ndiko wanakoelemea.
 
He is old school
...katika suala la makubaliano ya bandari wengi tumejua mia zao mbovu, hasa wanao utetea. Hili lina mstari mwekundu wa wanaipenda Tanganyika bila vyeo, utajiri, nasaba na husuda na wale wenye nia hasi na Tanganyika. Je huyo old school yupo upande gani? Halafu wasio werevu huzeeka pia. You can be old school of fools.
 
..Adam amempiga kijembe Maza ambaye wajomba zake ni Waarabu wa Oman.
Tanganyika haikuhitaji kero 24 za muungano. Ilihitaji mikataba mibovu tu ijitenge. Huu ni mwanzo. Ngoja tuone mwisho wa haya utaleta matokeo gani.
 
Akizungumza katika kipindi cha Good morning Wasafi FM, Malima ambae marehemu baba yake aliwahi pia kuwa waziri wa fedha kipindi cha Nyerere, amesema Kinachopingwa sio ufanisi wa bandari bali ni vipengele vya mkataba, na huko nyuma, 1998 Tanzania iliwahi Ingia mikataba mibovu ya madini, na alipokuwa waziri wa nishati miaka kumi baadae wakaikataa .

Akafafanua zaidi amesema kwamba Waarabu sio wajomba zetu na hivyo muhimu ni kuangalia vifungu vyenye shida virekebishwe kwa maslahi ya taifa na si vinginevyo.


Msikilize mwenyewe 👇

Sikujua kama huko chama pendwa bado wako watu wenye akili. Hongera RC kwa kusema kweli. Mungu akulinde
 
Eti waarabu wajomba zake..si akaishi nao sasa..tuacheni rasilimali zetu hatavizazi vyetu vitatakuja kusahihisha pale mlipo shindwa
Wewe mpuuzi na mjinga na kumbe una chuki za kidini na sio kukosa.
Malima amesema waarabu SIO wajomba. Akimaanisha tusiwaamini kupita kiasi. Mpuuzi wewe unaamua kupotosha kwamba kasema wajomba zetu?
 
Mkataba bado jamani, muelezwe vipi? Labda hamuelewi kuwa kuna kampuni tatu mpaka sasa zinagombania bandari ya Dar. Sasa nyinyi kuona Mkubaliano ya serikali ya Dubai na Tanzania, mkachukulia, ooh tayri. Hapana, mkataba bado una michaakato yake.
Wewe ajuza hakika umechanganyikiwa, hujui kwamba hujui na ndio maana unatumika kama tambara la kudekia sakafu. Hebu msome huyu mbunge anasemaje...

(nanukuu) Wabunge wa CCM tuliopitisha Mkataba wa Uwekezaji Bandarini tuko vizuri kichwani, pale Bungeni kuna wabunge wa CCM wako vizuri kichwani.

Mimi mwenyewe nimemaliza chuo Mzumbe wakaning'ang'ania nibaki kufundisha pale kwa sababu nina akili nyingi, nilipata GPA ya juu sana.

Kwa hiyo hatukupitisha mkataba bila kuusoma, na tusingezeweza kupitisha mkataba usio na maslahi kwa nchi yetu.
(mwisho wa nukuu)

By Elibariki Kingu

Kabla mkataba huo wa siri haujavuja, neno lililotumika ni mkataba. Baada ya wananchi wazalendo kuupigia kelele, kama ilivyo kawaida ya CCM wakaja na maneno mara azimio, mara makubaliano, mara hatua za awali na mauupuzi upuzi yote

Mkataba uliingiwa zaidi ya mwaka nyuma Rais alipotia sahihi yake.
 
Akizungumza katika kipindi cha Good morning Wasafi FM, Malima ambae marehemu baba yake aliwahi pia kuwa waziri wa fedha kipindi cha Nyerere, amesema Kinachopingwa sio ufanisi wa bandari bali ni vipengele vya mkataba, na huko nyuma, 1998 Tanzania iliwahi Ingia mikataba mibovu ya madini, na alipokuwa waziri wa nishati miaka kumi baadae wakaikataa .

Akafafanua zaidi amesema kwamba Waarabu sio wajomba zetu na hivyo muhimu ni kuangalia vifungu vyenye shida virekebishwe kwa maslahi ya taifa na si vinginevyo.


Msikilize mwenyewe 👇

This guy is smart! Ngoja tuone kama SSH atamtumbua! Na wale mawaziri, MaRC, Ma DC, MARAS, MADAS etc wanajitia uchawa katika mamlaka yao nao waondoe funza vichwani! Ahsante Comrade Malima kuna kiroboto mmoja DAS wa Busega anawashwa kuhitaji damu ajifunze haraka
 
Back
Top Bottom