RC Mtaka ataka wanafunzi wanaofanya makosa wafukuzwe shule

RC Mtaka ataka wanafunzi wanaofanya makosa wafukuzwe shule

Dogo Rajabu wa kigogo sekondari yeye breaktime anauzia wenzake bangi
Halafu eti huyu asifukuzwe shule wakati anauzaa madawa ya kulevya na kifungo chake ni miaka kadhaa
 
Huyu ataliwa kichwa, huko tu amepelekwa kwa maombi maalum.

Serikali tangu lini ikaweka sheria chungu dhidi ya raia wake.

Tunahitaji kuwa na sera madhubuti kweli kweli.
 
Loooh Igogo,Mwanza napaelewa sana. Hapo ndo base kuu ya wezi,vibaka na majambazi wa jijini Mwanza. Watoto wa hapo wamepinda kinoma, we chiembe nenda huko ukajionee.
Halafu eti wasifukuzwe shule. Yaani. Shule ipoteze rasilimali na miundombinu kusomesha majizi ambayo yataishia kupata Zero. Di Bora waishie tu la Saba?
 
Waungwana wamemfukuza mwenye uzi kwa uzi wake haha
Bora akajifiche maana leo ni mwana kulitafuta ni mwana kulipata. Sijui amewazaje kumgusa Mtaka. Naona ana test zali la kidole kwenye uji wa volcano.
 
We ndugu chiembe umesoma comments zilizofuatia andiko lako na umejifunza nini hapo?.

Usiweke au kuandika kwa usuda za kisiasa, kidini nk, kisa kiongozi fulani ni mtu fulani au katokana na mazingira fulani, hiyo ni mbaya sana ndg Mtanganyika.

Kwanza sheria za kufukuza shule mtoto nunda zipo na labda kama huna mtoto nakushauri nenda shule ya jirani kaongee na mwalimu mkuu umuulize je, mtoto anafukuzwa shule kwa kosa gani? -Alafu njoo hapa urekebishe mada yako.

Na watoto hawa wa kizazi kipya wanaolelewa na single parent unataka adekezwe wala asipewe onyo kali la kufukuzwa skuli unadhani kutakuwa na nidhamu hapo?.

Next time angalia logic yako na isimame na uhalisia wa maisha kulingana na matukio, siyo unamuingiza mfu kwenye scenerial isiyomuhusu, -Pole.
Sahihisha hapo kwa Single mother's. Huwezi kuniambia watoto wote watukutu wanalelewa na Single mothers. Wapo Single mothers strong Sana kuliko Sisi wanaume na wame produce vidume na wasichana imara mno kila sekta. Ziko nyumba zina wazazi wote lakini watoto wameishia kuwa hovyo. Ungefanya utafiti ndiyo ufanye hii painful attach hata kwa dada na mama zetu humu ambao wako imara mno kimalezi. Ninafahamu single mothers kadhaa ambao watoto wao ni mfano Bora mno. Tena form four wanatoka na single digits na nidhamu mtaani ni perfect mpaka na admire mkuu. Poleni Single mother.

Tena Bora single mothers. Wako single fathers wa hovyo mno na watoto wanaharibika na wengine wanalawiti watoto na kesi ni nyingi mno. Hebu wasemee na hawa. Hatujawahi kusikia single mother kabaka mwanaye wa kiume. Haya tuendelee na mada ya Mtaka maana mleta mara ameshajificha.
 
Sasa wakipigwa wanakufa wawafanyeje. Tulishakubaliana enforcing discipline ni kazi ya mzazi. Mwalimu ni kufundisha. Mtoto asiye na nidhamu arudishwe kwa mzazi.
 
Mwandishi wew Dikteta mkoloni mweusi. Kuchapa ni utumwa, wa kikoloni na bora wafukunzwe tu tufuate sheria RC yuko sahihi 100%
 
Sasa wakipigwa wanakufa wawafanyeje. Tulishakubaliana enforcing discipline ni kazi ya mzazi. Mwalimu ni kufundisha. Mtoto asiye na nidhamu arudishwe kwa mzazi.
Ndio hivyo mkuu. Asiefunzwa vizuri na ***** mwalimu hatomuweza
 
Je kama angefukuzwa shule asingekuwa jambazi? Yoyote anaye-support watoto watukutu wafukuzwe shule ni juha na hana akili timamu.
Ukiacha kuwa Mwanafunzi actual experience yako katika uemdeshaji au taratubu za Shule na upi? Tuanzie hapo kwanza ili tuende vyema katika huu mjadala kwa Nia njema tu ya kujenga
 
Hivi mbona shule za private hazina mitoto ya ajabuajabu kama gov
Government Kuna watu wenye akili Kama za mtoa mada, ndiko watoto wao wanakosoma (community schools) kwamba Mambo yaende hobela hobela na ndio maana hata products za hizo Shule kwa Sasa haziaminiki tofauti na zamani

Sababu kubwa Ni kwamba tangu form one jitu lilishajiharibia profile so hata ikifanyika vetting unakuta jitu halifit popote! Hawa ndio wakipewa ofisi za umma ndio wanakua wabidhirifu wakubwa na wasiokua na nidhamu!

Unaweza ukaona moulding au upribring ya watoto ilivyo tofauti katika Shule kwa kuzickasify namna hii

1. Government (State Schools)
2.institutional schools Kama seminary etc
3. Privately Owned Schools
4. Community Schools. (Shule za kata)

Hii number nne ndio mtoto akichapwa OCD, OCS, DC, Mwenyekiti wa CCM na wote wanaofanana na hao pamoja na mzazi wataamdamana dhidi ya mwalimu pamoja na watu wa human rights.

Wakati huo huo watu hao hapo juu hakuna hata mmoja mtoto wake anasoma katika Shule za namna inayofanana nahiyo isipokua number 1-3 ambapo Mwanafunzi akizingua tu Ni immediate dismissal!

Wao wanawapelekea watoto wao kwenye Shule ambazo ziko strict ili waje wawe warithi Bora ama wa nafasi zao au Mali zao Huku wakilinda image zao katika jamii!

Wakiitwa shuleni kuhusu indiscipline conducts za watoto wao huwatishia hatabkuwaweka rumande watoto wao lakini nenda huko katani au Shule za umma wanakuwa wakali kwa walimu tu ili kulinda maslahi na nafasi zao kwa wananchi ili wawaone watu wema wawachague tena!
 
Mtaka ni kama ana serikali yake ambayo haiendani na ya CCM na Samia, hivi mtoto unamfukuza shule ili iweje? Kwanza ni mtoto, anahitaji malezi na maangalizi.

Kwa aina ya waalimu tulio nao, hivi unawapa mamlaka yote hayo?

Mtaka ni moja ya members wazuri wa magrupu ya Chadema, na huwa mchangiaji mzuri wa fedha


Mtaka: Mwanafunzi mtukutu afukuzwe shule, asichapwe​


View attachment 2559219

Njombe. Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Anthony Mtaka amewaagiza wakuu wa shule za Serikali kuwafukuza wanafunzi watukutu badala ya kuwachapa viboko au kuwarudisha nyumbani.

Mtaka alisema hayo alipozungumza na wanafunzi wa Sekondari ya Wasichana ya Manyunyu, iliyopo Matembwe wilayani Njombe.

Alisema shule si sehemu za watu kufanya mizaha na wazazi wengi wanaheshimu sana shule binafsi lakini za Serikali mambo huwa tofauti.

“Kuna shule za binafsi zikiagiza mwanafunzi aje na nguo mbili wanaenda nazo hizohizo, ukienda na ya tatu unarudishwa, wanakuambia shule hii ni marufuku mtoto kuja na simu ukienda nayo unarudishwa nyumbani, huku kwenye shule zetu za umma tuna mizaha mingi,” alisema.

Mizaha hiyo alisema inasababisha mwanafunzi akifanya vituko na mwalimu akamwadhibu basi mwalimu atajadiliwa hadi kwenye mitandao ya kijamii na polisi watamkamata kuandika maelezo, lakini ujinga huo haufanyiki shule binafsi.

Alisema jamii inapozungumzia maadili ni lazima yasimamiwe na namna ya kuyasimamia ni kuyajenga tangu vijana wakiwa shuleni.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Valentino Hongoli alisema “mwaka jana mheshimiwa Rais alitupatia Sh60 milioni ambazo tulijenga madarasa matatu na ofisi shuleni hapa, kama tusingepewa watoto wangeshindwa kusoma.”

Mkuu wa Sekondari ya Wasichana Manyunyu, Advera Bagoka alisema wanafunzi waliotakiwa kujiunga kidato cha kwanza mwaka huu walikuwa 202, ila walioripoti ni 120 na 51 wamebadilisha shule, huku 31 hawajulikani walipo.

“Shule yetu ina uhaba wa walimu wa sayansi na hisabati,” alisema.
Yupo sahihi 100% . Kuliko kupambana nao Kwa viboko mwishowe uwaue bure.

Jukumu la malezi ni la mzazi suyo mwalimu. Adhabu akapate Kwa wazazi wake
 
Sheria zingetumika ipasavyo basi wanafunzi wengi sana wangefukuzwa shule. Basi tu busara huwa zinatumika.
 
Je kama angefukuzwa shule asingekuwa jambazi? Yoyote anaye-support watoto watukutu wafukuzwe shule ni juha na hana akili timamu.
Akiwa jambazi anakamatwa na vyombo vya dola anafungwa! Simle like that, asiye funzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu
 
Shule zetu zinaandaa kizazi hatari sana kisichojua Wala kutaka kujua na kufata sheria kwa ukweli mtaka yuko sahihi
Halafu kuchapa au kutoa adhabu Kali kumefukuzisha walimu wengi sana kazi au kuwaweka matatizoni
 
Mtaka ni kama ana serikali yake ambayo haiendani na ya CCM na Samia, hivi mtoto unamfukuza shule ili iweje? Kwanza ni mtoto, anahitaji malezi na maangalizi.

Kwa aina ya waalimu tulio nao, hivi unawapa mamlaka yote hayo?

Mtaka ni moja ya members wazuri wa magrupu ya Chadema, na huwa mchangiaji mzuri wa fedha


Mtaka: Mwanafunzi mtukutu afukuzwe shule, asichapwe​


View attachment 2559219

Njombe. Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Anthony Mtaka amewaagiza wakuu wa shule za Serikali kuwafukuza wanafunzi watukutu badala ya kuwachapa viboko au kuwarudisha nyumbani.

Mtaka alisema hayo alipozungumza na wanafunzi wa Sekondari ya Wasichana ya Manyunyu, iliyopo Matembwe wilayani Njombe.

Alisema shule si sehemu za watu kufanya mizaha na wazazi wengi wanaheshimu sana shule binafsi lakini za Serikali mambo huwa tofauti.

“Kuna shule za binafsi zikiagiza mwanafunzi aje na nguo mbili wanaenda nazo hizohizo, ukienda na ya tatu unarudishwa, wanakuambia shule hii ni marufuku mtoto kuja na simu ukienda nayo unarudishwa nyumbani, huku kwenye shule zetu za umma tuna mizaha mingi,” alisema.

Mizaha hiyo alisema inasababisha mwanafunzi akifanya vituko na mwalimu akamwadhibu basi mwalimu atajadiliwa hadi kwenye mitandao ya kijamii na polisi watamkamata kuandika maelezo, lakini ujinga huo haufanyiki shule binafsi.

Alisema jamii inapozungumzia maadili ni lazima yasimamiwe na namna ya kuyasimamia ni kuyajenga tangu vijana wakiwa shuleni.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Valentino Hongoli alisema “mwaka jana mheshimiwa Rais alitupatia Sh60 milioni ambazo tulijenga madarasa matatu na ofisi shuleni hapa, kama tusingepewa watoto wangeshindwa kusoma.”

Mkuu wa Sekondari ya Wasichana Manyunyu, Advera Bagoka alisema wanafunzi waliotakiwa kujiunga kidato cha kwanza mwaka huu walikuwa 202, ila walioripoti ni 120 na 51 wamebadilisha shule, huku 31 hawajulikani walipo.

“Shule yetu ina uhaba wa walimu wa sayansi na hisabati,” alisema.
Mbona suala la watoto watukutu kufukuzwa shule ni jambo la kawaida wala siyo jipya sema tu wewe umemuotea huyo Mtaka.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom