RRRR ya Rais Samia Watanzania wengi wanaoishi kimazoea hawatoielewa haraka

RRRR ya Rais Samia Watanzania wengi wanaoishi kimazoea hawatoielewa haraka

Acha mambo ya kitoto .Tusipende kukosoa kila kitu .Heshimu mamlaka
 
hii ni baadhi ya mapatano ya allah na binadamu [emoji867][emoji867][emoji867]
Sijakuelewa.

Wewe nenda kafanye drilling wizara ya kilimo, kuna visima zaidi ya 50,000 vinatakiwa haraka sana. Wewe unapoteza muda JF.

Wahi fursa za mama.
 
Upuuzi tupu

Bandari ni mali na urithi halali ya watanganyika
 
Ukitaka kuwa masikini nchi hii, nenda kalime hicho kilimo cha heka kumi kumi uone kama utatoboa. Viongozi wanawapa watoto wao kazi kwenye mashirika ya umma na serikali, na hao uvccm ndio wanawadanganyia na mashamba ya kwenda kushinda huko porini.

Nitajie mtoto wa kiongozi anayelima hizo heka 10 kumi za Bashe. Lakini naweza kukutajia msururu wa watoto wa viongozi walioko kwenye taasisi za umma.
Hilo laviongozi usijali, wewe fanya uarafiki nao. Geuza Tatizo kuwa fursa. Resilience.

Wacha kujitia kitanza kuhusu kilimo. Unaujuwa mpango wake? kama hutaki wewe kulima, nenda ukawe fundi? Kama hutaki nenda ukawe dereva, kama hutaki nenda kaowe au kaolewa na wanaotaka kulima, zote ni fursa.

Wacha ujinga kijana. Shirika lipi la umma unataka kazi mimi nifanyie mpango. naahidi hapahapa mbele ya watu wote wanaotusoma hapa.
 
Ujinga tu kama kawaida yako hakuna la maana uliloandika zaidi ya kupepelea waarabu.
 
Tunaitaka Bandari zetu

Hizi porojo apeleke kizimkazi Sisi hatuzitaki😕
 
RRRR za falsafa ya mama Samia ina manufaa makubwa sana, tena sana kwa kila Mtanzania na kwa Tanzania kwa ujumla.

R hizi 4 za mama Samia zina fursa kubwa sana ndani yake, kwetu sote. Nawaasa Watanzania tusikurupuke na tusibaki kutawaliwa kimazowea na wala tusiwe na fikra za mama Samia kuwa anatawala kama tulivyozowea.

Mama Samia amekwenda mbali sana, tena ya mazowea na upeo wa kawaida. Katuleta fursa za ajabu kwenye falsafa yake ya RRRR. Natumai wote tutachukuwa muda tuisome na tuielewe, tujielimishe ili tuzitumie fursa zinakuja na hizi RRRR.

Namshauri sana Waziri wa Habari na Wasemaji wote wa Serikali, kila mmoja kwa nafasi yake aielezee na kuifundisha falsafa kimaelezo na kivitendo. Na hili ni kwa mawaziri wake wote na watendaji waliomuelewa, waielezee na waifanyie kazi kwa vitendo ili Watanzania tuzione na kuzijuwa fursa ziliopo.

Nawaasa wale mawaziri na watendaji wakuu wa serikali ambao hawajamuelewa, wakiendelea kmazowea na kutoielewa hii falsafa ni heri wajiondoe wenyewe, la sivyo watashushwa njiani.

Nahisi, Hussein Bashe, kaielewa sana hii falsafa na anafanya kweli Reforms, kisasa. Upande mwingine, naona Kitila nae ameanza kumuelewaa. Sina shaka kabisa na Mchechu kuwa amemuelewa mama vilivyo na analidhihirisha hilo kinaga ubaga.

Watu ambao nawaona bado hawajamuelewa ni pamoja na Kassim Majaliwa na Makamo wa Rais. Nawwaona bado wanataka kuendelea kimazowea.

R ya kwanza ni Reconciliation, unaweza kutafsiri kama kupatanisha au mapatano lakini kiuhakika, falsafa hii ipo ndani ya Qur'an na inakwenda deeeper sana. Nawashauri wote, wapitoe aya zo zinazohusina na "reconciliation" ili waipate vyema.

Wengi wetu, hata mimi mwanzoni nilidhani inaishia juu ya meza na kupeana mikono na chadema. Nikaona mbona ipo "too shallow", lakini nilipoingia na kuanza kuichimba na kuichambuwa dhanna nzima kwa undani, nikaiona yenyewe tu, bila zile R nyingine mtu anaweza kuandika thesisis kumi au zaidi za PhD na zote zikapita with "flying colors".

Kwa kuwa dhanna hii moja ni bdefu sana tena, ntakuwa nikiitowa vipande vipande vyake kidogokidogo wakati uzi unaendelea.

Vijana zitumieni fursa, kuna watu watajaribu kuzibania kimazowea, msikubali, sasa hakuna mazowea. Pia nawashauri vijana ambao hawazioni fursa, waulize tuwaoneshe zilipo.

Ahsante sana mama Samia. You are the best.
Je, Mbunge wa Ngorongoro Mh. Ole Shangazi (CCM) na wapiga kura wake hawahusiki kwenye hiyo "R" ya kwanza? Au Quran inasemaje?
 
Mama Abdul Sasa Hivi Kila Jambo Lake Gumu Huo Ndiyo Ukweli Mchungu Ndugu Zangu
 
Je, Mbunge wa Ngorongoro Mh. Ole Shangazi (CCM) na wapiga kura wake hawahusiki kwenye hiyo "R" ya kwanza? Au Quran inasemaje?
Umeuliza maswali .matatu kwa mkupuo. Kwenye nyanja za elimu huo unaitwa ujinga. Ndivyo mwalimu wako alivyokufundisha? Au Sunday school?

Yachambuwe uulize moja moja, nikujibu, ndiyo kuelimika.
 
Back
Top Bottom