Saa 11:20 alfajiri unapishana na schoolbus zenye watoto wa miaka 4

Saa 11:20 alfajiri unapishana na schoolbus zenye watoto wa miaka 4

Ila kweli wanateseka aisee..wakifika nyumbani hakuna kucheza,ni kufanya homework na kula.Sasa wakicheza si watachoka sana jamani
Ni Uonevu usiomithilika kabisa huu mkuu
 
Na mabegi makubwa mgongoni kama wapanda mlima Kilimanjaro
Imekaaje hii[emoji848]

Saa 11:20 alfajiri Unapishana na schoolbus zimebeba wanafunzi wadogo wa miaka 4-6 wakipelekwa mashuleni.

Unabaki unajiuliza maswali mengi sana kichwani,

-Hivi Hawa watoto wameamshwa saa ngapi?[emoji848]
-Hivi Hawa watoto wameandaliwa kwa MDA gani?[emoji848]
-Hivi Hawa watoto wamekaa vituoni kusubiria school bus kwa MDA gani?[emoji848]

Wazazi, waalimu,Serikali, jamii na wahusika wote wa Hizi DAYCARE na PRIMARY SCHOOLS mnaofanya hivi mjitafakari sana kwa hili.

HAIINGII AKILINI KABISA[emoji3525]
 
Imekaaje hii[emoji848]

Saa 11:20 alfajiri Unapishana na schoolbus zimebeba wanafunzi wadogo wa miaka 4-6 wakipelekwa mashuleni.

Unabaki unajiuliza maswali mengi sana kichwani,

-Hivi Hawa watoto wameamshwa saa ngapi?[emoji848]
-Hivi Hawa watoto wameandaliwa kwa MDA gani?[emoji848]
-Hivi Hawa watoto wamekaa vituoni kusubiria school bus kwa MDA gani?[emoji848]

Wazazi, waalimu,Serikali, jamii na wahusika wote wa Hizi DAYCARE na PRIMARY SCHOOLS mnaofanya hivi mjitafakari sana kwa hili.

HAIINGII AKILINI KABISA[emoji3525]
Hawanunui magari ya kutosha,hapo watoto wapelekwe shuleni halafu wanafuatwa wengine kwa gari hilo hilo na unaweza kuta hiyo shule haipo mbali sana na makazi yao.
 
Nawaonaga jioni muda wa kurudi nyumbani, vimesinzia usingizi fofofo bus zima had huruma, sasa hapo ukute katoto kakike kamesukwa na dread za uzi kimevutwa nywele hatari, hapo unategemea mtoto atakua sawa kweli? Mtoto haogeshwi kichwa mwezi mzima kisa kimesukwa nywele halafu nywele zenyewe zinauma balaa, changanya na kukiamsha alfajiri hapo ni upuuzi mtupu
Nimejikuta nacheka balaa,napenda kusuka ila mwanangu big no akikua ataamua mwenyewe yaani unakuta kitoto kimesukwa nywele mzigo kichwani kimevutwa hadi huruma jamani kwakweli wazazi tujitafakari watoto wanapitia mateso.
 
Wenzetu Ulaya wana shule bora kuanzia level ya Kata.

Huku kwetu badala wazazi mji commit muboreshe mazingira ya shule zilizo jirani na makazi mnakimbilia kujaza ma bus ya watoto kuwasafirisha makilometa ya umbali bila sababu ya msingi.

Mtoto anakaa Chanika anasoma Olympio! Wa mbagala nae unalazimisha asome Olympio. Unategemea ataamshwa saa ngapi kupanda school bus?
Hiyo ni kazi ya serikali kuboresha mashule ya kata wanayojenga siyo siasa tu. Kwani hela ya serikali kazi yake nini kila kitu tujenge wananchi?
 
Imekaaje hii[emoji848]

Saa 11:20 alfajiri Unapishana na schoolbus zimebeba wanafunzi wadogo wa miaka 4-6 wakipelekwa mashuleni.

Unabaki unajiuliza maswali mengi sana kichwani,

-Hivi Hawa watoto wameamshwa saa ngapi?[emoji848]
-Hivi Hawa watoto wameandaliwa kwa MDA gani?[emoji848]
-Hivi Hawa watoto wamekaa vituoni kusubiria school bus kwa MDA gani?[emoji848]

Wazazi, waalimu,Serikali, jamii na wahusika wote wa Hizi DAYCARE na PRIMARY SCHOOLS mnaofanya hivi mjitafakari sana kwa hili.

HAIINGII AKILINI KABISA[emoji3525]
Change begins with you! Asilimia kubwa ya wanaolalamika humu ndiyo hao hao waliotufikisha hapa kwa kutofanya sehemu yao kikamilifu mahali fulani!

Ndiyo makandarasi walioshindwa kukamilisha ujenzi wa mabarabara waliokabidhiwa kujenga na hivyo kutusababishia mifoleni inayofanya watu kuanza safari usiku usiku kama wachawi ili tu kuwahi wanapokwenda, ndiyo wajenzi wa mashule, ndiyo wanandaa sera, ndiyo walimu wakuu, ndiyo wabunge, ndiyo mawaziri, ndiyo hao hao!

Mmejificha kwenye ID fake na sasa mnajidai kulalamika! Nendeni mkatimize sehemu zenu!'
 
Kama muda wao wa kulala sio zaidi saa kumi na mbili jioni(18:00) hakuna tatizo. Zaidi ya hapo sio afya

Wahusika wa shule (waalimu, wamiliki n.k) wangejibu hii hoja tuwasike na wao wanasemaje.

Inawezekana wao wanajua muda wa hao watoto kulala ni saa 18:00 jioni na pengine walishakubaliana na wazazi kuhusu swala hilo.

Vikao vya wazazi, waalimu (parents day) ni muhimu sana, kazi yake ndio kushuhulikia maswala muhimu kama haya.
 
Sema dar ndo ipo hvyo kwasababu ya foleni ila mikoani saa moja ndo wanaamka dar kila kitu shida.
Siyo sababu ya foleni ni uchache wa magari ya shule. Unakuta shule ipo segerea mwisho na watoto wanaishi kinyerezi afu wanashukuliwa saa12 kasorobo, hapo kuna foleni kweli??
 
Kama muda wao wa kulala sio zaidi saa kumi na mbili jioni(18:00) hakuna tatizo. Zaidi ya hapo sio afya

Wahusika wa shule (waalimu, wamiliki n.k) wangejibu hii hoja tuwasike na wao wanasemaje.

Inawezekana wao wanajua muda wa hao watoto kulala ni saa 18:00 jioni na pengine walishakubaliana na wazazi kuhusu swala hilo.

Vikao vya wazazi, waalimu (parents day) ni muhimu sana, kazi yake ndio kushuhulikia maswala muhimu kama haya.
Watanzania hatuna maZoea ya kulala saa 12 jioni, labda jela kwa Lazima.

Kwenye hizi familia zetu Ni nadra sana hizo kitu, KWANZA Ni wazazi wachache Sana MDA huo unawakuta nyumbani[emoji4]
 
Tatizo kubwa Sana hili mkuu
Sana....mtoto mpaka arudi home ni usiku na kesho alfajiri anaamshwa tena.

Kuna dem mmoja alikua anakaa Sinza halafu mtoto wake alikua anasoma Goba tena yupo grade 3.

Sasa siku ananihadithia eti jinsi anavyomuonea huruma mtoto wake kumuamsha sa 10 nilitamani nimtie makofi aisee halafu shule yenyewe ya kawaida tu ambako kila sehemu zimejaa,eti kisa mwenzie anaefanya nae kazi alimwambia ni shule nzuri
 
Change begins with you! Asilimia kubwa ya wanaolalamika humu ndiyo hao hao waliotufikisha hapa kwa kutofanya sehemu yao kikamilifu mahali fulani! Ndiyo makandarasi walioshindwa kukamilisha ujenzi wa mabarabara waliokabidhiwa kujenga na hivyo kutusababishia mifoleni inayofanya watu kuanza safari usiku usiku kama wachawi ili tu kuwahi wanapokwenda, ndiyo wajenzi wa mashule, ndiyo wanandaa sera, ndiyo walimu wakuu, ndiyo wabunge, ndiyo mawaziri, ndiyo hao hao! Mmejificha kwenye ID fake na sasa mnajidai kulalamika! Nendeni mkatimize sehemu zenu!'
Teh teh teh teh 😂 😂😂...umeamua kuwapa makavu...teh 😂😂😂
 
Elimu Bora au Bora elimu.
Kuna mdau kasema kwa uchovu wanaofika nao watoto, kule shuleni wanakuepo Kama masanamu TU kufata formality.

Ila akili yote hata haiko shuleni
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Elimu ya hii nchi imekaa katika mfumo wa kimagereza shule zimegeuka kuwa magereza ya watoto kibaya zaidi mzazi unalipia gharama za indirect imprisonment of your own fucking child...AMKENI
 
Back
Top Bottom