Saa 11:20 alfajiri unapishana na schoolbus zenye watoto wa miaka 4

Saa 11:20 alfajiri unapishana na schoolbus zenye watoto wa miaka 4

Hivi wewe na Mimi tunao comment kwenye huu Uzi si ni wahusika wa kuamsha watoto usiku?

Ambaye hahusiki ujue mtoto wake Yuko boarding au St Kayumba.
Nahusika humu na mtoto wangu haamshwi saa10 hata siku moja, ni ujuha kumuamsha mtoto mda huo kisa aende shule, maeneo ya karibu hakuna shule yenye viwango vya kumpleka mtoto?

Unaishi Mbezi mwisho unampeleka dogo Mikocheni, are you for real? Hiki kizazi wazazi hatuna busara kabisa.
 
Kuna matatizo sehemu nyingi hapa.

Hata wazazi tuna matatizo pia.
  • Inakuaje mzazi unakaa 12 km kutoka shuleni kwa mtoto tena umepanga? kwa nini usipange karibu na shule ya watoto wako unaamua kupanga karibu na kazini kwako?
  • Kwa nini mzazi usimtafutie mtoto shule karibu na nyumbani. Kama kwa radius ya 5km na hapo unapokaa hakuna shule nzuri, basi umekosea mahali pa kupanga/kujenga.
  • Si lazima masomo yaanze saa 1 asubuhi kila shule. Ni kukariri tu. Shule zinaweza kuwa na masaa tofauti ya kuanza masomo.
  • Shule zibanwe ziwe na mabasi mengi ili route zisiwe za kuzunguka sana. Hii itasaidia kupunguza muda wa watoto kuwa njiani. Wenye shule wasipobanwa kwenye eneo hili hawawezi kujali maana ni mahali wanapobana matumizi.
  • kama kwenye eneo moja kuna watoto wa shule moja wengi wazazi wanaweza ku opt kutolipia basi la shule wakatafuta usafiri wao wenyewe. Kuna mahali wazazi wamekodi noah inachukua watoto asubuhi na kuwarudisha jioni, badala ya basi la shule. Wanatumia pesa nyingi zaidi lakini kwa manufaa ya watoto wao
Kama hamna namna basi walau mtoto alale mapema ili apate masaa mengi ya kupumzika. Usimwache akaangalia tamthilia mpaka saa 4 usiku.
Upo sahihi, walau 5km distance! Sio mtoto anaenda 20km shule kila siku. Humtendei haki hata kidogo.
 
Wazazi wanazaa halafu hawataki kulea, wanajidai wanapeleka watoto shule ila sio kweli! Wanachofanya ni kuwanasukumia watoto kuepuka majukumu ya malezi

Kuna wakati unakuta vitoto vidogo miaka 2 na nusu, 3, 4, 5 boarding au kwenye school bus alfajiri unapata huruma hadi unatamani kumwomba Mungu awanyime wazazi wao hiyo pesa ya kuwapeleka huko.

Ukisikia pesa inakutumia badala ya wewe kuitumia ndio hapo
Boarding kwa umri huo ni kutelekeza mtoto, mbaya sana. Anadevelop tabia za ajabu, unamlaumu na kumpiga wakati ulimtupa akijifunzie huko.

Umeona athari za kuvuruga utamaduni? wanawake walipaswa wabaki na majukumu yao ya asili- kulea. Kula kwa jasho abaki nayo mhusika!
 
Upo sahihi, walau 5km distance! Sio mtoto anaenda 20km shule kila siku. Humtendei haki hata kidogo.
Wazazi wa familia 3 au 4 wanaweza kumrecruit mwalimu wa watoto wakamuandalia vifaa na mazingira biashara ya usumbufu ikaisha.
 
Wazazi wanazaa halafu hawataki kulea, wanajidai wanapeleka watoto shule ila sio kweli! Wanachofanya ni kuwanasukumia watoto kuepuka majukumu ya malezi

Kuna wakati unakuta vitoto vidogo miaka 2 na nusu, 3, 4, 5 boarding au kwenye school bus alfajiri unapata huruma hadi unatamani kumwomba Mungu awanyime wazazi wao hiyo pesa ya kuwapeleka huko.

Ukisikia pesa inakutumia badala ya wewe kuitumia ndio hapo
Toa nondo mama d mpaka waereweee😂😂😂

Mama mwenye busara zake

Ova
 
Hawa watoto wanapata muda kidogo wa kupumzika (kulala).

Isitoshe wanapewa 'home work' nyingi sababu masomo wanasoma mengi na hata mabegi yao makubwa sababu ya kubebeshwa madaftari mengi...

Hii sio sawa.
Hapa kwenye begi ndo panaponikera zaidi, utadhani mpagazi wa mt. Kilimanjaro

Kwani kuweka makabati huko mashuleni kila mtoto akapewa funguo yake ni /= kiasi gani?
Miundo mbinu mibovu ya shule, wamiliki njaanjaa akiona hana watoto anageuza mabanda ya kuku.
 
Tatizo ni uhaba wa mabasi kwenye hizo shule husika unakuta shule idadi kubwa ya wanafunzi lakini mabasi ya kukusanya wanafunzi yapo mawili au matatu.
Pia kuna haja ya kuelimisha wazazi ni kwa namna gani umbali wa shule na unapoishi vinavyo athiri afya ya akili na maendeleo ya taaluma ya mtoto.
 
Sana....mtoto mpaka arudi home ni usiku na kesho alfajiri anaamshwa tena.

Kuna dem mmoja alikua anakaa Sinza halafu mtoto wake alikua anasoma Goba tena yupo grade 3.

Sasa siku ananihadithia eti jinsi anavyomuonea huruma mtoto wake kumuamsha sa 10 nilitamani nimtie makofi aisee halafu shule yenyewe ya kawaida tu ambako kila sehemu zimejaa,eti kisa mwenzie anaefanya nae kazi alimwambia ni shule nzuri
Mpuuz uyo anaogopa wenzie watamuonaje, uku anahatarisha afya ya akili ya mwanae
 
Wazazi tumepata pesa ya kuwatesa watoto badala ya kuwatunza watoto. Mtoto anakua kwenye school saa11 alfajiri ameamka saa ngapi?

Halafu unampeleka mtoto mdogo miaka 3,4 shule saa 11 alfajiri ili iweje? Anaenda kukuletea pesa au mshahara.

Watoto kusoma katika umri mdogo ni sawa lakini sio kumuamsha alfajiri. Mtoto alale usingizi wake uishe, akue vizuri, apate muda wa kucheza, kulala na kusoma

Binafsi naprefer homeschooling kwa watoto wangu hadi 6yrs, na baada ya hapo sipeleki mtoto shule ya kumuamsha saa11.

Watasoma shule ya karibu na nyumbani au mimi nitahamia karibu na shule watakayosoma

Mtoto miaka2, 3, 4 aamke saa 11 mimi niamke saa11, HAPANA
Kiukweli hili halikubaliki mkuu[emoji3525]
 
Twende mbele turudi nyuma jamani!

Hivi mtoto wako wa miaka mitatu/minne (chekechea )unashindwa kumfundisha mwenyewe nyumbani?!

Mimi nilifundishwa nyumbani na mama tena huko kijijini nilipoanza la kwanza na waliosoma chekechea nikaongozea mbona?!!

Ujinga ni wa wazazi wa leo, acha waliwe mipesa na kutesa watoto wao kwa pesa zao wenyewe[emoji3525]
Kiukweli umeongea hoja ya msingi Sana, enzi hizo tulifundishwa na Bibi zetu.

Ikitokea miaka ya 2000 kukawa na zile twishen ndogo ndogo za pale mtaani, mtoto anashinda pale anacheza uku anajisomea kdg kidg.
 
Uko sawa 100% Mama D. Mtoto wa miaka 4 unamwamsha kwa alarm? Huyu anatakiwa alale mpaka aamke mwenyewe usingizi unapomwisha.
Kuna haja ya waalimu kuanza kuspecialise kwenye private schooling kwa watoto. Watapata sana watu
Sahii kabisa,
Private home schooling inaweza saidia hili tatizo.
 
Wazazi wanazaa halafu hawataki kulea, wanajidai wanapeleka watoto shule ila sio kweli! Wanachofanya ni kuwanasukumia watoto kuepuka majukumu ya malezi

Kuna wakati unakuta vitoto vidogo miaka 2 na nusu, 3, 4, 5 boarding au kwenye school bus alfajiri unapata huruma hadi unatamani kumwomba Mungu awanyime wazazi wao hiyo pesa ya kuwapeleka huko.

Ukisikia pesa inakutumia badala ya wewe kuitumia ndio hapo
Kabisa,
Wazazi wanaitumikia pesa, na pesa inapelekea kuzitesa damu zao wenyewe.
 
Kwa nini tusiwe na hulka ya kuboresha shule zilizopo karibu na mazingira yetu, hii tabia ya kuamsha watoto saa 11 sio poa hata. Mtoto aamke 12, aandaliwe vizuri hadi saa moja aende shule akiwa fresh.
Sahii kabisa mzee mwenzangu
 
Nahusika humu na mtoto wangu haamshwi saa10 hata siku moja, ni ujuha kumuamsha mtoto mda huo kisa aende shule, maeneo ya karibu hakuna shule yenye viwango vya kumpleka mtoto?

Unaishi Mbezi mwisho unampeleka dogo Mikocheni, are you for real? Hiki kizazi wazazi hatuna busara kabisa.
Huu upuuzi haufai hata kidogo
 
Tatizo ni uhaba wa mabasi kwenye hizo shule husika unakuta shule idadi kubwa ya wanafunzi lakini mabasi ya kukusanya wanafunzi yapo mawili au matatu.
Pia kuna haja ya kuelimisha wazazi ni kwa namna gani umbali wa shule na unapoishi vinavyo athiri afya ya akili na maendeleo ya taaluma ya mtoto.
Sahii kabisa,
Kwa hili wazazi Ni kiungo muhimu kulikomesha, elimu itolewe
 
Boarding kwa umri huo ni kutelekeza mtoto, mbaya sana. Anadevelop tabia za ajabu, unamlaumu na kumpiga wakati ulimtupa akijifunzie huko.

Umeona athari za kuvuruga utamaduni? wanawake walipaswa wabaki na majukumu yao ya asili- kulea. Kula kwa jasho abaki nayo mhusika!
Ukisasa na umjini mjini umetupofusha kuhatarisha maisha ya wanetu.

Hii ya kua wote baba na mama wafanyakazi Ina athari zake Sana.
 
Sio kweli Mbezi, Kimara, Segerea kote hakuna shule nzuri mpaka umpeleke mtoto wako Mikocheni saa kumi usiku kila siku, ni ulimbukeni tu.

WA adopt basi hao watoto wewe maana una uchungu kuliko wazazi wao
 
Back
Top Bottom