Sakata la Lissu v Tigo: Serikali haitahusika kama hakuna barua za Serikali kwenda Tigo

Shukrani sana mtoa uzi katika nyuzi zake nyingi anaona ana absolute truth, facts, Huwa anaumia sana akipata challenges zenye reference.
 
Hata tiGO under new supervision hawana kesi hapo!
-Utanunua kampuni na madeni kama yapo lakini siyo lawama, lawama ni poor service kwa kampuni kwa wakati wa usimamizi / lawama za management kwa wakati husika!
Kuvujisha taarifa za mteja ni kosa sio lawama
 
Mwasiliwa ameongea mbele za watu kuwa anawajua waliomshuti tigo awakumshuti wala serikali awana sheria ya kushuti watu ivyo pesa azina ya watanzania aifai kubebeswa zigo la watu wengine si anawajua kasema awashtaki wabaya wake.na awadai wao sio serikali pesa zetu tunataka zisaidia kuongeza madaktari walimu kujenga zahanati barabara maji, pesa yetu no kaka lisu tunakupenda tumeuzunishwa na yaliokutokea lkn watanzania usitubebeshe ili deni,, si unawajua wabayawako fungua kesi kuwashtaki wao. Ukiishtaki serikali utakuwa utapeli wa pesa za umma kupitia mahakama. nasema uwongo nduguzangu.
 

..waliomshuti ni watumishi wa serikali.

..na walifanya tukio wakitumia rasilimali za serikali, kama risasi, bunduki, magari, etc.

..labda kuwe na hoja wahusika walikuwa likizo ndio wametenda unyama ule.

..kutokana na hayo serikali itabeba lawama kwa kushindwa kusimamia na kuwadhibiti watumishi wake.

..italaumiwa pia kwa kutofanya uchunguzi, na kuwashtaki wahusika.

..serikali italazimika kuwashtaki watumishi wote waliohusika, na maswahiba wao walioko Tigo.

..kutokana na sababu na mazingira niliyoyataja hapo juu, serikali italazimika kumlipa fidia Tundu Lissu.
 
Mkuu unadhani kwa utawala usiofuata sheria, kwa kufanya uhalifu unaweza kukubali kufanya hivyo ikiwa wana nia ovu?.
 
Mkuu hapo n lissu na
Bilioneaaa mtarqjiwa

Tondu..lissu

Wao watasema walitoa wamepeleka wapi info
 
Mkuu umeweka vitu kama vitatu kwambo rasilimali kwakua niyaserikali moja ya sababu nianze kwanza na mtu anaetuumiwa kuratibu tukio uyu jamaa akuwa ktk mkoa wake na kisheria ukitoka ktk mkoa wako ww unamlaka yyte nje ya mkoa wako pili ikiwa sababu ni utumishi yani anawajibika mwajili kama ivi basi serikali inamadeni mengi mfano tu juzijuiz apa kulitokea polisi kupigana risasi kwasababu zao wenyewe.je ile famiria ya aliekufa inafaa kuishtaki serikali.na ikiwa ndio rasilimali lipo tukio la polisi kujipiga risasi mwenyewe kwasababu zake mwenyewe je nayo famiriayake iende mahakamani kuishtaki serikali sababu iyo bunduki ni Mali ya seeikali?
 
Mkuu umeweka vitu kama vitatu kwambo rasilimali kwakua niyaserikali moja ya sababu nianze kwanza na mtu anaetuumiwa kuratibu tukio uyu jamaa akuwa ktk mkoa wake na kisheria ukitoka ktk mkoa wako ww unamlaka yyte nje ya mkoa wako pili ikiwa sababu ni utumishi yani anawajibika mwajili kama ivi basi serikali inamadeni mengi mfano tu juzijuiz apa kulitokea polisi kupigana risasi kwasababu zao wenyewe.je ile famiria ya aliekufa inafaa kuishtaki serikali.na ikiwa ndio rasilimali lipo tukio la polisi kujipiga risasi mwenyewe kwasababu zake mwenyewe je nayo famiriayake iende mahakamani kuishtaki serikali sababu iyo bunduki ni Mali ya serikali
 
Mgema na Tembo wana story nzuri ssna kwenye eneo la sifa
 
Pia tumeona juzijuzi Lisu akisema baada ya tukio kuzuiwa kongamano kule mbeya na kina Awadhi, kupigwa baadhi yao kaka yetu Lisu alisema wataenda mahakamani kuwashtaki binafsi kina Awadh sio serikali.
 
Mm natetea tu rasilimali za watanzania masikini apa tulipo masikini dawa zatabu kwaiyo nikiona kuna dalili ya kuchotwa pesa moyo unauma sana pesa zetu sio za mama Abdur kama Lisu anataka tuamini kuishtaki serikali ni kuishtaki azina yetu mana serikali ikishindwa akamatwi mtu ni fidia kutoka azina. Apana awashtaki kimataifa wabaya wake kisha serikali ipewe maelekezo na mahakama wadaiwa wakamatwe wawakabidhi uko wanakotakiwa wafilisiwe pesa apewe Lisu. Azina asiguse chama kitaingia lawama kubwa itakuwa fursa kwa CCM kuwashtaki kwa wananchi embu waza Lisu amekamata ndege ya watanzania afu anakuja Tanzania!!!
 
Robert Heriel Mtibeli kumbuka hili...

## Msingi wa tatizo ni kesi ya "jaribio la mauji ya kisiasa na tendo la kigaidi" alilotendewa mwanasheria, mwanasiasa, mwanaharakati mkosoaji mkuu na mashuhuri Tanzania Mh. Tundu Lissu wa sera na mipango ya serikali chini ya CCM kwa miaka zaidi ya 20 sasa...

Maswali makubwa ambayo kila mtu hujiuliza ili kupata majibu yasiyo na shaka ni:

1. Ni kwanini walitaka kumuua mtu huyu...?

2. Nani alitoa amri ya kuuwawa mtu huyu..?

3. Kina nani walihusika kupanga na kutekeleza shambulio hilo...?

4. Kwanini Vyombo vya kisheria vya serikali ya Tanzania i.e Police, DCI, DPP nk vimeshindwa kutenda wajibu wao wa kisheria na kikatiba kuchunguza na kuchukua hatua? Nani anawazuia kutenda wajibu wao..?

##Kwa ushahidi ambao umeanza kuchomoza, TIGO kampuni ya mawasiliano ya simu chini ya mmiliki wake Millicon/Honora, kwa kutumia mifumo yao (hawa TIGO) ya mawasiliano ambayo victim Tundu Lissu ni mteja wao inaonesha walikuwa sehemu ya wawezeshaji wa unyama huu wa mauaji kwa njia moja au nyingine....

##It doesn't matter whether walikuwa na mawasiliano rasmi na mtuhumiwa namba 1 (serikali) au la. Hili litajulikana tu kwa taarifa ya uchunguzi mahususi uliofanywa na Mr. Michael Clifford anaoutumia kama ushahidi kudai yake haki yake toka kwa Millicon/Honora/TIGO (T) ambao anaendelea kuutoa mahakamani huko Uingereza....

NOTE:
√. Kwa maoni yangu, naweza kukubaliana na hisia zako kuwa, obvious serikali nzima haikuhusika isipokuwa watu wachache, wakubwa, wazito na wenye mamlaka na maamuzi makuu ndani ya serikali walioamua kuvunja sheria na katiba na kutumia vibaya mamlaka yao (abuse of power) kwa maslahi yao binafsi ya kisiasa kutenda tendo baya kabisa la kinyama (barbaric) la kumuua mtu huyu (Tundu Lissu) kwa sababu tu anahatarisha (jeopardize) mipango na maslahi yao hayo ya kisiasa....

√. Hawa ndio wanaotakiwa kujulikana ili hatua za kisheria dhidi yao ziwalalie na huyu mtu (Tundu Lissu) aweze kutendewa vyema na kupata haki yake. Na TIGO mpaka hapo wako kwenye position nzuri ya kufumbua fumbo hili kwa msaada wa Mr Michael Clifford....
 

..kama una uchungu wa kweli na hazina ya nchi basi unapaswa uwabane watekaji, watesaji, na wauwaji, walioko serikalini.

..unapaswa kuelewa kwamba matendo ya kinyama ya watumishi wa vyombo vya dola ndio yanayoweza kusababisha serikali / hazina kubeba mzigo wa kulipa fidia kwa wahanga.
 

Sheria ni kutafuta Loophole tu....Tobo la kutokea.
 
1. Ni kwanini walitaka kumuua mtu huyu...?

2. Nani alitoa amri ya kuuwawa mtu huyu..?

3. Kina nani walihusika kupanga na kutekeleza shambulio hilo...?
1. Kwasababu alikuwa Mpiga kelele/msaliti kwa mujibu wa mtoa order.
2.Nzirankende aka Jikono Jandama
3.Mkolomije na genge lake la wasiojulikana.
 
1. Kwasababu alikuwa Mpiga kelele kwa mujibu wa mtoa order.
2.Nzirankende aka Jikono Jandama
3.Mkolomije.
Huyu Mkolomije hivi ni kwanini anaogopega hivi?

Polisi, TISS, DCI, PCCB, na hata Rais mwenyewe aliyemteua eti anamuogopa. Why..?

Huyu jamaa bila shaka mizimu na miungu yake iko very powerful and manipulative kwa kiasi cha kutisha sana...!
 
Huyu Mkolomije hivi ni kwanini anaogopega hivi?

Polisi, TISS, DCI, PCCB, na hata Rais mwenyewe aliyemteua eti anamuogopa. Why..?

Huyu jamaa bila shaka mizimu na miungu yake iko very powerful and manipulative kwa kiasi cha kutisha sana...!

Anaogopeka kwasababu ametekeleza mission zao kubwa sana hivyo lazima wamlinde.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…