Sakata la mtoto wa Amber Lulu, Harmorapa akamatwa na Polisi

Sakata la mtoto wa Amber Lulu, Harmorapa akamatwa na Polisi

Msanii wa Bongo Fleva anayependa kiki Bongo, Hamorapa amekamatwa na polisi, leo Jumamosi, Mei 8, 2021, katika Ukumbi wa Hotel ya Kebbys, uliopo Mwenge, jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Kukamatwa kwa Harmorapa kunatokana na kauli yake aliyoitoa akidai kuwa mtoto wa Amber Lulu ni wa kwake kwani wanafanana.

Baada ya kauli hiyo mzazi mwenzake na Amber Lulu aanayejulikana kama Mr. Botion alimbana Harmorapa ambaye alikana na kusema kuwa mtoto huyo si wake.

lakini baada ya kuondoka alijirekodi tena kipande cha video akisema amenyanyaswa na kudharirishwa na Botion na wenzake hivyo akasisitiza kuwa mtoto yule ni wa kwake na atazungumza na wanahabari kuanika ukweli halisi, lakini wakati akiendelea kuzungumza na wanahabari ndipo Botion alitua na polisi wakamkamata na kumpeleka kituo cha polisi Mabatini.

Sasa hapo wanamkamata wakati kweli mtoto amefanana?
 
Ila hili sakata la huyu mtoto, anayetakiwa kutoa majibu ni Amber, maan mtoto mwenyewe inasemekana wa MAJANI.
Ndo madhara ya kuwa mdangaji, kila aliyekojoa anadai mbegu ni yake. [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Hatari sana
 
Hii Jinai au Madai?Wanasheria njooni maana mtu kasema mtoto ni wa wake.
 
Kweli hatuchagui wazazi, lakini imagine, mamaako ni Amber Lulu na babaako ndio awe Harmorapa. Lazima uwe maarufu town kabla ujafikisha miaka 10
 
Botion nime mvua vyeo vyote ndan ya 26 ni utoto anaofanya anatumia nguvu nyingi kupambana na fala
Hujui inakera kiasi gani mpaka yakukute,nakumbuka nilikuwa nashangaa mtu unakasirikaje ukitukanwa mpaka siku nilipotukanwa nna kinyongo mpaka kesho
 
Siajabu mama alipewa smart phone na Hamorapa leo anatumia nguvu kubwa kumtaka akane kuwa aliwahi kula kitumbua.
ungeyasikia maongezi ya harmorapa hakika usingesadiki maneno yake. Ni mpuuzi tu ndiyo anaweza kuelewa akili za huyu kijana. Baada ya kuambiwa wanafanana na mtoto wa amberlulu basi ikawa opportunity kwake ili atrend. Vaa viatu vya amberlulu ukiwa unajua fika hauna uhusiano wowote wala hukuwahi kutembea nae, Kisha usikie mtu huyo anatangaza habari Kama hizi. Lazima uchukue hatua. Anachokifanya Harmorapa ni uzalishaji wa wanawake, hata Kama ni kweli si angemfata muhusika wakayamaliza kimya kimya vyombo vya sheria si vipo. Huyu kijana anapaswa kupewa fundisho kabisa ili uwe mfano kwa wengine wenye tabia za kipumbavu Kama hizi.
 
Hivi Botion alitoka jela lini mpaka akaweza mtia mimba Ambar?
 
ungeyasikia maongezi ya harmorapa hakika usingesadiki maneno yake. Ni mpuuzi tu ndiyo anaweza kuelewa akili za huyu kijana. Baada ya kuambiwa wanafanana na mtoto wa amberlulu basi ikawa opportunity kwake ili atrend. Vaa viatu vya amberlulu ukiwa unajua fika hauna uhusiano wowote wala hukuwahi kutembea nae, Kisha usikie mtu huyo anatangaza habari Kama hizi. Lazima uchukue hatua. Anachokifanya Harmorapa ni uzalishaji wa wanawake, hata Kama ni kweli si angemfata muhusika wakayamaliza kimya kimya vyombo vya sheria si vipo. Huyu kijana anapaswa kupewa fundisho kabisa ili uwe mfano kwa wengine wenye tabia za kipumbavu Kama hizi.
Tatizo wote mazoba tu hata hao Amber na Abotion
 
Back
Top Bottom