#COVID19 Serikali isiwaache Wananchi katika mataa kwenye suala la Corona
Bora hata ingenyamaza isiseme kitu. Kiongozi wake anakataza wasaidizi wake na misukule ya MATAGA wasivae barakoa, na wao wanamsikiliza halafu wanakuja kutuambukiza huku mtaani!
Wakati anawakataza ulikuwepo bwashee?

Hii nchi inaongozwa kwa mujibu wa sheria au umesahau bwashee?
 
Baada ya kupata taarifa na kushuhudia misiba minane au kumi sasa. Nasema hivi huu ugonjwa upo hapa Tanzania.

Tatizo tu lililokuwepo ni kwamba. Kupata taarifa zake ni labda. Itokee msiba wa msanii kama ilivyo kwa cpwaa au mtu mkubwa. Ila mtaani huku. Mbona wakutosha tunawaezekea zege kwenye ardhi.

Liwalo na liwe upooooo.
 
Baada ya kupata taarifa na kushuhudia misiba minane au kumi sasa. Nasema hivi huu ugonjwa upo hapa Tanzania.
Tatizo tu lililokuwepo ni kwamba. Kupata taarifa zake ni labda. Itokee msiba wa msanii kama ilivyo kwa cpwaa au mtu mkubwa. Ila mtaani huku. Mbona wakutosha tunawaezekea zege kwenye ardhi.
Liwalo na liwe upooooo.
Hakuna anaesema haupo. Ni kuchukua tahadhari
 
Wewe kwenye familia yako umeawaachia kila mtu na lwake yaani aamue anavyotaka au unasimama kidete kuhakikisha kila mtu yuko salama na haleti maradhi ndani ya nyumba kutoka huko aendako?

Ukiweza kujibu hili then fikiria ungekuwa baba wa familia kuubwa iitwayo Taifa, ungefanyaje?
Wewe endelea kulumbana boss wako maalimu Seif anavaa barakoa!
 
Shida wapinzani wanataka tupigwe Lock down utafikir wao wana Chakula cha kutulisha..
 
Jamani kamvua na ubaridi Dar kameanza so tuchukue tahadhari...maana yule mdudu na baridi ni damu damu
 
Ndugu zangu,

Wahenga walisema hivi "Mficha maradhi kifo humuumbua" Amiri Jeshi mkuu wangu Magufuli Kifo kinakuumbua

Sioni tatzio kama ukikubali kwamba Korona Ipo na ukachukua hatua za lazima kuhangaika suala hili.Mbona watanzania watakupa ushirikiano tu. Si uliona mara ya kwanza walivonunua ndoo wakanawa mikono na dala dala zikawa level siti na barakoa wakavaa na kujifukiza majani ya ajabu wakajifukiza?Kwani unaona aibu ya nini?

Hizi siasa na maisha ya watu zinakusaidia nini?ZInakupa faida gani?Au mpaka afe mtu wako wa karibu sana kama mkeo/mtoto wako ndo utaelewa kwamba siada katika maswal aya afya ni marufuku?

Mheshimiwa Raisi,Watu wanakufa kama nzi,Waziri wako wa Afya anamsifia mume wako na kutoa matamko ya taarabu.Hivi mantuaonaje watanzania?Mnatuona sisi ni Mbuzi sana na tunafaa kufa tu maana hatuna umuhimu.

Haya umekataa habari ya chanjo,umekataa kufanya vipimo na kutoa takwimu hata kuhamasisha watu wajikinge nako pia hutaki.Tunajua ulikaa kupima kwa sababu hakuna pesa ya kununua vipimo na tunajua umekataa kuchukua chanjo kwa sababu ya ukata lakini kwani kunawa mikono na kuvaa barako nako kunahitaji PESA yako.Si useme tu.

Ona sasa jinsi kifo kinavyotuumbua.Watu wanakufa kama kumbikumbi unataka tuwale nyama?Unafikiri utakuwa huna hatia kama kiongozi mkuu wa nchi?Unafikiri wewe upo salama?

Mheshimiwa chukua hatua.Fanya uamuzi kama rais anayejali watu.hata kama ni kuwafungia watu ndani wafungieni ila jamani watu wanadanja kama mzaa vile.

Hii kitu sasa haichagua,inazoa tu watu.

Hii kweli ni CORONA sasa sijui Ndo tunakufa wote?
 
Shida wapinzani wanataka tupigwe Lock down utafikir wao wana Chakula cha kutulisha..
we TAGA, wapinzani wanahusikaje na ugonjwa? Si mliwapokonya madaraka? Wamemua kukaa kimya kabisa, pambaneni na hali zenu
 
Back
Top Bottom