Serikali kutodhibiti idadi ya wageni wanaoingia nchini kwa kisingizio cha Utalii, inahatarisha Usalama wa Taifa dhidi ya virusi vya Corona

Serikali kutodhibiti idadi ya wageni wanaoingia nchini kwa kisingizio cha Utalii, inahatarisha Usalama wa Taifa dhidi ya virusi vya Corona

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Mhudumu wa uwanja wa KIA amesema katika kipindi hiki ambapo ugonjwa wa Corona Virus umepiga sana China, idadi ya watalii kutoka China imeongezeka maradufu kuja nchini.

Wachina wenyewe wakihojiwa wamesema pamoja na utalii wamekuja kutafuta sehemu salama kukimbia ugonjwa huo kwao.

Hii hali ininatisha sana haswa ukizingatia mgonjwa wa kwanza kufa huko ulaya yaani Ufaransa ni mzee aliyekuwa ameenda kutalii.

Swali la kujiuliza ni, kwanini katika hali critical namna hii serikali inaendelea kutoa viza kwa wingi na kuwaruhusu Wachina kuingia kwa wingi namna hii?

Hebu tujiulize laiti nchi yetu ingekuwa imepigwa na Ebola au Corona wangeturuhusu kukimbilia kwao?

Hii hali ni ya ajabu sana, wakati serikali hii inasuasua kuwarudisha watoto wetu walioko Wuhan (sababu mojawapo ni kuhofia hao watoto kuleta maradhi nchini), hii ni double standard kubwa, iba maana tunaweka mbele pesa za kitalii kuliko usalama wa taifa letu?

Wenzetu Wakenya wamesitisha safari za ndege zao China kuepuka kuleta maradhi nyumbani lakini sisi tumefumba macho kwa sababu ya kuogopa kuwaudhi wachina.

Mashirika makubwa ya ndege kama vile British Airways nao wamesitisha safari za China na kuna nchi kama vile zimesitisha kupokea watalii wa Kichina, sisi tunakwama wapi?

Shirika la Ethiopian Airline ndo limekuwa mchawi zaidi, lenyewe linaweka mbele maslahi ya fedha na hivyo kuhatarisha bara zima la Afrika, limeshutumiwa sana kuendelea kufanya biashara katika kipindi hiki cha hatari.

Hapa chini nimeweka video ikionyesha dege la Ethiopia Airline likishusha mamia ya Wachina huko KIA.

---
Ugonjwa wa Corona umezidi kusambaa kwa kasi na kuingia kwenye nchi nyingi duniani licha ya tahadhari kubwa na teknolojia ya hali ya juu ya kuchuja wageni

Baada ya kuona ugonjwa huu haudhibitiki kirahisi sasa imepelekea nchi nyingi kukata mawasiliano kabisa na nchi zenye maambukizi makubwa ya ugonjwa huu kama China, Iran, Italia, Japan na Korea

Hata hivyo Tanzania haina habari, Tanzania imezidi kupokea watalii kutoka China huku ikijidai kuwa haijali raia anatokea wapi kwa kuwa ipo vizuri kwenye kujilinda

Hiki ni kichekesho ukizingatia facilities na teknolojia za Tanzania ukizilinganisha na nchi nyingine duniani ambazo zimefunga kabisa usafiri na nchi athirika kwa hofu ya kuenea ugonjwa huu,

nchi kama Urusi ambayo ni mshirika mkubwa wa China imepiga marufuku raia wote kutoka China sababu ya ugonjwa huu ambao aambukizi yake hayaonekani mpaka zipite siku 14, nchi nyingine zilizopiga marufuku kabisa raia wa China ni Australia, Singapore, Iran, Ufilipino, New Zealand n.k

Nchi nyingine zimefika mbali zaidi kwa kupiga marufuku kabisa hata raia wa nchi nyingine ambaye aliwahi kwenda China siku za karibuni

Nchi kama Saudi Arabia imesitisha ibada za Hijja ndogo kutokana na hofu ya maambukizi haya, na inaweza kupiga hata marufuku ya Hijja kubwa

Nchi nyingi za kiarabu pia zimekatisha kabisa safari zake na Iran ambayo ina waathirika ambao hawafiki hata 300 kwa hofu ya ugonjwa huu, lakini Tanzania inaruhusu watalii kutoka China kwenye maambukizi ya takribani 80,000



Rais Magufuli wewe na watendaji wako mnapata wapi ujasiri wa kuwaruhusu watalii kutoka China?

Rais Magufuli kuna clip ambayo imesambaa sana ikionyesha kujiwa na watalii wengi uwanja wa ndege wa kimataifa KIA kutoka China na mtendaji wa mamlaka wa uwanja wa ndege huo akitoa comments na kuthibitisha kuhusu ujio huo wa watalii.

Swali langu kwako Rais Magufuli, ina maana wewe na watendaji wa serikali yako mnajiona kama ni binadam wenye akili kubwa sana duniani kuliko binadam wengine wote? Au ndiyo ina maanisha kuwa watanzania wana njaa kubwa sana kiasi mbacho ikakufanya wewe na watendaji wako wa serikali yako mkakubali kuwaingiza watanzania kwenye riski kubwa ya kujipatia maradhi ambayo ulimwengu wote unatetemeka?

Watanzania wengi ndani na nje ya nchi yetu wamelalamika sana kuhusiana na uamuzi huo ambao wewe na watendaji wako mmeamua kuufanikisha. Watanzania wengi hasa walio nje ya nchi hawaelewi kwa nini serikali hiyo hiyo iliyokataa kuwarudisha vijana wetu wanaosoma huko kwenye mji wa mlipuko wa ugonjwa unaosababishwa na CORONA VIRUS, lakini hawa ma-tourist kutoka CHINA tunawapokea kwa mikono miwili? Ina maana wewe Rais Magufuli unajiamini kiasi hicho cha kuitumbukiza nchi yako kwenya janga kama hili ili mradi upate hela za miradi yako ya maendeleo?

Rais Magufuli mimi binafsi nilikuona ni mtu mwenye akili sana kuliko watanzania wote wengine, lakini kwa tukio hili inabidi niingie wasi wasi kuamini kuwa uwezo wako wa kufikiri mambo kama unalingana na yote uliyo tuuzia mpaka sasa. Usifikiri kuwa ni sifa kufanya vitendo vya namna hiyo, huko ni kujitengenezea kaburi letu wenyewe.

Usifikiri kuwa wewe na watendaji wako mna uwezo wowote ule wa kuweza kutibu ugonjwa huu kama utatokea Tanzania. Na hii nakuambia Rais wangu kuwa hata kama ungekuwa na hospitali ngapi na hata kama ungeangiza vifaa vya kisasa vya haina gani, nchi yako na watanzania kwa ujumla hawana uwezo wowote ule wa kutibu ugonjwa huu.

Pamoja na kuwa watanzania wamekuamini na kukusifu kwa matendo yako, lakini nakuomba kwa hili usimkufuru Mungu wako. Usijikute ukateketeza yote uliyoyafanikisha mpaka sasa. Kukiwa na Outbreack ya huu ugonjwa nchini, elewa kuwa Tanzania itateketea moja kwa moja. Tutaokota mizoga mpaka hapata kuwa na mtu tena wa kuokota mizoga hiyo.

Zaidi ya hapo naomba zingatia kuwa nchi yako haina wataalam wa kimaabara na wala hatuna research Institute yenye wataalam mbao wanatambulika kimataifa kuwa wana uwezo wa kufikiri beyond the horizone. Hao ma PHD holders wako wasikuzingue akili kiasi kwamba ukapoteza fahamu. Hao ni matheoretician tu na holders wa vyeti kwa ajili ya mishahara. Sio great thinkers hao. Waangalie wasije wakakuponza ukaharibu kila kitu.

Serikali ya nchi kama Ujerumani ina haha na kujaribu kuchukua njia zote zinazo wezekana kuzuia usambazaji wa huo ugonjwa wameshindwa sembuse serikali ya kitanzania ndiyo iweze?

Jumatatu iliyopita wajerumani walisheherekea Carnival, wenyewe wanaiita "Rosenmontag Zug" kwenye miji yao ya Duesseldorf, Cologne na Mainz. Mpaka kufikia asubuhi ya jumanne watu wawili walikuwa wamelazwa kwenye Hospitali yao ya jimbo la Nord Rhein Westfallia mjini Duesseldolf na mpaka leo tarehe 29.02 2020 tayari idadi ya watu zaidi ya 60 wamesha kuwa infected.

Ilianza na mtu mmoja kwenye Carnival yao Duesseldorf na hivi sasa majimbo manne yamekwisha kumbwa na ugonjwa huo, Hamburg, Hessen, North Rhine Westphalia na Baden Weurttenberg.

Inawezekekana nyie watanzania wa nyumbani mnachukulia kitu kimzaa mzaa sana. Lakini watanzania wengi ambao wako ughaibuni wana wasi wasi mkubwa sana na ndugu zao nyumbani na nchi yao pia. Hiki sio kitu cha kukichezea. Ni kitu hatari sana!

Nakuomba chonde chonde Rais wangu kuchukua hatua mara moja za kuzuia kumiminika kwa watu kutoka China. Maisha ya watanzania hata kama ni ya kisokwe, yanathamani kubwa sana kuliko hayo mabilion ya fedha yanayoingizwa na watalii. Hao watu wanao jiita watalii naomba wasubiri. Mali asili yetu na Mbuga za wanyama ziko na zitaendelea kuweko, lakini ndugu zetu kwa upande mwingine kama mlipuko.utatokea hawata kuwepo tena.

Rais Magufuli sisi masokwe hatuna uwezo hata mara moja wa kuzuia kuenea kwa ugonjwa unaosababishwa na CORONA VIRUS.

Sent using Jamii Forums mobile app



Pia soma
> Utalii: Wachina 600 kutua Tanzania wiki ijayo
> Serikali yatenga maeneo maalumu kwa watu watakaogundulika kuwa na Virusi vya Corona Tanzania

 
Hapa tulishakubaliana kuwa hatuna serikali. Hayo unayosema ni kama kumpigia mbuzi gitaa. Viongozi wetu wanataka watanzania tufe ila hawajapata njia muafaka ya kufanya hivyo ndiyo maana kila kukicha wanaamka na masharti mapya na ya hovyo karibu kila sekta

Sent using Jamii Forums mobile app

Serikali hii inatishia usalama wa nchi kwa kuruhusu watalii wa kichina kuingia nchini katika kipindi hiki hatari.

Wamewatekelekeza watoto wetu huko Wuhan lakini wanaruhusu wachina kutsfuta Ukimbizi wa Afya nchini kwa kisingizio cha utalii
 
Inamaana bado wanakuja,

Dah yani huu ni upuuzi sana,hata kama kuwaogopa basi viongozi wetu hawatufanyii haki kabisa.

Sent using Jamii Forums mobile app

Kwani serikali yetu inatuogopa au kutuheshimu sisi wananchi?

Serikali yetu inasikiliza tu pale ikiambiwa kitu na EU, China na Marekani, sisi inatuona kama sisimizi tusiokuwa na chochote mbele yake

Sasa ona wanavyohatarisha maisha ya wananchi kwa sababu ya kuogopa wachina
 
Kipindi ninatetea wale wanafunzi wa Kitanzania warudishwe nyumbani nilipokea matusi na kejeli!! Sasa ndo mpembue mliokuwa mnapinga. Wachina wanapata usafiri wa kuja huku ikiwa wao ndio wahanga wakubwa wa COVID-19 na mnawakataa watanzania wenzenu!

Ilipaswa uwekwe utaratibu wa kuwapokea hao wanafunzi lkn badala yake wanaingia wachina kwa wingi!! Huku ndo kuruka majivu na kukanyaga moto.. time will tell
 
Kipindi ninatetea wale wanafunzi wa kitanzania warudishwe nyumbani nilipokea matusi na kejeli!! Sasa ndo mpembue mliokuwa mnapinga.. wachina wanapata usafiri wa kuja huku ikiwa wao ndio wahanga wakubwa wa COVID-19 na mnawakataa watanzania wenzenu!.. ilipaswa uwekwe utaratibu wa kuwapokea hao wanafunzi lkn badala yake wanaingia wachina kwa wingi!! Huku ndo kuruka majivu na kukanyaga moto.. time will tell

Ni aibu kubwa sana kaka
Tunawapotezea watu wetu wenyewe
Tunaruhusu wachina waje wakati wa kipindi hiki corona
 
Ni aibu kubwa sana kaka
Tunawapotezea watu wetu wenyewe
Tunaruhusu wachina waje wakati wa kipindi hiki corona
Wapuuzi walikuwa wanafikiri kuna njia moja tu ya huo ugonjwa kuja hapa ati kwa kuwaleta hao wanafunzi!! .
Bora zimwi ulijualo unaweza ukaliepuka kuliko usilolojua!!

Tunafahamu kabisa wale wanafunzi wanaweza kuwa na maambukizi hivyo utaratibu wao wa kuwapokea unakuwa yakinifu wa hali ya juu na wanatengewa eneo maalum wakiwa chini ya uangalizi yakinifu wa madaktari kwa muda hata wa mwezi.. kinachotokea hivi sasa ni kupokea zimwi ambalo hatulijui.
 
Wapuuzi walikuwa wanafikiri kuna njia moja tu ya huo ugonjwa kuja hapa ati kwa kuwaleta hao wanafunzi!! .
Bora zimwi ulijualo unaweza ukaliepuka kuliko usilolojua!!

Tunafahamu kabisa wale wanafunzi wanaweza kuwa na maambukizi hivyo utaratibu wao wa kuwapokea unakuwa yakinifu wa hali ya juu na wanatengewa eneo maalum wakiwa chini ya uangalizi yakinifu wa madaktari kwa muda hata wa mwezi.. kinachotokea hivi sasa ni kupokea zimwi ambalo hatulijui.

Tatizo tuna watu wenye inferiority complex wamejaa kwenye sehemu za maamuzi.
 
Umenikumbusha jana mchana,niliingia sehemu kwenye restaurant moja katikati ya mji,nikakuta rundo la wachina kama nane hivi, kwakweli nilitamani nitoke mbio, ila sikujua hata ujasiri wa kuendelea kukaa pale niliutoa wapi,ingawa niliposhiba ndio nikawa najiuliza hivi kilichonifanya nisiondoke ni nini,tuombe mwenyezi Mungu atunusuru na hili janga.
 
Kibaya zaidi huenda hawa watalii wanatoka au wanafanya kazi katika miji iliyowekwa quarantine kama vile Wuhan, ambao walifanikiwa kutoka kabla ya quarantine kutangazwa, wengi waliondoka Wuhan kwa ajili kusherehekea mwaka mpya wa kichina na hao ndo wamesambaza maradhi katika majimbo mbalimbali ya china na hata nchi nyingine, Kutokana na wao kutoweza kurudi huko Wuhan baada ya siku kuu zao za kichina kuisha pengine ndiyo maana wanakuja huku Africa kungoja quarantine iondolewe. Lakini Je serikali yetu inaelewa inachokifanya katika kuhatarisha usalama wa nchi namna hii?
 
Back
Top Bottom