Serikali ya CCM mmeamua kutusaliti wananchi, Tunaenda kukumbwa na njaa kubwa hali ni mbaya

Serikali ya CCM mmeamua kutusaliti wananchi, Tunaenda kukumbwa na njaa kubwa hali ni mbaya

Serikali ya CCM chini ya Rais Samia Imeamua kwa makusudi kutuacha watanzania na kuangali maslai yao

Hali ni mbaya sana mtaani vyakula bei hazishikiki

Vyakula vinavushwa mipakani na kwenda nje ya nchi sisi hatupati

imefika hatua sasaivi mabwenyenye wananunua mzigo bado upo shambani wanavuna na kupeleka nje ya nchi, Kilimanjaro kuna njaa lakini mahindi yanapitia hapohapo kwenda kenya

Sasaivi unga wa sembe kilo moja 2000 hii haijawai kutokea kabisa

mchele 2400 kilo

Serikali ipo kimya tu wao wanahela za kula

CCM imeamua kutusaliti, sasaivi sokoni hatuoni mahindi yanatoka kwenye stock yanawekwa kwenye maroli yanavuka boda

tukisema hivi wanaona kama tunatania maana wao hali ya mtaani hawaijui

Sawa bwana
Acha uzushi Mzee,ikibidi njaa ikukumbe tuu la sivyo na wewe kalime..

Ukiona mtu anauza ujue anauza ziada..

Hiki ni kipindi cha wakulima kunufaika,ukitaka bei ya chini nenda shambani toka kucheza BAO huko mjini.
 
Hii serikali sidhani kama inajua implication ya hiki inachofanya kuruhusu chakula kusombwa na malori kwenda kenya. Au wanasubiri siku wananchi wakiandamana kwenda kwenye makazi ya rais kuomba msosi kama kule sri lanka ndo watajua hali imekuwa ngumu.
Alaa kwa hiyo chakula huwa kinasombwa tu, wewe hapo kiazi unajua implication yake?

Ni hivi ukitaka cha Bei rahisi nenda kalime.
 
Wapo baadhi ya wakulima wamejanjaruka na wanafanya kila wawezalo ili kupata faida na kilimo chao. Serikali ikianza kufunga mipaka itawaumiza hata hao wachache.
Waambie hao wapumbavu wakalime afu wakizalisha waiambie serikali ifunge mipaka..

Yalivyo mapumbavu yanashindwa kujua kwamba kilimo ni biashara kama biashara nyingine..

Mwaka ulioisha mchele umeleta pesa nyingi za kigeni kuliko zao lolote linaloitwa la biashara kama pamba,chai,kahawa na korosho.
 
unga kilo ni sh. 1300 acheni kupotosha.
mahindi huku namtumo songea bei chee kabisaa, Pia huku Galapo babati mahadi bei poa kabisaa.
Achana na wapumbavu tuu hao mkuu..

Mashineni Katavi mchele kilo ni 1700 tena supa na Michele imejaa..

Yanaropoka tuu bila hata Takwimu.
 
Wakati awamu ya nne, mkulima alipewa uhuru wa kuuza anapotaka. Ukawa mwanzo wa mkulima kupata faida. Kila mkulima akavutika kuongeza uzalishaji kwa kuongeza eka anazolima na kuongeza ubora kv mbolea, mbegu bora, kupanda kwa vipimo nk.

Faida katika kilimo ikawavutia waajiriwa kuingia ktk kilimo na baadaye wafanyabiara wakaingia. Hapo kilimo kikawa cha biashara na uzalishaji ukaongezeka maradufu.

Awamu ya tano ikaingia na mwelekeo kama wa mleta mada. Bei ya mazao ya chakula ikaporomoka. Wafanya biashara na waajiriwa wakajichomoa katika kilimo. Wakulima original wakapunguza eka na ubora wa kilimo mwaka hadi mwaka. Uzalishaji wa mazao ya chakula ukaporomoka sana.
Kwa mtu mwenye vision lazima atapenda model ya wamu ya nne. Mimi naipenda na mama anaipenda pia. Sababu inapaisha uzalishaji, mauzo nje ya nchi, mkulima na nchi inafaudika kwa uendelevu.
Kwa ambaye hana vision ataona karibu tu kama mtoa mada. Hilo lilitokea ktk awamu ya tano na kilimo cha mazao ya chakula kikakosa maana. Uzalishaji ukaporomoka vibaya. Mwendelezo huo ungetufikisha mahali nchi isijitosheleze kwa chakula na kuanza kuagiza toka nje.
Sera ya mama ya kilimo cha chakula ni BORA ashikilie hapohapo.
Masukuma gang na yule kichaa wao ndio waliharibu kilimo hapo katikati
 
VIONGOZI mmelala ngoja tuwape taarifa ambazo hata hamzijui enedeleeni kukaa kwenye viyoyozi lakini watu wakipata njaa kamwe hamtotawala vizuri jiongezeni mnaposhauriwa na watu waliopo ground
Njaa ipi hiyo? Kwamba chakula ni mchele na mahindi tuu au?

Kwamba watalima afu wauze chote waje kupata njaa au? Toa ujinga wako hapa Mzee.
 
Nani kakwambia mkulima ndiye anayenufaika na biashara hii ya chakula kupelekwa nnje ya nchi?!??
Njoo huku Kusini (Mtwara na Lindi) uone jinsi tunavyonunua ufuta kilo moja tsh 1100 - 2000 kutoka kwa mkulima na sisi tunauza tsh 3190 kwa kilo.
Mkulima ananufaikaje na bei hiyo ya 3190 kwa kilo!!??
Mnapenda kuongea vitu ambavyo hamvifahamu.
Wakulima wanaonufaika na bei kubwa ya mazao ni wakulima wakubwa tuu.
Wanufaika wakubwa wa kupanda kwa bei ya mazao ni watu wa kati (madalali) ma wafanyabiashara wa mazao.
Nikupe mfano mmoja,kuna kijiji ambacho wakazi wake walilima ufuta na kupata mavuno mazuri lakini changamoto yao ni kuwa umbali wa kutoka hapo kijijini mpaka kwenye mnada wa ufuta ni km 29.
Hakuna usafiri wa mabasi.
Mimi nimeenda huko nikawaambia nanunua ufuta kwa tsh 1200 kwa kilo,wamekubali kuliko kusubiri kwenda mnada ambao watauza kwa utaratibu wa stakabadhi ghalani itakayowachukua wiki kupata fedha yao.
Umeona mkulima anavyoteseka hapo sasa!!???
Mkuu hawa wanaojifanya wakulima humu JF ni madalali na wafanyabiashara wa mazao ambao serikali ikibana usafirishaji wa mazao biashara yao ya kulangua mazao kutoka kwa wakulima kwa bei chee na kuuza kenya itakuwa imetumbukia nyongo. Lakini ulichoeleza ndiyo uhalisia, mkulima hajawahi kufaidika na bei ya mazao kuwa juu zaidi ya madalali na walanguzi wa mazao wanaojiita wafanyabiashara ambao wamekuwa wakibana mizani na kujaza lumbesa kuzidi kumnyonya mkulima.
 
Tunakujua chawa wa kutetea utopolo, kwa hiyo huwezi kushangaza yoyote humu.
Upumbavu wenu wasimulieni wake zenu..

Ukitaka bei rahisi kalime,au Lima harafu waambie serikali wafunge mipaka..

Ila kwetu awamu ya 6,kilimo ni biashara kama hardware and the likes..

Awamu ya 6 sio wapumbavu kama awamu ya 5,tumeingiza bil.954 hatuwezi acha zipotee tunataka zilete tija kwa kilimo kuchangia 10% ya Pato la Taifa..

Ushenzi wenu mtafanya mkijapata madaraka na kuwaongoza wajinga
 
Upumbavu wenu wasimulieni wake zenu..

Ukitaka bei rahisi kalime,au Lima harafu waambie serikali wafunge mipaka..

Ila kwetu awamu ya 6,kilimo ni biashara kama hardware and the likes..

Awamu ya 6 sio wapumbavu kama awamu ya 5,tumeingiza bil.954 hatuwezi acha zipotee tunataka zilete tija kwa kilimo kuchangia 10% ya Pato la Taifa..

Ushenzi wenu mtafanya mkijapata madaraka na kuwaongoza wajinga
Unaongelea kilimo biashara kwenye nchi ambayo raia wake wengi ni mafukara wa kipato, wakiwemo na watumishi wanaolipwa mishahara kiduchu.....wewe jamaa huu uzwazwa sijui unautoa wapi.
 
Unaongelea kilimo biashara kwenye nchi ambayo raia wake wengi ni mafukara wa kipato, wakiwemo na watumishi wanaolipwa mishahara kiduchu.....wewe jamaa huu uzwazwa sijui unautoa wapi.
Ndio tunawatoa huko kwenye ufukara mlikokuwa mumewafukia sasa na njia rahisi ni kuwahakikishia soko.
 
Kumbuka kwamba kama wewe unavyofanya biasha upate faida, kilimo nacho ni biashara. Elewa kwamba sasa ni fursa ya mkulima kupata faida. Zingatia mkulima siyo punda wa taifa. Kama unaona vipi acha kupiga soga hapo mjini nenda kajilimie chakula chako.
Ona hii kenge...
 
Ndio tunawatoa huko kwenye ufukara mlikokuwa mumewafukia sasa na njia rahisi ni kuwahakikishia soko.
Aliyekwambia mkulima wa kawaida kule kijijini ananufaika na biashara ya mazao nani, mkulima amekuwa ni mtu wa kunyonywa na walanguzi na madalali kupitia lumbesa, kubana mizani na kupewa bei ndogo, jaribu kutumia akili kufikiri kwa kina.
 
Back
Top Bottom