Serikali yampa ajira Mwanamke anayekumbatia Watoto njiti hospitali ya Amana

Serikali yampa ajira Mwanamke anayekumbatia Watoto njiti hospitali ya Amana

So wanataka akasomee nini tena? kwanini asipewe course fupifupi za kuboresha anachokifanya? Sifa nyingi za kuajirika serikalini ni outdated. Huyo tayari ni skilled kwa hicho anachokifanya. Hivi waafrika alieturoga ni nani? Tunaamini zaidi kwenye vyeti(makaratasi) kuliko ujuzi halisi!!
Naunga mkono hii, kwenda chuo tena mambo mengi, bora waangalie anapataje mafunzo maalumu ili alisimamie hilo, sio tena kumpeleka chuoni.
 
Serikali kupitia Wizara ya Afya, imetoa ajira ya mkataba kwa Mariam Mwakabungu, mwanamke anayejitolea kukumbatia watoto niti waliotelekezwa katika Hosptali ya rufaa ya mkoa Amana jijini Dares Salaam.

Ajira hiyo imekuja siku moja tangu Rais Samia Suluhu Hassan kutuma salamu za pongezi zilizoambatana na fedha taslimu Sh milioni 2

Julai 16, gazeti la Mwananchi na mitandao yake ya kijamii ilichapisha habari hukuhusu Mariam Mwakabungu (25) ambaye ameokoa maisha ya watoto njiti watatu hospitalini hapo kwa kuwakumbatia kwa njia ya kangaruu baada ya kutelekezwa na mama zao.

Akizungumza na Mwananchi Digital leo Alhamis Julai 20, 2023 Waziri wa Afya Ummy Mwalimu ameeleza utaratibu utakaotumika katikia kumpa ajira Mariam.

"Tutampa ajira ya mkataba kwanza, changamoto iliyopo bado hana sita za kuajirika, tutamshauri ajiendeleze kielimu ili aweze kupata sifa za kuajirika Serikalini.

"Madaktari wanasema yule mama anajitoa na anapenda kufanya hiyo kazi ana moyo yaani ni kitu anapenda sasa kwa sababu hajasomea uuguzi itabidi aingize katika utaratibu huo ili aweze kupata sifa," amesema Waziri Ummy na kuongeza;

"Ana miaka 25 bado anamuda anaweza akaenda kusoma uguzi ngazi ya astashahada akawa muuguzi wa watoto njiti.

Tunaendelea kumpongeza a tutamshauri ajiendeleze kielimu ni jambo zuri na tumemuomba afanye hivyo, amesema.

Chanzo: Mwananchi

Pia soma
hivi yule majaliwa mkombozi wa wahanga wa ajali ya ndege ziwa victoria yuko wapi kwasasa
 
Mwaka 2016 October nilijifungua mtoto njiti kwa njia ya oparesheni akiwa na uzito wa kg 1.2 tu, mimba ilikua ya miezi 6 na wiki mbili.

Amekaa kwenye incubator kwa muda wa siku 32 uzito ukibaki vilevile kg 1.2 pamoja na kufuata njia zote za “kitaaluma na kisayansi “ wanazoelekeza wauguzi.

Siku ya 31 nilimfata daktari mkuu wa NICU na kumuomba nijaribu njia za “kienyeji na kiutamaduni “ alizowahi kutumia mama yangu miaka mingi nyuma, baada ya mjadala mrefu na viapo vya kutokuwajibika likinikuta jambo wakanihamishia chumba cha uangalizi kuona kama method zangu zitasaidia.

Method ya kwanza, kila muda tuliopangiwa wa kwenda kunyonyesha na kuwahudumia vichanga wetu, nilimkumbatia mtoto ngozi kwa ngozi huku nikimpa maziwa kupitia bomba la sindano maana hakuweza kunyonya ziwa mwenyewe by then, zoezi hilo lilikua linadumu kwa muda wa saa nzima na dakika 45 na dakika 15 nazitumia kumsafisha yeye, Mimi na mazingira yake kwanza.

Ndani ya siku 4, mtoto uzito uliongezeka kutoka kg 1.2 mpaka kg 1.8 just like that! Baada ya kutimiza siku saba mtoto akiwa na kg 2.08 niliomba nifanye method namba mbili, kuhamia nyumbani ambapo chumba cha kulala kiliandaliwa cha kwangu na mtoto tu.

Chumba tulikifunga pote, madirisha yalizibwa kwa plastic sheeting kuleta joto, mifuko special ya kutunza maji ya moto ilikua inawekwa kuzunguka kitanda muda wote, maji yalibalishwa kila asubuhi.

Mtoto alikaa kifuani kwangu ngozi kwa ngozi kila mara maana kazi yangu ilibaki kulea tu. Huko waliingia wale wenye nasaba na mtoto tena wakiwa wasafi bila harufu yoyote ya manukato ya aina yoyote. Muda wote nilikua naosha mwili wangu kabla ya mshika na maji ya moto bila sabuni. Hatukuruhusiwa maziwa ya kopo Kwahiyo alitegemea maziwa yangu tu tena kila baada ya nusu saa (literally 30 minutes).

Siku saba baada ya kuhamia nyumbani tukarejea hospital kupima uzito na kuangalia maendeleo, mtoto alikua na kg 3.1 mwenye nuru na afya njema sana na alianza kunyonya mwenyewe.

Check up nyingine ambayo ilikua ya mwisho tukafanya mwezi mmoja baadae ambapo alikua na kg 5.4 na macho yenye kuona kila kitu. Hii ilifanya mpaka yule Doctor mkuu wa NICU kuja nyumbani kuona haswa tunafanya nini na mtoto analishwa nini maana maziwa ya kopo walinikatalia kumpa wakisema yanaleta matokeo fake.

Baada ya uongozi wa pale NICU kuona hiyo method inafanya kazi wakaiendeleza kwa pale na kuwaelekeza pia namna ya kufanya nyumbani kwa wale wenye uwezo.

My baby girl is doing perfectly fine Alhamdulillah, class 4 sasa!

Hakuna kitu kitaizidi asili, asili inaumba, asili inatibu, asili inasahihisha, ila tu ukiipa nafasi.

KTY; Tanzania hii wapo wasomi wenye uelewa wa pande zote za shilingi na wanatambua kabisa kwamba haina pande mbili tu, tuheshimu Utu!
Sipingani na wewe,,,, nadhan hujanielewa nilichokua nakimaanisha....ni vizuri kama serikali imetambua mchango wake kwenye hilo...lakini pia inatakiwa waangalie namna ambavyo wanaweza wakaokoa maisha ya watoto wengine zaidi kupitia yeye,, kwa mfano wanaweza wakatangaza fursa kwa wamama wengine wengi zaidi wakapimwa afya zao ili kuepuka magonjwa ambukizi na kuwapa training fupi ya namna nzuri ya kutunza hao watoto njiti...kupitia hiyo tutaokoa maisha ya watoto wengi na kuwapa fursa pia wamama wenye mioyo ya kujitolea kama yeye....hope umenielewa vizuri sana😊🤗...na kingne wanasema changamoto ni vitanda vipo vichache na incubators zipo chache pia, wanaweza wakaanza na hivyo kwanza
 
Mwaka 2016 October nilijifungua mtoto njiti kwa njia ya oparesheni akiwa na uzito wa kg 1.2 tu, mimba ilikua ya miezi 6 na wiki mbili.

Amekaa kwenye incubator kwa muda wa siku 32 uzito ukibaki vilevile kg 1.2 pamoja na kufuata njia zote za “kitaaluma na kisayansi “ wanazoelekeza wauguzi.

Siku ya 31 nilimfata daktari mkuu wa NICU na kumuomba nijaribu njia za “kienyeji na kiutamaduni “ alizowahi kutumia mama yangu miaka mingi nyuma, baada ya mjadala mrefu na viapo vya kutokuwajibika likinikuta jambo wakanihamishia chumba cha uangalizi kuona kama method zangu zitasaidia.

Method ya kwanza, kila muda tuliopangiwa wa kwenda kunyonyesha na kuwahudumia vichanga wetu, nilimkumbatia mtoto ngozi kwa ngozi huku nikimpa maziwa kupitia bomba la sindano maana hakuweza kunyonya ziwa mwenyewe by then, zoezi hilo lilikua linadumu kwa muda wa saa nzima na dakika 45 na dakika 15 nazitumia kumsafisha yeye, Mimi na mazingira yake kwanza.

Ndani ya siku 4, mtoto uzito uliongezeka kutoka kg 1.2 mpaka kg 1.8 just like that! Baada ya kutimiza siku saba mtoto akiwa na kg 2.08 niliomba nifanye method namba mbili, kuhamia nyumbani ambapo chumba cha kulala kiliandaliwa cha kwangu na mtoto tu.

Chumba tulikifunga pote, madirisha yalizibwa kwa plastic sheeting kuleta joto, mifuko special ya kutunza maji ya moto ilikua inawekwa kuzunguka kitanda muda wote, maji yalibalishwa kila asubuhi.

Mtoto alikaa kifuani kwangu ngozi kwa ngozi kila mara maana kazi yangu ilibaki kulea tu. Huko waliingia wale wenye nasaba na mtoto tena wakiwa wasafi bila harufu yoyote ya manukato ya aina yoyote. Muda wote nilikua naosha mwili wangu kabla ya mshika na maji ya moto bila sabuni. Hatukuruhusiwa maziwa ya kopo Kwahiyo alitegemea maziwa yangu tu tena kila baada ya nusu saa (literally 30 minutes).

Siku saba baada ya kuhamia nyumbani tukarejea hospital kupima uzito na kuangalia maendeleo, mtoto alikua na kg 3.1 mwenye nuru na afya njema sana na alianza kunyonya mwenyewe.

Check up nyingine ambayo ilikua ya mwisho tukafanya mwezi mmoja baadae ambapo alikua na kg 5.4 na macho yenye kuona kila kitu. Hii ilifanya mpaka yule Doctor mkuu wa NICU kuja nyumbani kuona haswa tunafanya nini na mtoto analishwa nini maana maziwa ya kopo walinikatalia kumpa wakisema yanaleta matokeo fake.

Baada ya uongozi wa pale NICU kuona hiyo method inafanya kazi wakaiendeleza kwa pale na kuwaelekeza pia namna ya kufanya nyumbani kwa wale wenye uwezo.

My baby girl is doing perfectly fine Alhamdulillah, class 4 sasa!

Hakuna kitu kitaizidi asili, asili inaumba, asili inatibu, asili inasahihisha, ila tu ukiipa nafasi.

KTY; Tanzania hii wapo wasomi wenye uelewa wa pande zote za shilingi na wanatambua kabisa kwamba haina pande mbili tu, tuheshimu Utu!
NI kweli kabisa huko sahihi na hiyo njia imetumika tangu miaka ya 80 huko na mpk sasa nina ushahidi ya watoto wawili niliwaona kwa macho yangu wawili wengine aliwazaa wote njiti lkn kipindi hicho milokuwa mdogo sina akili
Nikisema tangu miaka ya 80
7bu huyo mama mtoto wa kwanza alimzaa 85 njiti wa pili 88 njiti watatu 95 njiti wanne 99 njiti na watatu 2007 njiti
Sasa huyo wa 99 na 2007 niliwashihudia 7bu akili timamu nilikuwa nazo sasa

Hvyo dadaangu humu wengi hawana akili hawajui nino wanachangia hvyo kwa swala alokuwa analifanya huyo DADA ni zaidi ya USHUJAA 7bu niliwaambia hao wanaopinga kwanza hawaju mtoto NJITI yupoje kimuonekano na kiumbo kama wangejua nina uhakika wasingeongea ujinga wao huo

Jambo la ziada kwa sasa kwa SEKTA YA UZAZI serikali imepiga hatua sana katika lengo la kupunguza VIFO VYA WATOTO WACHANGA kwa kiasi fulani wameviepusha kwa 80%
Hatua hii imeongezeka zaidi baada ya KUJENGA WODI mpya hizi za kisasa kwa HOSPTARI ZA AMANA TEMEKE NA MWANANYAMALA sijajua hali ya MIKKOANI ipoje ila kwa DSM wamejitahidi sana
 
Hizo nguvu si wangewekeza kwenye kununua incubators za kutosha.

Wabongo wapo busy kutetea Dp kisa inatumia mashine lakini wapo busy tena kumpongeza Rais kwa kutoa pesa za kukumbatia watoto badala ya kushauri zinunuliwe mashine za kutosha
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Itakuwa wanataka watanzania tujazane hospital tukakumbatie watoto.

Nchi ngumu hii[emoji1787]
Ili mradi tu wawatoe watu kwenye reli.
 
Naunga mkono hii, kwenda chuo tena mambo mengi, bora waangalie anapataje mafunzo maalumu ili alisimamie hilo, sio tena kumpeleka chuoni.
Nchi inaendeshwa kwa mujibu wa sheria. Waziri akijiamulia baadae likatokea tatizo ataingia matatizoni. Kama binti ana miaka 25 asisite kwenda shule ili apate ajira kirahisi kwa sababu pia inaonekana hana ajira ndo maana kaweza kufanya hilo zoezi.
 
Safi. Tunapongeza panapostahili na kukosoa panapostahili.
Incubators ni vile tunaishi dunia ya usasa na changamoto nyingi ndani yake, lakini joto la mama ni zuri. Naamini wamechukua hatua stahiki upande wa afya ya mwanadada anayefanya zoezi hilo maana ndiyo la muhimu kwa afya ya watoto wasipate maambukizi yoyote yale kutoka kwake.
 
Kutumia mtu badala ya incubators
Halafu litakuja kutokea janga, wote watamruka watadai utaratibu haukufuatwa, kama yule muosha vifaa. Yaani ccm ni balaa kwa Tz!
 
Ni wachache sana watakuelewa!
Kwa kifupi mtoto njiti hajakomaa hii ni pamoja na kinga pia.
Sitaki kwenda mbali kuhusu tahadhari za kuzuia magonjwa kutoka kwa huyu mama kwenda kwa hao njiti kama zinafuatwa.
Anyway twende tu..
Kwamba amana hawajui Hilo Ila wewe mkulima wa pilipili
 
Back
Top Bottom