Serikali yapiga marufuku matumizi ya vitabu 16 vikiwemo Wimpy Kid ili kulinda mila, desturi na tamaduni za Kitanzania

Mila, desturi na tamaduni za Tanzania sio sheria.

Marufuku ya Waziri pia sio sheria.

Nchi inapaswa kuongozwa na utawala wa sheria.

Tunataka sheria.
Angukia katiba mpya moja kwa moja ndiyo utaeleweka kiurahisi.
 
Mungu atusaidie hiki kizazi. Haswa sisi wenye watoto wa kiume🙌🏼 kila akirudi unamuuliza maswali tena kiupole ili asikufiche kitu. Malezi sasa yamebadilika sana inabidi mzazi uwe friendly mno
 
Kwa upande wa wazazi wa bongo ambao watoto wao wanagegedana vichochoroni majumbani mwao sidhani kama watahangaika na hili.
 
Hizo ndizo fake version nilizosema.

Watu wamelinganisha na vitabu halisi wakakuta hakuna vitu kama hivyo.

Kwa hiyo tumepiga marufuku vitabu kwa kuangalia fake news za Whatsapp?
Sorry mkuu. Hebu tuwekee ukurasa halisi
 
Hao watoto vitu wanavyojua hawajavisoma popote ila wanajua.

Tuulizeni na sisi wa vi tuition tuwaambie watoto wanayoyaongea
Wewe kama mzazi umechukua hatua gani kuwasaidia hao watoto? Au ulipo sikia umesikia unasubiria uje uulizwe halafu itasaidia nini?

Kumbe tunafanana na viongozi wetu,..... Vitabu viliruhusiwaje kuingia na kutumika bila kuangalia maudhui? Na alie ruhusu ni nani na anachukuliwa hatua gani kwa uharibifu aloufanya?
 
Hivyo vitabu vimeshawaharibu watoto wangapi
 
Prof. Mkenda anaweza kujitahidi sana kwa nafasi yake ila Taifa kama Taifa ikaruhusu huu Ushetani kwa kupitia Masharti ya Misaada

Ninakumbuka vizuri ile barua ya serikali kukanusha kupinga haya mambo baada ya Makonda kupinga tena serikali ilisema ule ulikuwa ni msimamo wa Makonda tu na sio wa serikali...UNAFIKI HUU

Serikali hasaa ndio ilipaswa ianze kupinga huu Ushetani na wote watakaoonesha kuasisi au kusupport wachukuliwe hatua kali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…