Serikali yatoa ufafanuzi wa akiba ya Fedha za Kigeni, makosa yalifanyika

Nyongeza tu...hii haikupaswa kuwa ufafanuzi bali ni masahihisho. Hapo bado hawajakubali kama wamekosea. Inafafanuwa pale ambapo jambo ulilolisema halijaeleweka na unasahihisha pale uliposema jambo ukakosea.
Ilishasemwa Rais hakosei, wanatembelea humo.
 
Exactly!! Badala yake wanasema eti UFAFANUZI [emoji13][emoji13]ilitakiwa iwe KUOMBA RADHI kwa taarifa isiyokuwa sahihi.
Kuna yule jamaa yenu jana, nadhani Mr BonT alisema, wakati akidhani anarekebisha kosa fulani hapa JF, kwamba ^hajakosea^ bali ^ame-overlook!^
 
Ivi si alikuwa anasoma kilicho andikwa au alikuwa anatoa kichwani?
Then if that is the case aliyendaa iyo speech nae kamuingiza chaka
Swali fikichi, fikishi, na fikirishi: ^Amekoseshwa mangapi?^
 
Nashauri apandishwe cheo cha juu ^car-bee-sir^ kwa vile ametuonesha jengo letu msingi wake ukoje!
 
Sasa mkuu Pasco kwani Rais huwa hapitiii hotuba yake several times kabla ya kuisoma kwa umma? Niliwahi kuona clip ya Barack Obama akifanya rehearsal ya hotuba yake kwa taifa na wasaidizi wake na niliona wakiondoa hiki na kuongeza hiki...
Na huwa wanakariri pia! So much dedication! So much love for one's country!
 
Walifanya makusudi kwa sababu wanajua Hangaya hotuba zake zinasikilizwa zaidi na wananchi wa vijijini hawana uwezo wa kungamua kuongopewa!
 

Pia miye nina wasiwasi maana hali ya akiba 2020 ilikuwa USD 4.8 bn chini ya John Pombe Magufuli, sasa hii nyongeza ya karibia dola USD 2bn inahitaji ufafanuzi kwa mwaka 2021 :

“Akiba ya fedha za kigeni imebaki katika viwango vya kuridhisha na kufikia USD Bil 4.8 mwishoni mwa December, 2020, hii inatosha kulipia uagizaji bidhaa

Source : https://www.bot.go.tz/PressRelease?lang=sw

Toka maktaba kabla ya gonjwa la covid-19 kuyumbisha uchumi, malipo kwa miradi mikubwa ya Stiegler's Gorge Rufiji kwa Egypt , SGR reli wa Turkey tena kwa USD hela za kigeni na wala hatujataja vita kubwa ya kiuchumi ya mabeberu hali ilisomeka hivi :


Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2019/20 akiba ya fedha
za kigeni imeendelea kuwa ya kuridhisha na kukidhi mahitaji ya
kuagiza bidhaa na huduma nje ya nchi. Hadi Aprili 2020, akiba ya
fedha za kigeni ilifikia dola za Marekani bilioni 5.3. Kiasi hiki
kinatosheleza mahitaji ya fedha za kigeni za kuagiza bidhaa na
huduma nje ya nchi kwa kipindi cha miezi 6.1 ikilinganishwa na dola
za Marekani bilioni 4.4 kilichotosheleza mahitaji ya fedha za kigeni
za kuagiza bidhaa na huduma kwa kipindi cha miezi 4.3 kwa kipindi
kama hicho mwaka 2015. Ongezeko hili lilitokana na kuongezeka
kwa uwekezaji wa kigeni na mauzo ya bidhaa na huduma nje ya
nchi. Aidha, kiwango cha akiba ya fedha za kigeni kilichofikiwa ni
zaidi ya lengo la kuwa na akiba ya kutosha kuagiza bidhaa na
huduma nje ya nchi kwa muda wa miezi 4.0 na pia ni juu ya lengo
la miezi 4.5 lililowekwa na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika
Mashariki na lengo la miezi isiyopungua 6.0 kwa nchi za Jumuiya ya
Maendeleo Kusini mwa Afrika - SADC.
 
Mkuu hebu tulia kwanza😂😂

Kweli wakibanwa zaidi watashuka
 
Samia ni binadamu kama sisi. Hayo ni makosa madogo madogo nani kwa mtu yoyote mwenye akili timamu anaweza kuelewa alikuwa anamaanisha nini!
Sasa siye ndo tuwe na kazi ya kuelewa anachotaka kusema? Kwanini asieleweke tangu mwanzo? Hiyo kazi yake haimpi luxury kufanya makosa ya namna hiyo, kwanini tunalazimishana kuamini ujinga

Hapa miaka ya nyuma kulikuwa na vitabu vya shule ya Msingi vilionekana kuwa na makosa ya wazi kabisa, watu walipoongea zilikuja hoja kama hizi eti hayo ni makosa ya kibinadamu tuvumiliane, ujinga tu!
 
Mkuu igogondwa , sio tuu rais anapitia, bali kuna watu maalum, paid by taxpayers money for doing that. Hizo ni figures and data hivyo uki feed wrong data , rais Samia sio mtu wa data na calculus kama JPM, what you feed in is what comes out.
P
Paschal No.

Wewe tuseme ni mtu wa kuchezea milion, siku nikichukua bank statement nikasoma Paschal acount yako ina billion 10 hutasituka? Nakwambia hata bibi yangu ambaye hakusoma ukisema hela ambayo hai make sense hua anagoma.
 
Hangaya mchumi kiwango cha nungwi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…