Shairi: Aikael Mbowe, Freeman Mwamba wa Tanzania


mi-CCM kwa nini kufukuzwa hawa imewauma hivi?

Mpaka mnatia huruma!
 
Kila mwananchi aliyefurahishwa na kamati kuu, hebu tupia japo ubeti mmoja hapa kuonyesha furaha yako!

Malenga wa malenga nami naongezea huu, kwani malaya wa kisiasa hawana nafasi CHADEMA:

CHADEMA ina wenyewe, siyo hawa domo kaya,
Ni Supika au jiwe, yamekuwa yenu haya?
Ni haki yetu wenyewe, kuwafurusha malaya!
Hongereni sana Mbowe, wewe ni mtu makini!

Cc: Team 666
 

Hahaaahaa ha haa. Uliowataja mmoja ana influence TSIS tangu akiwa uvcmc. Yeye ni kipandikizi. Arudi tu nyumbani.

Walirudi mamvi na kina zirro sembuse huyu?
 

Cc: Team 666
 
CCM wanatumia pesa za walipa kodi kuwanunua covid 19 wanandungai kwa gharama kubwa badala ya maendeleo ni matumizi mabaya ya pesa za walipa kodi
Nanyi chadema mmezidi umalaya toka muanze kujiuza hamjapata mtaji tuu mfanye mambo yenu?
Mlianza wabunge, mkajiuza
Wakaja madiwani, mkajiuza wee Hadi kichefuchefu
Sasa mmekuja jiuza covid 19!
Mtakwisha na ukimwi endeleeni kujiuza tuu.
 
Huyo si mwamba ni kamba,ukweli wajulikana
Yote hayo anaimba,mwisho atapatikana
Samahani ataomba,mkweli kujulikana
Ni mwamba aliyeshindwa,majeruhi toka Hai.

Sina budi kukujibu, we Lumumba buku saba,
Kubumba bumba sababu, hasa zile za mahaba,
Mazezeta mambumbumbu, ni fursa haswa Lumumba!
Sifia Mzee Baba, ukavune buku Saba.



Cc: Team 666
 
HONGERA NA PONGEZI[emoji120][emoji120]
 
Sina budi kukujibu, we Lumumba buku saba,
Kubumba bumba sababu, hasa zile za mahaba,
Mazezeta mambumbumbu, ni fursa haswa Lumumba!
Sifia Mzee Baba, ukavune buku Saba.



Cc: Team 666
Wala hapo huna jibu,ni lugha zilizopinda
Siasa za kujaribu,mwisho wake zinadunda,
Buku saba si sababu,Zezeta amekushinda
Duri na dawiri zari,tuipambe CCM
 
Mademu bomba wapo wengi. Hatutaki wadangaji
 
Picha ndiyo kwanza limeanza ujiandae na kuandika shairi lingine .Manake mapigo Yajayo ya upande wa pili Ni hatari ya kufa mtu usimuone Kobe kainama ujue anatunga Sheria. Watu watajuta na kulaumiana kwa yote waliyoamua.Mgawanyiko utanzia kamati kuu yao,Bawacha,Bavicha mpaka ngazi ya chini Mkoa kwa Mkoa,wilaya kwa wilaya,kata kwa kata,mtaa kwa mtaa,Kijiji kwa Kijiji,kitongoji kwa kitongoji.
 
Wala hapo huna jibu,ni lugha zilizopinda
Siasa za kujaribu,mwisho wake zinadunda,
Buku saba si sababu,Zezeta amekushinda
Duri na dawiri zari,tuipambe CCM

Kulikoni buku saba, ubeti umetungiwa?
Ulolipwa kwenye saba, itabaki ukigawa?
Wekeza japo akiba, ona nusu imeliwa!
Kama nusu imekwenda, subiri kuliwa wewe!

Uliambiwa ni ligi, au watoka Namungo?
Ati zezeta ni Kingi, wa pimbi kwenye mapango?
Pambeni mpake rangi, utajitenga urongo!
Kama nusu imekwenda, subiri kuliwa wewe!

Cc: Team 666
 
Mkuu Team 666 nadhani nimejitolea ya kutosha kuku tag kama ulivyoomba.

Wa huku kujitolea ni wajibu. Huku wa kubebwa kwenye malori au kulazimishwa kuhudhuria hawapo.
 
Brazaj huna hoja,kazi yenu kulalama
Siri kwetu ni umoja,huko kwenu uhasama
Hata mje kwa pamoja,Lumumba itawazima
Duri na dawiri zari,tuipambe CCM.
 
Brazaj huna hoja,kazi yenu kulalama
Siri kwetu ni umoja,huko kwenu uhasama
Hata mje kwa pamoja,Lumumba itawazima
Duri na dawiri zari,tuipambe CCM.

Hoja si kubumba bumba, bali ni kudadavua,
Kusifia kama Luba, lije jua au mvua?
Huo waitwa uzoba, nani asiye ujua?
Nusu tena imekwenda, subiri sasa kuliwa!
 
Brazaj umechoka,ujualo ni kubumba
Vina vimekukauka,na sera zenu sambamba
Malenga watakucheka,na kukuona mshamba
Duri na dawiri zari,tuipambe CCM
 
Ulisikia wapi?hakuna mkubwa zaidi ya Chadema ref Lowassa,Slaa.Kabwe nk nk
 
Brazaj umechoka,ujualo ni kubumba
Vina vimekukauka,na sera zenu sambamba
Malenga watakucheka,na kukuona mshamba
Duri na dawiri zari,tuipambe CCM

Nusu mbili zimekwisha, rasmi sasa u punga,
Vina unasahihisha, kwa 'scheme' ya kuvunga?
Kama ndiko kujishasha, ni sawia na kudanga!
Buku saba yote kwisha, sasa washindwe wenyewe!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…