Sheikh Mwaipopo: Muislam atakayehudhuria mkutano wa CHADEMA litakalomkuta ni juu yake

Sheikh Mwaipopo: Muislam atakayehudhuria mkutano wa CHADEMA litakalomkuta ni juu yake

PUMBAVU ZENU! Mimi ni muislamu na sikibali huu upuuzi wa mkataba wa kinyonyaji. Bandali akabidhiwe muwekezaji yoyote kwa mkataba ambao upo 50/50

Mwaipopo anakosea sana kufikiria wanaopinga huu mkataba wa ovyo ni Wakristo tu. Hili ni jambo la kitaifa toeni udini. TUNACHOTAK SERIKALI WALEKEBISHE BAADHI YA VIFUNGU KTK MKATABA KWANI HAVIKO SAWA
Kwenye Madini ni % ngapi kwa ngapi?
 
Mimi kama mkatoliki nimeshangazwa na idadi ya maaskofu kwenye huo mkutano wa kesho. Hili suala la bandari lina sura ya kidini?
Sasa kama mkataba unatetewa na Mashekhe tu ulitegemea, Maaskofu wasiupinge.

Tulikosea sana tulipoanza kuwasajili machifu, viongozi wa dini kuwapa sauti ya hoja za kisiasa.

Na kuanza kuwapa majukwaa watoe maoni yao ya kisiasa wazi wazi.

By the way utawala usio na ushawishi kwa wananchi huwatumia viongozi wa dini kama kivuli cha kufunika madhaifu yake.
 
Waislam tokeni chadema haraka iwezekanavyo.

Muislam anaebaki chadema huyo ni Muislam jina tu, siyo Muislam wa kweli.

Watu wanaupiga vita Uislam waziwazi bado mnawakumbatia tu?
Kwahio twende CCM? Muislam wa kweli Ni yule mwenye kuweza kutambua zuri na baya hivyo tutachambua wenyewe chuya na wali Ni upi.
 
Hahahah, kumbe kuna watu ni wendawazimu ila hawajijui kabisa! Kwa hiyo uislam ndio iwe ticket ya kuiuza Tanganyika na watu wake? Bila kujali dini, tumeuzwa wote, na hivyo wote tutahudhuris kwenye mkutano......

Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
 
Shekhe Mwaipopo kalewa pombe kali na mambo haramu yote anatumia. Uislamu anazugia tu kuwalaghai wajinga.

Pia mshirikina. Angekuwepo enzi uislamu upo moyoni kwa watu, angeumbuliwa kweupe na huo ushirikina wake na shirki zote anazofanya akiwa gizani.

Aisubiri siku ya upanga na maangamizi. Waislamu hatujafundishwa kukubali kuuzwa na madalali hata kama wamevaa shungi, vilemba na kanzu.

Ewe mtanzania amka sasa. Nchi inauzwa ukiwa unaona. Madalali wapo kazini kukuchuuza kama mbuzi wa vingunguti.
 
Mwaipopo ni tapeli, hana ushekhe wowote. Wanaofahamu historia yake hawawezi kupoteza muda kumsikiliza.

Huyu bwana alikuwa mkristo. Wakati wa utawala wa Mwinyi kulikuwa na vuguvugu la kuiingiza Tanzania kwenye uislam wa siasa kali. Akaona hiyo ni fursa kwake ya kuchota pesa ya waarabu. Akaslim, Waarabu wenye misimamo mikali wakamchukua bwana Mwaipopo na kumpeleka Uarabuni. Aliporudi, yeye na shekhe Kassim (marehemu), ndio wakawa nguzo ya mahubiri ya msimamo mkali ba chuki dhidi ya ukristo. Wakatengeneza vikundi vya kuvunja bucha za nyama za nguruwe.

Na kwa Zanzibar, maduka ya pombe yakawa yanachomwa moto. Nchi ikaingizwa kwenye jumuia ya uchumi wa nchi za kiislam, ambao sharti mojawapo ilikuwa kuhakikisha utawala wa juu wa nchi mwanachama unashikiliwa na Muislam.

Yote yalifanyika kwa siri kubwa. Ilipokuja kufahamika, kelele zikawa nyingi dhidi ya utawala wa Mwinyi. Mwalimu Nyerere naye akaja juu dhidi ya Mwinyi, ndipo Mwjnyi kwa shingo upande akaitoa nchi kutoka jumuia hiyo ya OIC, na kisha kukemea na kutangaza kuwa mtu akitaka kula nguruwe au nyoka au kunywa pombe, ni ruksa. Ndiyo akapewa jina la Ruksa. Akaacha kila kitu, kiwe kibaya au kizyri kiendekee. Ufisadi ukamea kwa kiwango cha ajabu, uchumi ukaparanganyika, mfumko wa bei ukawa wa juu kuliko nchi yoyote Duniani ukifikia 30%, tukazuiwa kupata mkopo wala msaada wowote toka taasisi zote za fedha Duniani.

Hata sasa, haitashangaza kama Mwaipopo atakuwa tayari amekwishachota pesa ya DP. Huyu bwana yupo tayari kufanya lolote alimradi ahakikishiwe pesa nzuri ya kutosha.

Waislam wanafahamika, na mashekhe wa kweli wanaosimama katika misimamo ya imani yao wanafahamika sana. Jana tulikuwa kwenye tukio moja la ibada ya kikristo lililohudhuriwa na shekhe wa mkoa, aliyltoa nasaha nzuri sana, na alishangiliwa na kupigiwa makofi kuliko kiongozi yeyote aliyrpata nafasi ya kutoa salamu.

Watu wasijifiche nyuma ya dini kutimiza malengo yao machafu.

Bandari ni zetu sote wa dini zote, tunadhulumika sote. Hata wakati wa dhiki, hakuna muislam ambaye huwa anasaidiwa na waarabu eti kwa sababu ni muislam.
Daaah we jamaa najuaga msomi na mchambuzi kwa maandiko yako marefu marefu, kumbe madini tena mfia dini hasa na kwasababu hiyo unaunga mkono CHADEMA kwasababu ya hilo maana huu uwongo ulioandika hapo ni balaa hebu kasome hata kitabu tu cha Mwinyi uone kaelezea vipi swala la OIC, halafu OIC na mabucha ya Nguruwe na pombe wapi na wapi? Uganda ni mwanachama wa OIC kunani kule?
 
Hahahah, kumbe kuna watu ni wendawazimu ila hawajijui kabisa! Kwa hiyo uislam ndio iwe ticket ya kuiuza Tanganyika na watu wake? Bila kujali dini, tumeuzwa wote, na hivyo wote tutahudhuris kwenye mkutano......

Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
Hoja kuntu kabisa hizi. FaizaFoxy njoo uzijibu.
 
Kwamba yeye ndie Mungu, yeye ni nani apangie wengine namna ya kuishi... Kwamba yeye ni vyema kumsikiliza lakini kumsikiliza Mbowe ni dhambi, huyo Mwaipopo ndie mjinga zaidi, mwambie majini yake mwisho ni kwa wale anaowamudu tu wengine tumeaga nyumbani, akae na unafiki wake huko.
Dunia ya sasa watu hawatishani kwa mambo kama haya. Dunia isingetengeneza silaha na osama asingetumia mabomu
 
Kweli dini ukiwa na mahaba nayo akili inalala!

Hivi kweli humu Jamiiforums tunae member aliyeweza ku-post ujinga kama huu?na pia inawezekana alienda kumsikiliza,hiyo dini inaharibiwa na watu kama hawa wanaofundisha watu kwamba lazima kila kitu kiende pamoja kwenye box la dini hata kwa mambo yanayoonekana wazi yanawaumiza kwenye maisha halisi wanayoishi.
 
Misimamo hivi ushafika hayo maeneo kweli?
Unaongeleaje sehemu usiyo wahi kanyaga?

Wana misimamo zaidi/ sawa na watu wa Pwani.

Usikalili
ukiwa na msimamo na huna hela na nguvu yako ya kiuchumi ndogo ni sawa na bure hamna chochote kujidanganya labda muwape nchi hao waarabu
 
Back
Top Bottom