SI KWELI Shemasi ‘George Rugambwa’ awauliza maswali sita Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC)

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Kuna ujumbe unasambazwa WhatsApp, una kichwa kinachosema Maswali Sita kwa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) je, ni wa kweli?
Kufuatia TEC kukanusha kuwepo kwa Shemasi yeyote katika Seminari ya Ntungamo, JamiiForums Imejiridhisha kuwa ujumbe wenye kichwa Maswali Sita kwa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) unaodaiwa kuandikwa na Shemasi George Rugambwa wa Seminari ya Ntungamo kuwa ni wa kuzushwa na hauna ukweli wowote.[emoji419][emoji375]

NB: kwa ithibati hiyo huo ujumbe ni non n void ufutwe haraka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maswali Sita kwa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC)

Na Shemasi George Rugambwa
Seminari ya Ntungamo, Bukoba

Leo TEC imetoa tamko lake kuhusu mkataba wa kuendeleza Bandari ya Dar es Salaam kati ya Tanzania na Dubai. Tamko
Huyo aliyeuliza hayo maswali na kudanganya utambulisho wake nimemdharau sana. Kiufupi namchukulia kama 🚮 tu.

Alishindwa nini kujitambulisha kama kweli ana akili timamu? Au ndiyo kusema anatuogopa Wakatoliki kiasi hicho, mpaka aje na utambulisho wake wa uongo?
 
Wanakitengo wa chama tawala mode of writing ni hiyo hiyo kwenye mada zao nyingi ndefundefu wanapokuwa viongozi wao wametoa boko

Sent using Jamii Forums mobile app
 
MKATABA WA BANDARI

Tamko la Kanisa lapingwa kila kona

Kutoka Ukurasa wa Sheikh Ibrahim Ghulaam

Muda mchache tu baada ya viongozi wa Kanisa Katoliki kutoa tamko kupinga mkataba huo, tayari watu wa kada na Imani tofauti wamekosoa na kulipinga tamko lao hilo na kuitaka Serikali iendelee na kuboresha mkataba huo kwa maslahi mapana ya Taifa na kamwe isishughulishwe na watu waliozoea kuitumia bandari kwa maslahi yao binafsi

Miongoni mwa wakosoaji wa tamko hilo la Kanisa Katoliki ni Shemasi George Rugambwa wa Bukoba ambae ameandika:

Maswali Sita kwa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC)

Na Shemasi George Rugambwa
Seminari ya Ntungamo, Bukoba

Leo TEC imetoa tamko lake kuhusu mkataba wa kuendeleza Bandari ya Dar es Salaam kati ya Tanzania na Dubai. Tamko lake limeelezewa kwa ufupi kupitia Katibu wake Padri Charles Kitima na baadaye likasambazwa kama nyaraka kwa wanahabari.

Kiufupi TEC wanasema maaskofu wakatoliki wanapinga mkataba huo wa Tanzania na Dubai na wanataka sauti ya wengi isikilizwe wakiwa na maana asilimia kubwa ya Watanzania wanaungana na kauli hiyo ya TEC.

Baado naamini ufafanuzi wa Padri Kitima unaweza kuwa na maneno yake binafsi ya ziada kwani alijipambanua awali kuwa na maslahi na jambo hili. Nitaandika zaidi ziku zijazo lakini maswali yangu kwa TEC kwa sasa ni haya ..

1. TEC inafahamu kwamba mwaka 1992 wakati Serikali inapitisha mfumo wa vyama vingi ulikuwa umekataliwa na asilimia 77 ya Watanzania? Hata hivyo serikali ikaamua uruhusiwe. Hakuna kumbukumbu za kanisa katoliki kupinga na kusema Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu.

2. TEC inafahamu kwamba mwaka 2001 baada ya matokeo ya Uchaguzi wa Zanzibar na mauaji ya wafuasi wa CUF mwezi Januari, asilimia kubwa ya Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla walitaka kuwepo na mfumo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar na SMZ na SMT chini ya Mkapa haikutaka? Hakuna kumbukumbu za kanisa katoliki kupinga na kusema Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu.

3. TEC inafahamu kwamba mwaka 2014 maaskofu wote Katoliki Tanzania akiwemo Kardinali Pengo na wasaidizi wake walipokea mamilioni ya shilingi pesa taslimu na nyingine kwenye akaunti zao kama Askofu Nzigilwa (milioni 80 benki) na Kilaini (milioni 40 benki). Inajua fedha hizo zilitoka katika kampuni yenye makando kando ya rushwa ya kihistoria Tanzania. Wananchi wengi walipiga kelele lakini fedha hizo hazikurudi wala hakuna kumbukumbu za kanisa katoliki kupinga na kusema Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu.

4. Padri Kitima anasema kwa zaidi ya miaka 60 ama toka tupate uhuru bandari yetu haijawahi kuendeshwa na wageni. Hii ni kauli yake au ya maaskofu wa TEC? Ni kweli TEC haifahamu kwamba kwa zaidi ya miaka 22 Bandari yetu ya Dar imekuwa chini ya kampuni ya TICTS ikiendeshwa kwa ubia na kampuni toka Hong Kong (Hutchsons?). Kama wanafahamu, wanakumbuka wabia wazawa wa kampuni hiyo wanahusika kwenye kuwapa hela maaskofu kama Rugemalira na IPTL yake walivyofanya? Hili wamewahi kuwaambia waumini wao katika mimbari za ibada?

5. TEC wanafahamu kwamba mwaka 1998 kwenye mauaji pale Mwembechai walikufa wasio na hatia na ilikuwa rai ya mamilioni ya Watanzania kutaka kuwepo na suluhu ya kisiasa? Hakuna kumbukumbu za kanisa katoliki kupinga na kusema Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu.

6. Padri Kitima anasema wananchi wamelikataa Bunge? Ametumia kipimo gani cha Kikatiba? Maana wananchi wanalikataa Bunge kwa kutowachagua Wabunge kwenye Uchaguzi. Hii “Vox Populi Vox Dei” ya TEC imetumia kigezo gani? Wananchi wakikataa Bunge pia si wameikataa Serikali? TEC inaomba vipi busara ya Mheshimiwa Rais ambaye wakati huo huo inasema serikali yake imekataliwa? Kuna kuchanganyikiwa na haraka kubwa kwenye tamko la TEC hata namna lilivyochapwa na kupangiliwa. Inanipa mashaka kwamba chombo hiki muhimu cha Kanisa kimekubali kutumika kwa maslahi binafsi bila tafakari ya kutosha.

Je hii “Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu” ni wengi wapi hasa? Na mungu anayetajwa hapa ni nani? Usikute mungu anayetajwa na kusemwa asikilizwe ni mungu au miungu watu waliokuwa wanaingiza miamala kwenye akaunti za baadhi ya maaskofu wetu na viongozi wengine wa dini miaka nenda rudi. Tujihadhari. Tusiigawa nchi kupitia madhabahu.

Mathayo 23:13

Ole wenu Mafarisayo wanafiki...
 

View: https://youtu.be/JXLHNt0loPU
TEC wametoa tamko rasmi la kupinga mkataba wa kubinafsisha Bandari kwa serikali ya Dubai. Tamko hili lilifafanuliwa kwa ufupi na Katibu wake Padri Charles Kitima, akieleza kuwa TEC wanataka sauti kinzani ya watu wengi wenye akili timamu isikilizwe.

Mtu aliyejitambulisha kama Shemasi George Rugambwa, kutoka Seminari ya Ntungamo ya Bukoba, amejitokeza na kuuliza maswali saba. Kimsingi anawalaumu TEC kwa kurejea ujumbe wa Kibiblia katika Mathayo 23:13, usemao kuwa; "Ole wenu Mafarisayo wanafiki."

Tumeamua kuyajibu maswali ya "Shemasi George Rugambwa" kama ifuatavyo;

1. Shemasi ameluliza: TEC inafahamu kwamba mwaka 1992 wakati Serikali inapitisha mfumo wa vyama vingi ulikuwa umekataliwa na asilimia 77 ya Watanzania? Hata hivyo serikali ikaamua uruhusiwe. Hakuna kumbukumbu za kanisa katoliki kupinga na kusema Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu.

Jawabu; Kauli mbiu ya TEC ni kwamba "Sauti ya Watu (wengi wenye akili timamu) ni sauti ya Mungu." Hawajasema kuwa "Sauti ya Watu (wote wakiwemo na vichaa) ni sauti ya Mungu," maana Mungu sio kichaa. Hivyo, maneno "asilimia 77 ya Watanzania" pasipo kikolezo (qualifier) hayana nafasi katika hoja ya TEC.

2. Shemasi ameluliza: TEC inafahamu kwamba mwaka 2001 baada ya matokeo ya Uchaguzi wa Zanzibar na mauaji ya wafuasi wa CUF mwezi Januari, asilimia kubwa ya Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla walitaka kuwepo na mfumo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar na SMZ na SMT chini ya Mkapa haikutaka? Hakuna kumbukumbu za kanisa katoliki kupinga na kusema Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu.

Jawabu; Kauli mbiu ya TEC ni kwamba "Sauti ya Watu (wengi wenye akili timamu) ni sauti ya Mungu." Hawajasema kuwa "Sauti ya Watu (wote wakiwemo na vichaa) ni sauti ya Mungu," maana Mungu sio kichaa. Hivyo, maneno "asilimia kubwa ya Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla" pasipo kikolezo (qualifier) hayana nafasi katika hoja ya TEC.

3. Shemasi ameluliza: TEC inafahamu kwamba mwaka 2014 maaskofu wote Katoliki Tanzania akiwemo Kardinali Pengo na wasaidizi wake walipokea mamilioni ya shilingi pesa taslimu na nyingine kwenye akaunti zao kama Askofu Nzigilwa (milioni 80 benki) na Kilaini (milioni 40 benki). Inajua fedha hizo zilitoka katika kampuni yenye makando kando ya rushwa ya kihistoria Tanzania. Wananchi wengi walipiga kelele lakini fedha hizo hazikurudi wala hakuna kumbukumbu za kanisa katoliki kupinga na kusema Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu.

Jawabu; Kauli mbiu ya TEC ni kwamba "Sauti ya Watu (wengi wenye akili timamu) ni sauti ya Mungu." Hawajasema kuwa "Sauti ya Watu (wote wakiwemo na vichaa) ni sauti ya Mungu," maana Mungu sio kichaa. Hivyo, maneno "Wananchi wengi" pasipo kikolezo (qualifier) hayana nafasi katika hoja ya TEC.

4. Shemasi ameluliza: Padri Kitima anasema kwa zaidi ya miaka 60 ama toka tupate uhuru bandari yetu haijawahi kuendeshwa na wageni. Hii ni kauli yake au ya maaskofu wa TEC? Ni kweli TEC haifahamu kwamba kwa zaidi ya miaka 22 Bandari yetu ya Dar imekuwa chini ya kampuni ya TICTS ikiendeshwa kwa ubia na kampuni toka Hong Kong (Hutchsons?). Kama wanafahamu, wanakumbuka wabia wazawa wa kampuni hiyo wanahusika kwenye kuwapa hela maaskofu kama Rugemalira na IPTL yake walivyofanya? Hili wamewahi kuwaambia waumini wao katika mimbari za ibada?

Jawabu; Padri Kitima anasema kwa zaidi ya miaka 60 ama toka tupate uhuru bandari yetu haijawahi kuendeshwa na wageni "pekee." Umelisahau neno hilo "pekee." TICTS ilikuwa na wabia wabantu kina Karamagi.

5. Shemasi ameluliza: TEC wanafahamu kwamba mwaka 1998 kwenye mauaji pale Mwembechai walikufa wasio na hatia na ilikuwa rai ya mamilioni ya Watanzania kutaka kuwepo na suluhu ya kisiasa? Hakuna kumbukumbu za kanisa katoliki kupinga na kusema Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu.

Jawabu; Kauli mbiu ya TEC ni kwamba "Sauti ya Watu (wengi wenye akili timamu) ni sauti ya Mungu." Hawajasema kuwa "Sauti ya Watu (wote wakiwemo na vichaa) ni sauti ya Mungu," maana Mungu sio kichaa. Hivyo, maneno "rai ya mamilioni ya Watanzania" pasipo kikolezo (qualifier) hayana nafasi katika hoja ya TEC.

6. Shemasi ameluliza: Padri Kitima anasema wananchi wamelikataa Bunge? Ametumia kipimo gani cha Kikatiba? Maana wananchi wanalikataa Bunge kwa kutowachagua Wabunge kwenye Uchaguzi. Hii “Vox Populi Vox Dei” ya TEC imetumia kigezo gani? Wananchi wakikataa Bunge pia si wameikataa Serikali? TEC inaomba vipi busara ya Mheshimiwa Rais ambaye wakati huo huo inasema serikali yake imekataliwa? Kuna kuchanganyikiwa na haraka kubwa kwenye tamko la TEC hata namna lilivyochapwa na kupangiliwa. Inanipa mashaka kwamba chombo hiki muhimu cha Kanisa kimekubali kutumika kwa maslahi binafsi bila tafakari ya kutosha.

Jawabu; Padre Kitia anasema kuwa "Kanisa Katoliki sio kikundi ha sala." TEC wamefanya kura ya maoni katika Parokia 3500 zilizotapakaa nchi nzima.

7. Shemasi ameluliza:Je hii “Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu” ni wengi wapi hasa? Na mungu anayetajwa hapa ni nani? Usikute mungu anayetajwa na kusemwa asikilizwe ni mungu au miungu watu waliokuwa wanaingiza miamala kwenye akaunti za baadhi ya maaskofu wetu na viongozi wengine wa dini miaka nenda rudi. Tujihadhari. Tusiigawa nchi kupitia madhabahu.

Jawabu; Kauli mbiu ya TEC ni kwamba "Sauti ya Watu (wengi wenye akili timamu) ni sauti ya Mungu (wa watu wote)." Hawajasema kuwa "Sauti ya Watu (wote wakiwemo na vichaa) ni sauti ya miungu watu." Hivyo, habari ya "kuigawa nchi kupitia madhabahu" haina nafasi.

Dawati la Mama Amon
"Sumbawanga Town"
Sumbawanga
 
Tuko pamoja Mama Amoni.


Haya majizi yanatafuta njiaaa za kuhalalisha wizi wao, ila ndo kwanza yanaharibu.

Tukiyaambia, Ukweli siku zote hishinda hayaelewi.


Haya Kesi ya Uhaini, Leo Ina dhamana🤣🤣🤣🤣🤣
 
Mama Amon hujajibu hoja hata moja za Shemasi Rugambwa. Ukizoandika ni pumba tu.



Mimi mwenyewe ni Mkatoliki na parokia ya Bikira Maria wa Huruma, Mbezi Beach Dar es Salaam. Nakiri kuwa nimesali Jumapili zote kuanzia mwezi Juni 2023 hadi leo na sikuona wala kusikia kura ya maoni juu ya kukodisha au kutokodisha bandari.



Unajinasibu kuwa wewe ni Mkatoliki toka Sumbawanga, kesho usiende kukomonika hadi uungame uwongo ulioandika hapa
 
Walokula pesa za DP World wanaungua matako ndio maana hawatulii. Mi nasema hiviiiii watulize dawa iwaingie vizuri waliendelea kutotulia sindano itavunjikia [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]nimeishia kucheka sana.

Next time watakuja na bruda ALEX PENGO kutoka seminary Moja huko swax[emoji28]
 
Huu mkataba ni wa moto sana
 
Imeshadhibitika source ya hilo andiko ni simu ya Zantel ambayo chimbuko lake ni Zanzibar! Waislamu wajinga wanajaibu kutumia kivuri cha dini kuwarubuni watu, ila waislamu wenye akili wameungana na watanzania kukemea huu mkataba mbovu! Nyi wachache wafia dini bila kuelewa, acha kupotosha umma. Huo mktaba ukipita (na haupiti) ni wewe na vizazi vyako mtaumia!
 
Hahahaaa!.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…