SI KWELI Shemasi ‘George Rugambwa’ awauliza maswali sita Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC)

SI KWELI Shemasi ‘George Rugambwa’ awauliza maswali sita Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC)

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Kuna ujumbe unasambazwa WhatsApp, una kichwa kinachosema Maswali Sita kwa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) je, ni wa kweli?

1692377824932.jpeg
 
Tunachokijua
Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (kwa Kiingereza Tanzania Episcopal Conference, TEC) ni muundo wa Kanisa Katoliki unaokutanisha maaskofu wake wote wa nchi ya Tanzania, wakiwa wanaongoza jimbo, au ni waandamizi, wasaidizi au wamestaafu.

Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) limetoa tamko tarehe 18, 08, 2023 juu ya mkataba (makubaliano) wa bandari ya Tanzania ambao wameweka msimamo wao wa kutouunga mkono mkataba huo.
F30BJgDWgAACEjR

Mara baada ya kutolewa kwa tamko hilo, umeonekana ujumbe ambao unasambaa kupitia mtandao wa WhatsApp, ukidaiwa kuandikwa na Shemasi George Rugambwa wa Seminari ya Ntungamo, Bukoba, Ujumbe huo una kichwa cha habari, Maswali Sita kwa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC)

1692369684035-png.2720856

Ni upi ukweli kuhusu ujumbe huu?

JamiiForums
ilifanya mawasiliano na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) ili kupata kujua ukweli wa ujumbe huo, ambao wamekanusha kuwepo kwa Shemasi mwenye jina la George Rugambwa katika hiyo Seminari wala kuwepo kwa Shemasi yoyote Seminari ya Ntungamo.

"Hakuna Shemasi katika hiyo Seminari anayejulikana kwa jina hilo na wala hakuna Shemasi kabisa katika hiyo seminari" Walisema TEC

Kufuatia TEC kukanusha kuwepo kwa Shemasi yeyote katika Seminari ya Ntungamo, JamiiForums Imejiridhisha kuwa ujumbe wenye kichwa Maswali Sita kwa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) unaodaiwa kuandikwa na Shemasi George Rugambwa wa Seminari ya Ntungamo kuwa ni wa kuzushwa na hauna ukweli wowote.
Maswali Sita kwa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC)

Na Shemasi George Rugambwa
Seminari ya Ntungamo, Bukoba

Leo TEC imetoa tamko lake kuhusu mkataba wa kuendeleza Bandari ya Dar es Salaam kati ya Tanzania na Dubai. Tamko lake limeelezewa kwa ufupi kupitia Katibu wake Padri Charles Kitima na baadaye likasambazwa kama nyaraka kwa wanahabari.

Kiufupi TEC wanasema maaskofu wakatoliki wanapinga mkataba huo wa Tanzania na Dubai na wanataka sauti ya wengi isikilizwe wakiwa na maana asilimia kubwa ya Watanzania wanaungana na kauli hiyo ya TEC.

Baado naamini ufafanuzi wa Padri Kitima unaweza kuwa na maneno yake binafsi ya ziada kwani alijipambanua awali kuwa na maslahi na jambo hili. Nitaandika zaidi ziku zijazo lakini maswali yangu kwa TEC kwa sasa ni haya ..

1. TEC inafahamu kwamba mwaka 1992 wakati Serikali inapitisha mfumo wa vyama vingi ulikuwa umekataliwa na asilimia 77 ya Watanzania? Hata hivyo serikali ikaamua uruhusiwe. Hakuna kumbukumbu za kanisa katoliki kupinga na kusema Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu.


2. TEC inafahamu kwamba mwaka 2001 baada ya matokeo ya Uchaguzi wa Zanzibar na mauaji ya wafuasi wa CUF mwezi Januari, asilimia kubwa ya Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla walitaka kuwepo na mfumo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar na SMZ na SMT chini ya Mkapa haikutaka? Hakuna kumbukumbu za kanisa katoliki kupinga na kusema Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu.

3. TEC inafahamu kwamba mwaka 2014 maaskofu wote Katoliki Tanzania akiwemo Kardinali Pengo na wasaidizi wake walipokea mamilioni ya shilingi pesa taslimu na nyingine kwenye akaunti zao kama Askofu Nzigilwa (milioni 80 benki) na Kilaini (milioni 40 benki). Inajua fedha hizo zilitoka katika kampuni yenye makando kando ya rushwa ya kihistoria Tanzania. Wananchi wengi walipiga kelele lakini fedha hizo hazikurudi wala hakuna kumbukumbu za kanisa katoliki kupinga na kusema Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu.

4. Padri Kitima anasema kwa zaidi ya miaka 60 ama toka tupate uhuru bandari yetu haijawahi kuendeshwa na wageni. Hii ni kauli yake au ya maaskofu wa TEC? Ni kweli TEC haifahamu kwamba kwa zaidi ya miaka 22 Bandari yetu ya Dar imekuwa chini ya kampuni ya TICTS ikiendeshwa kwa ubia na kampuni toka Hong Kong (Hutchsons?). Kama wanafahamu, wanakumbuka wabia wazawa wa kampuni hiyo wanahusika kwenye kuwapa hela maaskofu kama Rugemalira na IPTL yake walivyofanya? Hili wamewahi kuwaambia waumini wao katika mimbari za ibada?

5. TEC wanafahamu kwamba mwaka 1998 kwenye mauaji pale Mwembechai walikufa wasio na hatia na ilikuwa rai ya mamilioni ya Watanzania kutaka kuwepo na suluhu ya kisiasa? Hakuna kumbukumbu za kanisa katoliki kupinga na kusema Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu.

6. Padri Kitima anasema wananchi wamelikataa Bunge? Ametumia kipimo gani cha Kikatiba? Maana wananchi wanalikataa Bunge kwa kutowachagua Wabunge kwenye Uchaguzi. Hii “Vox Populi Vox Dei” ya TEC imetumia kigezo gani? Wananchi wakikataa Bunge pia si wameikataa Serikali? TEC inaomba vipi busara ya Mheshimiwa Rais ambaye wakati huo huo inasema serikali yake imekataliwa? Kuna kuchanganyikiwa na haraka kubwa kwenye tamko la TEC hata namna lilivyochapwa na kupangiliwa. Inanipa mashaka kwamba chombo hiki muhimu cha Kanisa kimekubali kutumika kwa maslahi binafsi bila tafakari ya kutosha.

Je hii “Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu” ni wengi wapi hasa? Na mungu anayetajwa hapa ni nani? Usikute mungu anayetajwa na kusemwa asikilizwe ni mungu au miungu watu waliokuwa wanaingiza miamala kwenye akaunti za baadhi ya maaskofu wetu na viongozi wengine wa dini miaka nenda rudi. Tujihadhari. Tusiigawa nchi kupitia madhabahu.

Mathayo 23:13
Ole wenu Mafarisayo wanafiki.

IMG-20230818-WA0117.jpg
 
Mkataba wa Bandari ulikuwa kisingizio tu.

nimefurahi sana Kanisa kurejea kwny ada yake baada ya likizo ya 2015-2021

Samia sasa anapitia waliyopitia Mwinyi na Jakaya
Mie kinachonipa faraja sana ni kuwa siku hizi Kanisa linatabirika hata kwa sie tusiokuwa Watabiri

Wale waliokuwa na mashaka mashaka na misimamo ya Kanisa sasa hivi mashaka yote yatakuwa yameondoka.

ila kizuri zaid ni kuwa siku hizi Wananchi wameelimika sana na hutumii maarifa mengi kuwaelimisha na kuelewa kama zamani

Serikali itaendelea kuungwa mkono kama kawaida. pamoja na vitimbi vyote 2005-2015 lakini bado hawakuweza kuzuia waliokusudia kuzuia na bado kwny Orodha ya Mgao wa Escrow wakawepo
 
"Na Shemasi George Rugambwa
Seminari ya Ntungamo, Bukoba"

Shemasi wa dini gani huyu?
 
Leo TEC imetoa tamko lake kuhusu mkataba wa kuendeleza Bandari ya Dar es Salaam kati ya Tanzania na Dubai. Tamko lake limeelezewa kwa ufupi kupitia Katibu wake Padri Charles Kitima na baadaye likasambazwa kama nyaraka kwa wanahabari.

Kiufupi TEC wanasema maaskofu wakatoliki wanapinga mkataba huo wa Tanzania na Dubai na wanataka sauti ya wengi isikilizwe wakiwa na maana asilimia kubwa ya Watanzania wanaungana na kauli hiyo ya TEC.

Baado naamini ufafanuzi wa Padri Kitima unaweza kuwa na maneno yake binafsi ya ziada kwani alijipambanua awali kuwa na maslahi na jambo hili. Nitaandika zaidi ziku zijazo lakini maswali yangu kwa TEC kwa sasa ni haya ..

1. TEC inafahamu kwamba mwaka 1992 wakati Serikali inapitisha mfumo wa vyama vingi ulikuwa umekataliwa na asilimia 77 ya Watanzania? Hata hivyo serikali ikaamua uruhusiwe. Hakuna kumbukumbu za kanisa katoliki kupinga na kusema Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu.


2. TEC inafahamu kwamba mwaka 2001 baada ya matokeo ya Uchaguzi wa Zanzibar na mauaji ya wafuasi wa CUF mwezi Januari, asilimia kubwa ya Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla walitaka kuwepo na mfumo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar na SMZ na SMT chini ya Mkapa haikutaka? Hakuna kumbukumbu za kanisa katoliki kupinga na kusema Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu.

3. TEC inafahamu kwamba mwaka 2014 maaskofu wote Katoliki Tanzania akiwemo Kardinali Pengo na wasaidizi wake walipokea mamilioni ya shilingi pesa taslimu na nyingine kwenye akaunti zao kama Askofu Nzigilwa (milioni 80 benki) na Kilaini (milioni 40 benki). Inajua fedha hizo zilitoka katika kampuni yenye makando kando ya rushwa ya kihistoria Tanzania. Wananchi wengi walipiga kelele lakini fedha hizo hazikurudi wala hakuna kumbukumbu za kanisa katoliki kupinga na kusema Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu.

4. Padri Kitima anasema kwa zaidi ya miaka 60 ama toka tupate uhuru bandari yetu haijawahi kuendeshwa na wageni. Hii ni kauli yake au ya maaskofu wa TEC? Ni kweli TEC haifahamu kwamba kwa zaidi ya miaka 22 Bandari yetu ya Dar imekuwa chini ya kampuni ya TICTS ikiendeshwa kwa ubia na kampuni toka Hong Kong (Hutchsons?). Kama wanafahamu, wanakumbuka wabia wazawa wa kampuni hiyo wanahusika kwenye kuwapa hela maaskofu kama Rugemalira na IPTL yake walivyofanya? Hili wamewahi kuwaambia waumini wao katika mimbari za ibada?

5. TEC wanafahamu kwamba mwaka 1998 kwenye mauaji pale Mwembechai walikufa wasio na hatia na ilikuwa rai ya mamilioni ya Watanzania kutaka kuwepo na suluhu ya kisiasa? Hakuna kumbukumbu za kanisa katoliki kupinga na kusema Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu.

6. Padri Kitima anasema wananchi wamelikataa Bunge? Ametumia kipimo gani cha Kikatiba? Maana wananchi wanalikataa Bunge kwa kutowachagua Wabunge kwenye Uchaguzi. Hii “Vox Populi Vox Dei” ya TEC imetumia kigezo gani? Wananchi wakikataa Bunge pia si wameikataa Serikali? TEC inaomba vipi busara ya Mheshimiwa Rais ambaye wakati huo huo inasema serikali yake imekataliwa? Kuna kuchanganyikiwa na haraka kubwa kwenye tamko la TEC hata namna lilivyochapwa na kupangiliwa. Inanipa mashaka kwamba chombo hiki muhimu cha Kanisa kimekubali kutumika kwa maslahi binafsi bila tafakari ya kutosha.

7. Je hii “Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu” ni wengi wapi hasa? Na mungu anayetajwa hapa ni nani? Usikute mungu anayetajwa na kusemwa asikilizwe ni mungu au miungu watu waliokuwa wanaingiza miamala kwenye akaunti za baadhi ya maaskofu wetu na viongozi wengine wa dini miaka nenda rudi. Tujihadhari. Tusiigawa nchi kupitia madhabahu.

Mathayo 23:13
....Ole wenu Mafarisayo wanafiki...
 
Na Shemasi George Rugambwa
Seminari ya Ntungamo, Bukoba

Leo TEC imetoa tamko lake kuhusu mkataba wa kuendeleza Bandari ya Dar es Salaam kati ya Tanzania na Dubai. Tamko lake limeelezewa kwa ufupi kupitia Katibu wake Padri Charles Kitima na baadaye likasambazwa kama nyaraka kwa wanahabari.

Kiufupi TEC wanasema maaskofu wakatoliki wanapinga mkataba huo wa Tanzania na Dubai na wanataka sauti ya wengi isikilizwe wakiwa na maana asilimia kubwa ya Watanzania wanaungana na kauli hiyo ya TEC.

Baado naamini ufafanuzi wa Padri Kitima unaweza kuwa na maneno yake binafsi ya ziada kwani alijipambanua awali kuwa na maslahi na jambo hili. Nitaandika zaidi ziku zijazo lakini maswali yangu kwa TEC kwa sasa ni haya ..

1. TEC inafahamu kwamba mwaka 1992 wakati Serikali inapitisha mfumo wa vyama vingi ulikuwa umekataliwa na asilimia 77 ya Watanzania? Hata hivyo serikali ikaamua uruhusiwe. Hakuna kumbukumbu za kanisa katoliki kupinga na kusema Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu.


2. TEC inafahamu kwamba mwaka 2001 baada ya matokeo ya Uchaguzi wa Zanzibar na mauaji ya wafuasi wa CUF mwezi Januari, asilimia kubwa ya Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla walitaka kuwepo na mfumo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar na SMZ na SMT chini ya Mkapa haikutaka? Hakuna kumbukumbu za kanisa katoliki kupinga na kusema Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu.

3. TEC inafahamu kwamba mwaka 2014 maaskofu wote Katoliki Tanzania akiwemo Kardinali Pengo na wasaidizi wake walipokea mamilioni ya shilingi pesa taslimu na nyingine kwenye akaunti zao kama Askofu Nzigilwa (milioni 80 benki) na Kilaini (milioni 40 benki). Inajua fedha hizo zilitoka katika kampuni yenye makando kando ya rushwa ya kihistoria Tanzania. Wananchi wengi walipiga kelele lakini fedha hizo hazikurudi wala hakuna kumbukumbu za kanisa katoliki kupinga na kusema Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu.

4. Padri Kitima anasema kwa zaidi ya miaka 60 ama toka tupate uhuru bandari yetu haijawahi kuendeshwa na wageni. Hii ni kauli yake au ya maaskofu wa TEC? Ni kweli TEC haifahamu kwamba kwa zaidi ya miaka 22 Bandari yetu ya Dar imekuwa chini ya kampuni ya TICTS ikiendeshwa kwa ubia na kampuni toka Hong Kong (Hutchsons?). Kama wanafahamu, wanakumbuka wabia wazawa wa kampuni hiyo wanahusika kwenye kuwapa hela maaskofu kama Rugemalira na IPTL yake walivyofanya? Hili wamewahi kuwaambia waumini wao katika mimbari za ibada?

5. TEC wanafahamu kwamba mwaka 1998 kwenye mauaji pale Mwembechai walikufa wasio na hatia na ilikuwa rai ya mamilioni ya Watanzania kutaka kuwepo na suluhu ya kisiasa? Hakuna kumbukumbu za kanisa katoliki kupinga na kusema Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu.

6. Padri Kitima anasema wananchi wamelikataa Bunge? Ametumia kipimo gani cha Kikatiba? Maana wananchi wanalikataa Bunge kwa kutowachagua Wabunge kwenye Uchaguzi. Hii “Vox Populi Vox Dei” ya TEC imetumia kigezo gani? Wananchi wakikataa Bunge pia si wameikataa Serikali? TEC inaomba vipi busara ya Mheshimiwa Rais ambaye wakati huo huo inasema serikali yake imekataliwa? Kuna kuchanganyikiwa na haraka kubwa kwenye tamko la TEC hata namna lilivyochapwa na kupangiliwa. Inanipa mashaka kwamba chombo hiki muhimu cha Kanisa kimekubali kutumika kwa maslahi binafsi bila tafakari ya kutosha.

Je hii “Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu” ni wengi wapi hasa? Na mungu anayetajwa hapa ni nani? Usikute mungu anayetajwa na kusemwa asikilizwe ni mungu au miungu watu waliokuwa wanaingiza miamala kwenye akaunti za baadhi ya maaskofu wetu na viongozi wengine wa dini miaka nenda rudi. Tujihadhari. Tusiigawa nchi kupitia madhabahu.

Mathayo 23:13

Ole wenu Mafarisayo wanafiki
 
Acha upuuzi, hayo yoote uliyoanisha haiweki uhalali wa kuachilia rasilimali zetu kiholela!!

Hakuna sehemu Watanzania wamewakataa DP World, watanzania tumekataa mkataba mbovu wa bandari!! Warekebishe huo mkataba hakuna mtu atakayepiga kelele tena!! Mbona rahisi tuu!!
 
Leo TEC imetoa tamko lake kuhusu mkataba wa kuendeleza Bandari ya Dar es Salaam kati ya Tanzania na Dubai. Tamko lake limeelezewa kwa ufupi kupitia Katibu wake Padri Charles Kitima na baadaye likasambazwa kama nyaraka kwa wanahabari.

....Ole wenu Mafarisayo wanafiki...
Two wrongs don't make it right.
 
Leo TEC imetoa tamko lake kuhusu mkataba wa kuendeleza Bandari ya Dar es Salaam kati ya Tanzania na Dubai. Tamko lake limeelezewa kwa ufupi kupitia Katibu wake Padri Charles Kitima na baadaye likasambazwa kama nyaraka kwa wanahabari.

....Ole wenu Mafarisayo wanafiki...
Roma imeshasema mkataba ule haufai na watanganyika hawautaki. “FINISH”
 
1. TEC inafahamu kwamba mwaka 1992 wakati Serikali inapitisha mfumo wa vyama vingi ulikuwa umekataliwa na asilimia 77 ya Watanzania? Hata hivyo serikali ikaamua uruhusiwe. Hakuna kumbukumbu za kanisa katoliki kupinga na kusema Sauti ya Wengi ni Sauti ya Mungu.
1. Uelewa wa watanzaia ulikuwa mdogo (Nyereere alikuwa dikitaita mkarimu)
2. KUBWA ZAIDI, maoni hayo hayakuwa yameratibiwa na Independent team, ni wao wao na matakwa yao. Ni sawa na tume ya sasa ya uchaguzi ambayo inateuliwa na rais akiwa naye ni mgombea!
 
Leo TEC imetoa tamko lake kuhusu mkataba wa kuendeleza Bandari ya Dar es Salaam kati ya Tanzania na Dubai. Tamko lake limeelezewa kwa ufupi kupitia Katibu wake Padri Charles Kitima na baadaye likasambazwa kama nyaraka kwa wanahabari.

Kiufupi TEC wanasema maaskofu wakatoliki wanapinga mkataba huo wa Tanzania na Dubai na wanataka sauti ya wengi
Mwisho umeandika utumbo wa chura
 
Back
Top Bottom