Shule zaandikiwa Barua kutoa takwimu za Idadi ya wanafunzi wa Kiislamu shuleni

Dunia haina SIRI.
 
Mimi nilichoona hapo kwenye hiyo barua, mbali na maudhui yahusuyo barua hiyo; ni kwamba barua imeanza na Namba 2. Namba moja imekwenda wapi? Haikutakiwa kuonekana na wasomaji ndani ya JF, au ni mwandishi kaisahau?

Pili, hao wanaoomba ruhusa ya kufanya utafiti hapo hawajatajwa kwenye barua hiyo, je, nao ni siri wasijulikane

Haya maswala ya dini yamekuwa mengi sana siku hizi huko serikalini. Hili siyo jambo zuri kwa nchi ambayo inaruhusu watu washiriki ndani ya dini yoyote bila kuhusisha dini hizo katika maswala ya kiserikali. Sasa hata serikali inajenga makanisa, hii siyo ajabu?
 
Wachukue tu..
Vitu vingine sio vya kuvipa attention kabisa
 
Mkurugenzi hana kosa alichofanya ni kuruhusu hao watu na kuomba wapewe ushirikiano sidhani kama kuna kosa au shida yoyote.
Umeeleza vizuri, lakini ninaloamini mimi, hizi shule za serikali hazina wajibu wowote na maswala ya dini. Mambo ya dini wachie wenyewe wenye dini zao wayashughulikie makanisani/misikitini au hata kwenye shule zao maalum.
 
Kama ukiiweka kishari itakuwa ila naona ni sawa tu kama wameomba ushirikiano
Lakini haya mambo siku hizi wanaweka wazi kwa sababu wanazojua wao
Mbona barua nyingi zinaandikwa za maombi haziwekwi mitandaoni?

Kulikoni?
 
Uko sahihi lakini swali linakuja je hicho ulichokisema ndicho kinachokusudiwa?.

Hakuna anaejua lengo la hilo suala hivyo ndio maana lazima watu tuhoji.
 
Wanasitisha ama kukataza!? kusitisha ina maana tayari walikuwa wamesharuhusu?

Usalama wawe makini, extremist is an extrimist, haijalishi ni muislam, mkristu, myahudi, hindu etc.
 
Nisahihishwe kama nitakua nimekosea.

Sensa ya hivi majuzi nchini ilihusisha mambo yanayohusiana na dini. Kwani katika matokeo ya utafutaji inaonyesha kuwa viongozi wa kidini walihimizwa kueneza ufahamu kuhusu matokeo ya sensa.

Hii inapendkeza kwamba sensa ilikusanya takwimu za ufuasi wa dini kwa kiasi fulani, kwani viongozi wa kidini-zote, walionekana kama washirika wakuu katika kuwasilisha matokeo hayo kwa jumuiya zao-

Barua za kuomba takwimu hizo sasa, kama alivyouliza mleta mada, ni kwa malengo yepi tena? Inafikirisha.

Ikumbukwe sensa, madhumuni yake kimsingi ni kufanya hesabu ya moja kwa moja ya kila mkazi nchini, Ofisi ya kitaifa ya Takwimu ya sensa ya 2022 hutoa ripoti kuhusu usambazaji wa idadi ya watu na maelezo ya idadi ya watu, ambayo kwa kawaida hujumuisha taarifa kuhusu mgawanyo wa imani/kididni.

Kwa msingi huo ina suggest pia, serikali ina takwimu za walimu na watoto waendao shule-kwa imani zao, dini zao.

Sasa ikiwa moja ya dhumuni la sensa ni kuisaidia serikali kutoa huduma za kijamii kama vile kujenga vituo vya afya na shule n.k Serikali inakosaje kujua ni watoto ama walimu wangapi wa dini ya waisilamu wapo Mikoani, wilayani, kata na hata kwenye hizo halmashauri- mashuleni? Kwanini waombe tena takwimu hizo kutoka halmashauri?

Wana lengo gani?

Anyway, ni vizuri tukajua kama ni kweli barua zilizosambazwa zina ukweli badala ya kufanya speculation. Hatahivyo nakataa kuna viashiria vya kibaguzi.
 
Wahaya bana. Kama wanyakyusa tu pale wanapojifanya wanajua sana uislam
 
Wenzetu wanajiandaa kuwapa wanafunzi jambia mishare na manati, ndo akili zao zinapoishia. Wakati Wenzao upande wa pili wanawapa watoto computer vitabu nk.
 
Bible knowledge na Islamic ndo upuuzi Gani?

Tuepukr haya mambo yataleta mfarakano
 
Taarifa haina shida kwa sababu lengo ni kupanga mipango ya kufundisha dini.

Tatizo lipo kwa mtoa mada!
 
Kwanini kila ilipo hii dini lazima ione inaonewa tu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…