Sijawahi kuona nchini yenye amani na usalama kama Zambia

Sijawahi kuona nchini yenye amani na usalama kama Zambia

Kwa kigezo cha pesa unasemaje kuhusu Somalia? 🤣🤣
 

Attachments

  • images (1).jpeg
    images (1).jpeg
    43 KB · Views: 16
Ku change hela kwa mkononi huko risky wabongo hawafai,wachache sana waaminifu
Ila kwenye hotel hapo ya Silverstone kna mbongo mmja huwa anabadili hela na yuko smart sana

Ova

Waliobaki wote wahuni, nilizoeana na jamaa anaitwa paulo, siku nimetoka zangu Angola, nimechoka nikaenda kulala lodge nikaona ngoja nimpigie paulo aje nichukue pesa kidogo shilingi, haaa dola 250 kapotea nayo hadi leo sijawahi kumuona nikajiuliza huyu dogo kapotea na hizi pesa kidogo atafanyia nini? Wakati tip tu nilikua naweza kumpa hata jiwe na nusu nikaona bwege kumbe alikua ananilia timing, nikahamishia mambo yangu yote kwa yule mpemba sijui msomali alikua na burea pale opposite na taqwa, nikazoea nikitaka kusafiri pana chimbo kariakoo nilikua nafuata, kuanzia dola hadi rand naruka nikiwa kamili kabisa, lakini kuchenji kama umeshindwa bora uende benki kuliko kwa wale mawinga washapotea na mitaji ya watu, sehemu ambayo kwenye chenji mawinga sio wababaishaji ni Rwanda lakini upande wetu pale rusumo ni weziwezi hatari, Uaminifu utaukuta asilimia kubwa kwa mkinga kwa bongo lakini jamii nyingine ni tia maji tia maji hakuna unafuu
 
Kwa wapambanaji kuna somo limeibuka kwenye thread hii la uaminifu, niwasihi kwenye biashara na kokote unakopambana uaminifu iwe nguzo yako kubwa kuna siku itakulipa ukiacha amani ambayo utaweza kwenda popote bila kujiuliza maswali, kudhulumu cha mtu mara nyingi itakurudia tu, ni vizuri kupambana kwa bidii sana lakini ujanja ujanja hautakiwi kwani kupotea kwenye ramani ni dakika chache sana.
 
Jamani jamani Wazambia wanao chenchi Hela boda ya Tunduma ni wapigaji Balaa usiyakanyage Mimi ni msafiri wa kila siku msijifariji Wapigaji wapo watu wanaibiwa kila siku mabegi na mizigo yao pale stend ya Lusaka inter city endeleen kujifariji tu
 
Ushamba mzigo kufika hapo Nakonde (border town) unaona umeyapatia!
Binadamu tunatofautiana, wewe kwako unaweza ona kufika nakonde sio kitu ila kuna sisi tunaona ni mafanikio maana hatujawahi fika na yeye kwake ni kitu kikubwa sana, nisamehe lakini umekaa na akili za kimasikini masikini sana mkuu
 
Uaminifu ni changamoto tena kuanzia juu, angalia report za CAG inasikitisha sana yaani watu wanawaza upigaji na huku street raia wanawaza kutapeli na kupiga tuu hakuna EMPATHY.
 
Habari zenu wana JF wenzangu, kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Katika zunguka zunguka yangu yote katika nchi mbali mbali nikianza na nyumbani Tanzania, kwa kweli sijawahi kuona nchi yenye amani na usalama wa hali ya juu kama Zambia.

Kwa wale wenzangu waliowahi kuikanyaga nchi hii bila shaka wataleta ushuhuda wa hiki ninachoongea. Zambia ndio nchi ambayo unaweza kununua kitu njiani huku basi linakwenda, cha ajabu kama ulitangulia kumpa muuzaji hela kubwa, basi muuzaj atalikimbilia hilo basi hadi ahakikishe amekurudishia chenji yako, kitu ambacho kwa nchi nyingi including Tanzania hakipo. Yani ukinunua kitu ukatangulia kutoa hela na basi likaanza kwenda, basi uhesabu ushapigwa, maana muuzaji hatokupa chenji yako, badala yake atakimbia zake akijua hauna uwezo wa kutoka ndani ya basi linalotembea ili umkimbize yeye.

Hiyo tisa, kumi ni pale unapofika Lusaka katika ile stand yao kuu inayoitwa Kaunda bus terminal. Aisee pale utakuta wale jamaa wanaochenji hela wakiwa na maburungutu ya dola za mia mia, hamsini hamsini nk wameziweka mezani kwa ajili ya kuwachenjia wasafiri mbali mbali wanaoshukia pale kutoka nchi mbali mbali. Lile soko liko wazi masaa 24, na hakuna anaeingia kuwasumbua au kuwaibia wale wanao anika madola yao hadharani kwa ajili ya chenji. Kwa Tanzania ukiwa na sh laki 1 ukienda kariakoo kununua kitu, basi muda wa kulipa inabidi usogee kona kidogo ndo uchomoe hela, tena kimagutu magutu unaangalia huku na kule ili usije fatwa na vibaka. Kwa Zambia hiyo haipo.

Kuna siku nilishuka pale na mzigo wa maana, kwa vile nina mjomba wangu anaishi pale ikabidi na mimi nichukue hata wiki moja ili niuze mzigo wangu mdogo mdogo. Aisee nilishangaa kuona jamaa amekuja na zaidi ya dola 2500 tena kaziweka mfukoni tu, hana wasi wasi wowote mpaka pale town lilipo duka la mjomba wangu, akanipa changu na mimi nikamkabidhi mizigo yake akaita gari akapakia akaondoka.

Mimi mcheche ukanishika nikifikiri labda kuna watu wametuona kwahiyo wanaweza kuja kutupora yale madola aliyoniachia jamaa, mjomba wangu akacheka na kuniambia kuwa hapa watu huwa wanatembea mpaka na dola elf 7 town, itakuwa mimi wa dola elf 2 bwana.

Ki ukweli style ya maisha ya pale niliipenda sana haswa kwa upande wa usalama, sema ndo hivyo sehemu ambayo haukuanzia maisha ukisema uende kuanza tena itachukua muda kutoka.

Hizi nchi zetu zingine usalama ni zero, mpaka inafika kipindi wengi wetu tunakuwa tunatembea na kadi za bank tu mifukoni, ili kuepusha wizi wa fedha unaoweza kutokea wakati wowote. Mpaka sasa sijajua ni mbinu gani wanayotumia hawa jamaa kudhibiti wizi na ujambazi katika maeneo mbali mbali ya mji wa Lusaka na Zambia yote kwa ujumla.
Huijui vizuri Zambia wewe kule uhalifu ni sawa na South Africa
 
Uaminifu ni changamoto tena kuanzia juu, angalia report za CAG inasikitisha sana yaani watu wanawaza upigaji na huku street raia wanawaza kutapeli na kupiga tuu hakuna EMPATHY.
Nchi yote hii kiongozi ambae hakupiga au asie na Mali hata 1 ya kisingiziwa Ni Nyerere tu, wengine wote waliofuata wali-set precedence ya upigaji nasi tunaifuata kiroho Safi.
 
Nadhani hata Uganda wizi wa kijinga hamna, askari wametapakaa sehem nyingi, kuna kijana alijaribu kuiba side mirror ya gari, alitandikwa shaba hapo hapo... Mwizi ni kutandikwa shaba tu
 
Back
Top Bottom