Siku Dkt. Bashiru, Prof. Kabudi au Balozi Polepole wakisimama dhidi ya CCM nitaogopa sana lakini Lissu, Lema na Mbowe hawana maajabu


Eti Poleple, Bashiru na Kabudi..... Kuna watu humu, akili zenu mnazijua wenyewe tu.
 

Inaonekana hili jambo la kuruhusiwa mikutano ya hadhara limeichanganya CCM. Sasa naona kila mmoja anajaribu kucheza mind games ili kupunguza hofu iliyotanda. Hakuna mwanaccm anaweza kujenga hoja na kukubali kuingia kwenye ushindani wa haki baada ya kutoa hoja zake. Wote wanategemea mbeleko ya vyombo vya dola kuweza kubaki madarakani.
 
Hawahawa wauaji wa watu waliokuwa wanaokotwa kwenye viroba? Kwanza Nashiru alikuwa MC au katibu mkuu? Mi nilikuwa sielewi kazi yake na chongolo amekuna kumfundisha nini mana ya katibu mkuu
 
Kweli kabisa hakuna alie nguvu nje ya ccm .....hakuna na hataweza ...so JK Membe wala Lowasa hakuna .....
 
Upinzani unahitaji watu wenye kariba ya hao niliowataja usonge mbele ,kizazi Cha lema ,lissu na Mbowe kinaurudisha nyuma sana upinzani
Unafikiri kuwa upinzani ni lelemama?
Huyo Jiwe mnayemtukuza kuwa alipambana na CCM ya mafisadi kwa nini asingeunda upinzani badala yake akawa anaunga mkono kila kitu cha Kikwete?
 
Nyie CCM mmeshaanza kuogopa CDM baada ya mama kulazimika kusalimu amri kwa kamanda Mbowe. Tulieni yule dikteta uchwara hayupo safari hii.
 
Jingasaana hivi unawezaje kuyasifu majinga matatu yaliyobebwa na magu nakushindwa kujibeba yenyewe!! Kucha kutwa yalimlamba viatu nakumwimbia nyimbo zilizo bora!!!
Wajinga watatu hao waliharibu katiba mpya na kulazimisha siasa za kupalilia chuki,wizi na uuwaji wa demikrasia huku wakishangilia ubabe mateso na dhulma walizotwishwa wananchi, walifanya hayo huku wakidansi ndombolo kama majuha.
Ustuletee upuuzi jukwaani kaa nao moyoni mwako, kama unawapenda sana kanywe nao chai na picha zao lalanazo... ptuuuh!
 
Endelea kusubiri karibu utajua😁😁😁
Karibu ndiyo hiyo watu wanalishwa ndizi mbichi au tusubiri waanze kulishwa mihogo mibichi 😝😝😝
 
hawa wazee wawe wapole tu hawana namna - watulie tuli.

Naona sasa wameelewa tulivyokuwa tunapiga kelele kuhusu katiba mpya.
 
Hawana lolote hao, wengine wametoka jalalani!
Kwa sasa wote ni vibogoyo wa kisiasa.
Hizo hoja unazozisema watazijengea wapi?
Ndani ya CCM wanaweza kusema, nje ya CCM ni mdebwedo tu!!
 
Sisiemu ni ileile fikra ileile itikadi ileile tuu majina tuu ndiyo tofauti hapo unategemea nini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…