Silaha za Urusi ni bora kuliko za Marekani, ni kimbilio la mataifa mengi kuanzia sasa

Silaha za Urusi ni bora kuliko za Marekani, ni kimbilio la mataifa mengi kuanzia sasa

Labda akiwa anapigana na LIBYA kama yote hayo anayo anangojea nini kuwahami wa UKRO NAZI kama alivyofanya kule LIBYA nk
Hapo UKRONAZI waliiomba hio No Action Talk Only (NATO)
waeke No Fly Zone mpaka leo umeona nini !!?
Ukitoa kifo NATO wanaiogooa RUSSIA kuliko chochote kile
Ukraine haiko NATO, EU wala interests za wests hazijaguswa unaingiaje kupigana?

Unauhakika ulivuka chekechea maana reasoning yako inatia wasiwasi
 
tumia akili bila msaads huo mdogo Kwa uwezo wa Ukraine angekuwa kafail vita so lzm utambue msaada wa Javelin kweny vita
Watu wasichokifahamu ni kwamba NATO kupitia Marekani, UK na Poland waliingia siku nyingi kule Ukraine kujiandaa na vita hii ya Sasa, kabla ya mwaka 2014. Walipeleka siliha nyingi za kisasa na mifumo ya ulinzi ya kisasa kabisa dhidi ya Russia. Waliimarisha Kambi za jeshi kila pahala muhimu, lakini silaha, mifumo ya ulinzi na maghala yote muhimu vililipuliwa vyote siku ya kwanza TU ya uvamizi wa Russia nchini Ukraine. Jambo hili liliwaduwaza Marekani na UK na NATO nzima.
 
India mwezi huu imechochea program yake ya kuongeza idadi ya fighter jets zisizozidi 114 kwa gharama ya dola bilioni 20 za Marekani. Kati ya ndege tano top contenders hakuna ndege ya Urusi. Ndege mbili za Boeing ya Marekani, Dassault Rafale ya Ufaransa, Lockheed Martin ya Marekani, Saab ya Sweden, consortium ya Europe wametinga na Eurofighter Typhoon yao. Russia imeleta Su-35 na Mig-35 zao ila hazipewi nafasi kubwa ingawa ndio zina bei ndogo zaidi.

India wana ndege za Urusi nyingi na wanaachana nazo taratibu, hata hii stealth Su-57 walianza nayo kipindi inaitwa PAK FA ila wakajiondoa baada ya gharama kupanda, specs kuwa tofauti na delays, wakaiacha Russia yenyewe. Mwaka 2019 waliagiza Dassault Rafales 36 baada ya mgogoro wa mpakani na China kwenye eneo la Ladakh. Kwanini hawakuongezea idadi ya Su-30MKI tena ambazo Hindustan pale India inaweza tengeneza components nyingi kulingana na mkataba maana MKI ni modification ya India tu. Rafale inapewa nafasi kubwa zaidi

India mwaka huu wamepiga chini mkataba wa kuongeza Kamov Ka-31 helicopters 10 za Urusi kwa ajili ya Navy yao, wakati huo procurement ya helicopters za Marekani inafanyiwa kazi. Kati ya ndege 114 hizo za future program India wanataka navy jet kwa ajili ya aircraft carrier yao. Kwahiyo hapo Russia hana chake, hapo kuna contenders wawili: Dassault Rafale na Boeing Super Hornet.

Tuachane na India ambayo ndio top Russian weapons importer duniani, twende kwa Egypt ambayo ndio top Russian weapons importer in Africa na Middle East, na wana ndege aina nyingi sana wanachanganya hawa sijui huwa wanawezaje maintenance. Egypt wana Rafales baada ya kuzipima dhidi ya Mig-29 wakagundua Mig-29 (ambazo waliagiza ziwe modified zije Mig-35 ila wakapewa Mig-29M2) na PESA radar yake haizidi Rafale. Na wamepunguza order quantity ilimradi wasivunje mkataba waliosaini 2018 kununua Su-35.

Indonesia mwaka jana iliachana na ndoto za Sukhoi wakati ilishatenga hela ikachukua Boeing F-15 kwa sababu hiyohiyo ya PESA radar kwenye karne hii.

Algeria ambayo ni ya pili kwa kununua silaha za Urusi hapa Afrika imeachana na Su-35 kisa PESA radar mwaka huu huu. Watu wanataka AESA wewe unawaletea Erbis-E radar ambayo ni PESA leo 2022 wanunua ndege wakae nazo miaka 30, wakitaka modifications uwapige hela tena.

Mikoyan ilianza hivihivi haifanyi investment kwenye modifications na new weapons systems, sasa naona na Sukhoi inaelekea ukouko. Hao wanunuaji wa hizo silaha wako wapi?

Kwanza nani kaona St. Petersburg Economic Forum iliyofunguliwa leo? Hawa team Moscow ukute hawajui hata uwepo wake wakati ndio Davos ya Urusi, viongozi waliokuwepo leo ni kina Armenia, Kazakhastan, Belarus na Mtaliban alikuwepo. Uache biashara na Canada ukafanye na Taliban si utaishia kuwauzia majambia
Tupe source yako ya habari hizi, maana unaongea kama vile wewe ni Waziri wa Ulinzi wa India. Hakuna nchi inaweka mipango yake ya kijeshi kama hivyo unavyosema wewe hapa. Kinachoichelewesha Russia pale donmbas ni raia wake. Urusi inaiona Ukraine kama sehemu ya Urusi ndio maana inatumia silaha zenue uwezo mkubwa sana wa kulenga targets TU. Kama ukrine isingefanya ujinga wa kuwatumia raia kama ngao ya kivita huenda asingekufa hata raia mmoja.
 
Ubora!! damn man!!

Air superiority Stealth technology??

F22 raptor (US) vs Su-37(russia) ???

Though f22 is older, achana na kila kitu including size, weight, speed, missilies used, payloads, range, ceiling height, etc

Consider one criteria, their radar technology.

RCS: F22 0.001 msq wakati RCS ya SU-37 ni 0.1 msq

This means at 500km range in a war fight, F22 sees you as a plane and shoots you down first while at 500km range, SU-37 anamuona F22 kama kandege au nyuki au ball bearing sababu ya Radar cross section area, RCS.

In a more clear way,
Range ya S-400 ni km 400, s400 inaona aircraft zenye RCS 4 so inaweza kumrecognize f22 at
On the other hand f22 inaweza ku geolocate s400kwa umbali wa
With F22 na F-35 and B-2 kama 100 hivi USA anaweza kumiliki anga lako within hours uku ukiwa bize na Abraham tanks on the ground.


USA ana F22 like 184+, russia like 12 hivi. Kwahiyo ndani ya saa chache US anamiliki nhi yako kutoka angani.


Forget F35-lightning II, B-2 bomber stealths fighters!!
Km hizo data ni sahih kwa nin us anakataa kutimiza matakwa ya zele kuhusu anga la Ukraine
 
Km hizo data ni sahih kwa nin us anakataa kutimiza matakwa ya zele kuhusu anga la Ukraine

Unaingia anga la ukraine means unajiunga na vita. How stupid can the US be ku escalate into full scale nuclear exchange? for fun au for what gain ?


Any NATO boots on Ukraine's ground is bullying action kwa Russia. It means wanamdharau. Russia atatumia Nuclear kuipiga Ukraine. NATO watakua forced nao kutumia nuclear and what is the end? You sit back and provide just weapons support kama kweli unatoa msaada na sio millitary forces.
 
Unaingia anga la ukraine means unajiunga na vita. How stupid can the US be ku escalate into full scale nuclear exchange? for fun au for what gain ?


Any NATO boots on Ukraine's ground is bullying action kwa Russia. It means wanamdharau. Russia atatumia Nuclear kuipiga Ukraine. NATO watakua forced nao kutumia nuclear and what is the end? You sit back and provide just weapons support kama kweli unatoa msaada na sio millitary forces.
Kakaaa, wewe uko hapo Tandale unakula mahindi choma. Wasikilize wamarekani wenyewe wanasema nini kuhusu jeshi lao dhidi ya lile la Urusi na China



 
Silaha za kirusi zilizofanya vizuri Ni pamoja na Iskander missiles,
Kalibre missiles,
Terminator mfano wa kifaru.
Bila kusahau
Russian Navy japo hiyo kalibre hutoka humo.
Pia hatuwezi kupuuza uwepo was kazi mzuri zinazoendelea kufanywa na mifumo ya Ulinzi wa anga Russian S 300 PMU,na s400
Lakini Kuna zile zilizofanya vibaya Sana Eg vifaru model ya T 72 ambacho Ni kizazi Cha tatu Cha vifaru .
Ukiachana na Hilo kina model hii ya kifaru inaitwa t90 imeendelea kufanya vizuri Mashariki mwa Ukraine licha ya uwepo was JAVELIN Anti Tank Missiles
 
Kuna ushabiki na uhalisia ,hii thread unaongea ushabiki na sio uhalisia ulivo.Ukweli ni kwamba NATO chini ya USA ni moto wa kuotea mbali na Urusi anawaogopa hao NATO .Na ukweli ni kwamba pamoja na Ukureine kuhalibiwa miundombinu yake lakini kwa msaada anapewa na NATO under USA hii vita atashinda na huu ndiyo unaenda kuwa mwisho wa Putin kama Rais wa Urus na Duniani pia.
Acha muda utatupa majibu ni nani kati ya NATO na Urus aliye na silaha Bora .
Tena kumbuka Hawa NATO chini ya USA ndiyo wanaongoza Dunia mifumo yote ya kuendesha Dunia wanayo wao iwe kijeshi,kiuchumi,na hata kitamaduni.Kwa Hali hiyo hii vita watamshinda Mrusi.
Unaweza bisha lakini huu ndiyo ukweli.
Wewe mbona hauongei uhalisia
 
Bila silaha za magharibi. Kyiv ingetekwa ndani ya siku tatu hadi nne.

bila silaha za magharibi Israel isingeshinda vita na mataifa ya waarabu ndani ya siku sita
.
Bila silaha za Magharibi marekani asingekua na uwezo wa kua na historia ya kupigana na mataifa zaid ya 100+.

Bila silaha za magharibi Taiwan ingeshachukuliwa na china kesho tu asubuhi.

Bila silaha za magharibi kusingekua na korea mbili kaskazin na kusini.

Bila silaha za magharibi Andunje asingetishia kutumia Nukes.

Malizia Bila nyingine unayoijua wewe.
Marekani kapigana vita 100 wap!?
 
Humu kumejaa ushabiki tu.
Muda utakuwa mwalimu mzuri, mimi nasubiri.
Ngoja nisubiri 23% ya mama july huku nikipiga kitu changu cha ugali mlenda hapa bila kusahau mihogo na kiporo cha wali.
 
20220630_140742.jpg
 
Vita ya Syria na Ukraine imeonyesha kuwa Silaha za magharibi (NATO) zimeonyesha uwezo mdogo sana dhidi ya zile za nchi za Magharibi. Nchi nyingi sasa zinawaza kwenda kununua silaha na mifumo ya ulinzi ya Urusi zenye ufanisi mkubwa kwenye uwanja wa vita kuliko zile za NATO.

NATO sasa inawaza kuachana na vita dhidi ya Urusi, hawaiwezi, wamekiri wenyewe kuwa mataifa yoooote ya ulaya na Marekani.

yanaiogopa Urusi, yaani NATO ni kwaajili ya Russia tu.


Kavulata sijui habari zako unachukua wapi? Sioni nchi zinazohamia upande wa silaha za kirusi. Una data zozote? Lete
 
Back
Top Bottom