Special thread: Kutana na waagizaji wa magari kutoka Japan
Mkuu hii Rav 4 Kilitime kwa sasa imeshuka hadi bei gani?
Ingewezekana kipindi hiki gari hizi ziwe zimeshuka kiasi boss, changamoto iliyotokea gari hizi hazijapungua sana bei ni madhara ya Corona ambapo shughuli za minada kule Japan zilisimama hivyo makapuni yakawa na stock kidogo, pia mataifa kama sisi Tanzania tukawa hatuagizi magari kwa wingi katika kipindi hicho.

Sasa mataifa yetu mengi yamefunguliwa na watu wamerejea kuagiza magari kwa wingi wakati gari zenyewe Japan bado hazijawa nyingi kwenye stocks hivyo wauzaji kule nje wamejikuta wanauza bei juu kidogo kama zile zile za awali kwa kua uhitaji ni mkubwa na gari ni chache.

Kwa wastani gari hizo tukipambana sana unaweza kuipata kwa mpaka 17m
 
sawa asante mkuu.

Pia ningependa kujua tofauti kati ya Rav4 toleo la kwanza,la pili na la tatu.

Ipi ni imara,fuel economy na bei ya spares?

Ukiwa kama mtaalamu utamshauri mteja achukue ipi kati ya hizo?
ingewezekana kipindi hiki gari hizi ziwe zimeshuka kiasi boss, changamoto iliyotokea gari hizi hazijapungua sana bei ni madhara ya Corona ambapo shughuli za minada kule Japan zilisimama hivyo makapuni yakawa na stock kidogo...
 
Hivi kuna tofauti kati ya toyota cami na camry??

afu pia mwenzenu sijui nini maana ya 2wd au 4wd nini kazi yake.. Ipi inafaa zaidi
Tofauti ipo ndugu. Toyota Cami ina muundo wa Rav 4 au Suzuki Escudo au Toyota Rush n.k...Kwa ufupi Cami ni Gari ya juu juu na imeundwa ikiwa na milango mitano, huku injini yake ikiwa na Cc 1300. Gari hii ni moja ya gari za Toyota ya juu juu yenye matumizi madogo ya mafuta na unayoweza kuimiliki kwa bajeti ya wastani (Inafaa zaidi kwa mizunguko ya kawaida).

Wakati Toyota Camry body yake ni muundo wa gari kama Toyota Chaser, Mark 2, Crown, Cresta n.k. Camry iliundwa ikiwa na injini kubwa na ndogo yaani ya Cc 2000 Vvti, ya Cc 2200 na Cc 2400Vvti.

Kuhusu 2WD na 4WD ni kwamba, kuna gari zimeundwa zikiwa zina difu mbele na nyuma hivyo dereva anapokwama kwenye tope anaweza kuingia hiyo gia husika (Inakuaga ka gia kadogo pembeni ya gia kubwa) au batani kwa gari za kisasa ili kufungua difu nyingine gari iweze kunasuka-hiyo ndio huitwa 4WD au Four Wheel Drive.

Lakini kuna gari nyingine ni za kisasa zaidi zina kitu kinaitwa AWD yaani All Wheel Drive-Hii maana yake ni kua gari itatumia miguu miwili tu kujisukuma lakini inapotaka kunasa bila dereva kubonyeza popote miguu mingine miwili itafunguka na kusaidia ile miwili ya mwanzo ili gari isinase (Hii ni automatic four wheel)

2WD maana yake ni Two Wheel Drive, yaani gari itatumia miguu miwili tu aidha ya mbele au nyuma kujisukuma...
 
sawa asante mkuu.
Pia ningependa kujua tofauti kati ya Rav4 toleo la kwanza,la pili na la tatu.
Ipi ni imara,fuel economy na bei ya spares?
Ukiwa kama mtaalamu utamshauri mteja achukue ipi kati ya hizo?
Ya kizamani yaani model ya 1996-1999 ni nzuri na ngumu kwenye body na injini yake ya 3s yenye Cc 2000 ambayo haina Vvti, kwa wastani hii huweza kwenda mpaka kilomita 10.5 kwa lita kutegemea na matumizi. Vifaa vyake vipo kila kona ya nchi kwa gharama za wastani. Kuiagiza huweza kukugharim 17 M

Toleo la pili maarufu kama killi time ya mwaka 2000 mpaka 2005 ina injini 2 tofauti yaani 1AZ ya Cc 2000 maarufu kama D4 ambayo hii hutumia umeme mwingi na matumizi ya mafuta ni juu kidogo kiasi cha mpaka kilomita 11 wakati kuna injini nyingine ndogo ya Vvti yenye Cc 1800 iitwayo 1ZZ. kwenye toleo hili unashauriwa utumie hiyo injini ndogo kwa kua inatumia mafuta chini kiasi cha mpaka kilomita 15 kwa lita na wakati huo huo inatengenezeka kirahisi kuliko huyo mwenziwe. Kuiagiza huweza kukugharim 18 M

Toleo la tatu ni Rav 4 ya mwaka 2006- 2008 maarufu kama Miss TZ au Push to Start. Hii ni nzuri pia na ina injini moja ya Petrol yenye Cc 2400 Vvti na injini nyingine ya Diesel inayopatikana zaidi Uingereza yenye Cc 2200. Kwa huku kwetu inayoagizwa zaidi ni hiyo ya Petrol na ina matumizi mazuri pia ya mafuta kwa kua hukadiriwa kwenda hadi kilomita 13.5 kwa lita. Kuigagiza huweza kukugharim 24 M

Kwa ufupi Rav 4 zote ni nzuri isipokua hiyo moja yenye injini ya 1AZ au D4, vifaa vyake vinapatikana kila kona kwa bei za wastani na gari zote ni imara kutegemea na matumizi pia. Cha muhim ukitaka kuagiza hakikisha inatokea soko la Japan, isiwe Singapore, Dubai wala Uingereza maana matunzo ya maeneo hayo sio mazuri sana kama Japan na pia gari yako itafanyiwa ukaguzi wa ubora ikitokea Japan pekee
 
Ya kizamani yaani model ya 1996-1999 ni nzuri na ngumu kwenye body na injini yake ya 3s yenye Cc 2000 ambayo haina Vvti, kwa wastani hii huweza kwenda mpaka kilomita 10.5 kwa lita kutegemea na matumizi. Vifaa vyake vipo kila kona ya nchi kwa gharama za wastani. Kuiagiza huweza kukugharim 17 M..
Asante kwa shule. Oktoba nakuja ofisin mpaka Sasa nimesanya 3000USD zipo DTB
 
Mkuu nakukubali sana unaipenda kazi yako.

Naomba dondoo kidogo kuhusu Nissan Dualis ukilinganisha na Rav 4.

1.Utumiaji wa mafuta.

2.Uimara wake.

3.upatikanaji na gharama za spea.

(ikiwezekana utupe na uwiano wa bei ukilinganisha na rav 4).

Kwa mfano kama shock up ya rav 4 ni 150000 je ya Nissan Dualis itakuwa bei gani?kama taa ya Rav 4 ni 200000 je ya Nissan Dualis itakuwa bei gani?Hii itatusaidia watu wa kipato cha chini na kati kufanya maamuzi.
Karibu sana ndugu. Tuna kiu ya kukuhudumia na kufikia matarajio yako siku za badae
 
Mkuu hauna testimony za wateja uliowahudumia? Madalali wa kibongo fanyeni biashara kisasa
Zipo nyingi sana boss. Nakutumia chache sana za hivi karibuni

592B8EB2-9758-48C9-8669-3E7D55BAFAFD.jpeg
15B03FB5-5B9B-41C8-A882-51B76AAD74F6.jpeg
9C19061D-FFBC-4B7B-A692-6A7D0AE22777.jpeg
DD516E71-9FBC-4665-A667-671D7FA8E40B.jpeg
A85521E7-6A81-4118-9281-147C14D0F6FE.jpeg
0B142CAF-B77E-427E-9AC4-369382DC4067.jpeg
14FAC7FA-EC3E-456D-A99D-1F25FAB1E306.jpeg
E99E3A4A-FE52-4FCF-9685-0845ED05863A.jpeg
90426AFE-7577-4516-959E-8E09382746B5.jpeg
18503CB6-B1BF-4068-AEFB-5A6E7C03720A.jpeg
404DC4EF-7FCF-4DE0-B9A0-58B4A3CF291D.jpeg
 
KIMOKIMOMWEMOTORS
Naomba kujua gharama ya Premio yenye walau CC 1500 kwa sasa, naomba ufafanuzi wa Mwingine kama Ulaji wa Mafuta, Spair na vingine mtakavyoona Muhimu nivijue kwenye gari hili.
 
KIMOKIMOMWEMOTORS
Naomba kujua gharama ya Premio yenye walau CC 1500 kwa sasa, naomba ufafanuzi wa Mwingine kama Ulaji wa Mafuta, Spair na vingine mtakavyoona Muhimu nivijue kwenye gari hili.
premio zina aina 3 ya injini. Ipo injini yenye Cc 1500 ina Vvti, Ipo yenye Cc 1800 ina Vvti pia na ipo yenye Cc 2000 ambayo haina Vvti. injini inayoshauliwa zaidi ni hizo 2 zenye Vvti. Kama utakua mtu wa safari sana vizuri utumie hiyo ya 1800, kama mizunguko ya kawaida na safari chache hiyo ya 1500 inatosha sana. Hizi injini mbili ni nzuri sana kwenye matumizi mazuri ya mafuta na hata kudumu na vifaa vyake vipo kila kona hapa Tanzania kwa gharama za wastani.

Mara nyingi kuagiza gari hizi inaweza kugharim kati ya 11.8m mpaka 12.8m kutegemea na tutakavyoipata. Kwa ujumla ni gari nzuri na imara kwa kiasi chake iwapo barabarani
 
KWA NINI UAGIZE KUTOKEA SOKO LA JAPAN BADALA YA NCHI NYINGINE?

Utangulizi

Kwa kua tuna uzoefu mzuri kwenye eneo hili la magari yatokayo nje, tumeona ni vyema leo tugusie kwa ufupi changamoto zinaweza kumpata mtu anayeagiza gari yake nje ya Japan.

Kabla ya kuamua kulipia gari husika ni muhim ukaangalia kwa uhakika gari yako inatokea nchi gani. Mfano, kwenye website ya kampuni kama Beforward utakuta baadhi ya Gari zimeelezwa kwamba zipo U.K au Dubai au U.S au Singapore au Korea au Japan...si kila gari utakayokuta kwenye website husika ipo Japan na hili ni muhimu ulizingatie

Baadhi ya Watu walioagiza magari kutoka nchi kama Uingereza, Singapore, Dubai n.k walipotumia gari zao kwa mda mfupi zilipata matatizo ya kiufundi ikilinganishwa na wale walioagiza magari kama hayo kutokea soko la Japan.

KINACHOVUTIA MTU KUAGIZA GARI KUTOKA NCHI KAMA UINGEREZA AU SINGAPORE BADALA YA JAPAN

1. Gharama ndogo.

Bila kujua kwamba unanunua gari hiyo kwa bei chini sana lakini mwisho wa siku yaweza kuja kukusumbua na kukufanya utumie gharama zaidi kwenye matengenezo

2. Viti vya ngozi na mvuto wa ndani.

Hii iko zaidi kwenye gari zinazotokea Singapore. Hawa jamaa ni wazuri sana kwenye kumvutia mteja kwa macho na hata picha wanajua kuzipiga vizuri, lakini ni mara chache kukuta gari zao hazina matatizo mengine ya kiufundi hivyo usivutike na mvuto wa viti vya ngozi pekee unatakiwa kuangalia mbali zaidi ya viti.

3. Majina ya magari.

Kwa mfano mteja atasema anataka Mazda 6 na sio Mazda Atenza au anataka Mazda 3 na sio Mazda Axella, Mwingine atasema anataka Toyota Yaris na sio Toyota Vitz au anataka Honda Jazz na sio Honda Fit n.k ila ukweli ni kua Yaris ndio Vitz, Axella ndio Mazda 3, Honda Jazz ndio Fit n.k kilichofanya gari zitofautoane majini ni kusudio la nchi gari husika itakapokwenda kutumika.

CHANGAMOTO ANAZOWEZA KUPATA MTEJA ANAYEAGIZA GARI NJE YA JAPAN

1. Hayafanyiwi ukaguzi kabla ya kutafutiwa meli kama ilivyo kwa gari za Japan hivyo kuna uwezekano gari yako ikaja na matatizo ya kiufundi na badala yake ukaguzi hufanywa hapa hapa TZ baada ya gari kufika.

2. Kuna uwezekano gari yako itokayo nje ya Japan haswa Singapore na Dubai ikawa imechezewa kilomita ili kukuvutia zaidi na mwisho wa siku ndio huishia kukusumbua tofauti na kilomita zake zilivyo chache na ukizingatia kwao hizi sio biashara kuu sana hivyo serikali hazijaweka nguvu za kutosha kudhibiti hili.

3. Utalazimika kuingia gharama ya Ukaguzi baada ya gari kufika ambayo yawezekana hata hukuiwazia. Gari za Japan zinafanyiwa ukaguzi kule kule na Gharama yake unakua umeilipa kwenye CIF tofauti na zinazotoka mataifa mengine.

Mwisho

Uamuzi ni wa mteja husika kuamua gari yake anataka itokee kwenye soko la nchi gani. Kuna gari ambazo hazipatikani kwenye masoko ya Japan, hivyo unakua huna namna zaidi ya kuchukua kutoka hayo masoko mengine. Lakini pia hii haiondoshi ukweli kua gari zilizotengenezwa ulaya ni bora zaidi kuliko za Japan, hapo juu tumeelezea zaidi ubora wa soko la gari used na sio gari ikiwa mpya kabisa.
 
Asante Sana mkuu Kwa elimu Pana

Mimi nimeagiza Toyota rumion ya 2008 kupitia SBT Tanzania juzi tarehe 19/08 na baada ya kufanya malipo ya awali (CIF) nilitumiwa email Ile juzi na Jana pia nimepata email kutoka NBC bank kuwa pesa Yangu imeshatumwa

(2) pia nilitumiwa email ya SWIFT COPY nahisi kutoka BOT kuwa pesa imeshafika Kwenye account ya SBT Japan lakini mpaka mida hii bado sijapata mrejesho kutoka SBT Japan kama wamepata hela Yangu.

(3) customer care wa hapa DAR waliniambia kuwa nitapata email Yao kuanzia leo lkn bado ingawa sina mashaka na Hilo Ila ningependa kujuwa maana ya BILL OF LADING maana pale NBC bank nimeambiwa documents zikishafika nipele Copy ya hiyo bill kwaajili ya ushahidi juu ya pesa zinazotumwa nje

Asanteeee!!!
 
Back
Top Bottom