Spika Tulia: Tusichanganye Maadili ya Mtanzania na Imani za kidini. Lipi kosa la walimu waliosimamishwa kazi Kwa kucheza muziki? Warudisheni kazini

Sijawahi kuona mchaga mpumbavu kama huyu profesa. Yaani hajui hata taratibu ya kumfukuza mtumishi wa umma!!

Tanzania nchi yangu.
 
Kwa kosa la kupiga wimbo usio na maadili na wenye kuhamasisha ngono. Ni mjinga pekee anaweza kupiga wimbo wowote mahali popote. Mkuu wewe unaweza kupiga wimbo "Zagamua" mbele ya wanao?
Mkuu Acha waruhusu zipigwe tu
Wao si ndiyo wanataka hivyo
Asilimia kubwa mitoto ya walalahoi
Ndiyo uimba miziki hiyo
Wao watoto zao sjui kama wanakatikaga mauno

Ova
 
Siyo kila kitu kinaitaji kufanyika uchunguzi. Hili la mziki linaitaji uchunguzi gani? Huyu Prof. hafai kabisa kuwa waziri, kama maamuzi yake ni ya hovyo kiasi hicho. Wimbo huo unachezwa na kuimbwa kila pahala ikiwemo mikutano ya CCM. Yeye kama waziri kwanini hajawai kuchukuwa hatua ya kufungia wimbo huo?. Si maadili mtoto akiusikia huo wimbo shuleni, lakini akiusikiliza sehemu nyingine hayo maadili ubadilika? Prof. Kawaonea hawa walimu....ana sababu zake zaidi ya maadili.
 
Wadau wengi humu wanaotetea huu upuz ni wajinga,nahisi wanafurahia
Watoto zao kukatika mauno na wakiwapima bkr zote washatolewa
Acha waendelee kusikiliza miziki hiyo
Tu

Watoto wa viongozi wao wanalelewa kwenye mfumo mzuri,huwezi sikia mtoto anasikiliza na kumfatilia zchu
Au asikilize mziki ameyatimba

Lakini ndiyo hivyo,shauri zaooo
Ni kuachana nao Acha waendelee
Kukatika mauno ngonongono
Na mpaka 2030 vitoto vitakuwa vimechakaqq

Ova
 
Hawa walimu ingekuwa mimi ningewafukuza kabisa kazi. Ningekuwa tayari kupoteza uwaziri kwa sababu yao
Utakuwa umekurupuka kama waziri husika...yaani wimbo iruhusiwe na BASATA bila kusema wimbo zipi zichezwe wapi alafu unakuja kuwafukuza walimu.
 
uwe unaandika taarifa sahihi, wale walimu hawakuondolewa kazini ila walishushwa vyeo maana walikuwa walimu wakuu. Hata hivyo bunge kupitia spika ilisema km kweli hawakuwepo kwenye vituo vyao vya kazi wakati ule muziki unachezwa ndio warudishiwe vyeo vyao. Km walikuwepo shuleni basi adhabu ya kushushwa vyeo ni sahihi na iendelee yaani wabaki walimu wa kawaida na siyo walimu wakuu. Kaa tulia kijana unawahi wapi mwisho unakuja kupotosha watanzania.
 
Kulalamika kwa wazazi hakuwezi kumfanya Waziri afanye maamuzi ya hovyo. Kinacho ongelewa hapa ni mziki usiokuwa na maadili uliopigwa na kuchezwa shuleni. Yeye kama waziri tena wa elimu, ameshidwa nini kuupiga burn huo wimbo? Watoto tunaishi nao kwenye jamii, waziri atuthibitishie kama kweli hao watoto hawajawai kuusikia na au kuucheza huo wimbo uko mitaani.
 
Wanawalea kwa nidhamu ili waje kuwaongoza watoto wanaokata viuno shuleni kwenye vumbi. Watoto wa darasa la nne tayari akili ipo kingonongono, Waziri akisimama kulinda maadili wanamuita mjinga.
 
Amma? ... lakini maudhui ya kawimbo mbona yanafungamanafungamana na uhabarishaji!!!?
... INA MAANA KWELI MWANA KAPONA? 😅
Zamani ilikuwa ni wizara moja Wizara ya Habari,Utamaduni na michezo ila wakazitengenisha wakapata wizara mbili ya kwanza ikawa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambayo Waziri ndo nape na
Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo ambayo waziri wake ni Proff Ndumbaro na naibu ni mwanaFA
 
hivi hata taarifa za kiswahili hamuwezi kuelewa, hakuna mwalimu aliyefukuzwa kazi, ni kwamba walishushwa vyeo wale waliokuwa walimu wakuu wa zile shule 2. Bunge kupitia spika limesema km wale walimu wakuu walikuwepo shuleni wakati watoto wanachezeshwa ule muziki basi adhabu ya kushushwa vyeo ni sahihi. Hata hivyo spika akaongezea kuwa yeye ana taarifa ya ziada kutoka vyanzo vingine ya kuwa wale walimu wakuu hawakuwa shuleni wakati wa lile tukio. Akasema km hivyo ndivyo basi warudishiwe vyeo vyao bila kuwataka kukata rufaa kwa mamlaka yao ya nidhamu ambayo ni mkurugrnzi mtendaji wa Halmashauri husika
 
Siyo kila nyimbo inapigwa kila mahali, watoto wanapaswa kufundishwa maadili mema, Maudhui ya ile nyimbo yanafaa watu walioko kwenye ma-bar na magenge mengine ya wahuni
Haka kama mama kima ni ka-hovyo sana. Mbona kenyewe hakafuati taratibi sehemu nyingi tu. Kanataka ku-lecture watu kufuata taratibi wakati kenyewe ndiyo ibilisi mkubwa wa kuvunja taratibu?
 
Ok sawa
 
Kuna sehemu umeona nimeandika kufukuzwa kazi mkuu Au wewe ndo umekuja na perception zako kichwani..
Taarifa ni kwamba wamevuliwa vyeo wakati huo huo wamesimamishwa kupisha uchunguzi
 
Naona mambo mengi muhimu zaidi ya bunge kuongelea kwenye ripoti ya CAG, kuliko hii issue ndogo, au ni mimi sielewi??!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…