Suala la Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na Vipengele kadhaa vya Kisheria

Suala la Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na Vipengele kadhaa vya Kisheria

Nyani Ngabu.
The issue is not about "shall be eligible", that is not a problem at all because eligibility does not imply "A must get something"

The Place where Magufuli made a mistake is in violating the following subsection:

View attachment 1254046

That I may agree with.

Ila kwa wale walioleta mambo ya shall be eligible kuwa kwamba ni lazima na hakuna jinsi, sikubaliani nao.

Shall be eligible for renewal doesn’t mean shall be renewed. Period.
 
Kuna vipengele vipya vinajadiliwa vinasema kumuondoa baada ya miaka mitano kufuate process kama ya impeachment.

Inaonekana Magufuli hajaifuata process hiyo, na hapo ndipo anaweza kuwa kavunja katiba.

Profesa Shivji katweet kuhusu hii process.

Maandiko yangu ya awali hayakuwa informed kuhusu hiki kipengele.

Thanks @MissileofTheNation
Mkuu Kiranga,hapa umeonyesha uungwana wa hali ya juu. Pongezi kwako.
 
Sikubaliani na lugha iliyotumika kwenye hiyo sec 3.

Haipo definitive. Hakuna haja ya kuandika shall be eligible.

Andika tu ‘shall be renewed’ na hakuna ubishi.

umeona maneno "... and any decision not to renew his service shall follow the same procedure as that contained in article 144(3) of the constitution..."

Umeiona hiyo part?
 
umeona maneno "... and any decision not to renew his service shall follow the same procedure as that contained in article 144(3) of the constitution..."

Umeiona hiyo part?

Nimeona.

Sina tatizo na hiyo lugha hapo.

Mimi tatizo langu lilikuwa ni kwenye ‘shall be eligible’.

Hilo umekubali kuwa si ishu na kwamba hiyo lugha hailazimishi uteuzi tena.

Kama Magufuli hakufuata taratibu, basi kakosea.
 
That I may agree with.

Ila kwa wale walioleta mambo ya shall be eligible kuwa kwamba ni lazima na hakuna jinsi, sikubaliani nao.

Shall be eligible for renewal doesn’t mean shall be renewed. Period.

yah you are right

Mimi na Kiranga huko mwanzoni tulikuwa na mawazo kama yako kabisa kuhusiana na issue ya "shall be eligible". kwamba that is a non issue at all

Ila tukabadiri mawazo kuhusu uhalali wa uteuzi mpya baada ya kuona kifungu cha sheria kinachosema kuwa kama Raisi hataki kumuongezea CAG mkataba wa miaka mingine mitano basi lazima afuate ibara ya 144(3) yenye masharti magumu ya kumtoa CAG
 
Ila kuna vifungu vingine vya katiba vinavyomtaka Magufuli kuunda impeachment tribunal ili kumuondoa CAG ambaye hajafikisha umri wa kuondoka na wala hana maradhi ya kumfanya asiweze kazi yake.

Hivyo ndivyo vifungu vya katiba alivyovunja Magufuli.
Magufuli hajavunja kifungu chochote cha katiba.

Wanachoshindwa kuelewa watu wengi ni gist ya Ibara ya 144, ambayo lengo lake ni kuweka utaratibu wa kumuondoa CAG ndani ya muda wake alioteuliwa wa miaka mitano.

Katiba linapokuja swal la tenure of office of CAG ipo silent.

Office of CAG ni zao la sheria ya Bunge ambayo ni THE PUBLIC AUDIT ACT,2008, hii ndio imeestablish office of CAG baada ya Constitution kuitambua, hivyo basi kwakua kuna parent ACT inayo establish hiyo office linapokuja swala la tenure ya office of CAG lazima turely na provisions za hiyo parent act.

Sasa parent act kwa office ya CAG imeset time limit ya five years na renewal of another one term only , hivyo kama akifaninkiwa kuwa na term nyingine hapaswi kuzidi ten years,

Kama kusudio la sheria ni kwa CAG Kuserve kwa muda wa miaka kumi ilishindikana nini kusema hivyo katika hicho kipengele. Ili kuondoa utata sheria imgesema wazi kabisa kuwa tenure yake ni two terms of five years each,lkini sheria haijasema hivyo, kilichopo ni fixed period of five years .

Wnachoshn dwa kuelewa hapa hawa watu ni kuwa CAG was not removed from office, his tenure expired thus he was replaced.

Linapokuja swala la replacement sasa huko Ibara ya 144 haihusiki, ila kamma ni rem oval basi section 7 y Public Audit Act, na Ibara ya 144 vinahusika.
 
Kwa mujibu wa Sheria ya Ukaguzi ya Taifa Na. 11 ya Mwaka 2008 kifungu cha 6(1) "basic tenure" ya CAG ni miaka mitano na sheria inasema anaweza (Shall) kutumikia vipindi viwili vya miaka mingine mitano.

CAG anaulinzi mkubwa kisheria na moja ya ulinzi wake ni kuwa akiwa katikati ya tenure yake hawezi kuondolewa hivi hivi bila masharti kadhaa kufuatwa, lazima utumie masharti ya Ibara ya 144(3) ya Katiba au yeye mwenyewe achukue hatua under subsestion 2 ya hiyo Sheria ya Ukaguzi niliyoitaja hapo juu. Lakini kwa ujumla anaweza kuondolewa, si ngumu. Nitaeleza.

View attachment 1253918

Matumizi ya neno "Shall" lililotumika katika Sheria ya Ukaguzi kwenye kifungu cha 6 .

Kwa heshima na taadhima, Sheria hapo haijakusudia ulazima na ndio maana sheria haifasiriwi kwa matakwa ya mtu bali sheria zenyewe zinavyokusudia kufasiriwa katika muktadha wa jambo husika na lengo la mtunga sheria.

Katika muradi wa sheria na taratibu za kiutawala (admimistrative law point of view) sheria zinajulikana kuwa zitajitafsiri zenyewe na msingi unaokubalika ni kuwa kila ambapo tenure inapomalizika na kuwepo kwa kanuni ya kuongezewa tena kipindi cha pili neno "Shall" halina maana kama ilivyo katika Sheria ya Kufasiri Sheria (The Interpretation of Laws Act), hapa maana huwa ya kimazingira zaidi (contextual meaning) na haiwi LAZIMA bali INAWEZA.

Na moja kwa moja ni kuwa kuongezewa kipindi cha pili Mtendaji yeyote mwenye vipindi viwili na hata Rais mwenyewe sio "automatic" lazima kuwe "subject to good performance."

Na anayeamua akuongezee tenure ya pili, hiyo sheria haijambana, ni yule yule mwenye mamlaka ya kuteua na kukutengua.

Rais anapewa mamlaka hayo kwa CAG na watendaji wengine Serikali aliowateua kwa sheria yoyote kwa mamlaka aliuonayo katika Ibara ya 36. Tena 36(3) ndio inampa mamlaka ya jumla zaidi ya kudeal na tatizo lolote kwa nia ya kuweka utulivu katika utumishi kwa kuweza kumtengua mtu yeyote aliyemteua.

View attachment 1253920

Ukifasiri neno "shall" katika Sheria ya Ukaguzi ili kumtetea CAG Assad kwamba ilikuwa lazima aendelee miaka mitano ya pili ni kuleta dhahama kubwa nchini inayoweza kushawishi hata Uchaguzi Mkuu wa Mwakani usifanyike. Najua utashangaa!!!

Ndio, tafsiri ya Zitto na wenzake ni ya hatari zaidi kwa nchi kwani ukisoma Ibara ya 40 ya Katiba inapozungumzia Rais aliyeko madarakani kwa kipindi cha miaka mitano ya mwanzo kuwa anaweza kuchaguliwa tena kwa miaka mingine mitano ya pili na ya mwisho neno lililotumika ni "shall."
View attachment 1253921


Kama tafsiri SISISI na "#shallow" ya ACT ni ya kufuatwa basi kwa muktadha wa neno "Shall" pia katika Ibara ya 40 ya Katiba, Rais Magufuli naye mwakani hakuna haja ya kupimwa utendaji wake kwa kurudi katika sanduku la kura, aendelee tu, kusiwe na uchaguzi, aapishwe moja kwa moja kuendelea na Urais maana "shall" ina maana ya LAZIMA.

Lakini hapana, muradi wa "shall" katika masuala ya utawala sio kama inavyotumika katika sheria za kawaida, hapa bado dhana ya mhusika kuwa "subjected to good performance" kwa kutazamwa utendaji wake kama unaridhisha mamlaka ya uteuzi (kwa kesi ya CAG) na kwa kurudi kuomba kura tena kwa wananchi (kwa kesi ya Rais) ndio utaratibu kabla ya kulamba awamu ya pili.

Kitaalamu ni kuwa CAG aliyemaliza muda wake hakuonewa na kama ni kuonewa au aliyemteua ana nia mbaya angeweza kuondolewa hata kabla hajamaliza miaka hii mitano.

Ibara ya 144(2) inampa madaraka Rais kumuondoa CAG kwa sababu ya utendaji mbovu, maradhi au sababu nyingine yoyote.

View attachment 1253922

Nimeona wengi wanasema Rais hawezi kufanya hivyo mpaka aunde Tume, si kweli. Watanzania tuachane na kasumba ya kutosoma kwa umakini.

Tuzisome sheria vyema na tunaposhindwa kuelewa tuwatafute wataalamu sio wanasiasa.

Katika Ibara ya 144(3) Rais ataunda Tume (If) kwa maana ya "kama" ataona kuchunguza sababu hizo za kumuondoa CAG kunafaa kuchunguzwa. Maana yake akijiridhisha hana haja ya kuunds Tume.

View attachment 1253923

Kisheria na Kikatiba, namsifu sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk Magufuli na wataalamu wake wa sheria, hakika ni wabobezi, wanazisoma sheria zetu kwa utulivu na kuzifasiri kwa mujibu wa viapo vyao.

Naamini Rais Mhe. Dk Magufuli hakuwa na jambo baya la kutaka kumfukuza CAG isipokuwa "subject to good performance" anahitaji kasi zaidi katika eneo hilo na utulivu zaidi na kuaminika zaidi kwa kiongozi wa muhimili huo ambako Assad alishafeli kwa kufikia hatua ya kugombana na mhimili wa Bunge.

Kwa uchambuzi huu kudai Rais kavunja Sheria ni uchochezi mkubwa usiofaa kufumbiwa macho.


/chanzo Wakili wa Kujitegemea fb
Mkuu wazo kuu asante ila nina swali kidogo. Unaposema hata BILA uchunguzi Rais anaweza kumuondoa CAG tueleweshane kidogo. Kifungu cha sheria hapo juu kinasema "and shall not be so removed except in accordance with the provisions of sub-article 4 of this article. Huoni hapo rais analazimishwa kufata taratibu za sub-article 4. Tueleweshane tafadhali
 
yah you are right

Mimi na Kiranga huko mwanzoni tulikuwa na mawazo kama yako kabisa kuhusiana na issue ya "shall be eligible".

Pamoja na hizo taarifa ‘mpya’, msimamo wangu kuhusu ‘shall be eligible for renewal’ haujabadilika.

Shall be eligible for renewal siyo sawa na shall be renewed.

Walioleta hapa hicho kipengele hawakuelewa maana yake.

Kwa hiyo hapo bado nasimamia kuwa nipo sahihi.

Ila tukabadiri mawazo baada ya kuona kifungu cha sheria kinachosema kuwa kama Raisi hataki kumuongezea CAG mkataba wa miaka mingine mitano basi lazima afuate ibara ya 144(3) yenye masharti magumu ya kumtoa CAG

Kama Rais hakufuata utaratibu kama inavyotakiwa, basi atakuwa kakiuka sheria.

Mwanzoni watu walitumia zaidi hisia na ndo maana wakaleta vifungu ambavyo sivyo, kama hicho cha shall be eligible nk.

Lakini pia, je, tunajua kwa uhakika kuwa rais hajafuata utaratibu unaotakiwa au tunasadiki tu?

Ni nini kinachofanya watu waseme kuwa rais hajafuata utaratibu unaotakiwa?
 
Nina imani kabla ya kuandaa uzi huu, ulipitia uzi huu kwanza.
Hasa kipengele hiki
Mkuu JITEGEMEE, ndo nimepitia baada ya wewe kuniwekea hiyo post lakini kama zilivyo posts zingine, naona mkazo umewekwa kwenye neno SHALL!

Hapa ningependa kurudia tena na tena... hakuna anayetafsiri matumizi ya neno SHALL bali neno hilo limetafsiriwa na LAW INTERPRETATION ACT Ibara ya 53(2) kwamba:-
Where in a written law the word "shall" is used in conferring a function, such word shall be interpreted to mean that the function so conferred must be performed.
Sasa haya madai yenu ya mara kwa mara kwamba "tafsiri yetu" mnayatoa wapi?!

Maelezo yangu YOOOTE yamejikita kwa kuangalia vifungu vya sheria yetu wenyewe, na wala sikufanya reference kama vile inavyosema Translegal kwamba:-
(MODAL VERB) when drafting a legal document, the term shall is used to indicate that something must be done, as opposed to the term may which simply means that something is allowed (ie that it can be done, but does not have to be done)

Au kama wanavyosema USLEGAL kwamba:-Shall Law and Legal Definition:-
The word ‘Shall’ has the following meanings: An imperative command; has a duty to or is required to. For example, the notice shall be sent within 30 days. Usually ‘shall’ used here is in the mandatory sense.


Pasipo na interpretation ya kisheria ya neno SHALL always panaleta mkanganyiko lakini sisi tayari tunayo interpretation! Ni kutokana na huo mkanganyiko, ndo maana hata katika sheria za Marekani na nchi zingine wana-drop hilo neno SHALL kwa sababu ni confusing!

Wakati kwenye law schools inafundishwa SHALL ni SHURUTI, kwenye matumizi ya kawaida SHALL sio shuruti! Ni kutokana na huo mkanganyiko ndio maana wenzetu wana-replace neno SHALL na MUST lakini sisi hatujafanya hivyo, na kwahiyo inabaki kama tafsiri yetu kisheria inavyosema kwamba:-
Where in a written law the word "shall" is used in conferring a function, such word shall be interpreted to mean that the function so conferred must be performed.
Kama sio SHURUTI, our Interpretation Law Act Ibara ya 53(1) inakuambia neno linalotumika ni MAY:-
Where in a written law the word "may" is used in conferring a power, such word shall be interpreted to imply that the power so conferred may be exercised or not, at discretion.

SHALL2.png


AGAIN, hiyo sio "tafsiri yetu" bali ndiyo tafsiri ya kisheria!
 
Magufuli hajavunja kifungu chochote cha katiba.

Wanachoshindwa kuelewa watu wengi ni gist ya Ibara ya 144, ambayo lengo lake ni kuweka utaratibu wa kumuondoa CAG ndani ya muda wake alioteuliwa wa miaka mitano.

Katiba linapokuja swal la tenure of office of CAG ipo silent.

Office of CAG ni zao la sheria ya Bunge ambayo ni THE PUBLIC AUDIT ACT,2008, hii ndio imeestablish office of CAG baada ya Constitution kuitambua, hivyo basi kwakua kuna parent ACT inayo establish hiyo office linapokuja swala la tenure ya office of CAG lazima turely na provisions za hiyo parent act.

Sasa parent act kwa office ya CAG imeset time limit ya five years na renewal of another one term only , hivyo kama akifaninkiwa kuwa na term nyingine hapaswi kuzidi ten years,

Kama kusudio la sheria ni kwa CAG Kuserve kwa muda wa miaka kumi ilishindikana nini kusema hivyo katika hicho kipengele. Ili kuondoa utata sheria imgesema wazi kabisa kuwa tenure yake ni two terms of five years each,lkini sheria haijasema hivyo, kilichopo ni fixed period of five years .

Wnachoshn dwa kuelewa hapa hawa watu ni kuwa CAG was not removed from office, his tenure expired thus he was replaced.

Linapokuja swala la replacement sasa huko Ibara ya 144 haihusiki, ila kamma ni rem oval basi section 7 y Public Audit Act, na Ibara ya 144 vinahusika.

Halafu, ni kweli Rais hajafuata taratibu au tunasadiki tu kuwa hajafuata taratibu?
 
Mjadala mtamu sana,nimejifunza kitu humu kuwa Watanzania wengi ( hapa naomba niongeze msisitizo "wengi wanaoonekana kuwa ni wasomi" si watu wanaopenda kusoma mara mbili mbili na kuelewa kile walichokisoma) .
Watu wanakurupuka sana.
 
Chige mhenga mwenzangu hongera kwa kusimamia unachokiamini kuwa ni sahihi na kutupa darasa. Kiranga, Nyani Ngabu na wengineo nao pia nawapa heko kwa kutoa somo.
Hii ndio JF ya "Jambo Forum" ninayoikosa.
 
Pamoja na hizo taarifa ‘mpya’, msimamo wangu kuhusu ‘shall be eligible for renewal’ haujabadilika.

Shall be eligible for renewal siyo sawa na shall be renewed.

Walioleta hapa hicho kipengele hawakuelewa maana yake.

Kwa hiyo hapo bado nasimamia kuwa nipo sahihi.



Kama Rais hakufuata utaratibu kama inavyotakiwa, basi atakuwa kakiuka sheria.

Mwanzoni watu walitumia zaidi hisia na ndo maana wakaleta vifungu ambavyo sivyo, kama hicho cha shall be eligible nk.

Lakini pia, je, tunajua kwa uhakika kuwa rais hajatuata utaratibu unaotakiwa au tunasadiki tu?

Ni nini kinachofanya watu waseme kuwa rais hajafuata utaratibu unaotakiwa?

Kwenye "Shall be eligible for renewal" kweli watu walifuata hisia, na nilipambana nao sana humu kuhusiana na hilo kwamba ni kutokana na wao kutoelewa lugha, maana Shall be Eligible inamaanisha Shall be Considered but kuwa Considered haimaanishi It must be you who get a job

lakini baadae nilipoona subsection 3 ya sheria inayosema "....kama hata renew mkataba wake basi sababu za kutorenew zifuate process ya ibara ya 144(3)", then nikatambua sasa kama alivyotambua profesa Shivji kuwa kama hakuna sababu za kumuondoa CAG kwa mujibu wa ibara 1443(3) basi Sheria inataka CAG atumikie mihula miwili.

KWA HIYO JPM amevunja Sheria, Uteuzi wake ni batili ila kwa Mujibu wa Udikteta atafanya naye kazi lakini kwa mujibu wa Sheria huyo CAG mpya ni Feki
 
Mkuu amevunja Katiba ya nchi na pia subsection 3 ya Public Audit Act 2008.Hili halina ubishi.Inasikitisha sana yaani kuona Sheria ya nchi inavunjwa kwa mambo nyeti kama haya.Huwa sina kawaida ya kumjadili Rais negatively,hata akifanya mambo yasiyonifurahisha i opt to keep quiet but hili la kuvunja Katiba hapana.Hatuwezi kulikalia kimya.Ni hatari na anajenga bad precedence.Taifa la watu milioni zaidi ya 50 tukijenga utamaduni wa kutothamini sheria za nchi,then kuna nchi tena hapo?Im dissapointed by him this time.Let me just log off.
 
Halafu, ni kweli Rais hajafuata taratibu au tunasadiki tu kuwa hajafuata taratibu?
Rais amefuata taratibu;

Maamuzi yake yametokana na tafsiri sahihi ya sheria.

Kwakuwa kaongozwa na sheria katika kufanya maamuzi, ni sahihi kusema kuwa amefuata taratibu.
 
Kwenye "Shall be eligible for renewal" kweli watu walifuata hisia, na nilipambana nao sana humu kuhusiana na hilo kwamba ni kutokana na wao kutoelewa lugha, maana Shall be Eligible inamaanisha Shall be Considered but kuwa Considered haimaanishi It must be you who get a job

lakini baadae nilipoona subsection 3 ya sheria inayosema "....kama hata renew mkataba wake basi sababu za kutorenew zifuate process ya ibara ya 144(3)", then nikatambua sasa kama alivyotambua profesa Shivji kuwa kama hakuna sababu za kumuondoa CAG kwa mujibu wa ibara 1443(3) basi Sheria inataka CAG atumikie mihula miwili.

KWA HIYO JPM amevunja Sheria, Uteuzi wake ni batili ila kwa Mujibu wa Udikteta atafanya naye kazi lakini kwa mujibu wa Sheria huyo CAG mpya ni Feki

Kama sheria inataka CAG atumikie mihula miwili, kwa nini isiseme tu moja kwa moja kuwa hivyo ndivyo itavyokuwa?

Kwanza, kwa nini kuwepo hata na mihula miwili?

Kwa nini term isiwe fixed for 10years?

Sikubaliani na tafsiri ya Shivji.

And yes, I can disagree with him.
 
Well, kama ni hivyo basi Assad aende mahakamani.

Manake kama ni dhahiri namna hiyo kama ulivyowasilisha, the whole thing should be a slam dunk open-and-shut case.

Pia nimeona kuna tatizo kubwa sana la uelewa wa lugha ya Kiingereza.

Suala la ‘shall be eligible for renewal’ ni suala jepesi sana lisilohitaji hata mabishano.

Ila sasa sishangai kwa nini hata baadhi ya watu walikuwa wana cite hicho kipengele kuwa ndiyo kimevunjwa!
Mkuu siyo ishu ya Assad kwenda mahakamani. Ni issue ya kwamba tuna Rais mvunja katiba
 
Mkuu amevunja Katiba ya nchi na pia subsection 3 ya Public Audit Act 2008.Hili halina ubishi.Inasikitisha sana yaani kuona Sheria ya nchi inavunjwa kwa mambo nyeti kama haya.Huwa sina kawaida ya kumjadili Rais negatively,hata akifanya mambo yasiyonifurahisha i opt to keep quiet but hili la kuvunja Katiba hapana.Hatuwezi kulikalia kimya.Ni hatari na anajenga bad precedence.Taifa la watu milioni zaidi ya 50 tukijenga utamaduni wa kutothamini sheria za nchi,then kuna nchi tena hapo?Im dissapointed by him this time.Let me just log off.
Hakuna Subsection 3 ya section 6 of the Public Audit Act,2008.
 
Back
Top Bottom