Swali kwa Ayubu Rioba: Siku hizi sera ya Taifa inaruhusu taasisi za kidini kunufaika na fedha za walipa kodi kupitia TBC?

Swali kwa Ayubu Rioba: Siku hizi sera ya Taifa inaruhusu taasisi za kidini kunufaika na fedha za walipa kodi kupitia TBC?

Taifa hili linakwenda kusherehekea miaka 60 ya uhuru desemba mwaka huu.

Sababu kubwa ya kuweza kudumu mpaka hapa lilipo ni uwezo wetu wa kuvumilia na kuishi kama ndugu, uwezo wa kujishusha.

Tungeendekeza akili kama za Huyu mleta mada siku nyingi zilizopita tungeshavunja hii nchi.

Tulifundishwa kuvumilia tangu tukiwa chekechea, kukaa Dawati moja mkristo na muislamu. Ukifika muda wa mkristo kwenda mafundisho anakwenda na muislam kwenda kusoma dini yake anakwenda.

Mawazo ya aina hii ndio yanayovunja nchi kama yakiachwa yaendelezwe pasipo kukemewa.
Umesema kweli sana.Huyu atakuwa sio mtanzania,karibia familia nyingi za kitanzania,wako nusu waislamu na nusu wakristo,na wanashirikiana kwenye misiba na furaha.
 
Msingi ya uwepo wa Taifa letu ni Mkutano wa Berlin wa mwaka 1884 hadi 1885 ambapo wakoloni mabeberu wa Ulaya walijigawia vipande vya maeno Africa na kuwa makoloni yao. Baada ya kuondoka Tulibaki na mataifa huru na dini pia ikiwemo ile iliyoletwa na waarabu waliokuwa wanafanya biashara ya utumwa.
Wewe bado una mawazo ya enzi za mawe za biashara ya utumwa.Biashara ya utumwa,hakuna kabila halikuwahi kutoshiriki biashara hii duniani,wapo pia waarabu waliuzwa utumwani.Na sisi waafrika,yapo makabila yaliuza pia wenzao utumwani,kwa kuwauzia wageni.Unafikiri mgeni aataweza kufanya biashara bila baraka ya mwenyeji?
 
Nyie wafia dini mna matatizo makubwa sana.
Hakuna anayejishughulisha na watu wa dini moja kushirikiana na dini nyingine. Kinachopingwa na taasisi za serikali kama TBC kuwa jukwaa dini YOYOTE.

Wewe Sheikh nenda Redio Maria au Sauti ya Injili kawaombe wakupe kipindi cha kaswida au mawaidha na hakuna mtu atakayejisumbua na huo ushirikianao.
Umesema kweli sana.Huyu atakuwa sio mtanzania,karibia familia nyingi za kitanzania,wako nusu waislamu na nusu wakristo,na wanashirikiana kwenye misiba na furaha.
 
Ni akili ya ajabu kutaka kumtenganisha,mwenye dini kutumia baadhi ya miundombinu ya walipa kodi,na kumuachia huyo huyo atumie miundombinu mengine ya walipa kodi,kwa kisingizio cha dini.Umzuie asutumie Tv ya Taifa,huku anatumia barabara,shule,vivuko,viwanja vya michezo,viwanja vya ndege,madaraja nk
 
Nyie wafia dini mna matatizo makubwa sana.
Hakuna anayejishughulisha na watu wa dini moja kushirikiana na dini nyingine. Kinachopingwa na taasisi za serikali kama TBC kuwa jukwaa dini YOYOTE.

Wewe Sheikh nenda Redio Maria au Sauti ya Injili kawaombe wakupe kipindi cha kaswida au mawaidha na hakuna mtu atakayejisumbua na huo ushirikianao.
Huwezi kumtenganisha mlipa kodi,na alichokilipia kodi,kwa kukitumia kwa njia yoyote iwayo,madhali hajavunja sheria.
 
Zingatia haya:

1. Taifa-mtu mmoja mmoja + ndoa + familia + ukoo + kabila

2. Lugha ya Taifa inatokana na lugha za kikabila.

3. Kwa hiyo, vipindi vya kikabila vinavyotumia lugha ya Taifa ruksa ktk TBC

Kumbuka:

4. Hata usajili wa Radio za FM zinazosikilizwa huko mikoani una kifungu kinakataza matumizi ya lugha za kibalia. Yaani, ni lazima zitumie lugha ya Taifa ktk programu zake.
Duh! haueleweki.

Hicho kiswahili mbona nacho kina maneno kibao tu kutoka kwenye lugha zengine hata maneno ya kiarabu yamo humo ,sasa nashindwa kukuelewa?

Halafu huwezi kuweka makabila ya watu ukatoa imani zao.
 
Taifa hili linakwenda kusherehekea miaka 60 ya uhuru desemba mwaka huu.

Sababu kubwa ya kuweza kudumu mpaka hapa lilipo ni uwezo wetu wa kuvumilia na kuishi kama ndugu, uwezo wa kujishusha.

Tungeendekeza akili kama za Huyu mleta mada siku nyingi zilizopita tungeshavunja hii nchi.

Tulifundishwa kuvumilia tangu tukiwa chekechea, kukaa Dawati moja mkristo na muislamu. Ukifika muda wa mkristo kwenda mafundisho anakwenda na muislam kwenda kusoma dini yake anakwenda.

Mawazo ya aina hii ndio yanayovunja nchi kama yakiachwa yaendelezwe pasipo kukemewa.
Sioni kama unaelewa maana ya tunu ya uvumilivu. Jisomee tena bandiko, sehemu inayojadili pingamizi na jawabu lake.
 
Duh! haueleweki.

Hicho kiswahili mbona nacho kina maneno kibao tu kutoka kwenye lugha zengine hata maneno ya kiarabu yamo humo ,sasa nashindwa kukuelewa?

Halafu huwezi kuweka makabila ya watu ukatoa imani zao.
Taifa ni kitu kimoja chenye vitu vingi ndani mwake.

Umoja wake unatokana na sifa mtambuka (universals)

Kitu kimoja kimoja ndani ya Taifa, mfano kabila lako, kinatambulishwa na sifa za kipekee (particulars)

Kabila lako linazo sifa za kipekee zipi? Ni hizi hapa: Lugha ya kikabila, mila, na desturi zenu.

Taifa la Tanzania ni kitu kimoja kwa sababu ya sifa gani Mtambuka? Hizi hapa: Lugha ya Taifa, akili, utashi, vinasaba vya kibinadamu, serikali moja inayosimamia sera, sheria na taasisi zisizofungamanisha masuala ya kidini, nk.

Taasisi mojawapo ni TBC.

Hapo vipi?

NImeeleweka!
 
View attachment 1792731
Dk. Ayub Chacha Rioba, Mkrugenzi Mtendaji wa TBC

Swali hapo juu linatokana na ufa kati ya yale nilioyoyaona leo na matarajio yangu kwa kuzingatia misingi ya kikatiba hapa Tanzania na kwingineko.

Niliyoyaona TBC1

Leo nimeona matukio mawili yasiyo ya kawaida kwenye luninga ya Taifa TBC1, inayoongozwa chini ya Ukurugenzi wa Dk. Ayub Rioba.

  1. Asubuhi kabla ya kipindi cha Bunge cha mswali na majibu TBC1 walirusha kipindi cha "Madrasa" kilichokuwa na ujumbe unaotembea kwa upande wa chini ukisomeka "Mashindano ya Kuhifadhi Kurani Tukufu kwa Waislamu Wanawake Yameandaliwa na Taasisi ya Kiislam ya African Relief Foundation."
  2. Mchana, mara tu baada ya matangazo ya Maadhimisho ya miaka 40 ya kuanzishwa kwa SADC, ambako Ayub Rioba alikuwa mwongozaji, kilifuata kipindi ncha swala ya Kiislamu.
Nafahamu pia kwamba, TBC1 imekuwa na kawaida ifuatayo:
  1. Kila alfajiri madhehebu ya dini tofauti hupewa muda wa kusoma sala ya asububi.
  2. Kila usiku wa kati, kabla ya saa sita, madhehebu ya dini tofauti hupewa muda wa kusoma sala ya kufunga siku.
  3. Kila Jumapili pia, madhehebu ya dini tofauti hupewa muda wa kusoma ibada za Jumapili.
Matarajio kwa mujibu wa Katiba

Lakini, matarajio yangu ni kwamba, kwa kuwa TBC ni mali inayoendeshwa kwa kodi ya umma chini ya usimamizi wa serikali isiyofungamana na dini yoyote, kama tunavyosoma kwenye katiba ya nchi, basi yafuatayo yanapaswa kuonekana:

  1. Programu zenye sura ya kitaifa katika ngazi ya maudhui
  2. Programu zenye sura ya kitaifa katika ngazi ya lugha
Hii maana yake ni kwamba, yafuatayo hayapaswi kuonekana:
  1. Programu zenye sura ya kisekta katika ngazi ya maudhui
  2. Programu zenye sura ya kisekta katika ngazi ya lugha

Pia, dini nyingi tayari zinavyo vyombo vyake vya habari kwa ajili ya kuendesha shughuli zake za kidini. Kanisa Katoliki wana Tumaini TV, KKKT wana Upendo TV, Waislam wana Iman TV, Wapagani wa "Ramli TV," nk

Nakumbuka kuwa, kwa sehemu kubwa, sala nyingi za madhehebu ya KiIslamu zinatumia lugha ya Kiarabu, jambo ambalo linakiuka sera ya kujenga umoja wa kitaifa kwa kutumia lugha ya Taifa.

Hata ibada kadhaa na litania nyingi za Kikristo zinasomwa kwa lugha ya Kilatini ambayo sio lugha ya Taifa.

Nakumbuka kuna wakati Kardinali pengo alikuwa anaitwa na wazee wetu wa kule Mwenge Parokiani, Dar es Salaam, ili akawaendeshee ibada kwa lugha ya Kilatini, kama walivyokuwa wamezoea zamani, kabla Kanisa Katoliki halijatunga sera ya kuendesha ibada kwa Kiswahili na kimila.

Kwa hiyo, katika mazingira ya sasa, yafuatayo ni matarajio yangu:

  1. Kanisa Katoliki waendeshe programu zao za kisekta kupitia Tumaini TV,
  2. KKKT waendeshe programu zao za kisekta kupitia Upendo TV,
  3. Waislam waendeshe programu zao za kisekta kupitia Iman TV,
  4. Wapagani waendesha programu zao za kisekta kupitia "Ramli TV," nk
Uhalisia wa mambo

Pamoja na matarajio haya, uhalisia wa mambo ni kwamba, matakwa ya Katiba ya Tanzania kuhusu umuhimu na ulazima wa kutenganisha dini na dola hayajatimia kama ifyatavyo:

  1. Kanisa Katoliki wanaendesha programu zao za kisekta kupitia TBC1,
  2. KKKT wanaendesha programu zao za kisekta kupitia TBC1,
  3. Waislam wanaendesha programu zao za kisekta kupitia TBC1,
  4. Shughuli za Bunge zinaanza kwa kusoma dua kwa "Mola",
  5. Viapo vya watumishi wa umma vinamaliziwa kwa maneno "Ewe Mwenyezi Mungu Nisaidie," wakati Katiba ya nchi haitambui neno "Mungu."
Kama Katiba ya nchi inayakataza mambo haya, kwa nini tunayatenda, kama ambavyo mfano wa TBC1 leo umeonyesha?

Ni muhimu swali hili lijibiwe ili tujichunguze kama vyombo vya habari vya kitaifa vinakweza maslahi ya vikundi kama vile taasisi za dini au vinatweza maslahi ya pamoja kama vile umoja wa kitaifa.

Napendekeza kwamba ni kosa kutumia kodi ya raia asiye na dini kuhudumia taasisi za kidini. Ni kama ambavyo ni kosa kutumia kodi ya mtu asiye na chama cha siasa kutoa ruzuku kwa chama cha siasa. Kuna tatizo hapo.

Angalizo la kisera

Nakumbusha kwamba, kote duniani, sera za kutenganisha dini na dola hugawanyika katika sehemu mbili:

  1. Sera zinazofuata mtindo wa Kimarekani.
  2. Sera zinazofuata mtindo wa KIjerumani.
Sera zinazofuata mtindo wa Kimarekani. Hapa, serikali huyapiga kisogo masuala yote ya dini, kiasi kwamba hakuna senti ya mlipa kodi inatumika kufadhili taasisi za kidini. Habari ya sijuo airtime kwa programu za kidini, sijui kufungua bunge kwa dua, hakuna.

Sera zinazofuata mtindo wa KIjerumani. Hapa, serikali haiyapigi kisogo masuala yote ya dini, kwani kuna senti fulani ya mlipa kodi inatumika kufadhili taasisi za kidini. Kwa mfano, huko Ujerumani, mfumo wa "TRA" yao unatumika kukusanya sadaka kutoka kwa waumini ambao ni waajiriwa, halafu sadaka hiyo inakabidhiwa kwa makanisa yaliyosajili waumini wao. Lakini, mfumo huu unabagua baadhi ya madhehebu ya kidini.

Mapendekezo

Hivyo basi, kwa kuwa Sera zinazotenganisha dini na dola kwa kufuata mtindo wa Kijerumani zina ubaguzi; na kwa kuwa sera zinazotenganisha dini na dola kwa kufuata mtindo wa Kimarekani hazina ubaguzi, napendekeza yafuatayo:

  1. Kwamba, programu zote za kidini, ambazo kwa sababu hiyo ni programu za kisekta ziondolewe katika TBC;
  2. Kwamba, programu zote za kidini, ambazo kwa sababu hiyo ni programu za kisekta ziendeshwe kupitia vituo binafsi vya madhehebu ya kidini;
  3. Kwamba, TBC ijielekeze katika programu zenye kujenga umoja wa kitaifa kwa kueneza lugha ya Taifa, na sio lugha nyinginezo;
  4. Kwamba, utaratibu wa kusoma dua mwanzoni mwa shughuli za Bunge ufutwe.
  5. Kwamba, Bunge litunge sheria inayotoa mwongozo rasmi kuhusu sera ya kutenganisha dini na dola hapa nchini Tanzania. Yaweza kuitwa "The Wall of Separation Between Religion and State Act."
Naomba kuwasilisha.
1. TBC ni chombo cha umma na kinachoendeshwa na fedha za walipakodi.
2. Walipakodi wa Tanzania ni waumini wa dini mbalimbali na wadau wa vyama mbalimbali vya siasa na pia wanatoka sekta rasmi na isiyo rasmi.
3. Kipindi chochote kinachowahusu Watanzania kisiasa, kiuchumi, kijamii na kiutamaduni (dini au imani ni sehemu ya utamaduni) kinaweza kurushwa na TBC kwa utaratibu usioweza kuleta manung'uniko kutoka kwa wadau wengine.
4. Kipindi chochote kinachowagawa Watanzania kwa namna yoyote ile hakipaswi kurushwa na TBC.
5. Vipindi ulivyovitaja kama havihusiani na No 4 havina shida kama vikirushwa na TBC maana wenye dini au imani hizo ni walipakodi pia na ni sehemu ya umma wa Watanzania.
 
View attachment 1792731
Dk. Ayub Chacha Rioba, Mkrugenzi Mtendaji wa TBC

Swali hapo juu linatokana na ufa kati ya yale nilioyoyaona leo na matarajio yangu kwa kuzingatia misingi ya kikatiba hapa Tanzania na kwingineko.

Niliyoyaona TBC1

Leo nimeona matukio mawili yasiyo ya kawaida kwenye luninga ya Taifa TBC1, inayoongozwa chini ya Ukurugenzi wa Dk. Ayub Rioba.

  1. Asubuhi kabla ya kipindi cha Bunge cha mswali na majibu TBC1 walirusha kipindi cha "Madrasa" kilichokuwa na ujumbe unaotembea kwa upande wa chini ukisomeka "Mashindano ya Kuhifadhi Kurani Tukufu kwa Waislamu Wanawake Yameandaliwa na Taasisi ya Kiislam ya African Relief Foundation."
  2. Mchana, mara tu baada ya matangazo ya Maadhimisho ya miaka 40 ya kuanzishwa kwa SADC, ambako Ayub Rioba alikuwa mwongozaji, kilifuata kipindi ncha swala ya Kiislamu.
Nafahamu pia kwamba, TBC1 imekuwa na kawaida ifuatayo:
  1. Kila alfajiri madhehebu ya dini tofauti hupewa muda wa kusoma sala ya asububi.
  2. Kila usiku wa kati, kabla ya saa sita, madhehebu ya dini tofauti hupewa muda wa kusoma sala ya kufunga siku.
  3. Kila Jumapili pia, madhehebu ya dini tofauti hupewa muda wa kusoma ibada za Jumapili.
Matarajio kwa mujibu wa Katiba

Lakini, matarajio yangu ni kwamba, kwa kuwa TBC ni mali inayoendeshwa kwa kodi ya umma chini ya usimamizi wa serikali isiyofungamana na dini yoyote, kama tunavyosoma kwenye katiba ya nchi, basi yafuatayo yanapaswa kuonekana:

  1. Programu zenye sura ya kitaifa katika ngazi ya maudhui
  2. Programu zenye sura ya kitaifa katika ngazi ya lugha
Hii maana yake ni kwamba, yafuatayo hayapaswi kuonekana:
  1. Programu zenye sura ya kisekta katika ngazi ya maudhui
  2. Programu zenye sura ya kisekta katika ngazi ya lugha

Pia, dini nyingi tayari zinavyo vyombo vyake vya habari kwa ajili ya kuendesha shughuli zake za kidini. Kanisa Katoliki wana Tumaini TV, KKKT wana Upendo TV, Waislam wana Iman TV, Wapagani wa "Ramli TV," nk

Nakumbuka kuwa, kwa sehemu kubwa, sala nyingi za madhehebu ya KiIslamu zinatumia lugha ya Kiarabu, jambo ambalo linakiuka sera ya kujenga umoja wa kitaifa kwa kutumia lugha ya Taifa.

Hata ibada kadhaa na litania nyingi za Kikristo zinasomwa kwa lugha ya Kilatini ambayo sio lugha ya Taifa.

Nakumbuka kuna wakati Kardinali pengo alikuwa anaitwa na wazee wetu wa kule Mwenge Parokiani, Dar es Salaam, ili akawaendeshee ibada kwa lugha ya Kilatini, kama walivyokuwa wamezoea zamani, kabla Kanisa Katoliki halijatunga sera ya kuendesha ibada kwa Kiswahili na kimila.

Kwa hiyo, katika mazingira ya sasa, yafuatayo ni matarajio yangu:

  1. Kanisa Katoliki waendeshe programu zao za kisekta kupitia Tumaini TV,
  2. KKKT waendeshe programu zao za kisekta kupitia Upendo TV,
  3. Waislam waendeshe programu zao za kisekta kupitia Iman TV,
  4. Wapagani waendesha programu zao za kisekta kupitia "Ramli TV," nk
Uhalisia wa mambo

Pamoja na matarajio haya, uhalisia wa mambo ni kwamba, matakwa ya Katiba ya Tanzania kuhusu umuhimu na ulazima wa kutenganisha dini na dola hayajatimia kama ifyatavyo:

  1. Kanisa Katoliki wanaendesha programu zao za kisekta kupitia TBC1,
  2. KKKT wanaendesha programu zao za kisekta kupitia TBC1,
  3. Waislam wanaendesha programu zao za kisekta kupitia TBC1,
  4. Shughuli za Bunge zinaanza kwa kusoma dua kwa "Mola",
  5. Viapo vya watumishi wa umma vinamaliziwa kwa maneno "Ewe Mwenyezi Mungu Nisaidie," wakati Katiba ya nchi haitambui neno "Mungu."
Kama Katiba ya nchi inayakataza mambo haya, kwa nini tunayatenda, kama ambavyo mfano wa TBC1 leo umeonyesha?

Ni muhimu swali hili lijibiwe ili tujichunguze kama vyombo vya habari vya kitaifa vinakweza maslahi ya vikundi kama vile taasisi za dini au vinatweza maslahi ya pamoja kama vile umoja wa kitaifa.

Napendekeza kwamba ni kosa kutumia kodi ya raia asiye na dini kuhudumia taasisi za kidini. Ni kama ambavyo ni kosa kutumia kodi ya mtu asiye na chama cha siasa kutoa ruzuku kwa chama cha siasa. Kuna tatizo hapo.

Angalizo la kisera

Nakumbusha kwamba, kote duniani, sera za kutenganisha dini na dola hugawanyika katika sehemu mbili:

  1. Sera zinazofuata mtindo wa Kimarekani.
  2. Sera zinazofuata mtindo wa KIjerumani.
Sera zinazofuata mtindo wa Kimarekani. Hapa, serikali huyapiga kisogo masuala yote ya dini, kiasi kwamba hakuna senti ya mlipa kodi inatumika kufadhili taasisi za kidini. Habari ya sijuo airtime kwa programu za kidini, sijui kufungua bunge kwa dua, hakuna.

Sera zinazofuata mtindo wa KIjerumani. Hapa, serikali haiyapigi kisogo masuala yote ya dini, kwani kuna senti fulani ya mlipa kodi inatumika kufadhili taasisi za kidini. Kwa mfano, huko Ujerumani, mfumo wa "TRA" yao unatumika kukusanya sadaka kutoka kwa waumini ambao ni waajiriwa, halafu sadaka hiyo inakabidhiwa kwa makanisa yaliyosajili waumini wao. Lakini, mfumo huu unabagua baadhi ya madhehebu ya kidini.

Mapendekezo

Hivyo basi, kwa kuwa Sera zinazotenganisha dini na dola kwa kufuata mtindo wa Kijerumani zina ubaguzi; na kwa kuwa sera zinazotenganisha dini na dola kwa kufuata mtindo wa Kimarekani hazina ubaguzi, napendekeza yafuatayo:

  1. Kwamba, programu zote za kidini, ambazo kwa sababu hiyo ni programu za kisekta ziondolewe katika TBC;
  2. Kwamba, programu zote za kidini, ambazo kwa sababu hiyo ni programu za kisekta ziendeshwe kupitia vituo binafsi vya madhehebu ya kidini;
  3. Kwamba, TBC ijielekeze katika programu zenye kujenga umoja wa kitaifa kwa kueneza lugha ya Taifa, na sio lugha nyinginezo;
  4. Kwamba, utaratibu wa kusoma dua mwanzoni mwa shughuli za Bunge ufutwe.
  5. Kwamba, Bunge litunge sheria inayotoa mwongozo rasmi kuhusu sera ya kutenganisha dini na dola hapa nchini Tanzania. Yaweza kuitwa "The Wall of Separation Between Religion and State Act."
Naomba kuwasilisha.
Hiyo TBC umeijua leo kuhusu kujipendekeza?
Walakini nakuona wewe ni wale wenye wenye udini udini kwenye mbongo zao.
Kama wewe ni mkristo basi unapaswa kujua Kuwa UKRISTO unatangaza UPENDO na MSAMAHA.
 
3. Kipindi chochote kinachowahusu Watanzania kisiasa, kiuchumi, kijamii na kiutamaduni (dini au imani ni sehemu ya utamaduni) kinaweza kurushwa na TBC kwa utaratibu usioweza kuleta manung'uniko kutoka kwa wadau wengine.
Maneno "dini au imani ni sehemu ya utamaduni" yana utata.

Dini unayoitaja ni sehemu ya utamaduni wa kabila au ni sehemu ya utamaduni wa Taifa?

Tanzania tuna utamaduni wa kitaifa.

Lakini, Tanzania hatuna dini ya kabila.

Pia, Tanzania hatuna dini yaTaifa.

Kwa hiyo, hoja yako hapo juu unapata ubutu mkubwa, na kimsingi inakufa.

Irekebishe.
 
Taifa ni kitu kimoja chenye vitu vingi ndani mwake.

Umoja wake unatokana na sifa mtambuka (universals)

Kitu kimoja kimoja ndani ya Taifa, mfano kabila lako, kinatambulishwa na sifa za kipekee (particulars)

Kabila lako linazo sifa za kipekee zipi? Ni hizi hapa: Lugha ya kikabila, mila, na desturi zenu.

Taifa la Tanzania ni kitu kimoja kwa sababu ya sifa gani Mtambuka? Hizi hapa: Lugha ya Taifa, akili, utashi, vinasaba vya kibinadamu, serikali moja inayosimamia sera, sheria na taasisi zisizofungamanisha masuala ya kidini, nk.

Taasisi mojawapo ni TBC.

Hapo vipi?

NImeeleweka!
Sasa lugha ya taifa ambayo ina maneno ndani yake na mengi kutoka lugha za mataifa mengine hili unalizungumziaje?

Na yapi ni mavazi yetu kama taifa la Tanzania?
 
Ni akili ya ajabu kutaka kumtenganisha,mwenye dini kutumia baadhi ya miundombinu ya walipa kodi,na kumuachia huyo huyo atumie miundombinu mengine ya walipa kodi,kwa kisingizio cha dini.Umzuie asutumie Tv ya Taifa,huku anatumia barabara,shule,vivuko,viwanja vya michezo,viwanja vya ndege,madaraja nk
Hoja yako iko hivi:

  1. Kila mlipa kodi anayo haki ya kutumia miundimbinu ya walipa kodi kama vile barabara, shule, vivuko, viwanja vya michezo, viwanja vya ndege, madaraja, vyombo vya habari kama vile TBC, nk, endapo hiyo ni miundombinu ya umma;
  2. Vyombo vya habari kama vile TBC ni sehemu ya miundombinu ya umma
  3. Kwa hiyo, kumzuia mwenye dini kutumia TBC ambayo ni sehemu ya miundombinu ya walipa kodi na kumuachia atumie miundombinu mengine ni undumilakuwili.
Hoja yako ina tatizo moja. Hujasema huyo mlipa kodi anaruhusiwa kutumia miundimbinu hiyo kwa ajili gani.

Miundombinu ya umma ni maslahi ya pamoja. Muumini akipita katika barabara kwenda kwenye eneo lake la kusalia sawa.

Lakini akitumia barabara kama kituo cha sala ni kosa, maana anawakwaza wasioamini naye, kwa kuwazuia kuendelea na ratiba zao.
 
Sasa lugha ya taifa ambayo ina maneno ndani yake na mengi kutoka lugha za mataifa mengine hili unalizungumziaje?

Na yapi ni mavazi yetu kama taifa la Tanzania?
Lugha ya Taifa ni mali ya Taifa.

Neno la Kiingereza au Kiarabu likikopwa na kutoholewa linaanguka katika lugha mpya.

Mfano neno shirt limekopwa na kutoholewa likawa shati.

Hili sio neno la Kiingereza tena.

Ni Kiswahili.

Ni vivyo hivyo kwa mavazi.
 
Nawachukia wakristo kwa sababu wanajali dini yao kuliko watu, wamejaa unafiki. Akitawala mkristo hata akiua wanakaa kimya, watu wakipotea wanakaa kimya. Lakini mama ametufanya tutabasamu nyinyi mnanuna, alafu wanatulazimisha tusiyaone mema anayotutendea bali tumtazame kama muislamu na hivyo kumchukia yeye na mema yake.
 
Kumbe tatizo ni maandishi yaliyoandikwa chini ya TV screen eti

"MASHINDANO YA TAIFA YA QURAAN"
Mashindano ya taifa hiyo ndo nyuzi yenyewe, TV ya taifa ipo kwa ajili ya kutangaza habari za kitaifa whether ni mambo ya Dini, Siasa, Uchumi au Kabila. Chamsingi ni ukubwa wa habari.

Nahisi muandishi anasumbuliwa na chuki ya Udini. Natamani angetumia muda wake kuandika mambo muhimu yenye maslahi aachane na hizi chuki.
 
Nawachukia wakristo kwa sababu wanajali dini yao kuliko watu, wamejaa unafiki. Akitawala mkristo hata akiua wanakaa kimya, watu wakipotea wanakaa kimya. Lakini mama ametufanya tutabasamu nyinyi mnanuna, alafu wanatulazimisha tusiyaone mema anayotutendea bali tumtazame kama muislamu na hivyo kumchukia yeye na mema yake.
Utaumiza moyo wako kukaa na chuki za kijinga na kupumbavu, wape elimu mahali unadhani msimamo wao hauwasaidii, halafu wewe uwe na maisha meupeee moyoni mwako
 
Kumbe tatizo ni maandishi yaliyoandikwa chini ya TV screen eti

"MASHINDANO YA TAIFA YA QURAAN"
Mashindano ya taifa hiyo ndo nyuzi yenyewe, TV ya taifa ipo kwa ajili ya kutangaza habari za kitaifa whether ni mambo ya Dini, Siasa, Uchumi au Kabila. Chamsingi ni ukubwa wa habari.

Nahisi muandishi anasumbuliwa na chuki ya Udini. Natamani angetumia muda wake kuandika mambo muhimu yenye maslahi aachane na hizi chuki.
Kwa ujumla mwandishi kaandika Andiko la kijinga lisilo pakegi ya yupi ndiye Mtanzania na yupi anastahili kuitumia TBC na nini maana ya Utaifa Kwa ujumla na Sura hiyo ya Utaifa inayo sehemu ipi ukitazama unauona huo utaifa

Anayelipa Kodi ili TBC ifanye kazi ni Nani, mwandishi na Andiko lake hajamtaja ni Nani mlipa Kodi anayesababisha TBC iwe hewani??
 
Back
Top Bottom