Uchaguzi 2020 Tamaa za Wateule wa Rais kutia nia Ubunge zitawaponza wengi. Ushahidi huu hapa wa Rais Magufuli na Humphrey Polepole

Ili kujificha vizuri katika kichaka cha hivyo viapo ni vyema ukaweka hivyo vipengele hapa ili tujiridhishe vinginevyo kinachofanyika kina utata.
Kwa kuwa sijaona hivyo viapo, nalazimika kutumia matukio ya nyuma ambpo watumishi wa kada mbalimbali waliruhusiwa kushiriki mchaksto wa kuchaguliwa chini ya utaratibu Fulani.
Wakuu wamikoa, wilaya, makatibu wakuu na watumishi wengine walitoka na kwenda kugombea. Utaratibu huu ulibadilishwa lini?
Nje ya mada hivi Dodoma INA DC mpya?
 
Leo hii tayari usha mkana Makonda? [emoji23][emoji23] ama kweli ccm kwao kipau mbele chao ni mkono kwenda kinywani
 
Hivi Makonda atamchagua nani? Kwa lipi? Kwa umaarufu upi aliyo nao?
Usiamini hata chembe akisemacho JPM. Makonda, Mnyeti, Gambo, Tulia, mtoto wa Lowasai, n.k wametumwa.

Wakikatwa hawa wote ndipo umuamini.
 
Jpm anapata picha jinsi watakavyomkimbia 2025, atakuwa mpweke hasa kuanzia 2023
 
Wote kabla ya kwenda kugombea wameomba kibali hivyo huwezi kuwahukumu wakati wameruhusiwa na mkuu wao!
 
Kwani wapi pameandikwa kuwa uteuzi ni ndoa ya kikristo haivunjiki? Sheria gani inamuondolea mtu haki ya kikatiba ya kuchagua na kuchaguliwa mara baada ya kuteuliwa? Ajabu hasa ni nini na ni nani aliwahi kudumu milele kwenye ukuu wa mkoa au wilaya kwa sababu hakugombea? Acheni ushamba.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…