TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
Naomba kujua kama nina vigezo vya kupewa tarif, ili nisisumbuke kufuatilia maana nilipopeleka barua niliambiwa tarif imesitishwa kwa muda

Namba ya mita yangu ni 221 325 3284 1
 
Kwanza hongereni sana kwa kujiweka hapa na kuwa tayari kujibu maswali ya wateja. Nahitaji user manual ya wasion meter WHCi04.
 
Maoni yangu kutoka moyoni ni kwamba hilo shirika libinafsishwe kwa sababu serikali imeshindwa Kuliendesha.
 
Hivi kwann sisi wakazi wa viwege kwa mpemba majohe gongolamboto wilaya ya ilala mkoa daresalam, mmetupangia kuhudumiwa kisarawe mkoa wa pwani?

Na kwanini miundombinu ipo tayari kwa maana ya nguzo na waya na transformer zimefungwa na zimewashwa taa, tangia February hadi leo hakuna hata nyumba moja mlioiunganishia Umeme?

Tatizo ni nini? Mbona kila kitu tayari
 
Hivi kwann sisi wakazi wa viwege kwa mpemba majohe gongolamboto wilaya ya ilala mkoa daresalam, mmetupangia kuhudumiwa kisarawe mkoa wa pwani? Na kwanini miundombinu ipo tayari kwa maana ya nguzo na waya na transformer zimefungwa na zimewashwa taa, tangia February hadi leo hakuna hata nyumba moja mlioiunganishia Umeme? Tatizo ni nini? Mbona kila kitu tayari
Tunaomba namba ya simu.....eneo..


Na tatizo haswa ni nin..
 
Tanesco tunalia na bili asilimia 23 za kununua umeme wa Luku mnatukata yaani nikinunua LUKU ya elf10 napata UNIT ZA ELF 7.utaona ktk msg ati VAT18%....REA,3%....SERVICE CHARGE,3%...kwanini hamna huruma?mimi mAoni yangu kungeanzishwa tu kampuni binafsi ya umeme ili TANESCO mpate changamoto kama alivoipata TTCL baada ya kuwakaribisha makampuni binafsi
 
Tanesco tunalia na bili asilimia 23 za kununua umeme wa Luku mnatukata yaani nikinunua LUKU ya elf10 napata UNIT ZA ELF 7.utaona ktk msg ati VAT18%....REA,3%....SERVICE CHARGE,3%...kwanini hamna huruma?mimi mAoni yangu kungeanzishwa tu kampuni binafsi ya umeme ili TANESCO mpate changamoto kama alivoipata TTCL baada ya kuwakaribisha makampuni binafsi
Tunaomba namba yako ya mita tukuelezee ulichokatwa maana umeme wa tsh 10000 unapata unit 28.kama.upo tarif 1
 
Tunaomba msaada wenu tusambaziwe umeme,sisi wakazi wa kata ya ITENDE MBEYA JIJI.
nguzo za umeme zimepangwa kwa kufuata barabara,sasa sisi wananchi tusio barabaran tuko gizani!

tumejikusanya tunaohitaji kufungiwa umeme tumefika watu 100 na tumefanya wiring tayari!

TANESCO MBEYA wanasema hawana nguzo,sasa ninyi makao makuu mtatusaidiaje?hata mkitutafutia jibu la uhakika-NI KWANINI KATA YA ITENDE AMBAYO IPO KARIBU KABISA NA CITY CENTRE,HAIJASAMBAZIWA UMEME MPAKA LEO?

majibu ya makao makuu yataniridhisha sana kuliko hawa wa MKOANI wanaodai eti hakuna nguzo!
 
Nakumbuka kuwaandikia hapa tatizo la Mangamba chini iliyoko manispaa ya Mtwara kutopewa umeme zaidi ya Mwaka sasa.

Nguzo na baadhi ya nyaya zimewekwa na kila zinapofika nyaya za kumalizia kujenga mradi wanazipeleka maeneo mengine kwa sababu hakuna transfoma. Tumefuatilia mara nyingi mkoani na majibu tunayopewa ni kwamba makao makuu ya TANESCO hawajaleta transfoma ila zilikuwa zimeshaagizwa.

Ninaomba majibu ya maswali yafuatayo. Tangu mwaka 2015 bado transfoma ziko njiani? Je mradi mdogo kama huo wa nyumba zizisozidi 200 unachukua muda gani? Mbona kuna miradi mingine iliyofuata imekamilika katika maeneo mengine au Mtwara kuna tatizo gani? (ushahidi ninao)

Tumeandika barua kwa Mkurugenzi mkuu kulalamikia hili lakini hatujajibiwa mnataka tupeleke wapi malalamiko yetu? Hamuoni kuwa ni tatizo kukosa huduma kwa kipindi kirefu kiasi hicho? Wakazi wa Mangamba Mtwara tunahitaji majibu yanayoonyesha tutapata lini umeme.
 
Naomba ufafanuzi hivi kwanini,umeme nanunua bei sawa na wanao tumia unit zaidi ya sabini kwa mwezi wakati mimi natumia unit takribani stini na mbili kwa mwezi.

Wakati huohuo jirani yangu anapata unit nyingi akinunua kwa kiasi cha hela km ntakayonunua mimi, Naomba mnielimishe tafadhali
 
Licha ya Mkoa wa Mtwara kuwa na kituo chanzo kikuu cha uzalishaji wa Gesi asilia ,lakini mambo ni kinyume kabisa na mategemeo ya wananchi wa mkoa huu kwani tangia mwezi january mwaka huu 2017 kumekuwa na mgao wa umeme, katika maeneo mbalimbali umeme unakatika asubuhi na kurudi jioni au umeme kukatika jioni mpaka saa tano usiku.

Mpaka sasa Uongozi wa shirika la Tanesco mkoa hawajatoa maelezo yeyote kuhusu mgao huu kuwa unasababishwa na nini na tatizo hili lini litakoma,cha kusikitisha hakuna chombo cha habari kilicho report juu ya mgao huu wa umeme mkoa wa mtwara ambao umekuwa kikwazo kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa wakazi wa Mkoa wa Mtwara.
 
Tanesco. Nawachukia kama nn hasa tawi la masasi mtwara
 
jamaa inabidi asiwe peke yake kujibu madai hayo ya wananchi!maana ni mengiii!
 
Licha ya Mkoa wa Mtwara kuwa na kituo chanzo kikuu cha uzalishaji wa Gesi asilia ,lakini mambo ni kinyume kabisa na mategemeo ya wananchi wa mkoa huu kwani tangia mwezi january mwaka huu 2017 kumekuwa na mgao wa umeme,katika maeneo mbalimbali umeme unakatika asubuhi na kurudi jioni au umeme kukatika jioni mpaka saa tano usiku.Mpaka sasa Uongozi wa shirika la Tanesco mkoa hawajatoa maelezo yeyote kuhusu mgao huu kuwa unasababishwa na nini na tatizo hili lini litakoma,cha kusikitisha hakuna chombo cha habari kilicho report juu ya mgao huu wa umeme mkoa wa mtwara ambao umekuwa kikwazo kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa wakazi wa Mkoa wa Mtwara.
Tumeipokea kwa uchunguzi na hatua zaidi
 
Naomba ufafanuzi hivi kwanini,umeme nanunua bei sawa na wanao tumia unit zaidi ya sabini kwa mwezi wakati mimi natumia unit takribani stini na mbili kwa mwezi. Wakati huohuo jirani yangu anapata unit nyingi akinunua kwa kiasi cha hela km ntakayonunua mimi, Naomba mnielimishe tafadhali
Tunaomba namba yako ya mita
 
Naomba kuuliza unapo badilishiwa mita kutoka hizi za zamani nakuwekewa mita za luku kuna kiasi chochote unatakiwa ulipe?

Je zile unites unazozikuta kwenye mita baada ya kubadilishiwa niza bure au unatakiwa uzilipie????
Maana kuna MTU hapa kaambiwa alipie
 
Naomba kuuliza unapo badilishiwa mita kutoka hizi za zamani nakuwekewa mita za luku kuna kiasi chochote unatakiwa ulipe?
Je zile unites unazozikuta kwenye mita baada ya kubadilishiwa niza bure au unatakiwa uzilipie????
Maana kuna MTU hapa kaambiwa alipie
Ninavyojua.

1. Unapobadilishiwa mita hulipi chochote bali wanachukua usomaji wa mwisho wa ile mita na kwenda kutoa ule uliosomwa kabla ya huu usomaji wa mwisho ili wakwambie deni lako.

2. Units unazo zikuta kwenye mita mpya ambazo ni 50 kwa single phase meter na 150 kwa three phase meter sio za bure. Zile zinatangulia ili wanapoendelea kufanya usajili nawe unaendelea kutumia. Ndio maana ununuzi wa kwanza kwenye meter mpya kama ni single phase unashauriwa ununue walau umeme wa kuanzia Tsh 20,000/= ambazo ni Units 56 lakini wewe utapata units 6 tu huku zile 50 ukiwa umezilipa.

Na manunuzi yanayofuata yanakuwa ya kawaida. Hapa ni kwa mteja wa Tariff 1 tu.
Nadhani umenielewa.
 
Ahsante TANESCO na hongera kwa hatua hii.... Wale waliosoma PR wamemsoma sana dada Badra, umeeda extra mile ahead, big up.

Hata kama hamna competitors, you have to show that you care like this.
 
Back
Top Bottom