Weka hizi
0330 6421 0123 7626 2826

TANESCO "Tunayaangaza maisha"
Kama ulinunua mara mbili weka na hizi
3934 2223 6110 4391 2163

TANESCO "Tunayaangaza maisha"
 
TANESCO mie ni mkazi wa Mabwepande Mji Mpya SACCOS next block baada ya wahanga, mwaka Jana mwezi wa 8 mlipita na gari lenu mkatutangazia kwamba mtaleta umeme hivyo wakija Watu wakituambia tuchange hela tusitoe na kweli baada ya mwezi mkaanza kuleta nguzo.

imepita miezi 6 sasa tangia muweke nguzo na hadi kufika mtaa wa SACCOS zinahitajika nguzo kama 7,ni nini kilichokwamisha mradi Huo wa REA? Tupo karibu na Chuo cha kilimo Mabwepande ,ukitaka kunipata nipigie namba yangu ni 0678308942.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sawa tutawasiliana na wewe kwa maelezo zaidi

TANESCO "Tunayaangaza maisha"
 
Naomba kujuzwa namna ya kuingiza umeme wa luku kwa hizi mita za kuingiza kwa rimoti kama umeme ukiwa umeisha kabisa ili nisiwe naenda kwa jirani kuingizia umeme.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naomba kujuzwa namna ya kuingiza umeme wa luku kwa hizi mita za kuingiza kwa rimoti kama umeme ukiwa umeisha kabisa ili nisiwe naenda kwa jirani kuingizia umeme.

Sent using Jamii Forums mobile app
Zima switch zote za ukutani kwenye nyumba..baada ya hapo washa switch moja tu ya ukutani na chomeka hio rimoti hakikisha unatumia betri zenye nguvu sana..baada ya kuchomeka itawaka rimoti na kuaandika Connect... baada ya hapo weka umeme wako ukimalizia na alama ya Ok au enter.

Muhimu sana kubakikisha switch zote zimezimwa hata switch za taa pia zima

Akikuketea error 77
Fanya hivi
Weka namba yako ya mita ikifiatiwa na zero kisha weka tena namba ya mita alafu bonyeza ok...
Mfano mita yako ni 1234567

Itakuwa hivi
123456701234567
Ok au enter

Alafu weka umeme wako


Kwa msaada unaweza kupiga 0768985100

TANESCO "Tunayaangaza maisha"
 
Nyie tanesco mungu anawaona mjue,
nimefika ofisi ya gongo la mboto kuomba kubadilishiwa tarrif toka 4 kwenda 1,nimepewa fomu nimejaza tangu mwezi wa sita mpaka leo kimyaaaa!

Kwani hii huduma inalipiwa? Kama inalipiwa sh ngapi?

Tangu niweke umeme matumizi yangu hayajawahi kuzidi units 50 kwa mwezi sasa kwa nini hamtaki kunibadilishia?
Fundi wenu ananiambia mpaka aje akague,sasa anakagua nini wakati akiangalia tu kwenye kompyuta anaona matumizi

kama nadanganya si itarudi kwenye tarrif 4 tatizo nini sasa.
Sijui niende kwa meneja au nae atanizingua!

Yaaani nyie tanesco,
nipo kitunda shule
jina, mwinyimvua a. Abubakari
mita no.37136082536
mkoa wa gongo la mboto
 
Tumeipokea mpendwa mteja tunaifatilia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkoa TANESCO [HASHTAG]#Kilimanjaro[/HASHTAG] wakamata wezi na wahujumu wa miundo mbinu ya shirika kwa mikoa ya Arusha, Moshi na Manyara




TANESCO "Tunayaangaza maisha"
 
Mkoa wa TANESCO Simiyu watoe elimu ya matumizi bora ya umeme na usalama Bariadi pamoja na kupokea changamoto wanazozipata




TANESCO "Tunayaangaza maisha"
 
mimi ni mkazi wa kiwalani nawalalamikia tanesco .mita ilikua mbovu nikabadilishiwa bahati mbaya mita ya zamani ilikua na salio la umeme nikaambiwa niandike barua ya kuomba kurudishiwa nimeandika imekuwa ngumu kurudishiwa . ni kitu kidogo sana hiki kwanini wananizulumu haki yangu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunaomba namba ya mita za zamani na mpya , namba ya simu na ofisi ipi uliomba huduma

TANESCO MAKAO MAKUU

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umeshafika ofisi ya Yombo kupata msaada zaidi

TANESCO "Tunayaangaza maisha"
 
Kuna matapeli wawili wanapita huku mitaa ya Chanika nyeburu wakiwachangisha watu fedha ili wawafanyie mpango Wa Umeme haraka wana uniform na Vitambulisho vya tanesco

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…