TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
Hii taarifa ya ITV leo, kuwa kiongozi mmoja ameagiza wananchi walioshindwa kulipia kuunganishwa umeme washitakiwe,ni kweli au?!
 
TANESCO hivi siku hizi inachukua miezi mingapi kumfungia umeme mtu ambaye amelipia service line na hahitaji nguzo?

Ni mwezi sasa tangu tulipie service line lakini naona kimya
Je umelipa lini

Jina

Simu

Wilaya tafadhali
 
Mimi ni mteja wenu na matumizi yangu ni madogo sana. Niliomba kunadilishiwa tarrif 4 tangu August last year ofisi ya Mbezi lakini mpaka leo sijapata hiyo huduma. Ni kitu gani kinachowakwamisha lakini
 
Tanesco mnaleta lini SEAL Bagamoyo ili tupate kuunganishiwa nishati ya umeme??? Tumelipia umeme miezi mitatu sasa tunaambiwa hakuna SEAL je hizo SEAL zinafanya kazi gani????
 
Tanesco mnaleta lini SEAL Bagamoyo ili tupate kuunganishiwa nishati ya umeme??? Tumelipia umeme miezi mitatu sasa tunaambiwa hakuna SEAL je hizo SEAL zinafanya kazi gani????
Tafadhali onyesha umelipia lini

Jina

Simu kwa hatua zaidi
 
Naomba kujua kila kitu kuhusu 0 tariff
  • inamhusu mteja wa aina gani
  • awe na sifa gani
  • viwango vya malipo ili kuipata
  • faida na hasara za hiyo huduma
  • je ukijiunga waweza kujitoaje kama mteja anaiona haimfai
  • inachukua muda gani tangu kuiomba mpaka kuipata
  • utaratibu wa kuipata ukoje
 
Hbr, mimi ni Mkazi wa Wilaya ya Mtwara Jimbo la Nanyamba. Swali langu kwa wanaohusika ni kwa nini umeme unakatika inafika zaidi ya mara 10 kwa siku katika maeneo kuanzia wilaya ya Mtwata vijijini, na Tandahimba?
 
Hbr, mimi ni Mkazi wa Wilaya ya Mtwara Jimbo la Nanyamba. Swali langu kwa wanaohusika ni kwa nini umeme unakatika inafika zaidi ya mara 10 kwa siku katika maeneo kuanzia wilaya ya Mtwata vijijini, na Tandahimba?
Ahsantw kwa taarifa mpendwa mteja wetu tafadhali onyesha namba ya simu kwa hatua zaidi
 
Samahani, naomba nisaidie please! Nimenunua LUKU message ikafutika kwa bahati mbaya
Meter number:07052851222
 
Tanesco Tanga mmeanza mgap wa umeme? Mbona mwatukatia umeme kila wasaa bila taarifa tena kwa muda mrefu. Twauliza mara leo Kange hakuna, kesho makorora mara mwakidila na kwingineko. Shida nini??
 
Tanesco Tanga mmeanza mgap wa umeme? Mbona mwatukatia umeme kila wasaa bila taarifa tena kwa muda mrefu. Twauliza mara leo Kange hakuna, kesho makorora mara mwakidila na kwingineko. Shida nini??
Je ni eneo gani? Wilaya na namba ya simu tafadhali
 
Tanesco Tanga mmeanza mgap wa umeme? Mbona mwatukatia umeme kila wasaa bila taarifa tena kwa muda mrefu. Twauliza mara leo Kange hakuna, kesho makorora mara mwakidila na kwingineko. Shida nini??
Kwa kweli kwa Tanga umeme umekua changamoto kila siku au baada ya siku moja lazima umeme ukatike, Mikanjuni sasa hivi hamna umeme!!! Inachosha kwa kweli na hatutaarifiwi kama ni mgao au la!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Walaya: Ilala
Kituo: G/mboto
Tanesco kuna shida gani? nimelipia umeme mwezi mmoja na nusu umepita sijafungiwa umeme! Humu nimelalamika wee lakini hamna hatua yoyote:

Wilaya:Ilala
Kituo:G/mboto
Simu: 0622239935
 
Tanesco kuna shida gani? nimelipia umeme mwezi mmoja na nusu umepita sijafungiwa umeme! Humu nimelalamika wee lakini hamna hatua yoyote:

Wilaya:Ilala
Kituo:G/mboto
Simu: 0622239935
Ahsante kwa taarifa tunaifanyia kazi
 
TANESCO Kimara jana mlikata umeme,leo tena mmekata saa hizi,bado mnakatakata umeme.Hivi kuna shida gani Kimara jamani?mbona mko hivi?mtatuliza lini umeme wa Kimara?
 
Tanesco mm nko morogoro kididimo huku umekatika leo siku ya pili pc zote zimezima chaji na kesho nina test asubuhi hivi nikifeli itakuwaje
 
Back
Top Bottom