Yaani hili shirika wanafanya kazi kimazoea sana, unaweza mkata mtu makofi eti. hapo utakuta umepewa majibu mepesi mepesi tu huku jamaa anabinya binya kismart phone chake yupo facebook[emoji24][emoji24]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tanesco mmenisikitisha sana yani, nimeweka malalamaiko yangu humu ila mmeyapita kama vile hamjayaona

Nimefata process zote za kuwekewa umeme kwangu, na nimelipia kwa muda stahiki ili nifungiwe umeme ila nimeambiwa nisubiri ndani ya muda wa ndani ya siku 30 za kazi, nimesubiri muda huo umepita bila kupewa huduma yeyote

Nimeenda ofisini pale ofisi ya mbezi naambiwa hawana vifaa vya kunigungia umeme nisubiri mpaka vifaa vitakapokuja

Nimeendelea kusubili ila kimya, na sehemu yangu sio ya nguzo ni ndani ya mita 30

Naomba mnijibu kama huduma yangu stahiki ntapata au mnanirudishia pesa yangu nikanunulie sola

Mmenifanya nimekereka sana kuhusu ili shirika la umeme

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umelipa kwa jina gani na namba yako ya simu mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sheria inakutaka ununue umeme wa tsh 9150 ambao ninujit 75 kwa mwezi wewe ulikuwa unanunua unit 77 hivyo ulivuka takwa hilo na sasa upo tarif inayoendana na matumizi yako

Sent using Jamii Forums mobile app
Umemjibu kijumla sana mkuu, unakuta mwingine hajui limitations zenu kwakua akupata elimu ya kutosha, na isitoshe pamoja na kupata hizo unit 77 lakin bado unakuta hizo unit zinatumika zaidi ya mwezi.

Lakini nyie badala ya kumpa elimu na kujilizisha kimaesabu kama maelezo yake ni sahihi kimaesanu nyie mnakimbilia kumwambia majibu kama uliyojibu hapo juu, It is not fair.

Hata mimi nina tatizo kama hilo lakini kwakua nyinyi ndio mmeshika mpini sina namna, maisha magumu mjue..
 
Tunapmba namba yako tukupigie

Sent using Jamii Forums mobile app
 
NDUGU MPENDWA MTEJA

Tunapenda kupatie ufafanuzi wa swala lako kama ifuatavyo


Utaratibu ni kuwa kama mteja amenunua Transformer na lipo kwenye eneo lake, hilo ni mali yake hii ni kwa mujibu wa kanuni za umeme (Electricity Regulations 4(5) under "Reinbursement scheme") inaruhusu. Tukitaka kuitumia kwa kuunga wateja wengine lazima tupate ridhaa yake. Lakini vilevile wale wanaotaka kuungwa hapo watachangia kwenye gharama aliyotoa huyo mteja wa mwanzo ili mradi laini hiyo haijapita miaka 4 tangu ijengwe.
Huo ndio muongozo wetu na kama utakuwa na swali zaidi tupatie kwa ufafanuzi zaidi


TANESCO HUDUMA KWA WATEJA

MAKAO MAKUU

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu asante, kwa mfano transforma nimenunua mimi lakini haijawekwa eneo langu inakuwaje? Na kama line ipo zaidi ya miaka 4 inakuwa vipi pia
 
Mkuu asante, kwa mfano transforma nimenunua mimi lakini haijawekwa eneo langu inakuwaje? Na kama line ipo zaidi ya miaka 4 inakuwa vipi pia
Kinachoangaliwa ni umilili yaani ownership je ni mali yako au yetu.aidha mara nyingi mtu analipia transfomer linalomuhudumia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa mkuu ninaweza kununua transforma likawe lenu? Kwa vigezo gani na wakati hata risiti za manunuzi ninakuwa nazo?
Kwa mujibu wa kanuni za umeme baada ya miaka minne linakuwa la TANESCO hii ni kutokana na ukweli kwamba kuanzia kipindi hicho litakuwa linahudumiwa na sisi na hitilafu yeyote itakayotokea ikiwemo kulibadilisha kama limekufa ni gharama zetu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sheria inakutaka ununue umeme wa tsh 9150 ambao ninujit 75 kwa mwezi wewe ulikuwa unanunua unit 77 hivyo ulivuka takwa hilo na sasa upo tarif inayoendana na matumizi yako

Sent using Jamii Forums mobile app

Kama matumizi yangu yamepungua hadi kufikia unit 68 kwa mwezi nifanyaje ili nirudishwe kwenye tarif inayo nifaa?
 
Kama uliwahi kuwa tarif 4 ukatolewa hauwezi kuridishwa tena kwa mujibu wa Sheria mpendwa mteja

Sent using Jamii Forums mobile app

Asante kwa majibu! Pia naomba unisaidie hili, ninahitaji kuhamisha line ya umeme kutoka nyumba moja kwenda nyingine zote zipo kwenye kiwanja kimoja.

Nafanya hivyo kwasababu nataka kuifanyia marekibisho makubwa nyumba iliyo na line kwa sasa, je nifate utaratibu gani?
 
Tafadhali fika ofisi ya eneo lako na barua ukielekeza kwa manager ili kazi hiyo iwe rasmi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…