TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
Sikh imefunguka kwa umeme kukatika kikawaida lazima ukatike Mara 5 kila Sikh
Cha kushangaza kuna majitu yanamlaumu mzalendo January makamba,hivi hawajui mitambo ilikuwa imechakaa kipindi cha mwendazake
Makamba ni genius sana jamaa in kichwa mnooo
Kweli wewe chizi
 
Kwann mnakatakata umeme sana aisee? Ina maana enzi za hayati Magufuli hizo changamoto mlizokua nazo sasa hivi, kipindi kile hazikuwepo? Mbona mnamdharau Madam president kiasi kikubwa hivyo?

Au kwa sababu haongei na hafanyi tit for tat kama hayati Magufuli? 😡
 
Shirika la Umeme Tanzania - (Tanzania Electric Supply Company Limited - TANESCO), Tunaomba mtupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri kupitia huu uzi nasi tutawajibu.

Tunawaomba mzingatie yafuatayo ili kurahisisha ufafanuzi na ufumbuzi wa tatizo au taarifa husika;

1. ENEO HUSIKA

(Mnaweza kuwa eneo moja lakini mnahudumiwa na transfoma au njia ya kusambaza umeme (feeder) tofauti)

2. NAMBA YA SIMU

(Wakati mwingine umeme upo kote isipokuwa kwako hivyo na rahisi kuwasiliana na wewe)

3. KARIBU NA NINI

(Kuna alama vitu au watu mashuhuri karibu na eneo lako mfano ofisi ya Serikali ya Mtaa, Mahakama, Kituo cha Polisi nk)

4. JINSI YA KUFIKA MAKAZI YAKO

(Toa ufafanuzi wa jinsi ya kufika makazi yako,chukulia unamuelekeza mtu ambaya hajawahi kufika kabisa)

5. MKOA,WILAYA NA KITONGOJI/KIJIJI

(Taarifa hii ni muhimu sana kusaidia kubaini eneo husika lipo wapi kwani yapo maeneo yanayofanana kwa majina lakini yapo Mikoa tofauti mfano Magomeni ipo Dar es Salaam na Mkoa wa Mtwara pia.)

6. KAMA NI TATIZO LA MITA NINI KINATOKEA UKIWEKA UMEME

(Kila mita ina ujumbe wake unaoashiria kitu fulani hivyo kubainisha ujumbe kunamsaidia mpokea taarifa kukupatia maelezo sahihi mfano mita namba 24339173921 inaonyesha error 77)

7. KAMA NI KUSHINDWA KUNUNUNUA UMEME UNAPATA UJUMBE GANI NA UNANUNUA KWA NJIA GANI

(Ujumbe huu ni muhimu sana kuweza kubaini chanzo cha tatizo pamoja na njia iliyotumika kununulia umeme mfamo Mpesa, Tigopesa, Maxcom nk)

TUNAENDELEA KUWASIHII WATEJA WETU KUZINGATIA UTOAJI WA TAARIFA SAHIHI NA FASAHA KWA HUDUMA BORA ZAIDI KUTOKA TANESCO.

ENDELEA KUFURAHIA HUDUMA BORA KUTOKA TANESCO

Vilevile pitia threads hizi kupata Maelezo ya ziada;

LUKU:Mfumo wenye Tija kwa Wateja na TANESCO

Fahamu mita za LUKU zinazofungwa majumbani

Zijue taratibu za kufuata ili kufungiwa umeme na TANESCO

Kw mawasiliano Kituo cha Miito ya Simu (+255) 22194400 or (+255) 768 985 100 Mitandao ya kijamii Tanescoyetu (@tanescoyetu) | Twitter Facebook: Tanesco Yetu

HAPA CHINI NI NAMBA ZA SIMU ZA MIKOA

Ofisi ya Mkoa wa Mbeya Simu ya Mkononi (+255) 757 529 380 ya Mezani (+255) 252 504 219

Ofisi ya Mkoa wa Ilala Simu ya Mkononi (+255) 784 768 586 ya Mezani (+255) 222 133 330

Ofisi ya Mkoa wa Kinondoni Kusini (Magomeni) Simu ya Mkononi (+255) 715 271 461/ (+255) 784 271 461

Ofisi ya Mkoa wa Kinondoni Kaskazini (Mikocheni) Simu ya Mkononi (+255) 784 768 584 / (+255) 716 768 584 ya Mezani (+255) 222 700 367/ (+255) 222 701 602 / (+255) 222 774 098

Ofisi ya Mkoa wa Temeke Simu ya Mkononi (+255) 712 052720 / (+255) 758 880155 / (+255) 732 997361

Ofisi ya Mkoa wa Pwani Simu ya Mkononi (+255) 78 5122020 / (+255) 65 7108782ya Mezani (+255) 23 2 402 386

Ofisi ya Mkoa wa Arusha Simu ya Mkononi (+255) 75 8 174 343 Mezani (+255) 272 506 110

Ofisi ya Mkoa wa Tanga Simu ya Mkononi (+255) 658 122 412/ (+255) 687 677 667 Mezani (+255) 27 2 646 779

Ofisi ya Mkoa wa Kilimanjaro Simu ya Mkononi (+255) 765 397 925/ (+255) 682 771 310 Mezani (+255) 272 755 007/8

Ofisi ya Mkoa wa Manyara Simu ya Mkononi (+255) 689 795 599 / (+255) 75 9 534 130 Mezani (+255) 272 530 590

Ofisi ya Mkoa wa Mwanza Simu ya Mkononi (+255) 759 777 786 / (+255) 687 910 202 Mezani (+255) 282 501 060 / (+255) 282 500 090

Ofisi ya Mkoa wa Geita Simu ya Mkononi (+255) 744 085 696 Mezani (+255) 28 2520330

Ofisi ya Mkoa wa Kagera Simu ya Mkononi (+255) 78 5 787 898 / (+255) 75 3 120 701 Mezani (+255) 282 220 061

Ofisi ya Mkoa wa Mara Simu ya Mkononi (+255) 762 165 087 / (+255) 732 985 672

Ofisi ya Mkoa wa Simiyu Simu ya Mezani (+255) 282 700 180

Ofisi ya Mkoa wa Dodoma Simu ya Mkononi (+255) 782 161 643 Mezani (+255) 262 321 728

Ofisi ya Mkoa wa Morogoro Simu ya Mkononi (+255) 68 4889272 / (+255) 65 4829046 Mezani (+255) 232 613 501/2

Ofisi ya Mkoa wa Singida Simu ya Mkononi (+255) 71 4 477 445 / (+255) 732 960 924 / (+255) 689 373 757 Mezani (+255) 262 502 133

Ofisi ya Mkoa wa Tabora Simu ya Mkononi (+255) 786 558 510 / (+255) 763 162 868

Ofisi ya Mkoa wa Shinyanga Simu ya Mkononi (+255) 754 521 070 Mezani (+255) 28 2762120

Ofisi ya Mkoa wa Kigoma Simu ya Mkononi (+255) 78 3720598 Mezani (+255) 28 2802668

Ofisi ya Mkoa wa Katavi Simu ya Mkononi (+255) 68 8345200

IMETOLEWA NA:- Ofisi ya Uhusiano

TANESCO Makao Makauu.

NAMBA ZA SIMU ZA MADAWATI YA DHARURA YA TANESCO MIKOA YOTE

1. Ilala

0222133330/ 0784 768586/ 0715 768586.

2.Kinondoni Kusini (Magomeni)

0784271461/ 0715271461

3. Kinondoni Kasikazini(Mikocheni)

0784 768584/ 0716 768584

4. Temeke

0222138352/ 0732 997361/ 0758881055/ 0712 052720

5. Pwani
078 5122020/065 7108782/023 2402386

6. Mbeya
0759 777781/0787 023422


7.Arusha
0758174343/
0622612501/
+255 27 2506110

8.Tanga
0658 122 412/0687 677 667/ 027 2646 779

9. Kilimanjaro
0765 397 925/0682 771 310/ (+255) 272 755 007/8

10 Manyara
0689 795 599/ 0627938951

11. Mwanza
0759 777 786/0687 910 202/
(+255) 282 501 060 / (+255) 282 500 090

12. Geita
0744 085 696/(+255) 28 2520330

13.Kagera
078 5 787 898 / 075 3 120 701/(+255) 282 220 061

14.Mara
0788 950 688/
028 262 2020/
0762 165 087

15.Simiyu
+255 282 700 180/0626383440/0745044072

16. Dodoma
0782 161 643/(+255) 262 321 728

17. Morogoro
068 4889272 /065 4829046/ (+255) 232 613 501/2

18 Singida
071 4 477 445 /0732 960 924 / 0689 373 757/(+255) 262 502 133

19. Tabora
0786 558 510 /0763 162 868

20. Shinyanga
0754 521 070/(+255) 28 2762120 /
0783 521 070

21. Kigoma
078 3720598/(+255) 2988226

22. Katavi
0688345200

23. Rukwa
0252161120/0768879813
24. Songwe
0684 611716/0763 430381.

25. Ruvuma
0252602281/0763 194 979/0787 758 986

26. Njombe
0744703988

27. Mtwara:
0789 999942/023 2333902

28. Iringa 0262702019/0739203015

29. Lindi
0752518247/0685692786


Kituo cha Miito ya simu/Call Centre Makao Makuu

0768 985 100/0222194400

Facebook
www.facebook.com/tanescoyetu

Twitter
www.twitter.com/tanescoyetu

Tovuti
www.tanesco.co.tz

Barua pepe
Customer.service@tanesco.co.tz

Imetolewa na:
Ofisi ya Uhusiano
TANESCO Makao Makuu
Bhana Tanesco mbeya wamebadil kaz badala ya kufanya umeme upatkane wao wameamua kufanya kaz ya kukatata umeme usipatikane tena bila taarifa kila siku lazma umeme ukate shda nn hatupew taarifa sijui hii mnatusaidiaje
 
Anaupiga mwingi sana,kama kuna meneja nchii hii anayejali matengenezo ya mitambo basi nii yeye

Sehemu kubwa ya mwanza kila Siku haina umeme kisa mzalendo huyuu anahangaikia matengenezo ya mitambo chakavu

Apandishwe cheo haraka hataa wauza majenereta hapa town wanamkubali sanaaa
 
TANESCO wakazi wa Goba njianne nyuma ya ofisi ya KIURE hatuna umeme kwenye nyumba kadhaa.

Tunaomba msaada wa haraka usiku huu maana hili joto sio poa.
 
Tanesco naleta malalamiko kutoka kwa wananchi mitaa ya Mapalilo na kawawa ndani ya mamlaka ya mji mdogo wa KIBAIGWA mkoa Wa DODOMA.

Octoba-2021 Ulikuja mradi wa REA wakasambaza nguzo kwa baadhi ya nyumbani na wengine wakaachwa kwa maelezo dhaifu ya upungufu wa nguzo lakini hata Wale waliopewa nguzo mpaka leo haijulikana mradi umekwama au laaah ukimya usio wa kawaida na hata wanapoulizwa baadhi ya wanohusika hawatoi majibu ya kueleweka.

Kutucheleweshea umeme ni kutucheleweshea maendeleo tunaomba muangazie maisha yetu kwa haraka.
 
Tanesco naleta malalamiko kutoka kwa wananchi mitaa ya Mapalilo na kawawa ndani ya mamlaka ya mji mdogo wa KIBAIGWA mkoa Wa DODOMA. Octoba-2021 Ulikuja mradi wa REA wakasambaza nguzo kwa baadhi ya nyumbani na wengine wakaachwa kwa maelezo dhaifu ya upungufu wa nguzo lakini hata Wale waliopewa nguzo mpaka leo haijulikana mradi umekwama au laaah ukimya usio wa kawaida na hata wanapoulizwa baadhi ya wanohusika hawatoi majibu ya kueleweka. Kutucheleweshea umeme ni kutucheleweshea maendeleo tunaomba muangazie maisha yetu kwa haraka.
Ngoja aje akuulize
wilaya
mkoa
Namba ya simu
Pamoja na maelezo yako mazuri ila Bado akija atakuuliza hayo maswali hapo juu.

Hivi Tanesco wanatuchukulia watanzania wote ni wajinga haiwezekani Kila mtu anawalalamikia wao utadhani huo umeme wanatupa bure, watanzania tuamke.
 
Tanesco wilaya ya Hai mna tatizo gani!?
Umeme unawaka na kuzimika mara kwa mara hamuoni mnaharibu mali za watu? Toka jana usiku hadi sasa umeme umekatika zaidi ya mara nne. Tatizo nini?
 
TANESCO Nina tatizo la makato ya Debt collected (Kodi ya pango) kwenye mita yangu ninavyojua malipo ni elfu 10 kwa mwaka Sasa nikipiga mahesabu nimeshalipia zaid ya hyo na bado wanaendelea kukata.

Lingine kwenye sehem ninayofanyia biashara wanafanya hivyo hivyo na hyo nyumba moja tunatumia mita 5 yan kula mtu na yake na wote tunakatwa naomba Kama unaweza kunipa ufafanuzi kidogo
 
Jamani tanesco wilaya ya kilombero (mlimba) mnatufanyia nini hiki? Kila siku za mpira hasa Simba na yanga mnakata umeme,,watu wanaishi kwa kutegemea vibanda umiza acha kufanya ivo tafadhali
 
TANESCO Nina tatizo la makato ya Debt collected (Kodi ya pango) kwenye mita yangu ninavyojua malipo ni elfu 10 kwa mwaka Sasa nikipiga mahesabu nimeshalipia zaid ya hyo na bado wanaendelea kukata.
Lingine kwenye sehem ninayofanyia biashara wanafanya hivyo hivyo na hyo nyumba moja tunatumia mita 5 yan kula mtu na yake na wote tunakatwa naomba Kama unaweza kunipa ufafanuzi kidogo
Tafadhali onesha namba ya mita kwa hatua zaidi
 
Tafadhali onesha namba ya mita kwa hatua zaidi
Malipo yamekamilika.01318959580
9001220660845157097
Units 106.7KWH

Token 7355 9635 5842 0416 5357

Cost 31,147.55
VAT 18% 5,606.55
EWURA 1% 311.48
REA 3% 934.42
Debt Collected 2,000.00
TOTAL 40,000.00 07/03/22 08:45

Screenshot_20220307-142147_1.jpg
 
Malipo yamekamilika.01318959580
9001220660845157097
Units 106.7KWH

Token 7355 9635 5842 0416 5357

Cost 31,147.55
VAT 18% 5,606.55
EWURA 1% 311.48
REA 3% 934.42
Debt Collected 2,000.00
TOTAL 40,000.00 07/03/22 08:45View attachment 2142093
Je tatizo ni nini hapo?Tafadhali tujulishe, umekatwa kodi ya majengo kwa muda wa miezi minne
 
Tuliaminishwa sana na viongozi kuwa mitambo ya Tanesco zilikuwa zikifanya kazi bila marekebisho kwa muda wa miaka mitano. Ndiyo maana umeme unakatika katika.

Tukaaminishwa tena na viongozi wazalendo wa nchii kuwa maji yamepungua kwenye mabwawa ya kuzalisha umeme na hii imechangiwa na ukame ndiyo maan umeme unakatika katika ovyo ovyo.

Taseco ikatangaza siku 10 kwa ajili ya mate matengenezo ya mitambo ya umeme ili kumaliza kabisa tatizo la kukatika kwa umeme. Na hii ilifanywa kwa weledi mkubwa tukafunga mkanda siku kumi. Umeme unakatwa saa moja asubuhi unarudi kesho yake yaani saa sita usiku. Tumevumilia nchi ikiwa gizani na kuamini sasa lile tatizo la umeme kukatika katika ovyo inakomeshwa kisawa sawa.

Baada ya ukame mashee na mapadre na viongozi wakuu wa serikali na wananchi kwa ujumla wetu tukafunga na kumwomba Mungu atupe Mvua. Hakika Mungu akajibu maombi Yetu tukapata mvua mabwawa ya kufua umeme yamejaa, mpaka Leo mvua bado zinanyesha sehemu nyingi ya Tanzania.

Naomba kuuliza Tanesco tatizo nini sasa kama mitambo yamerekebishwa na mengine kubadilishwa na mabwawa ya kufua umeme yamejaa na maji. Kwann umeme unaendelea kukatika ovyo je bado kuna mgao wa umeme. Toka last week umeme maeno ya Tegeta mpaka wazo madale yote hayana umeme.

Leo toka asubuhi umeme hakuna shughuli zetu zimesisima. Waziri husika na wahusika wote wa Tanesco tatizo ni nini?

Kwanni mnatuonea sana sisi tabaka la chini?

Wengine hatuna pesa ya kununua Majenerata na solar mnatusaidiaje?
 
Back
Top Bottom