TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
SHIRIKA LA UMEME TANZANIA (TANESCO)

TAARIFA KWA WATEJA WALIOUNGWA KATIKA GRIDI YA TAIFA

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawataarifu Wateja wake kuwa mnamo majira ya Saa moja na dakika mbili asubuhi imetokea hitilafu katika Gridi ya Taifa na hivyo kusababisha Mikoa yote iliyo unganishwa katika Gridi kukosa umeme.

Jitihada zinaendelea kurejesha umeme kwa haraka na tutaendelea kutoa taarifa zaidi.

Shirika linaomba radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza.

Tafadhali usishike wala kukanyaga waya uliokatika au kuanguka

Tovuti: www.tanesco.co.tz

Mitandao ya Kijamii
www.facebook/tanescoyetultd /twitter.com/tanescoyetu

Imetolewa na:-
Ofisi ya Uhusiano
TANESCO Makao Makuu

30/11/2017
Asante kwa Taarifa Mkuu Tanesco.

Jitahidini hivi hivi inapendeza
 
CCM taifa hili limewashida hakuna jipya zaidi ya kuudanganya umma kua mnapendwa, nakumbuka wakati mnaingia madarakani 2015 mlisena kua matatizo sugu kama ya Umeme yatakua historia kwa uwepo wa basi kutoka Mtwara. Sasahihi ni mgao wa Umeme kimya kimya nchi nzima bila hata taarifa tofauti na zamani. Mnaogopa nini kuutangazia umma kua kuna mgao wa Umeme? Mnajua mnawaathiri vipi wananchi na biashara zao? Si bora mtu awe na raarifa ili aweke Sola au jrnereta kabisa kuliko usanii huu?

Mliingia kwa mbwembwe mkatimua Mkurugenzi mkuu wa TANESCO kwa madai kua anahujumu shirika, leo hii yapata miaka miwili serikali ya awamu ya 5 iko madarakani lakini matatizo ya Umeme yako pale pale, usanii mtupu. Mnashindwa nini kusema kua hali ni tete mkaeleweka? Kwanini mtaabishe wafanya biashara bila sababu hata hatuelewi nini kinaendelea.

Niulize, hayo mambo makubwa yanayofanywa ni yapi? Kufuta elfu 20 za ada za sekondari? Mambo makubwa ni kunyanyasa watumishi wa umma ambao hawapati stahiki zao kwa hadaa za nyongeza kiduchu cha mishahara?

Naamini, bila CCM kuondoka madarakani wananchi wataendelea kuteseka maisha yao yote huku wachache wakiendelea kuneemeka maisha yao yote.
 
Kwa kweli hili ni janga kubwa na bora kuwe na taarifa ili tujipange nimetoka nyumbani almost 26km kuja kibaruani nafika hamna umeme na jana kulikuwa hamna umeme pia Tanesco na wahusika wote
 
Huku kwetu ni balaa yanii ni bora mtu uwe na taarifa. Ofisi yetu kwa mwezi umeme wa Tanesco tunalipa wastani was laki moja na nusu lakini tokea shida imeanza takribani wiki mbili sasa wastani kwa wiki tunatumia mafuta ya shs laki mbili kwa ajili ya kuendesha genereta na uzalishaji umepungua

Nidhamu ya woga ni mbaya sana.. Au kwa sababu ikulu kuna umeme 24/7 ndo manaana tanesco inaogopa kutangaza mgao was umeme? Watu wanaogopa kutangaza mgao wa umeme kisa kuogopa kutumbuliwa.
 
Habarini za asubuhi wanajamvi,,na imani mupo salama kabla simu yangu haijazima kutokana na matatizo ya MGAO WA UMEME KUANZIA SAA 1 ASUBUHI HADI SAA 12 JIONI ningependa tu kuwashauri tununue POWER BANK
 
Back
Top Bottom