TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
jamani hii ni ishu muhimu sana humu kuna uzi wa tanesco hebu wajitokeze watuambie ukweli kuhusu hili je ni laki tatu au ni elfu 99 bila nguzo :tusijekuwa tunapigwaga na wajanja
 
jamani hii ni ishu muhimu sana humu kuna uzi wa tanesco hebu wajitokeze watuambie ukweli kuhusu hili je ni laki tatu au ni elfu 99 bila nguzo :tusijekuwa tunapigwaga na wajanja
Gharama ya kawaida ni 320k unapata control number kabisa hakuna kupigwa mkuu.. ukikna malipo ya serikali unaambiwa masuala ya control number ujue hapo hakuna kupigwa.

Ongezeko la gharama litategemea na umbali wa nyumba yako kutoka kwenye nguzo
 
Gharama ya kawaida ni 320k unapata control number kabisa hakuna kupigwa mkuu.. ukikna malipo ya serikali unaambiwa masuala ya control number ujue hapo hakuna kupigwa.

Ongezeko la gharama litategemea na umbali wa nyumba yako kutoka kwenye nguzo
mfano mimi nataka kuweka umeme subhouse kubwa tayari na hiyo sub iko pembeni tu mwa nyumba kubwa na nguzo ipo hapo nikushusha tu waya je ni hiyo 320 au itapungua?
 
mfano mimi nataka kuweka umeme subhouse kubwa tayari na hiyo sub iko pembeni tu mwa nyumba kubwa na nguzo ipo hapo nikushusha tu waya je ni hiyo 320 au itapungua?
Kama unaongeza mita kwa nyumba ile ile gharama inakuwa pungufu ya 320k , inakuwa something like 177k ivi
 
Kama unaongeza mita kwa nyumba ile ile gharama inakuwa pungufu ya 320k , inakuwa something like 177k ivi
samahani mkuu nisaidie zaidi hapo, yaani niachomaanisha ni kuwa nina nyumba kubwa yenyewe imekamilika sasa nimejenga nyumba nyingine pembeni sasa hapo naomba upya au naomba kuwekewa sub mita tu ?
 
samahani mkuu nisaidie zaidi hapo, yaani niachomaanisha ni kuwa nina nyumba kubwa yenyewe imekamilika sasa nimejenga nyumba nyingine pembeni sasa hapo naomba upya au naomba kuwekewa sub mita tu ?
Unaomba upya kama kawaida.. utaratibu ni ule ule wiring》mchoro》survey 》 umeme
 
Mkuu fuata taratibu hizo nilizokuambia huwezi kupigwa pesa.
Mf. Umemchukua kishokabkapiga wiring alafu kapotolea mbali kaz et amemaliza ukienda TANESCO watakudai mchoro kama huna utaambiwa utandaliwa engineer
wa TANESCO gharama lazima ziongezeke.
Kuhusu surveyor nenda kamchukue umpeleke kwenye site direct bila hata malipo tena akikutoza umepigwa mjini hapa tena wanapewa pesa na ofisi na pia wewe unamuongezea pesa pole sana.
Waunganishaji ni kweli wanababaisha kutaka pesa,ukiwa na na roho nyepesi unatoa pesa kwanini usiende kwa meneja wa kituo na ushahidi ukiona unazinguliwa ukiwa mzembe utapigwa sana.
Eti eeh...sawa.
 
Namimi naomba niulize hv kwa mfano nyumba yangu iko umbali wa kufikiwa na nguzo km kumi za umeme utaratibu upo vipi? Je naweza kuzigharamia nguzo na kufungiwa umeme.
 
Namimi naomba niulize hv kwa mfano nyumba yangu iko umbali wa kufikiwa na nguzo km kumi za umeme utaratibu upo vipi? Je naweza kuzigharamia nguzo na kufungiwa umeme.
Hapo inabidi kuwa mvumilivu hadi hapo Tanesco wenyewe wapitishe nguzo maeneo hayo ,nguzo 10 ni nyingi sana hawapaswi kumbebesha gharama mteja.
 
Boss, sijui kuna tofauti gani katika hizi gharama za kulipia kuvuta umeme wa Tanesco. Nimelipa Tsh. 320,920 kwa huduma hiyo bila nguzo.

Sasa hiyo Tzs 27,000 au 99,000 utakuwa unazungumzia Nanjilinji vijijini huko.

Na umwambie asisahau Tzs 20,000 ya surveyor na angalau Tzs 10,000 ya kuambia "yaani tumehangaika kweli kutafuta nyumba yako", "subiri, tunakuja, kuna wengi tunawafungia", "unatoa chai tuje hapo fasta", n.k

Kimsingi kihalali, usipungukiwe na Tzs 330,000
Umeme ulopewa ww ni 3 phase mkuu hyo 99 wa single phase chief
 
Umeme ulopewa ww ni 3 phase mkuu hyo 99 wa single phase chief
Naomba mnieleweshe vizuri, hiyo Tzs 99k ni gharama ya nini?

Kuvuta umeme kwa umbali unaopaswa kuweka nguzo moja ni sh ngapi?

Na kuvuta umeme bila nguzo inakuwa kiasi gani?

NB: Kuna mmoja alivyoandika, ni kana kwamba wengi wetu tumepigwa kwa kulipa hiyo Tzs 321k, kwamba unamfuata surveyor akakupimie, unafuata fundi wakakufungie, yaani kirahisi hivyo, na ukisumbuliwa unaenda kwa Meneja...amenitia shaka na nadhani ameongea kwa uzoefu wa kuwa mwajiriwa wa shirika.

Ingawa kama uko idara tofauti na hiyo ya Distribution na huna nafasi fulani, staff wenzio wanakupitisha kwenye msoto vizuri tu, nimeshuhudia hili.

Malipo yamepokelewa kwenda TANESCO
Ankara Na: 99103185.....
Kiasi: 320960 TZS
Risiti Na: 920160........
Tarehe: 2020..........
Kupitia:EC100612.......
 
Unatatikiwa nyumba yako iwe imesukwa mfumo wezeshi wa kuingiziwa umeme(wiring).
Kisha fundi aliefanya kazi akuandalie mchoro wa jinsi wiringi ilivyo na upigwe muhuni na mhandisi(fundi anajua anaupateje)
Kisha unaenda ofisi ya TANESCO iliyo karibu unapewa fomu ya kuomba kuunganishiwa umeme inambatanishwa na mchoro wa nyumba na nakala ya kitambulisho Chako(NIDA au cha kura)
Utasubiri mpaka zamu yako utakapofikia kuunganisha utafanyiwa ivyo.
Gharama zipo za namna mbili elfu 27,000/= kwa umeme wa vijijini REA
elfu 99,000/= kama si wa REA.
Naomba comment hii niscreenshoot kwa matumizi ya baadae
 
Privacy ya mtoa taarifa Ni muhimu Sana. Cjajua kwann mnatakaga namba za simu wakati swala Ni kutoa Taarifa ya kusumbua umeme maeneo tajwa. Ingekuwa Ni ishu yangu binafsi kuwa mita au nyumba yangu umeme unasumbua sawa ningewapa namba

Kuweka namba hapa wakati tatizo ni la eneo kubwa Ni hatari kidogo Kwasababu kuna watu kukatika umeme kwao Ni faida. Watu wa Sola wanatoa huduma Ya kuchaji kwa Bei Gali Sana linapotokea tatizo la umeme. Nafikiri mtakuwa mmenielewa vizuri

Nashuari issue Ya umeme km Ni tatizo linalohusu jamii nzima Basi mtoa taarifa sip lazima atoe namba kwa usalama
Ni maoni yangu tu , samahani nitakuwa nimetoa contraversal opinion
Mteja anaweza kutuma taarifa kamili inbox sio lazima hapa kwa kuwa tunapenda kufatilia na kumpa mrejesho

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Privacy ya mtoa taarifa Ni muhimu Sana. Cjajua kwann mnatakaga namba za simu wakati swala Ni kutoa Taarifa ya kusumbua umeme maeneo tajwa. Ingekuwa Ni ishu yangu binafsi kuwa mita au nyumba yangu umeme unasumbua sawa ningewapa namba

Kuweka namba hapa wakati tatizo ni la eneo kubwa Ni hatari kidogo Kwasababu kuna watu kukatika umeme kwao Ni faida. Watu wa Sola wanatoa huduma Ya kuchaji kwa Bei Gali Sana linapotokea tatizo la umeme. Nafikiri mtakuwa mmenielewa vizuri

Nashuari issue Ya umeme km Ni tatizo linalohusu jamii nzima Basi mtoa taarifa sip lazima atoe namba kwa usalama
Ni maoni yangu tu , samahani nitakuwa nimetoa contraversal opinion

ndugu mteja,
mfumo wetu wa Huduma kwa wateja unataka mteja kuweka namba yake simu kwa ajili ya ufuatiliaji na maelekezo mengine, unaweza kutuma namba ya simu private kwenye inbox yetu na tutaipata lakni sio lazma kuweka hapa. hata sisi tunashauri wateja kuwa katika kuhakikisha usalama wao tunashauri watumie namba zao inbox
 
Pongezi nyingi kwa TANESCO, hasa kitengo cha dharura, kwa utendaji kazi uliotukuka.
 
Mimi ni mkazi wa kijiji cha Kasela D kata ya Uyogo,Urambo Tabora.
Shida yangu ni kuhusu kuunganishwa umeme kwa 27,000/ lakini huku meneja wa TANESCO Urambo alikuja kufanya mkutano akasema ni kaya 29 tu ndio zitaunganishwa kwa TSHs 27,000/ kati ya kaya 350.hao wengine wataunganishwa kwa shilingi 117,000/ ndani ya mita 30 bila gharama za nguzo ,ikiwa kuna kuweka nguzo pesa itazidi.
Mpaka sasa ni kaya 5 zilizopata umeme zingine wamesema wataendelea kutumia sola kama ndiyo hali inakuwa tofauti na matamko ya waziri na serikali.
Serikali imetumia pesa kubwa kufikisha huo umeme katika kijiji husika lakini matokeo yake watu 5 tu ndio wanatumia.
Maoni yangu TANESCO waaambaze nguzo kila mtaa ili watu waunganishe na umeme.
Pia watu wote walipe 27,000/ kama serikali inatamka.ni mimi
Donald Musimu -0782100081 urambo
 
Back
Top Bottom