TANESCO Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na hata ushauri
Tuliaminishwa sana na viongozi kuwa mitambo ya Tanesco zilikuwa zikifanya kazi bila marekebisho kwa muda wa miaka mitano. Ndiyo maana umeme unakatika katika.

Tukaaminishwa tena na viongozi wazalendo wa nchii kuwa maji yamepungua kwenye mabwawa ya kuzalisha umeme na hii imechangiwa na ukame ndiyo maan umeme unakatika katika ovyo ovyo.

Taseco ikatangaza siku 10 kwa ajili ya mate matengenezo ya mitambo ya umeme ili kumaliza kabisa tatizo la kukatika kwa umeme. Na hii ilifanywa kwa weledi mkubwa tukafunga mkanda siku kumi. Umeme unakatwa saa moja asubuhi unarudi kesho yake yaani saa sita usiku. Tumevumilia nchi ikiwa gizani na kuamini sasa lile tatizo la umeme kukatika katika ovyo inakomeshwa kisawa sawa.

Baada ya ukame mashee na mapadre na viongozi wakuu wa serikali na wananchi kwa ujumla wetu tukafunga na kumwomba Mungu atupe Mvua. Hakika Mungu akajibu maombi Yetu tukapata mvua mabwawa ya kufua umeme yamejaa, mpaka Leo mvua bado zinanyesha sehemu nyingi ya Tanzania.

Naomba kuuliza Tanesco tatizo nini sasa kama mitambo yamerekebishwa na mengine kubadilishwa na mabwawa ya kufua umeme yamejaa na maji. Kwann umeme unaendelea kukatika ovyo je bado kuna mgao wa umeme. Toka last week umeme maeno ya Tegeta mpaka wazo madale yote hayana umeme.

Leo toka asubuhi umeme hakuna shughuli zetu zimesisima. Waziri husika na wahusika wote wa Tanesco tatizo ni nini?

Kwanni mnatuonea sana sisi tabaka la chini?

Wengine hatuna pesa ya kununua Majenerata na solar mnatusaidiaje?
Hahahha.. mtaelewa tuu.. hahah.. mnakomeshwa maana mliishi vzur sana kipind cha nyuma kwa mzee magu..
 
Je tatizo ni nini hapo?Tafadhali tujulishe, umekatwa kodi ya majengo kwa muda wa miezi minne
Kuna kipindi walikata elfu sita kwa pamoja na malalamiko haya niliyasikia pia kwa watu wengine.

Hamuwezi kunipatia code niwe naangalia jinsi nilivokatwa kwa sbb Kodi ni elfu 10 kwa mwaka Sasa kwa namna hii Mwaka itakua hata 50k, kuna mtu wa tanesco niliwah kumuuliza akaniambia Kodi ni ishu ya TRA
 
Habari Tanesco! Tatizo langu ni Rushwa kukithiri ktk shirika letu hili... Wakazi wengi nikiwemo Mimi tumelipia umeme tokea October/November mwaka Jana lakini mpaka Leo hatujafungiwa hii ni kwa wilaya ya Ilemela_Mwanza!

Walitutumia ujumbe kua wale wote waliolipia kabla ya 05/01/2022 watawekewa umeme kabla ya 31/03/2022 tukasema sawa.

Ajabu kunaa nyumba ambazo tunaona wamefanya wiring ata wiki haijaisha wanawashiwa umeme.

Ukienda Tanesco kuulizia wanakupa majibu ya kua ndo kwaanza tumewafikia wateja wa 20/09/2021 sasa unajiuliza ivi hawana uongo mwingine kila siku ni tupo mwezi wa 9 tu.

Anyway kinachonisikitisha ni vijana wao wanaoitwa ma surveyors wanapiga simu kwetu kua BOSs una laki 2 kesho nikuletee mita? Namba tunazo na ata recordings za hizo simu tunazo.

Rushwa, Rushwa imetamalaki Tanesco Ilemela Mwanza!
NB... Tanesco naomba ujumbe huu muufikishe Kwa Meneja wa Tanesco Ilemela Mwanza haraka iwezekanavyo lasivyo tusilaumiane!
 
Habari Tanesco! Tatizo langu ni Rushwa kukithiri ktk shirika letu hili... Wakazi wengi nikiwemo Mimi tumelipia umeme tokea October/November mwaka Jana lakini mpaka Leo hatujafungiwa hii ni kwa wilaya ya Ilemela_Mwanza! Walitutumia ujumbe kua wale wote waliolipia kabla ya 05/01/2022 watawekewa umeme kabla ya 31/03/2022 tukasema sawa... Ajabu kunaa nyumba ambazo tunaona wamefanya wiring ata wiki haijaisha wanawashiwa umeme...Ukienda Tanesco kuulizia wanakupa majibu ya kua ndo kwaanza tumewafikia wateja wa 20/09/2021 sasa unajiuliza ivi hawana uongo mwingine kila siku ni tupo mwezi wa 9 tu.. Anyway kinachonisikitisha ni vijana wao wanaoitwa ma surveyors wanapiga simu kwetu kua BOSs una laki 2 kesho nikuletee mita? Namba tunazo na ata recordings za hizo simu tunazo... Rushwa, Rushwa imetamalaki Tanesco Ilemela Mwanza!
NB... Tanesco naomba ujumbe huu muufikishe Kwa Meneja wa Tanesco Ilemela Mwanza haraka iwezekanavyo lasivyo tusilaumiane!
[emoji848][emoji848][emoji848]
 
TANESCO kama kuna mgao basi tupeni taarifa kuliko kukata kata umeme bila watu kujiandaa.
Siku ya tatu now huku Bunju B mnakata umeme asubuhi unarudi almost saa kumi na mbili na nusu.

Waziri akiulizwa oh, nipe week mbili za matengenezo, sijui kufikia March kutakuwa hakuna mgao lakini hakuna kinachotokea.

Basi mshaamua kuwa mnakata toeni taarifa tusinunue vitu vya kuharibika.
 
TANESCO kama kuna mgao basi tupeni taarifa kuliko kukata kata umeme bila watu kujiandaa.
Siku ya tatu now huku Bunju B mnakata umeme asubuhi unarudi almost saa kumi na mbili na nusu.
Waziri akiulizwa oh, nipe week mbili za matengenezo, sijui kufikia March kutakuwa hakuna mgao lakini hakuna kinachotokea.
Basi mshaamua kuwa mnakata toeni taarifa tusinunue vitu vya kuharibika.
The same like here wazo madale yote.

Mkuu Waziri alipata mitamboo imechakaa anarekebisha. Tumpe miaka 5 ya matengenezo
 
Nikinunua umeme naambiwa invalid offset branch code hii maana yake ninini?
 
Jamani mimi malalamiko yangu ni kuhusu nyie Tannesco Mbezi Beach mmekuja nyumbani kwangu mkafunguliwa mlango /geti na kijana mkatoa linguzo lenu lililioza mkaliacha ndani kwangu na mawaya yenu ,mkavunja vigae vya nyumba mkaondoka na kuacha mguzo wenu mchafu nyumbani mdani kwangu sio ustarabu.

Naomba mje kutoa tuwe wastaarabu jamani.
 
Mmenipa hasara ya kutafuta fundi atengeneze vigae na mauchafu yenu mkayaacha. Sasa mimi nguzo naipeleka wapi na kwa nini mmeiacha.

Nina hasira sana leo kwa sababu mmekosa ustaarabu
 
Habari Tanesco! Tatizo langu ni Rushwa kukithiri ktk shirika letu hili... Wakazi wengi nikiwemo Mimi tumelipia umeme tokea October/November mwaka Jana lakini mpaka Leo hatujafungiwa hii ni kwa wilaya ya Ilemela_Mwanza! Walitutumia ujumbe kua wale wote waliolipia kabla ya 05/01/2022 watawekewa umeme kabla ya 31/03/2022 tukasema sawa... Ajabu kunaa nyumba ambazo tunaona wamefanya wiring ata wiki haijaisha wanawashiwa umeme...Ukienda Tanesco kuulizia wanakupa majibu ya kua ndo kwaanza tumewafikia wateja wa 20/09/2021 sasa unajiuliza ivi hawana uongo mwingine kila siku ni tupo mwezi wa 9 tu.. Anyway kinachonisikitisha ni vijana wao wanaoitwa ma surveyors wanapiga simu kwetu kua BOSs una laki 2 kesho nikuletee mita? Namba tunazo na ata recordings za hizo simu tunazo... Rushwa, Rushwa imetamalaki Tanesco Ilemela Mwanza!
NB... Tanesco naomba ujumbe huu muufikishe Kwa Meneja wa Tanesco Ilemela Mwanza haraka iwezekanavyo lasivyo tusilaumiane!
Mkuu unachopitia ndo napitia na mimi nipo Ilemela kata ya kahama huku ni ukiritimba tu unafanyika jirani zangu wamefunga wiring baada yangu ila cha ajabu wana umeme,mi nimelipia tangu October 2021 hadi Leo nazungushwa tu naona jamaa wanataka rushwa, ofisi ya TANESCO Nyakato Mwanza ina wapiga dili wengi sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu unachopitia ndo napitia na mimi nipo Ilemela kata ya kahama huku ni ukiritimba tu unafanyika jirani zangu wamefunga wiring baada yangu ila cha ajabu wana umeme,mi nimelipia tangu October 2021 hadi Leo nazungushwa tu naona jamaa wanataka rushwa, ofisi ya TANESCO Nyakato Mwanza ina wapiga dili wengi sana

Sent using Jamii Forums mobile app
Tafadhali onesha

Jina

Eneo

Wilaya

Simu

Umelipia lini

Kwa hatua zaidi
 
Back
Top Bottom