Tanzania na Equinor / Shell yasaini mradi wa thamani dola bilioni 30

Tanzania na Equinor / Shell yasaini mradi wa thamani dola bilioni 30

Huu sasa ndio mradi wa kweli wa maendeleo ya kweli wenye impact ya kweli kwenye uchumi wa nchi yetu kwasababu mradi huu ni mradi wa FDI, doleri bilioni 30 sawa na Trillion 70 za madafu, zinaletea kutoka nje zinakuwa injected ndani ya nchi yetu!, hii sio kitu ndogo!.

Japo bado hatujajua contents za huo mkataba, but definitely ule wasiwasi wangu kuhusu Gesi asili: Is it "day light robbery?" Watanzania tunaibiwa mchana kweupe! unakwenda kutokea!. Kuna kitu nilikisema hapo kuwa Tanzania tusipokuwa makini, kinakwenda kutokea, kwa ya juu juu niliyo sikia, nilichohofia kisitokee, ndicho kinakwenda kutokea!.

All and all, tumefika mahali lazima tukubali matokeo...

Pia Waziri wa Nishati, Mhe January Makamba, hili amelizungumza vizuri hapa


P

Ni pesa nyingi sana. Tahadhari mradi usije ukatengeneza ukanda mwingine wa Msumbiji ya Kaskazini.

Inaonesha ni vitu pacha.
 
Kiukweli on technicalities na costings mimi ni zero!. Nadhani hata hiyo LNG plant site kuwa off shore it has something to do with cost.
P
Ndio maana ukaambiwa kwenye gesi hujui kitu. Sasa ulikuwa unasifia nini na wakati hujui?
Yani hata details ndogo sana na kufanya comparison kupata reflection huwezi tiyari ushakimbilia kusifia. Alafu msomi mmoja pale UDSM mwenye alama za juu ila kazi kusifia wakati hujui unasifia nini
 
Sasa JK si walisema ni fisadi ndio maana nahoji kwa huyo mzalendo, msafi, malaika, kwanini alitamka kujitoa OGI iliyolazimu disclosure of matters with public interests kama mikataba ya rasilimali n.k?? Mpaka mikataba ya Bombardier, Ndege za ATCL kukamatwa ikawa Siri, Makubaliano ya Serikali na Barrick yakawa Siri maana hatujui hiyo kampuni inaendeshwa kwa mkataba upi n.k

Sasa kituko wafuasi wa mzalendo wanamuita Mama fisadi (Of course CCM wote wezi) anauza nchi kisa mikataba ya gesi haijawekwa wazi. Sasa ndio najiuliza huu unafiki ni kwa faida ya nani? Aliyezuia utekelezaji wa TAIT ni nani? Aliyeitoa Tanzania OGI ni nani??

Ndio natoa taarifa sasa kwamba mama naye hawezi iweka wazi sababu hata mtangulizi wake hakuweka na ndio hapo nasema JPM aliweka precedence mbovu.
Kusimama na kumtetea Magufuli ni kujitoa ufahamu na kujivunjia heshima, pamoja na kwamba alikuwa na kelele nyingi sana za hadaa, kuwazubaisha wananchi.

Tofauti, kama ipo tofauti kati yake na huyu Samia na Kikwete, hawa wawili hawajinadi na kuweka mbele lebo ya 'uzalendo' kama ngao yao ya kujikinga na uhalifu mkubwa wanaowafanyia waTanzania.

Hawa wanatumia lugha na ujanja ujanja wa kulainisha mitizamo juu ya mambo mabovu wanayoyafanya.

Siwezi kamwe kuwasifu kwa lolote juu ya kuifaidisha Tanzania, zaidi ya hao wanaoshughulika nao na wao wenyewe.
 
The fact kua reserve yetu in term of cubic ni less than mozambique bt mradi wetu una cost more than them must be a red flag, hakuna mzungu anafanya hio biashara kichaa, unless wamekaa gharama kubwa in purpose ili ROI ichukue muda mrefu.
Duh, hebu ifafanue vizuri hii mkuu 'Gobole', mbona inatisha?

Unayo gharama ya mradi wa Msumbiji?

Kama ni kweli, inafaa kushikilia hapo hapo ili tuweze kudadavua vizuri gharama za miradi hii miwili.
 
Kama huwezi kuona kasoro kubwa iliyopo katika utaratibu wetu katika kuwawezesha na kuwatumia wataalam wetu hadi hapa tulipofikia kama taifa, miaka 60 na zaidi baada ya uhuru; nadhani hiyo "optimism" unayoiomba sijui itapatikana lini, baada ya miaka mia?

Bottomline ni kwamba kama tunavyotawanya raslimali alizotujalia Mwenyezi Mungu, ndivyo hivyo hivyo tunavyotawanya raslimali ya watu wetu, wataalam wengi tulio nao kwa kutowapanga vizuri, kuwawezesha ili waweze kutumia utaalam wao kwa manufaa ya taifa hili.

Hadi hapo tutakapopata uongozi unaotambua kasoro hii na kuirekebisha, tutaendelea tu kuwa vitegemezi kwa hawa hawa wanaokuja kuzoa mali zetu na kuendelea kutuachia ufukara wetu.
Kwani china iliendeleaje? Si mpaka ilipofungua mipaka yake na ikashusha labor cost, masharti ya uwekezaji, Kodi, thamani ya pesa n.k Ili wawekezaji wamwagike na Leo hii imeshakua na viwanda vya wenyeji imetapakaa sababu ya technology spillover in fact na sisi tukiweza ku tap teknolojia wanazokuja nazo then tutaweza kuwa na local capacity ila hakuna nchi iliendelea bila FDI maana uchumi unahitaji fedha za kigeni na heavy manufacturing sector for value addition.

2. Alafu kama haufahamu exploration ya mafuta nimesahau ni Safu ya milima gani ila wametumika wataalamu wa TPDC kwenye process nzima. Kuna document moja ntaipandisha humu inaeleza Miradi kadhaa ya gas exploration huko Mnazi Bay na Mtwara ambayo TPDC walikua involved directly kwenye process. So sio kama hatuna wataalamu Wala uwezo nadhani tunakosa tu Capital ya ku facilitate hizo gharama na hauwezi ukakopa Mradi mkubwa hivo na hauna uzoefu sidhani kama Kuna nchi zingekubali ku risk.

3. Tanzania imeanzisha Sovereign Wealth Fund ambayo mapato yote ya gesi yatakazopatikana yatawekwa huko Ili tuweze kutunza thamani ya Gesi hata muda ambao gesi hiyo itaisha or uzalishaji utapungua so hizo ni positive moves ambazo ilipaswa tupongeze kwa hatua ya sasa.

Jamani tuwe optimistic maana kulalamika bila ku keep track ya progress haina manufaa.
 
Kwani china iliendeleaje? Si mpaka ilipofungua mipaka yake na ikashusha labor cost, masharti ya uwekezaji, Kodi,
Mkuu Zitto Jr, ninakumbuka tulishalizungumzia hili la wachina kati yako na mimi, kama siyo wewe, basi nitakuwa ni pengine mkuu Yoda.
Sikubaliani na hii dhana potofu kabisa kwamba wachina walisubiri kuingia watu wa nje ndipo maendeleo yao yakapatikana.
Huu ni upotoshaji.
Ukisema "kupata msukumo" wa haraka katika maendeleo yao, hapo tunaweza tukajadili hilo.

Mchina amejiandaa mwenyewe, kwa juhudi zake hadi hapo alipoamua kuingia duniani kuungana na wengine. Mchina alikuwa na ujuzi wake wa kufanya mambo, ndiyo maana mashirika yake yapo duniani kote leo hii, na hakuna anayetilia mashaka juu ya uwezo wake katika jambo lolote.
Huwezi kusema, haya yote aliyaokoteza harakaharaka katika miaka mitano baada ya kufungua nchi yake.
 
in fact na sisi tukiweza ku tap teknolojia wanazokuja nazo then tutaweza kuwa na local capacity ila hakuna nchi iliendelea bila FDI maana uchumi unahitaji fedha za kigeni na heavy manufacturing sector for value addition.
EeeenHeeee!

"Na sisi tukiweza kutap teknologia wanazokuja nazo..." China na Tanzania, vitu mbalimbali kabisa, mkuu wangu Zitto Jr..

Kulikuwa na takwa la uwepo wa kuwafundisha waTanzania kupata uwezo/uzoefu kwa makampuni yanayowekeza, na ilikuwa kumewekwa kiasi cha mwekezaji anachotakiwa kuleta watu wake..., hili limelegezwa kwa jina la kuvutia uwekezaji. Na muda wa hao wageni wanaoajiriwa ulikuwa na kikomo kabla ya kumpata mTanzania kushika nafasi, hilo nalo limelegezwa au halipo kabisa.
Najua unaelewa ninachokisema hapa.

Kwa hali hii ya uvutiaji wa uwekezaji, huwezi kamwe kusema utajenga uwezo wa wananchi wako 'kutakeover' majukumu na kujenga uwezo wa wananchi wako. It's just a joke!
 
Kwenye suala la uvunaji gas, ni kati ya makosa makubwa ya ajabu aliyoyafanya Magufuli. Leo hii Tanzania isingekuwa inafukuzana na vikodi vya kwenye Mpesa.

Mapato ambayo yangepatikana kwenye mradi wa gas, yakilinganishwa na dhahabu, yangekuwa sawa na kulinganisha bahari (gas) na tone (dhahabu) la maji.

Lakini Kivuruge aliharibu, wawekezaji wakaondoka, alipogundua kuwa ameharibu akaanza kuwasihi kwa siri warudi, wakagoma. Walipogoma akaanza kuongea uwongo eti gas ya Tanzania imeuzwa kwa wachina? Wajinga, bila hata ya kujiuliza imeuzwa kwa namna gani, wakamwamini.

Leo ni kama tunaanza upya,wakati tulikuwa tumekaribia hatua ya uzalishaji.

Hapo ndiyo unaona jinsi mtu mmoja anavyoweza kuleta madhara makubwa
 
2. Alafu kama haufahamu exploration ya mafuta nimesahau ni Safu ya milima gani ila wametumika wataalamu wa TPDC kwenye process nzima. Kuna document moja ntaipandisha humu inaeleza Miradi kadhaa ya gas exploration huko Mnazi Bay na Mtwara ambayo TPDC walikua involved directly kwenye process. So sio kama hatuna wataalamu Wala uwezo nadhani tunakosa tu Capital ya ku facilitate hizo gharama na hauwezi ukakopa Mradi mkubwa hivo na hauna uzoefu sidhani kama Kuna nchi zingekubali ku risk.
Usihangaike na kuitafuta makaratasi yahusuyo haya uliyoyazungumzia hapa, kwa sababu ninafahamu vyema jinsi gesi ile ilivyokuwa ikiungua kule Kilwa wakati inavumbuliwa na watu wetu wenyewe.
Tulikuwa tunapiga hatua. Sasa hivi tumewafifisha sana watu wetu kuonyesha uwezo wao walionao. Badala yake, wengi wao wanakimbilia kwenye siasa, kama walivyo waandishi wa habari na wengi wengine ili wakafaidi keki ya cnhi, kwani huko ndiko inakopatikana kiurahisi.

Tulikuwa na mipango mizuri kabisa ya ujenzi wa viwanda vya madawa, ili nchi yetu ijitosheleze kwa madawa muhimu kwa magonjwa yanayotukabili. Hatukuwa na wataalam wa kufanya shughuli huko, wakasomeshwa wengi nchi za nje, na wakapata ujuzi unaoweza kuupata popte duniani katika fani hiyo.
Sasa angalia tulipo na maswala ya upatikanaji wa dawa nchini mwetu! Siyo kwamba hakuna wataalam katika fani hiyo, lakini hakuna uongozi unaoelekeza juhudi hizo zifanyike kwa ufanisi.
Tunagusia gusia tu kila jambo, hatuna popote tunapojiimarisha ili tupate ufanisi.
 
Nilichopenda na realistic timeline! Miaka 7!
Ila, ingekuwa mtu fudenge ungesikia jukwaani mradi lazima ukamilike 2025! Ili azindue hata kama ni theluthi Tu iliyokamilika!
 
Kwenye suala la uvunaji gas, ni kati ya makosa makubwa ya ajabu aliyoyafanya Magufuli. Leo hii Tanzania isingekuwa inafukuzana na vikodi vya kwenye Mpesa.

Mapato ambayo yangepatikana kwenye mradi wa gas, yakilinganishwa na dhahabu, yangekuwa sawa na kulinganisha bahari (gas) na tone (dhahabu) la maji.

Lakini Kivuruge aliharibu, wawekezaji wakaondoka, alipogundua kuwa ameharibu akaanza kuwasihi kwa siri warudi, wakagoma. Walipogoma akaanza kuongea uwongo eti gas ya Tanzania imeuzwa kwa wachina? Wajinga, bila hata ya kujiuliza imeuzwa kwa namna gani, wakamwamini.

Leo ni kama tunaanza upya,wakati tulikuwa tumekaribia hatua ya uzalishaji.

Hapo ndiyo unaona jinsi mtu mmoja anavyoweza kuleta madhara makubwa

Tuambie mapato yanayopatikana kwenye gas Mtwara umefaidika na nini mpaka sasa???
 
Ziara ya mheshimiwa rais huko Oman ameongozana na January Makamba waziri wa nishati, waziri atumie wasaa huu kuangalia suala la gesi asilia LNG Oman wamefanikiwa vipi nasi tuige

12 June 2022
Muscat, Oman

Morning Minute : Oman LNG's revenues reach over $3 billion in 2021


Source : Omani News Agency

1655029930-1655029930-hbafu2akddl3.jpg

Muscat: The revenues of the Oman Liquefied Natural Gas (LNG) Company’s revenues increased by 31 per cent to reach more than $3 billion at the end of 2021.

“The revenues of the Oman Liquefied Natural Gas Company at the end of 2021 witnessed a growth of 31 per cent to reach 3,278 million US dollars compared to the end of 2020, as a result of the rise in global energy prices,” Oman News Agency (ONA), said in a statement.

The annual report indicates that the company’s net income at the end of 2021 increased by 34 per cent to reach $886 million. The company has allocated about $37 million to its social responsibility programs and initiatives.

The report shows that the liquefied natural gas sector provided government revenues from gas to about 2,873 million US dollars during the past year.

The production rates of the Oman Liquefied Natural Gas Company increased to record levels of 10.6 million metric tons during 2021. It is hoped that the production capacity of locomotives will reach more than 11 million metric tons after the completion of strategic projects in the industrial complex in Qalhat
 
Mkuu Zitto Jr, ninakumbuka tulishalizungumzia hili la wachina kati yako na mimi, kama siyo wewe, basi nitakuwa ni pengine mkuu Yoda.
Sikubaliani na hii dhana potofu kabisa kwamba wachina walisubiri kuingia watu wa nje ndipo maendeleo yao yakapatikana.
Huu ni upotoshaji.
Ukisema "kupata msukumo" wa haraka katika maendeleo yao, hapo tunaweza tukajadili hilo.

Mchina amejiandaa mwenyewe, kwa juhudi zake hadi hapo alipoamua kuingia duniani kuungana na wengine. Mchina alikuwa na ujuzi wake wa kufanya mambo, ndiyo maana mashirika yake yapo duniani kote leo hii, na hakuna anayetilia mashaka juu ya uwezo wake katika jambo lolote.
Huwezi kusema, haya yote aliyaokoteza harakaharaka katika miaka mitano baada ya kufungua nchi yake.
Kipindi Cha chairman Mao au Chiang Kai Shek China ilikua na uchumi Gani ndugu yangu, sembuse Japan was a power but China ilikua maskini kuna mpaka wakati watu zaidi ya million 20 walikufa kwa njaa.

Ukweli ni kuwa toka waache ujamaa na kuhamia ubepari (Yes you heard it right, ubepari) ndioo wawekezaji walimwagika na ndio hata private Chinese entrepreneurs wakapata capacity ya kwenda ku compete na west. Nimekueleza pia walikua Wana tap technology spillover kiasi kwamba reverse engineering iliwezesha waweze kutengeneza bidhaa zao kwa wingi na kuuza nje. Hata Leo hii viwanda vya assembly vingi vimejengwa china na Asia maana labor Iko chini so obviously ajira, branding, technology spillover, multiplier effect etc imekuza uchumi wa China, sasa unawezaje ondoa role ya FDI China hata kama itachangia 30% ya ukuaji wao?

Kujiandaa Is one thing execution is another ndio maana utakuta kuna nchi Zina potential ila hazisongi mbele sio kama hazina wasomi au Nia ila kuna component moja tu ikitick basi uchumi unapaa. So usiondoe role ya FDI China unless uje na data hapa za kwamba china ilikua Ina uchumi mkubwa before wawe open economy .
 
EeeenHeeee!

"Na sisi tukiweza kutap teknologia wanazokuja nazo..." China na Tanzania, vitu mbalimbali kabisa, mkuu wangu Zitto Jr..

Kulikuwa na takwa la uwepo wa kuwafundisha waTanzania kupata uwezo/uzoefu kwa makampuni yanayowekeza, na ilikuwa kumewekwa kiasi cha mwekezaji anachotakiwa kuleta watu wake..., hili limelegezwa kwa jina la kuvutia uwekezaji. Na muda wa hao wageni wanaoajiriwa ulikuwa na kikomo kabla ya kumpata mTanzania kushika nafasi, hilo nalo limelegezwa au halipo kabisa.
Najua unaelewa ninachokisema hapa.

Kwa hali hii ya uvutiaji wa uwekezaji, huwezi kamwe kusema utajenga uwezo wa wananchi wako 'kutakeover' majukumu na kujenga uwezo wa wananchi wako. It's just a joke!
Mkuu acha kauli za jumla jumla, binafsi nimewahi fanya tafiti nikagundua kuna huduma nyingi tu za kiafya tulikua tunazifuata India na kwingineko ila kwa sasa zinafanyika bongo tena hospitali za serikali na tukaestimate gharama iliyookolewa na tukakuta Mabilion yameokolewa ila nyie hamuoni hayo mnaangalia tu gap ilipo. Hata makampuni ya ndege kuna pilots weusi wengi kuliko miaka 20 nyuma so tusijilimit kwamba kuna sekta hatuwezi tap technical know-hows etc.

Kuna mahali unadai Sheria zimelegezwa yes inaweza kuwa short term benefits za Kodi zinaangaliwa ila tukubali Sheria nyingi sahivi zimebana kuliko huko nyuma kuna reforms za Transfer payments, 16% shares kuwa publicly traded, local content, kuna kuacha walau 25% kama sikosei ya mapato kwenye benki za ndani, kuna limitation ya Kuhamisha pesa nje kutoka Kwa wawekezaji n.k so kuna Sheria zimebana upande mmoja na kuachiwa upande mwingine sasa ni hatari wewe kuangalia tulipolegeza bila kusahau akishafika kuna mahali atabanwa.

Miaka 10 iliyopita hata capital gain tax ilikua hailipwi wakiuziana hisa Leo huoni reforms unalalamika component moja tu?

Mimi siitetei CCM ila kwenye mijadala ya kitaifa tunajaribu kuwa balanced Ili tunapofikiria tusiwe biased otherwise tutakua tunapinga Kila Mradi kwa kigezo Cha kwamba "tutaibiwa". As if huo Mradi wakipewa wakina Rostam au Makamba ndio hawatoiba??
 
Tuambie mapato yanayopatikana kwenye gas Mtwara umefaidika na nini mpaka sasa???
Kuna sovereign wealth fund imefunguliwa so gesi ya Mtwara kwa inayouzwa mapato yataenda kwenye huo Mfuko ambao unainvest in multiple projects nje na ndani ya nchi.

Kingine gesi ya Mtwara Leo hii imesababisha 60% ya umeme wa Tanzania kutegemea gesi meaning ime double capacity ya umeme wetu at least kwa demand ya miaka 5 iliyopita.

So tusibeze tu Kila kitu faida zinakuja taratibu, Bomba lilicost Mabilion na uchimbaji matrillion so Mradi utajilipa after years kuweni wavumilivu huku mkichekelea umeme wa gesi hapo ulipo na ukipikia gesi maana ushasahau Kuni na mkaa!!!
 
Ziara ya mheshimiwa rais huko Oman ameongozana na January Makamba waziri wa nishati, waziri atumie wasaa huu kuangalia suala la gesi asilia LNG Oman wamefanikiwa vipi nasi tuige

 
Back
Top Bottom