Tanzania tuachane mfumo wa kupandishia watu mishahara bila kuwa na vigezo vya utendaji (performance)

Tanzania tuachane mfumo wa kupandishia watu mishahara bila kuwa na vigezo vya utendaji (performance)

Umetazama upande mmoja wa shilingi, serikali yenyewe nayo itengeneze mazingira mazuri ya kazi kwa watumishi wake, kwamfano ;
  1. Vitendea kazi ni duni sana katiika maeneo mengi ya kazi kiasi kwamba kama mfanyakazi angetakiwa kumaliza kazi ndani ya saa moja, basi anatumia masaa mawili au matatu kwakuwa vifaa vya kazi ni duni
  2. Huduma nyingi za kiutumishi ziko hafifu sana katika maeneo ya kazi, kwamfano, mtumishi anakaa mbali na sehemu ya kazi, usafiri ni shida, kama anatumia usafiri wa bus la ofisi muda mwingi bus linachelewa kufika kituoni kuwachukua wafanyakazi na kuwarudisha kwasababu nyingi tu ikiwemo foleni, ubovu wa bus, kukosekana kwa mafuta nk, hata kwa wale wanaotumia usafiri wa mabasi ya biashara, huko ndiyo usiseme.
  3. Watumishi hawapewi nyumba za kuishi karibu na kazini walipo, matokeo yake wanapanga nyumba, kodi inakuwa kubwa, wanalazimika kwenda kupanga au kujenga vyumba viwili au vitatu mbali kabisa kwenye nafuu ya bei ya vyumba au viwanja, unategemea mtumishi wa namna hiyo atakuwa na perfomance kazini? Labda uwe boss, una usafiri wa kupewa na ofisi au nafasi yako nzuri una uwezo wa kujaza mafuta kwenye gari lako.
  4. Serikali haitoi nauli wala communication allowance kwa watumishi wa kada ya chini, hii inawapunguzia uwezo wa utendaji kazi watumishi wake, yapo mashirika binafsi yanatoa huduma hizi kwa watumishi wao na mambo yanakwenda vizuri, lakini ikiwa mtumishi hapewi subsidy ya vitu kama hivyo matokeo yake anatumia mshahara wake kuisaidia serikali kufanya mawasiliano na wakuu wake na pia kwenda na kurudi kazini, wakati mwingine anatumia nauli yake kwenda kufuatilia masuala ya ofisi kwasababu ofisi haina fungu la nauli wala simu.
Kabla ya kuwalaumu watumishi, ipo haja serikali ijjitazame je imetimiza wajibu wake kwa watumishii wake katika kila eneo la kazi?
Hayo yafungulie uzi wa mada yake.. Hapa mada ni namna ya kuongeza mishahara na vyeo.

Hakuna aliyelaumiwa hapa. Kusema watu wana underperform siyo kulaumu bali vigezo vyao vikiainishwa halafu hujawapa vitendea kazi watakuwa na haki ya kuachana na hiyo kazi, kwanini ufanye kazi sehemu ambayo haikupi vitendea kazi? utakuwa juha au haufahamu "fundamentals" za kazi yako.

Mfano wewe fundi mekanika uambiwe tengeneza magari bila spana? Ukikubali si wewe ndiye juha au mzembe, hakuna zaidi.
 
Mawazo mazuri mkuu...ila nani atafanya hio appraisal kwa mwenzake?? kila mtu ana interests zake akiwa kazini, the whole system iko corrupted
 
Mfano nchi niliyokuwepo kuna "performance appraisal" lakini inajazwa na "Private inspecting consultants". (Factor) kigezo cha kwanza kabisa ni katika kila kazi kuna kitu kinaitwa "fundamentals "za hiyo kazi. Inspector ndicho kitu cha kwanza anatazama. Asiyefata "fundamentals" za hiyo kazi anarudishwa akaisomee tena hiyo kazi (akiwa kazini),
Kwa hapa kwetu usishangae huyo inspector atapewa mlungura anaishia zake siku imeingia🤣
 
Bado sana,Kazi zenyewe hizi za Mjomba na Shangazi.
 
Kwa hapa kwetu usishangae huyo inspector atapewa mlungura anaishia zake siku imeingia🤣
Hapo kutakuwa kuna uzembe kwa mtoa na mpokea hilo hongo.

Nyerere aliwahi kuongelea rushwa ya kwetu huku na ya nchi zilizoemdelea. Ilikuwa kama hivi (simnukuu neno kwa neno bali nilivyoelewa mimi) Kule alisema anapewa mkandarasi kazi kwa kuwa ana mtu wake hapo alipopewa hiyo kazi lakini kazi inafanyika. Hapa kwetu anapewa mtu hiyo kazi kwa kuwa kuna mtu wake na kazi haifanyiki.

Utajaza mwenyewe.
 
Hapo kutakuwa kuna uzembe kwa mtoa na mpokea hilo hongo.

Nyerere aliwahi kuongelea rushwa ya kwetu huku na ya nchi zilizoemdelea. Ilikuwa kama hivi (simnukuu neno kwa neno bali nilivyoelewa mimi) Kule alisema anapewa mkandarasi kazi kwa kuwa ana mtu wake hapo alipopewa hiyo kazi lakini kazi inafanyika. Hapa kwetu anapewa mtu hiyo kazi kwa kuwa kuna mtu wake na kazi haifanyiki.

Utajaza mwenyewe.

Nakumbuka alitolea mfano wa ujenzi wa barabara kama sijakosea sana alikuwa ameulizwa swali na mwandishi wa habari, anyway ndiyo sisi hao
 
Hapo ni kama kusema CAG anapokea hongo?
Mkuu, kuna uzi humu unawalalamikia hao watendaji wa CAG kuwa wamekula sana rushwa huko walikopita kufanya kazi, bahati mbaya sikumbuki title yake
 
Bado sana,Kazi zenyewe hizi za Mjomba na Shangazi.
Ndio hivyo, hayajaanza leo, wakati wa Nyerere tulikuwa tunaziita "undugu-naizeshen".

Tena ni bora sasa kwa Mama hatulioni hilo. Ingekuwa linaonekana tungeona Waunguja wamejaa kila sehemu. Umesahau juzi tu, wakati wa bwana yule?
 
Nakumbuka alitolea mfano wa ujenzi wa barabara kama sijakosea sana alikuwa ameulizwa swali na mwandishi wa habari, anyway ndiyo sisi hao
Yes.Sawa kabisa.
 
Ndio hivyo, hayajaanza leo, wakati wa Nyerere tulikuwa tunaziita "undugu-naizeshen".

Tena ni bora sasa kwa Mama hatulioni hilo. Ingekuwa linaonekana tungeona Waunguja wamejaa kila sehemu. Umesahau juzi tu, wakati wa bwana yule?


Nice to see you tonight, 👍🤣

Nilikufungulia uzi humu sikuoni rafiki, furaha yangu kukuona.

Sikujua kama nachangia uzi wako kiongozi
 
Kweli kabisa. Ni mfumo ambao hata tuhangaike vipi na takwimu hautotupandishia uchumi kwa haraka. Ukichukulia kuwa Serikali ndio moja ya waajiri wakubwa sana Tanzania na nnauhakaika over 90% ya waajiriwa serikalini ni underperformers.

Wengi wanaokimbilia kazi za serikalini ni wazembe na wabadhirifu.
Mixer wakikutana na hawa so called wanasiasa alooh hii nchi bado sana
 
Hujajibu swali nililokuuliza. Sasa wewe mjuaji lijibu kwanza swali hilo halafu uendelee na ujuwaji wako. Linakushinda nini kujibu? nakuongeze swali lingine hapa chini...

Hiyo katiba iliandika wapi kuwa kupandishwa mishahara na vyeo mpaka kutegemee huruma ya Rais?


Wewe itakuwa katika wale wfanyakazi wazembe ambae hutaki "performance" yako ipimwe. Endelea kusubiri huruma ya Rais.
Kwani hoja ya msingi ni kupanda kwa mshahara? Ambapo wewe unadai eti mpaka mtu afanyie appraisal? Hii haipo kikatiba maana ibara ya 23 inaweka wazi kuwa mtumishi ana haki ya kupata mshahara stahiki kukidh mahitaji yake.

Hapa Tanzania unachodai kuwa hakifanyiki kinafanyika sana. Ndio maana kila mwaka watumishi wanajaza Opras kusimamiwa na wakuu wao wa kazi. Wewe hujui kitu umekurupuka
 
Tanzania tuachane kabisa na mfumo wa kuwapandishia watu mishahara au vyeo bila kuwa na vigezo na vipimo vya "performance" zao.
Nashauri kwanza viwekwe vigezo na vipimo vya "performance" kazini ndivyo vitumike kuwapandisha watu vyeo na mishahara.

Ni wepesi sana kupanga vigezo vya ubora wa utendaji kwa kila kazi katika kila sehemu ya kazi. Tena siku hizi kila kitu kinakuwa kwenye data base kidigitali ni wepesi sana. Wale watendaji bora (best performers) watapanda mishahara na vyeo haraka na wale wazembe (kama ilivyo kwa Watanzania wengi) watasota hapo hapo na mshahara wa "entry level" mpaka wabadilike au wajiachishe wenyewe kazi.

Mfumo huu wa "performance based" upo na unatumika sana ulimwenguni, hususan kwenye kazi zisizo za Serikali, pia serikali nyingi zimeanza kutumia mfumo huo, bila kuoneana aibu wala huruma za kijinga.

Uzoefu wangu wa kufanya kazi za kuajiriwa kwa muda mrefu sana katika nchi zilizoendelea umenifundisha hayo.
Nianze kwa kukupongeza Mkuu Dada yetu FaizaFoxy kwa mada hii. Hizi ndio mada za kwa maslahi ya taifa. Naunga mkono hoja

Mimi nilianzia kazi serikalini early 1990s. Mwaka 1998 mradi wa PSRP ilikuja na kuleta Sheria mpya ya utumishi wa umma, sheria No. 8 ya Mwaka 2002 ili introduce performance appraisal system ya OPRAS, kila mwanzo wa mwaka unajiwekea smart objectives na bosi wako, katikati ya mwaka mnafanya MTR, na mwisho wa mwaka mnafanya review based on performance ya zile SMART objectives.

Haya yote yalifanyika kupitia PSRP Project, sasa sijui hali ikoje.
P
 
Nianze kwa kukupongeza Mkuu Dada yetu FaizaFoxy kwa mada hii. Hizi ndio mada za kwa maslahi ya taifa. Naunga mkono hoja, Mimi nilianzia kazi serikalini early 1990s. Sheria mpya ya utumishi wa umma, ya1999, ili kuzuia introduce performance appraisal system ya OPRAS, kila mwanzo wa mwaka unajiwekea smart objectives na bosi wako, katikati ya mwaka mnafanya MTR, na mwisho wa mwaka mnafanya review based on performance ya zile SMART objectives.

Haya yote yalifanyika kupitia PSRP Project, sasa sijui hali ikoje.
P
Mzee Paskali mimi sio mtumishi ila nina mwenzangu ni mtumishi wa umma. Opras huwa zinajazwa kila mwaka. Na ndik tahmini pekee ya kujua utendaji kazi wa mtumishi .

Afisa utumishi ndio huwa anafanya appraisal na kuzituma mahala husika.

Ibara ya 23 ya katiba ya JMT inatoa haki ya mtumishi yoyote yule kupata mashahara unaokidhi mahitaji. Hii haimanishi kuwa lazima afanyiwe tathimini maana haki ya kukidhi mahitaji ni haki ya kikatiba.
 
Mzee Paskali mimi sio mtumishi ila nina mwenzangu ni mtumishi wa umma. Opras huwa zinajazwa kila mwaka. Na ndik tahmini pekee ya kujua utendaji kazi wa mtumishi .

Afisa utumishi ndio huwa anafanya appraisal na kuzituma mahala husika.

Ibara ya 23 ya katiba ya JMT inatoa haki ya mtumishi yoyote yule kupata mashahara unaokidhi mahitaji. Hii haimanishi kuwa lazima afanyiwe tathimini maana haki ya kukidhi mahitaji ni haki ya kikatiba.
Mkuu Idugunde , appraisal haifanywi na ofisa utumishi, inafanywa na your line manager, kazi ya ofisa utumishi ni usimamizi na kuzituma.

Sijaingia kwenye hicho kifungu cha katiba kuhusu mishahara, ila kwenye hili la mishahara, niliwahi kutofautiana na Blaza wangu,Rais hana mamlaka ya kupunguza mshahara wa mtumishi yeyote
kufunga macho kufungua!, aliweza!. Aliwezaje?!, sijui!.
P
 
Bi Faiza nakuunga mkono kwa asilimia zote

Tena mimi huwa natamani hata mchakato wa kuajiri waalimu ziingizwe interviews, haiwezekani graduates wengi mtaani lakini kigezo bado ni degree!!

Mwisho wa siku waalimu wanaochaguliwa wengine ni tia maji tia maji na wakishaingia hawafanyiwi review yoyote hata wakifelisha consistently.
 
Tanzania tuachane kabisa na mfumo wa kuwapandishia watu mishahara au vyeo bila kuwa na vigezo na vipimo vya "performance" zao.
Nashauri kwanza viwekwe vigezo na vipimo vya "performance" kazini ndivyo vitumike kuwapandisha watu vyeo na mishahara.

Ni wepesi sana kupanga vigezo vya ubora wa utendaji kwa kila kazi katika kila sehemu ya kazi. Tena siku hizi kila kitu kinakuwa kwenye data base kidigitali ni wepesi sana. Wale watendaji bora (best performers) watapanda mishahara na vyeo haraka na wale wazembe (kama ilivyo kwa Watanzania wengi) watasota hapo hapo na mshahara wa "entry level" mpaka wabadilike au wajiachishe wenyewe kazi.

Mfumo huu wa "performance based" upo na unatumika sana ulimwenguni, hususan kwenye kazi zisizo za Serikali, pia serikali nyingi zimeanza kutumia mfumo huo, bila kuoneana aibu wala huruma za kijinga.

Uzoefu wangu wa kufanya kazi za kuajiriwa kwa muda mrefu sana katika nchi zilizoendelea umenifundisha hayo.
Wazo zuri....ila subirini tustaafu

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Hapa Tanzania appraisal hufanyika kila mwaka. Na kuna form inaitwa Opras huwa inajazwa. Lakini kima cha chini dunia nzima hakijawahi kufanyika kutolewa ubaguzi.

Kwa ufupi tahimini hapa Tanzani hufanyika kila mwaka sema wewe hujui lolote ni mlopokaji tu.
Sasa wewe unaandika halafu unajipinga mwenyewe. Unaelewa ulichokiandika? Au ndio meamka nazo "kangala"?
 
Back
Top Bottom