Tatizo la kununua Umeme wa LUKU: Waziri Kalemani amsimamisha kazi kwa siku 10 Meneja wa TEHAMA wa TANESCO

Tatizo la kununua Umeme wa LUKU: Waziri Kalemani amsimamisha kazi kwa siku 10 Meneja wa TEHAMA wa TANESCO

Umekomboka vipi.kudumu mrefu maana yake nini. ungesema haina kikomo.ya muda itakwisha tu na unaweza kununua siku mitambo imelala kama wakati huu. jiongeze

Duh.. una tatizo.. sasa swahili kama inakushinda.. si ujifunze.. ungenishukuru nimekupatia mwanya wa kujua unaweza ukaweka wa kudumu miezi mingi au hata mwaka na sio.. hiyo unafanya ya masaa kwa masaa au siku kwa siku..

Jinsi muntu qnataka kuishi.. ni chaguo..

Kazi iendeleee
 
Waziri wa Nishati, Medard Kalemani amewasimamisha kazi kwa siku 10 Meneja wa TEHAMA na Huduma za Biashara wa TANESCO, Lonus Feruzi na wasaidizi wake Frank Mushi na Idda Nja.

Ametaka watoe maelezo ya tatizo la mifumo ya LUKU, na kuagiza maelezo yao yasipojitosheleza waondolewe kazini.

==
Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani amemsimamisha kazi kwa siku kumi Meneja wa Tehama na huduma za biashara wa Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) Lonus Feruzi na wasaidizi wake Frank Mushi na Idda Njau, ili watoe maelezo kufuatia kuwepo kwa tatizo katika huduma ya manunuzi ya LUKU kupitia njia za Kielekroniki.

Dkt. Kalemani amewaambia Waandishi wa habari mkoani Dar es salaam kuwa, endapo maelezo yao hayatajitosheleza Watumishi hao waondolewe kazini.

Kwa muda wa takribani siku tatu, wateja wa TANESCO wameshindwa kununua umeme wa LUKU kwa njia.ya Kielekroniki, na hivyo kulilazimu shirika hilo kuwaelekeza Wateja wake kununua umeme kwenye ofisi zake za mikoa na wilaya katika maeneo mbalimbali nchini.
Angemsimamisha kimya kimya halafu angetutangazia huduma imerejea Kisha atupe mrejesho wa hatua alizochukua ndio ningemuona mzalendo, vinginevyo ni zile Kiki Kama Kiki nyingine.
 
Nimenunua kwa NMB Mkononi imekubalii..
Daaa afadhali, maana sio kwa foleni ile iliyopo tanesco
 
Hivi systems zikiwa hacked halafu wahuni wakachukua hela, Tanzania kuna sheria za kulazimisha shirika kutoa habari hizo?

Maana mifumo yetu ya ICT security ni hafifu sana, na mitandao siku hizi imejaa hackers na watu wanaodai ransomware, wananchi watajuaje hizi habari kama TANESCO hawajashurutishwa kisheria kutoa habari hizi?
 
Hivi systems zikiwa hacked halafu wahuni wakachukua hela, Tanzania kuna sheria za kulazimisha shirika kutoa habari hizo?

Maana mifumo yetu ya ICT security ni hafifu sana, na mitandao siku hizi imejaa hackers na watu wanaodai ransomware, wananchi watajuaje hizi habari kama TANESCO hawajashurutishwa kisheria kutoa habari hizi?
Umenikumbusha jamaa wa Colonial Pipeline!

Wana supply takriban 45% ya mafuta upande wa East Coast.

Jamaa wamelipa $4.4 kwa hackers waliodukua mfumo wao wa uendeshaji!

Kama kampuni kubwa kama Colonial Pipeline [iliyo Marekani…their headquarters are kitty corner from me], inadukuliwa na kushikwa mateka kwa zaidi ya wiki mpaka inalazimika kulipa mamilioni ya dola [in terms of bitcoin], kudukua taasisi za Kitanzania ni cha mtoto!

Siku tunaweza kuamka na habari kuwa benki za NBC na CRDB zimedukuliwa au spitali ya Muhimbili imedukuliwa na taarifa za wagonjwa ziko mikononi mwa hackers!

The threat to cybersecurity is real!
 
Umenikumbusha jamaa wa Colonial Pipeline!

Wana supply takriban 45% ya mafuta upande wa East Coast.

Jamaa wamelipa $4.4 kwa hackers waliodukua mfumo wao wa uendeshaji!

Kama kampuni kubwa kama Colonial Pipeline [iliyo Marekani…their headquarters are kitty corner from me], inadukuliwa na kushikwa mateka kwa zaidi ya wiki mpaka inalazimika kulipa mamilioni ya dola [in terms of bitcoin], kudukua taasisi za Kitanzania ni cha mtoto!

Siku tunaweza kuamka na habari kuwa benki za NBC na CRDB zimedukuliwa au spitali ya Muhimbili imedukuliwa na taarifa za wagonjwa ziko mikononi mwa hackers!

The threat to cybersecurity is real!
Mbona unaongea kwa sauti… shhhhhhhhhh….tafadhali. Copycats wapo tena wanaweza kutumia RaaS (Ransomware as a Service) halafu mnagawana Dau!
 
Uzembe ni kwamba jamaa hawakuwa na backup plan incase mfumo umezingua
 
Hivi systems zikiwa hacked halafu wahuni wakachukua hela, Tanzania kuna sheria za kulazimisha shirika kutoa habari hizo?

Maana mifumo yetu ya ICT security ni hafifu sana, na mitandao siku hizi imejaa hackers na watu wanaodai ransomware, wananchi watajuaje hizi habari kama TANESCO hawajashurutishwa kisheria kutoa habari hizi?
Kwa nini unadhani mifumo yetu ya ICT ni dhaifu sana? Ingekuwa dhaifu si kila siku mabenki yangepoteza fedha au serikalini fedha zingepotea. Kuna tofauti ya mifumo kuwa dhaifu na mfumo kupata hitilafu.
 
Navyoona Mimi amekurupuka kwa kuwasimamisha bila ya ku solve kwanza tatizo.
Hao waliosimamishwa huenda ndo key players na Wana Access katika Manipulation za Database za mtandao mzima.
Ni vizuri angewaacha wafanye kazi watoe incident Report,halafu ndo awasimamishe.
Pamoja na hayo lazima kuwe na Backup plan endapo kukitokea tatizo Kama hili "Backup Plan "iko Automated.
Kitengo Cha Programing na Electronic Team nzima lazima iwe na Utaalamu ambao ni "Asymetrical"mfano akiondoka A1,A2 anaweza ku manipulate sawasawa na A1.
Suala la kuwasimamisha kazi bila tatizo kutatuliwa naona Muheshimiwa kalichukulia hasira na kisiasa na Kama binadamu na kiongozi hakuna jinsi ambapo angeweza ku strike balance bila kufanya hivyo.
Hawa wakitoa technical Reasons zozote wakarudishwa kazini Basi kimantiki Mheshimiwa Waziri ataonekana Ni mwenye maamuzi ya jazba ,wakati namjua Ni msomi kwa kushuka chini kwa level hiyo
Hilo la backup linafikirisha sana, maana always kwenye IT backup ni ushauri wa kila siku yaani ni sawa na dose ya daktari 2 kutwa mara tatu . Kama hawakuwa na backup then ni tatizo, na sipendi kuamini shirika kubwa kama TANESCO wasiwe na backup
 
Hao wamefanywa kuwa mbuzi wa kafara hii issue ilitakiwa ianze na waziri mwenyewe.
 
Kwa nini unadhani mifumo yetu ya ICT ni dhaifu sana? Ingekuwa dhaifu si kila siku mabenki yangepoteza fedha au serikalini fedha zingepotea. Kuna tofauti ya mifumo kuwa dhaifu na mfumo kupata hitilafu.
Nimefanya kazi katika mifumo hiyo, level ya juu kabisa Tanzania, na tangu nilipofanya kazi mpaka sasa hakuna kilichobadilika sana. Naongea na watu wanaofanya kaz kwenye hiyo mifumo.

Hali ni mbaya sana kuliko wengi wanavyofikiri.

Ikulu ya Tanzania mpaka utawala wa Kikwete ilikuwa inatumia email ya Yahoo.

System Administrators wengi hawajui curent threats. Na hivyo hawana patching strategy.Hili ni tatizo dunia nzima, nachelea Tanzania ni zaidi.

Mimi nauliza, Tanzania kuna sheria za kulazimisha organizations kufanya disclosure kukiwa na wizi wa kumtandao?

Wewe unajibu mbona hatuoni wakiibiwa?

Sasa wakiibiwa na wewe usipofahamishwa kwa sababu hakuna sheria ya kushurutisha disclosure, utajuaje wameibiwa?

Unaelewa benki inaweza kuibiwa hela zako nyingi na wewe usijue, kwa sababu benki inaweza kuzungusha pesa tu, ukija kutoa hela wewe wakakupa za Juma, akija Juma wakampa za Rose, na as long as wote hamji kutoa hela siku moja benki itaendelea kufanya kazi kama vile hela hazijaibiwa?
 
Mbona unaongea kwa sauti… shhhhhhhhhh….tafadhali. Copycats wapo tena wanaweza kutumia RaaS (Ransomware as a Service) halafu mnagawana Dau!
Professional hackers don’t need no ideas from me!
 
Back
Top Bottom