Tofauti kati ya Waarabu, Warusi, Wamarekani na wazungu kuhusu utu wa mtu

Tofauti kati ya Waarabu, Warusi, Wamarekani na wazungu kuhusu utu wa mtu

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
21,470
Reaction score
40,593
Ulaya na Marekani, Serikali inawajibika kwa wananchi ila Uarabuni na Urusi wananchi ndiyo wanawajibika kwa serikali. Matokeo yake Marekani na Ulaya inawezekana wananchi kuandamana kwa maelfu kupinga kinachofanywa na serikali na wasiuawe kwa kukukusudia.

Lakini kwenye nchi nyingi za Kiarabu na Urusi, wananchi wakiandamana ni lazima kwa kukusudia watauawa, kuteswa na kufungwa jela bila wakati mwingine kanuni za kisheria kufuatwa.

Marekani na ulaya watu wao wakiuawa vitani, wananchi wanataka kujua ni kwa nini ndugu zao wamepelekwa vitani. Kuanzia vita ya Vietnam, Operesheni ya Somalia, vita ya Ghuba na hata sasa ya Ukraine, wananchi wa ulaya wasiozipenda vita hizo, huandamana kuonesha hisia zao.

Fikiria kama Wanajeshi wa Urusi waliouawa zaidi ya 20,0000 ingekuwa wanajeshi hao ni Wamarekani ama wametoka kwenye nchi mojawapo wa ulaya. Unadhani wananchi wa nchi hizo wangekaa kimya?
 
Nchi ya kiarabu ipi kuwa specific kulikuwa na Arab spring tumeiona Maraisi kibao wamejiuzulu nchi zilizotokea machafuko baada ya hayo maandamano ni Libya na Syria na kote tunajua nani alikua anadondosha silaha watu wapigane.

Leo Kuna maandamano Tunisia ya Amani tu sababu Raisi ni kibaraka wao ila Angekua Gadaffi ndo Raisi wa Tunisia sasa hivi waandamanaji wangekua na SMG zilizodondoshwa.
 
Vipi hapo wanapo sifiwa kuupiga mwingi ni wanainchi wanaowajibika kwa serikali au Ni serikali inayo wajibika kwa wanainchi?

BTW, Ufaransa watu wanaandama kutokana na hali ngumu ya maisha, wakimtaka Macron ajiuzulu, na zaidi watu wametiwa nguvuni. Vipi huko Ni serikali inawajibika kwa wanainchi au ni vice versa?
 
Nje kidogo na mada.. tetesi zilizopo ni kwamba maafisa wa Urusi na watu binafsi walio na Mari nyingi pale cremia wanaziuza kwa kasi sana Mari zao na kuhamisha familia zao nje ya cremia.. Kuna kitu kinakuja hapo mbele.
Mari nyingi pale cremia..

Cremia ndio wapi kaka, mari ndio nini, huyu huyu mari wa turgut?🤣

UTani tu 🤣
 
Vipi hapo wanapo sifiwa kuupiga mwingi ni wanainchi wanaowajibika kwa serikali au Ni serikali inayo wajibika kwa wanainchi?

BTW, Ufaransa watu wanaandama kutokana na hali ngumu ya maisha, wakimtaka Macron ajiuzulu, na zaidi watu wametiwa nguvuni. Vipi huko Ni serikali inawajibika kwa wanainchi au ni vice versa?
Hiyo ni versa vice 🤣
 
Arab spring tumeiona Maraisi kibao
Hiyoo arab spring si ndiyo inasemwa kuwa Marekani kawachochea waarabu dhidi ya serikali zao kwa maslahi ya Marekani?

Leo Marekani wanashambuliwa Syria kwa kuwa wao ndiyo walengwa na adui namba moja wa Waarabu kwa kuwa wanaonekana wapo Syria kwa maslahi ya Israel.

Kwa ivo kuiweka Arab spring kwenye usawa na hiki tunachokijadili, utakuwa unaikosea dhana uliyo nayo kuhusu ufanano wa maandamano unayotaka kuyalinganisha..
 
Back
Top Bottom