Tuchuguzeni kwa makini hizi kelele zinazopigwa kuhusu Ubinafsishaji Bandari, mbona kama kuna Vigogo wawili wanapigania Maslahi yao binafsi?

Mleta masa kwa hiyo unataka kwasababu gati nyingine zipo, basi hizo ulizoona chache ndio tuzitoe sadaka kwa mwarabu?!

Umebahatika kuusoma ule mkataba uone ulivyo na vipengele vya kipuuzi?

Mungu akusamehe kwa haya mawazo yako.
 
Ungewataja basi hao vigogo maana umekuja na hekaya za abunuwasi tu hapa
 
Kufikiri kwako kupo chini sana. Wenzako wanaongea hili wewe upo na lile
 
Haustahili neno tu,nakuwazia kitu kibaya mno
 
Ubinafsishwaji wa hio bandari ni gati namba 5 Mpaka 7 au gati namba 5 Mpaka 8 ?
 
Nakutumia mkataba inbox uone mwenyewe tulivyopigwa.
 
Unakielewa ulichoandika mkuu?
 
Acha upotoshaji,

Mkataba unasema bandari zote za Tanga, Mtwara, zote za bara zitakuwa chini ya DP World.

Mkataba pia unadai hautovunjwa, Wala kuahirishwa, Wala kusuluhishwa popote katika mahakama yoyote,

Huko ni kuuza Nchi na kubaki na Uhuru wa bendera pekee.

Sa100 Hana uchungu na Nchi yetu.

Sa100 must go!!!!
 
Huo mkataba ni wa miaka mingapi?
 
Upo sahihi mleta mada naungana na wewe kuna watu hawajawahi import hata pencil ikashushwa bandarini ila wapo na the so called "bandari imeuzwa".

Hii propaganda ni ya wahuni wachache wanaotumia ujinga wa baadhi ya wananchi kutetea deal zao zisibume, mbona Southampton port wapo hawa hawa DP does that mean UK ni wajinga na hawajali maslahi yao? Tupunguze ujuaji.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…