James Comey
JF-Expert Member
- May 14, 2017
- 8,759
- 14,831
Milambo mshindi wa kombe la ishi ile kampeni ya ukimwi na kondom 2022.Kagera rangers, faru dume, Sinza stars, Linea Messina, afc leopard, nyarugusu, milambo ya Mburahati, Oman,
Umeisahau mashada kwa ukanda huo wa vuruguKagera rangers, faru dume, Sinza stars, Linea Messina, afc leopard, nyarugusu, milambo ya Mburahati, Oman,
Wa kina Dame wamepiga sana watu sana ktk mechi miaka hiyoWewe ndio age mate wangu humu. Kulikuwa na Msako FC, Mfano FC [hii alicheza Mtwa Kihwelo],
Ngurumo FC, Yetu Afrika, Manta Line [zote Mburahati/Kigogo/Luhanga/Mabibo]. Kulikuwa na Kiboko Msheli [Magomeni], Kagera Shooting aka Kombo Ulaya. Jahazi ya Ilala, Mogo FC ya Ukonga, Vita FC, Magomeni Mapipa. Sifa United na Faru FC za Manzese.
Enzi hizo ilikuwa ubabe ubabe, baada ya mechi lazima vurugu zitokee.
Vv
Kipindi hiko ngumi zilikuwa zinawaka muda wowote. Nakumbuka kuna mechi moja ya ndondo huku Morogoro Vijijini Kati ya vijiji vya Hembeti na Kijiji kimoja cha wamasai kinaitwa Kambala. Hahaaa zikaanza kuchapwa, masai wakala kichapo wakaanza kukimbia na wakifika kwenye majumba ya wenyeji wa Hembeti wanawafukuza.Wa kina Dame wamepiga sana watu sana ktk mechi miaka hiyo
Mwamba huyo hapo hahahahaha viwanja vyote kuanzia Las vegas, Msisiri,kinondoni, UKIMWI n.k wanamwelewa .......[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]View attachment 2580946
Kipunje huyo hapo.
Nondo, aiseeeehhh kulikuwa na Kiwiku na Kibesi bila kumsahau Maswini mwamba alikuwa kuvua nguo na kukimbia uchi ground wakati ball linatembea ni kawaida tu.....Na jamaa yao anaitwa KIWIKU.
White star ilikuwa igumila kama nakumbumbuka vizuri, kina SHABANI KICHUYA NA SHABANI MANUPA ilikuwa hatari.......Hatari sana hao watu kuna ile White yakina mbamba mwishoni ya miaka ya 90 inachukua ubingwa pale uwanja wa kinondoni shule ya msingi kabla kambangwa haijajengwa ilikua hatari,shule ya kambangwa imesaidia kuleta elimu ila imeua elimu kata ya mwananyamala maana ule uwanja ndio ulikua uwanja mkubwa wa kucheza kwa gozi viwanja vya kule msisiri vyote vidogo na vyakuchezea chandimu
Sent from my SM-G9650 using JamiiForums mobile app
ShokaNondo, white star mwananyamala.
Hawa jamaa ndio waliosababisha lile vagi kule Ukombozi manzese mpaka kuna jamaa akauawa uwanjani kwa kupigwa na kitu kizito watu wakakimbia na na nondo ikavirugika....wakaja kina Jonas mkude wakajitahidi kuirudisha lakini wapiNa jamaa yao anaitwa KIWIKU.
Upo sahihi kabisaWhite star ilikuwa igumila kama nakumbumbuka vizuri, kina SHABANI KICHUYA NA SHABANI MANUPA ilikuwa hatari.......
Kina mbamba kule ni CHAUKUCHA[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] kwa kopa ile aseeeehhhhh ilikuwa ni kwikwi
Uwanja naukumbuka na sana maana mi nmesoma pale pale shule ya Msingi na nimekaa maeneo yale yale ya mahakamani kwa juu kidogoWakati hata sekondari ya kambanwa haijajengwa, uwanja ulikuwepo pale ilipojengwa ile ghorofa.Timu ilikuwa ya pascal ambae ni padri mtoto wa mama bahati.
Hao Young Boys walikuwa wanapiga mpira hatari. Niliwashuhudia siku moja. Anyway, nilipenda battle la Bomu na Ashanti japo mi nilipenda siku ikicheza Sifa Politan na Kagera Rangers.Kama Mada Inavyosema.
Mimi nimekulia Morogoro na nimecheza sana ndondo miaka ya late 1990's na 2000's nikitokea timu ya Ghetto Boys ya Mvomero.
Katika makuzi yetu tulikuwa tunacheza sana ndondo huko Mvomero na Moro kwa Ujumla na katika mashindani ya Kiwilaya na Mkoa tulikuwa tunakutana na timu za Wilaya nyingine au mikoa mingine pale uwanja wa shujaa Morogoro Mjini.
Timu nyingi zilitoa wachezaji wa iliyokuwa ligi daraja la Kwanza sasa Ligi Kuu mfano Reli, Moro United, Mtibwa Sugar n.k za Moro na nyingine nyingi za nje ya Moro kama Prisons, AFC, Simba na Yanga n.k.
Wachezaji maarufu wa Ndondo ambao binafsi nimewashuhudia na kimsingi walikosa njia nzuri tokana na "Zama za giza tulizokuwa tunacheza na kizazi," ila wangekuwa wachezaji bora nchini na duniani kama wangecheza sasa ni kama wafuatao:
1. David Izengo-Toka timu ya Magereza huyu kwangu mimi ni mchezaji bora kumshuhudia kwa macho yangu nchini sema zama alizokuwa ziliua kipaji chake akaja cheza Prison. Hapa "Triple C" hamfikii.
2. Paul Mokiwa alicheza reli Morogoro na baadaye Prison ambapo alipata majeraha na kuacha kucheza Mpira.
3. Ramadhani Lundenga. Alikuwa ndugu na Hashimu Lundenga na alikuja chezea Yanga B.
4. Abu Ramadhani alikuja chezea Yanga.
5. Salum wa Gheto Boys ya Mvomero
6. Mimi Jimmy Gatete a.k.a mungu ya Magoli toka ghetto boys ya Mvomero.
7. Kipa Maarufu wa Ndondo Yusuph Dezo toka Timu ya Kishingo ya Dakawa pale alikuwa anampiga mikwara Kaseja kuwa yeye Kaseja ni "Tanzania 2" mbele yake naye ni "Tanzania 1" ila mfumo tu umembeba.
Timu maarufu za Ndondo Moro ninazozifahamu na tulizokutana nazo kwenye michuano mbalimbali ni:
1. Jamaica ya Moro Mjini.
2. Young Boys ya Mikese.
3. Jiwe ya Dumila.
4. Ghetto Boys na Asec za Mvomero.
5. Burkina ya Moro Mjini.
6. Kulikuwa na timu moja ya Kihonda waliyokuwa wanachezea akina Ulimboka Mwakingwe, Jumanne Shengo Tondoro na akina Kaseja siikumbuki vizuri.
7. Kulikuwa na timu moja toka turiani iliyokuwa ina wachezaji toka mtibwa kipindi hiko akina Mkangwa, salhina mjengwa, Zuberi Katwila, Mecky n.k
Je, wewe unaikumbuka timu gani maarufu ya ndondo ya mtaani kwenu na wachezaji maarufu waliokuwa wanaichezea?
Nakumbuka Dar walikuwa na Abajalo ya Sinza waliyocheza akina "Kali Mangonga Ongara Mbele kwa Mbele."
Mtaa wa igumila ulikuwa na mademu wakali aiseeeeehhhh dah
Kuna mzee aliitwa mzee crispiny chini pale kidogo kwa akina GAGA ALICHEZA SANA MPIRA AKAITWA HIVYO HUYO DOGO.Uwanja naukumbuka na sana maana mi nmesoma pale pale shule ya Msingi na nimekaa maeneo yale yale ya mahakamani kwa juu kidogo
Sent from my SM-G9650 using JamiiForums mobile app
Akina mkude wenyewe wakawa walevi, wakawazaa watoto kama akina Amani george, kina lau wakaanza toka.Sema msisiri walipokulia malaya, pombe, kamari vikawapoteza.Hawa jamaa ndio waliosababisha lile vagi kule Ukombozi manzese mpaka kuna jamaa akauawa uwanjani kwa kupigwa na kitu kizito watu wakakimbia na na nondo ikavirugika....wakaja kina Jonas mkude wakajitahidi kuirudisha lakini wapi
Kibesi bado ana urefa urefa ni swala tano sana, maswini ni kama kichaa tu, Kiwiku toka ile ishu ya kinu alitulia.Naona na uzee.Nondo, aiseeeehhh kulikuwa na Kiwiku na Kibesi bila kumsahau Maswini mwamba alikuwa kuvua nguo na kukimbia uchi ground wakati ball linatembea ni kawaida tu.....
Alafu kulikuwa na Shoka ya msufini magengeni kule msisiri dah