Urais, Fomu kuhakikiwa na Kutangazwa Kuteuliwa , kisha kusubiria kama kuna pingamizi
Baada ya fomu kuhakikiwa na kutangazwa kuteuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa kila kitu kipo sawa kuna zoezi muhimu la kubandika majina ili umma kuwafahamu.
Muda wa pingamizi ni kuanzi saa 10:00 jioni ya tarehe 25 Agosti 2020 hadi saa 10:00 jioni siku inayofuata yaani tarehe 26 Agosti 2020.
Zoezi hilo muhimu ni hatua inayofuata ni kusikia kama wagombea wamewekewa pingamizi na wale wadau wanaotambulika na Tume ya Uchaguzi, kisha wagombea wateuliwa kupata nafasi ya kujibu.
Wenye haki ya kuweka pingamizi ngazi ya Urais na Makamu ni hawa wadau watatu yaani Mkurugenzi wa Uchaguzi, Msajili wa Vyama Vya Siasa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Pingamizi ngazi ya Urais linatakiwa kuletwa kwa maandishi katika fomu namba 9A na pingamizi hilo liwakilishwe ndani ya muda muafaka unaoanzia muda uliotajwa hapo juu na sababu za pingamizi litajwe.
Hivyo waliotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi ngazi ya Urais kama wateule baada ya kuhakiki fomu na nyaraka wote wanaweza kuwekewa pingamizi muda wowote kuanzia muda wa saa 10:00 jioni ya leo tarehe 25 Agosti 2020 na mwisho wa kuwakilisha pingamizi ni kesho saa 10:00 jioni tarehe 26 Agosti 2020.
Baada ya fomu kuhakikiwa na kutangazwa kuteuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa kila kitu kipo sawa kuna zoezi muhimu la kubandika majina ili umma kuwafahamu.
Muda wa pingamizi ni kuanzi saa 10:00 jioni ya tarehe 25 Agosti 2020 hadi saa 10:00 jioni siku inayofuata yaani tarehe 26 Agosti 2020.
Zoezi hilo muhimu ni hatua inayofuata ni kusikia kama wagombea wamewekewa pingamizi na wale wadau wanaotambulika na Tume ya Uchaguzi, kisha wagombea wateuliwa kupata nafasi ya kujibu.
Wenye haki ya kuweka pingamizi ngazi ya Urais na Makamu ni hawa wadau watatu yaani Mkurugenzi wa Uchaguzi, Msajili wa Vyama Vya Siasa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Pingamizi ngazi ya Urais linatakiwa kuletwa kwa maandishi katika fomu namba 9A na pingamizi hilo liwakilishwe ndani ya muda muafaka unaoanzia muda uliotajwa hapo juu na sababu za pingamizi litajwe.
Hivyo waliotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi ngazi ya Urais kama wateule baada ya kuhakiki fomu na nyaraka wote wanaweza kuwekewa pingamizi muda wowote kuanzia muda wa saa 10:00 jioni ya leo tarehe 25 Agosti 2020 na mwisho wa kuwakilisha pingamizi ni kesho saa 10:00 jioni tarehe 26 Agosti 2020.