Tunasisitiza haki kutendeka kwa mashehe wa Kiislamu wa Uamsho kutoka Zanzibar

Tunasisitiza haki kutendeka kwa mashehe wa Kiislamu wa Uamsho kutoka Zanzibar

BAK

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2007
Posts
124,790
Reaction score
288,165
TUNASISITIZA HAKI KUTENDEKA KWA MASHEHE WA KIISLAMU WA UAMSHO KUTOKA ZANZIBAR

Tarehe 27 Februari 2021, nilikuwa miongoni mwa viongozi waliokuwa wamealikwa na ACT Wazalendo kuhudhuria Dua ya kumuombea Maalim Seif Sharif Hamad aliyekuwa Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar aliyefariki hivi karibuni.

Siku hiyo, Sheikh Ponda aliongea jambo linaloutesa sana moyo wangu. Aligusia suala la Mashehe wa Kiislamu wa Uamsho kutoka Zanzibar wanaoshikiliwa Tanzania Bara kwa miaka kadhaa sasa! Jambo hili linautesa moyo wangu kwa kuwa naona haki yao imecheleweshwa mno!

Kuna 'watu' waliwahi kuniambia kuwa suala lao ni 'nyeti' hivyo halihojiwi! Maswali ni mengi kuliko majibu. Kuendelea kuwashikilia Mashehe hao pasipo maelezo yanayoeleweka kutachochea chuki za kidini. Hii ni kwa sababu wafuasi wa Mashehe hao wanaendelea kunung'unika chinichini kwa chini.

Najisikia kuwiwa af kuwapazia sauti yangu Mashehe hao pia! Haijalishi wametenda kosa zito kiasi gani, lakini haki yao katika nchi inapaswa ilindwe. Wanatakiwa watendewe haki kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar na Katiba ya Tanzania. Kutendewa haki kwao ni pamoja na kusikilizwa kwa kesi yao kwa haraka kama wana kesi ya kujibu.

Kama Askofu, ninaungana na Sheikh Ponda katika kuwapazia sauti Mashehe wa Kiislamu wa Uamsho kutoka Zanzibar wanaoshikiliwa Tanzania Bara kuwa watendewe haki kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar na Katiba ya Tanzania. Vinginevyo, waachiliwe huru pasipo masharti ye yote!

Mambo kama hayo ndiyo yalinisukuma kuanzisha kampeni za kuhamasisha umma wa Watanzania kuhusu umuhimu na uhitaji wa Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya!

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfutate!

Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula - Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki na Mwenyekiti Mwenza wa Umoja wa Makanisa ya Moravian ya Uamsho Duniani.
 
Ukikosea ukaanzisha mambo ya ugaidi hakuna atayekutetea sana sana labda wanasiasa
Nao sio wote, huo mkondo alioenda ndio kakosea kabisa. Wazungu ni wahanga wa ugaidi wa hao mashehe. Yaani hapa hakuna mzungu atam support Mwamakula kwa lolote. Kajiingiza kwenye mdomo wa mamba hata akienda kuomba Visa ya kusafiri nchi za wazungu hapati kama ilivyo kwa shehe Ponda ni blacklisted kwa wazungu. Mwamakula ka ji register mwenyewe kwenye blackist kwa hili tamko.
 
Nao sio wote huo mkondo alioenda nfio kakosea kabisa .Wazungu ni wahanga wa ugaidi wa hao mashehe.Yaani hapa hakuna mzungu atam support Mwamakula kwa lolote.Kajiingiza kwenye mdomo wa mamba hata akienda kuomba Visa ya kusafiri nchi za wazungu hapati kama ilivyo kwa shehe ponda ni blacklisted kwa wazungu.Mwamakula ka ji register mwenyewe kwenye blackist wa hili tamko
Kwa wazungu akafanye Nini si tumekubaliana hakuna kupiga magoti kwa wazungu
 
Hawa mashekh wa Zanzibar wamenikumbusha kina Sheikh Rogo na Makaburi wa Mombasa Kenya. Yaani walikuwa wanapigwa risasi kimasikhara tuu...tena Makaburi alikuwa anajua ni suala la wakati tuu atauawa. Duuuh hatari.
 
Binafsi nafurahia mashehe kuwa ndani na natamani wateswe zaidi. Ugaidi walio kuwa wakihubiri na kuuhimiza hadharani ulikua unaelekea kuichafua nchi yetu totally. Waendelee kuwekwa kizuizini kwa maslahi mapana ya nchi...
 
Nao sio wote huo mkondo alioenda nfio kakosea kabisa .Wazungu ni wahanga wa ugaidi wa hao mashehe.Yaani hapa hakuna mzungu atam support Mwamakula kwa lolote.Kajiingiza kwenye mdomo wa mamba hata akienda kuomba Visa ya kusafiri nchi za wazungu hapati kama ilivyo kwa shehe ponda ni blacklisted kwa wazungu.Mwamakula ka ji register mwenyewe kwenye blackist kwa hili tamko
Sasa kama wana makosa ya kigaidi si mahakama itoe hukumu tujue kua wamehukumiwa kuliko kuwaweka tu Mkuu?

Kumbuka hata wewe muda wowote unaweza kuswekwa ndani Mkuu!
 
Acha kuchanganya Kati ya mashehe na magaidi kama Taifa tunajua mahubiri yao jinsi yalivyosababisha makanisa kuchomwa Zanzibar na bara, mashekhe wa kweli kumwagiwa tindikali, mapandi kuuwawa na wengine kujeruhiwa, Mwl Nyerere kutukanwa na kulaaniwa hadharani kwenye mahubiri ya hawa uamsho na watu toka bara kubaguliwa na kunyanyasika huko visiwani.

Kwa ufupi walikamatwa wakati wa utawala wa raisi, makamu na waziri mkuu wote waislamu wenzao hivyo tunaamini kilichofanyika kina maslahi mapana ya Taifa letu. Wabaki huko kwanza.
 
Kajifunze kwanza kuandika pia uwe unafuatilia mambo kwa kina ili ujue nini kinachoendelea badala ya KUKURUPUKA.
Mbona hamkuwachagua chadema waliohaidi kiwatoa?
 
Hawa mashekh wa Zanzibar wamenikumbusha kina Sheikh Rogo na Makaburi wa Mombasa Kenya. Yaani walikuwa wanapigwa risasi kimasikhara tuu...tena Makaburi alikuwa anajua ni suala la wakati tuu atauawa. Duuuh hatari.
Tokea makaburi apigwe risasi,ushasikia mabomu Mombasa?
 
Acha kuchanganya Kati ya mashehe na magaidi kama Taifa tunajua mahubiri yao jinsi yalivyosababisha makanisa kuchomwa Zanzibar na bara, mashekhe wa kweli kumwagiwa tindikali, mapandi kuuwawa na wengine kujeruhiwa, mwl nyerere kutukanwa na kulaaniwa hadharani kwenye mahubiri ya hawa uamsho na watu toka bara kubaguliwa na kunyanyasika huko visiwani. Kwa ufupi walikamatwa wakati wa utawala wa raisi, makamu na waziri mkuu wote waislamu wenzao hivyo tunaamini kilichofanyika kina maslahi mapana ya Taifa letu. Wabaki huko kwanza
... kwa matukio hayo nasita sana kuwatetea masheikh wa Zanzibar; japo wanasiasa watajitia unafiki kuwatetea kwa maslahi ya kisiasa, lakini wale jamaa walitaka kuiharibu nchi!
 
Wakati ule wa uamsho, Zanzibar ilichafukwa na mauwaji ya viongozi wa dini, makanisa kuchomwa, mashekhe kumwagiwa tindikali, na nakumbuka kipindi hicho tuliwahi kuagiza CIA kuja kufanya upelelezi wa mauwaji ya viongozi huko Zanzibar, au akili yangu ilikuwa haijakomaa?
 
Back
Top Bottom