Uchaguzi 2020 Tundu Lissu aanza kukumbana na wananchi wakitaka maendeleo ya vitu

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu aanza kukumbana na wananchi wakitaka maendeleo ya vitu

Hivi Lissu ana mpango wa kwenda kuomba kura Chato na Kigamboni? Akiffika huko atawaambia kuwa uwanja haustabili kujengwa? Na Kigamboni atawaambia daraja lao ni la kupunga upepo?
Acha upotoshaji wako wa kishetani, Lisu hajazungumzia Daraja la Kigamboni na wala hawezi kuliongelea kwani ni muhimu sana, Lisu kaongelea daraja la kutoka Aga kan kwenda Oyestarbay linalojengwa sasa chini ya utawala huu wa kidikteta, chato lazima Lisu aende na huko atawauliza umuhimu wa huo uwanja wa kutua Ndege za viongozi wa east Africa tu pasipo Abria wengine kuutumia
 
Nimewasikia wananchi wa eneo moja huko Mufindi kama sikosei kwenye mkutano wa ndugu Tundu Lisu kuwa hawana barabara pamoja na maji na wamesema wanaomba akichaghuliwa awatengenezee hivyo vitu.

Nikajiuliza kwa nini hao watu hawahitaji maendeleo ya watu wao wametaka maendeleo ya vitu?

Majibu ya Tundu Lissu ni kwamba, hata yeye anashangaa kwa nini mpaka sasa hawana barabara na maji na kwamba mpaka huko alipotokea mpaka kufika pale jana yake ametembea kwenye njia ya vumbi mpaka alipofika kwenye mkutano akawa amechoka sana hadi kutaka kuahirisha mkutano.

Swali langu kwa Tundu Lissu.
Kama yeye na pesa aliyonayo na magari aliyotumia bado amepata maumivu kwa kupita barabara ya vumbi, je anakubali maendeleo ya vitu ni moja ya kurahisisha maendeleo ya watu?

Anaweza kufahamu kuwa kuna watu pia wanahitaji usafiri wa ndege kuwapeleka sehemu husika na pengine kunusuru maisha yao tofauti na wangetumia barabara wasingepona kutokana na umbali?

Je, unaweza kuwa na mapesa mengi na magari mazuri lakini ili ufike kwako ni lazima ukanyage tope kwa kusukuma gari yako na ukifika kwako huna hata umeme unatumia kibatari na gari yako inakuwa chafu muda wote na ndani mwako vumbi kibao kutokana na barabara ya vumbi ambayo magari yakipita vumbi yote inajaa ndani mwako.

Je, utafurahi na maisha hayo ya uchafu kila siku ila una pesa?

Je, Tundu Lissu akiingia madarakani atatekeleza maombi ya hao wananchi ya barabara na maji waliyoomba au atataka awajaze pesa ili wawe na furaha kwanza?

Itakuwa wewe ndiye mzito wa kuelewa sera CDM hakuna mahali ambapo inasema kufanya maendeleo ya miundo mbinu ni makosa ila mara zote wanasema maendeleo ya miundo mbinu yaende sambamba na maendeleo ya watu.

Kama serikali ina pesa ya kujenga SGR isiseme haina pesa ya kulipa nyongeza ya mishahara kwa wafanyakazi au pension au mikopo ya kusomesha wanafunzi au madawa katika hospitalini au huduma ya maji hivyo vyote ni vya muhimu kwakuwa kila kinachofanyika kilenge kumpunguzia mwananchi adha katika maisha yake ili aweze kulala pazuri, ale vizuri, avae vizuri atibiwe vizuri na watoto wake wapate elimu nzuri pia.

Sasa hii ya kusema mishahara haiwezi kuongezwa kwakuwa inajengwa SGR siyo sawa kwasababu mlengwa wa kwanza katika maendeleo ni mtu mwenyewe halafu mengine yafuate. Kwahiyo sioni kosa la kuhitajika barabara kwa jimbo la mdabulo. Sera ya CDM inasisitiza uhuru haki na maendeleo ya watu.

Chochote kinacholeta maendeleo ya watu kifanywe. Lakini siyo Haya maisha ya miaka mitano ya kumfanya mwananchi kuzidi kuwa masikini ashindwe hata kununua uniform ya mtoto wake aende shule kwa sababu kuna SGR inajengwa au Ndege zimenunuliwa Hiyo siyo sawasawa.
 
Unadhani hiyo pesa ya Chato na hilo daraja la baharini vingemaliza matatizo ya barabara Tanzania nzima?

Tunasema hivyo havikupaswa kuwa kipaumbele kwa sasa tena mara 100 lingejengwa daraja la magomeni hapo ambapo mvua ikinyesha barabara haipitiki kusingekuwa na kelele sasa lile daraja kule linakokwenda hata folen huwa hakuna folen huwa iko maeneo ya mwenge pale na pale salender kutokana na magari yanayotokea mwenge na kinondoni.

Magari yanayotokea kule masaki huwa hayana foleni pale muda wote huwa ni magari ya kawaida ndiyo maana kama unatoka mjini ukishapita traffic light za ubalozi wa urusi ukielekea barabara ya coco beach huwezi kuta folen kwahiyo lile daraja halikuwa kipaumbeli cha mambo muhimu ya kufanya.

Pia lingeweza kujengwa hata ile barabara ya kilwa kutoka kituo cha bandari kuunganisha majani ya chai hakuna mtu ange hoji lakini kule kwakwele ni matumizi mabaya ya kodi za wananchi mimi mwenyewe naishi kinondoni lakini hilo daraja hapana halikupaswa kuwa kipaumbele.
 
Maendeleo ya vitu yaendayo kuboresha maisha ya watu yagusayo maisha ya watu. Kujenga Ikulu mpya Hali toshelevu ya awali ipo, kujenga Chato na Dodoma hivi haviwasaidii watu bali ni hitaji la mtawala na sio kipaumbele Cha wananchi na wala havigusi maisha ya watu sababu si hitaji la lazima.

Ninkweli kabisa ndiyo maana hata Nyerere aliyeanzisha wazo la kupeleka Dodoma makao makuu ya serikali hakuwahi kupeleka sababu aliona kuwa kuwaendeleza watu kwanza ndiyo kipaumbele cha muhimu zaidi

Hata marais wote watatu waliofuata waliliona hilo pia kwamba hicho siyo kipaumbele sababu tayari serikali ilikuwa na ofisi zake PAO moja na ikulu ambayo inatosha kufanya kazi za utawala.

Sasa kitendo cha kusitisha malipo ya nyongeza za mishahara ya watu malipo ya pension za wastaafu kununua madawa ya hospitalini na hata kusambaza maji na pesa kujengea majengo ya serikali Dodoma sidhani kama hicho kilikuwa ni kipaumbele kwa uchumi huu tulionao pengine muda ungefika wa kufanya hivo ila siyo sasa ambapo pesa SA kusomesha watoto wetu wa primary na secondary tunasaidiwa na wafadhiri.

Tulihitaji mjadala wa lini serikali ihamie Dodoma na mbona hilo halikuwa hata kwenye ilani ya uchaguzi ambayo ingesaidia wanainchi kuamuwa kama hiyo sera inafaa.
 
Hivi Lissu ana mpango wa kwenda kuomba kura Chato na Kigamboni? Akiffika huko atawaambia kuwa uwanja haustabili kujengwa? Na Kigamboni atawaambia daraja lao ni la kupunga upepo?

..I would not advice him to visit Chato.

..lakini kama akienda basi atafute hitaji la kweli la wananchi wa Chato.

..halafu awaulize kama kati ya hilo hitaji lao na uwanja wa ndege kipi kitakuwa faida kwao.

..daraja la coco-beach does not make sense to me, siyo priority ukilinganisha na barabara kama za Kilombero na Mlimba.
 
LISSU hana focus kwenye kampeni zake. Kila mtu anajua umuhimu wa daraja la baharini kuwa ni kupunguza foleni iliyopo ktk barabara ya Ali Hassani Mwinyi na Ocean Road. Anapopinga daraja hilo, watu wa OSTERBAY wote na maeneo ya jirani hawatampigia kura.

..mimi nitakuwa mfaidika wa daraja hilo lakini siliungi mkono.
 
Acha upotoshaji! Watanzania tulio wengi tunataka maendeleo ya vitu yaende sambamba na maendeleo ya watu! Hakuna mfanyakazi atakayekubali kunyimwa haki zake za msingi mfano kupandishwa daraja kwa wakati, kisa eti unajenga barabara au kununua ndege!

Mbona wakati wa JK hizo barabara, madaraja, nk vyote hivyo vilijengwa kila kona ya nchi! Lakini bado ajira kwa wahitimu wa vyuo vikuu, haki za wafanyakazi na makundi mengine katika jamii ziliheshimiwa?

Iweje huyu mtu wenu aone barabara na ndege ni vitu vya muhimu sana kuliko haki za wengine? Mbona hatujawahi kumsikia akijipunguzia mshahara na posho zake?

Hata Rais angekua ni Lissu au Hashimu Rungwe, bado hizo barabara zingejengwa tu. Hilo ni moja ya jukumu la serikali yoyote ile duniani. Na kodi tunazolipa na mikopo ya ndani na nje ya nchi, hufanikisha zoezi hilo.
Hovyo
 
Jamani hata nyerere alisema tunataka maendeleo ya vitu yanayogusa maisha ya watu, niwapi Lisu amepinga miradi ya maji na barabara ? Barabara nisehemu yamaisha yawatu wote Kila siku maji nisehemu yamaisha ya watu Kila siku,,
 
Lissu anawapa makavu live...

Ccm toka uhuru mpaka leo wananchi tunapewa ahadi za maji kweli?
 
Jamani hata nyerere alisema tunataka maendeleo ya vitu yanayogusa maisha ya watu, niwapi Lisu amepinga miradi ya maji na barabara ? Barabara nisehemu yamaisha yawatu wote Kila siku maji nisehemu yamaisha ya watu Kila siku,,
Wanamlisha maneno ili wapate unafuu, lakin hizi sio nyakati za giza kila mtu anajua ukweli
 
Lissu anawapa makavu live...

Ccm toka uhuru mpaka leo wananchi tunapewa ahadi za maji kweli?

Bora CCM inatoa ahadi za maji. CHADEMA haina ahadi ya kutoa. Inahamasisha nchi kufanya vurugu tu. Pamoja na madhaifu ya CCM lakini kuna unafuu kuliko CHADEMA. Wanayoyasema hawayafanyi ndani ya chama. Hawana rekodi ya utendaji iliyotukuka. Bado wanatakiwa wajisahihishe sana ili watupe imani. Sasa hivi CHADEMA ni kama SACCOS ya Wizi mtupu.
 
Maendeleo ya vitu yaendayo kuboresha maisha ya watu yagusayo maisha ya watu. Kujenga Ikulu mpya Hali toshelevu ya awali ipo, kujenga Chato na Dodoma hivi haviwasaidii watu bali ni hitaji la mtawala na sio kipaumbele Cha wananchi na wala havigusi maisha ya watu sababu si hitaji la lazima.

Sio kosa lako. Ni kosa la wazazi wako ambao hawakukupeleka shule
 
Bora CCM inatoa ahadi za maji. CHADEMA haina ahadi ya kutoa. Inahamasisha nchi kufanya vurugu tu. Pamoja na madhaifu ya CCM lakini kuna unafuu kuliko CHADEMA. Wanayoyasema hawayafanyi ndani ya chama. Hawana rekodi ya utendaji iliyotukuka. Bado wanatakiwa wajisahihishe sana ili watupe imani. Sasa hivi CHADEMA ni kama SACCOS ya Wizi mtupu.
We unafikiri ccm bila Dola kuna lolote hapo..??!

Chadema bila wasanii umeiona??.. Hujasikia Sera za Lissu?
 
Acha upotoshaji! Watanzania tulio wengi tunataka maendeleo ya vitu yaende sambamba na maendeleo ya watu! Hakuna mfanyakazi atakayekubali kunyimwa haki zake za msingi mfano kupandishwa daraja kwa wakati, kisa eti unajenga barabara au kununua ndege!

Mbona wakati wa JK hizo barabara, madaraja, nk vyote hivyo vilijengwa kila kona ya nchi! Lakini bado ajira kwa wahitimu wa vyuo vikuu, haki za wafanyakazi na makundi mengine katika jamii ziliheshimiwa?

Iweje huyu mtu wenu aone barabara na ndege ni vitu vya muhimu sana kuliko haki za wengine? Mbona hatujawahi kumsikia akijipunguzia mshahara na posho zake?

Hata Rais angekua ni Lissu au Hashimu Rungwe, bado hizo barabara zingejengwa tu. Hilo ni moja ya jukumu la serikali yoyote ile duniani. Na kodi tunazolipa na mikopo ya ndani na nje ya nchi, hufanikisha zoezi hilo.
Eti bwana,kienyeji sana aisee....kwamba ....Nakunyima hiki,nitengeneze kile...!!?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
..bila shaka kungekuwa na unafuu kuliko sasa hivi.

..wewe jiulize wananchi wangapi wanatumia huo uwanja wa ndege wa kimataifa wa chato?

..binafsi angejenga barabara za lami chato au geita nisingemlaumu hata kidogo.

..angewekeza kwenye vyuo vya ufundi badala ya uwanja wa ndege ningeunga mkono uwekezaji huo.

NB:

..daraja la baharini la kupunga upepo Dsm wangeshawishi lijengwe na sekta binafsi. Na wanaotaka kupita huko wangelipia kama tunavyofanya kwenye daraja la kigamboni.
Geita yote hakuna Chuo Cha Ufundi Stadi,enzi.na.enzi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom