Tundu Lissu: Aliyenipa ushahidi wa pesa za Abdul na mama yake kwa sasa ni marehemu

Tundu Lissu: Aliyenipa ushahidi wa pesa za Abdul na mama yake kwa sasa ni marehemu

Mgombea Uenyekiti wa Chadema Tundu Lissu amefunguka kupitia Twitter space jinsi alivyokusanya ushahidi wa kutosha kuhusu rushwa ya pesa za Abdul na mama yake kwa viongozi wa Chadema.

Ameeleza kuwa mmoja wa wajumbe wa kamati kuu ya Chama cha CHADEMA aliyempatia ushahidi wa kina kuhusiana na tuhuma hizo na aliyemsaidia kuthibitisha tuhuma hizo mbele ya kamati kuu ya Chama cha CHADEMA kwa sasa ni Marehemu. Hata hivyo Lissu alikataa kumtaja Mjumbe huyo akidai kwamba haitasaidia kitu chochote.

Na alipoulizwa iwapo kifo cha Mzee Ali Kibao kinahusiana na tuhuma za pesa za Abdul aliomba asilizungumzie Hilo kwa sasa.
Ukiconect dot, unaelewa kwa nini dj alimtetea masauni msibani.
 
Lisu anajua anachofanya! Lisu ni mropokaji ila anaropoka vitu ambavyo ni sahihi yaani hana uwezo wa kutunza siri li friji lake haligandishi. Anachosema sasa ndo ukweli wenyewe kwamba mauaji ya wanachadema yanafadhiliwa na mamlaka ya juu ndani ya Chadema yenyewe.

Kuna wanachadema wamepotea wengine hawakuwa hata na athari zozote kwa serikali hata wananchi wengi wamewajua baada ya kutangazwa kuwa wamepotea au wamekua akiwemo huyo babu Kibao.

Hao watu watakuwa walionekana threat kwa mtu au kundi flan ndani ya CHADEMA na kundi hilo likaamua kuwaondoa kikatili wakijua atakayesingiziwa ni serikali/usalama/polisi ila sasa ukweli unaanza kuonekana.

Yaani CHADEMA inaua Chadema
 
Dot zinaunganishwa hivi.

Kuvuja au kuanza kwa harakat za fedha za Abdul na mama yake ni lini?

Tangu hapo mjumbe gani Kamati Kuu CHADEMA amefariki?

Mzee Kibao alikuwa mjumbe Kamati Kuu? Maana kifo chake kilikuwa na dalili za mtu aliyeuawa kutokana na kuvujisha "Siri" Fulani

Mzee Kibao aliuawa kukiwa na ishara kwamba alikuwa akiwakimbia watu Fulani aliokosana nao Dar.
Hao watu fulani ambao wamekuja na silaha na pingu ambaohawajulikani.
 
Wafuasi wa CHADEMA kama mtafuatilia vizuri kupotea kwa ben Saanane mtagungua kuna mtu yuko CDM anashikiana na watekaji ingiwa ni ngumu haya machawa kina Tindo ,Erythrocyte kuelewa
Huo ni wajibu wa vyombo vya dola, peleka ushahidi ili huyo mtu wa cdm aaumbuke. Badala ya kuwabambikizia kesi, ushahidi wako ungekuwa mzuri.
 
Nilikuwa najiuliza sana sababu za Mzee Kibao kufanyiwa unyama ule.

Kwanza nilikuwa hata sijasikia uwepo wa mtu kama huyo ndani ya CHADEMA; kwa sababu sikuwahi hata kusikia akitamka lolote hadharani.

Sasa majibu yame patikana.
Mkuu, Kibao alikuwa ni mtu wa karibu sana wa Mbowe. Na alikuwa anajua mengi.

Tutafakari:
1. Mwenyekiti anafuatwa gerezani na ''watu wasiojulikana'' na kufanya mazungumzo ya kina.

2. Anatolewa gerezani na kwenda kwa mama moja kwa moja na wafanya mazungumzo ya faragha wao wawili tu.

3. Abdul na makapu yake yaliyojaa fedha anamtembelea mwenyekiti na baadhi ya viongozi wa chama na anaondoka makapu yakiwa tupu.

3. Mwenyekiti anaambiwa amuunganishe Abdul na Lissu ili naye apate mgao wake na anamteua Wenjele kufanya hiyo kazi.

4. Wenjele na Abdul wanakwenda na makapu yao yaliyojaa fedha kwa Lissu lakini Lissu anayakataa.

5. Lissu anafanya uchunguzi mkali na wa siri na mzee Kibao anampa details zote.

6. Lissu anaanika hadharani kuhusu makapu ya fedha.

7. Mwenyekiti anaitisha kikao ili amwadhibu Lissu

8. Lissu anatoa ushahidi wa kina na mwenyekiti anaufyata.

9. Mwenyekiti anagundua kumbe Kibao alitoa siri.

10. Mwenyekiti anamrudia Abdul na kumweleza alichofanya Kibao, na Abdul anamwambia mama, na mama anamwambia mkuu wa ''wasiojulikana'' na ''wasiojulikana'' wanatumwa kufanya waliyofanya.

11. Wakati wa mazishi ya Kibao, familia inakuja juu lakini mwenyekiti anaingilia kati kinafiki na kusema wawe na adabu.
 
Mgombea Uenyekiti wa Chadema Tundu Lissu amefunguka kupitia Twitter space jinsi alivyokusanya ushahidi wa kutosha kuhusu rushwa ya pesa za Abdul na mama yake kwa viongozi wa Chadema.

Ameeleza kuwa mmoja wa wajumbe wa kamati kuu ya Chama cha CHADEMA aliyempatia ushahidi wa kina kuhusiana na tuhuma hizo na aliyemsaidia kuthibitisha tuhuma hizo mbele ya kamati kuu ya Chama cha CHADEMA kwa sasa ni Marehemu. Hata hivyo Lissu alikataa kumtaja Mjumbe huyo akidai kwamba haitasaidia kitu chochote.

Na alipoulizwa iwapo kifo cha Mzee Ali Kibao kinahusiana na tuhuma za pesa za Abdul aliomba asilizungumzie Hilo kwa sasa.
oooh ngoja tukae pale na tuone
 
Back
Top Bottom