Tundu Lissu: Nitakwenda Chato, nitamwambia Magufuli amka uone Rais Samia anavyofanya

MAMA yuko makini sana sema kuna watu wameingiza chokochoko za kuligawa hili taifa kibara na pwani
 
Nimesoma hayo maneno ya Lissu, kijasho chembamba kimenitoka, kweli Samia ni shetani, sawa na mbwa anayekula watoto wake, lakini pia Magufuli kwa hili la kulinda rasilimali za taifa lazima aenziwe, alikuwa mzalendo kweli, kama alivyosema Lissu.
 
Ya Nyerere siyajui sana lwa sababu zama zake sikuwa na hizo akili, ila kwa uzalendo sidhani kama kuna kiongozi anamfikia JPM.

Imagine mtu alitandikwa 30+risasi tena kipindi cha Magu lakini anakiri namna hii, mimi ni nani.
 
Kama Lissu anaenda na miye nitaenda,

Acha nifundishe kabisa vipindi vyangu vyote weekend hii Ili Jumatatu nikajiunge naye

Viva Lissu
 
Rubbish, Lisu siyo kuwa anamuunga mkono magufuli, NO, A BIG NO! Ila anasema hakuiba na kama aliiba siyo kiwango cha kuuza bandari zetu. lakini he was instrumental katika kumpiga Risasi Lisu!
Lissu anajua kuwa waliompiga Risasi wapo hai,

Mbona uelewa wako ndogo hivi??

Mara kadhaa, Lisu anarudia kusema Magu hakuwa MWIZI!!!

Uzalendo wa Magu Si wa kutiliwa shaka Nchi hii!!
 
Ya Nyerere siyajui sana lwa sababu zama zake sikuwa na hizo akili, ila kwa uzalendo sidhani kama kuna kiongozi anamfikia JPM.

Imagine mtu alitandikwa 30+risasi tena kipindi cha Magu lakini anakiri namna hii, mimi ni nani.
Nitaenda naye Chato
 
Kila mwanadamu ana mazuri na mabaya...

Magufuli akiwa hai, wapinzani walitumia mabaya take kumnyuka kisiasa na sasa yu mfu wapinzani wanatumia mazuri yake kuwanyuka walio hai...

Theory hiyo hiyo inatumika kwa Samia sasa...
 
Usalama Wa nchi Yetu umevurugwa.

Bandari imegawiwa mabepari Wa kiarabu na kiamerika.

Dubai ni chambo tuu lakini Nyuma Yao wapo Wamarekani Kwa ajili ya kuiba Madini Yetu . Kudhibiti ndoto za Urusi na China kuteka Soko na rasilimali za Afrika.

Mama ameinguzwa chaka na kuhatarisha usalama Wa nchi. Hawa miaka yote ni wafadhili Wa ugaidi na magaidi Duniani kote wakishirikiana na Wamarekani . Ndio maana Suala la bandari limekuja Kwa kutumia fedha na Kununua watu na propaganda za Udini.

Kila MAHALI Afrika penye rasilimali kuna vurugu zinazohusisha Udini na ukabila . Wanifaikaji Wa vurugu hizo ni watawala na Wezi Wanaoitwa wawekezaji.

Watawala nchi inapokosa uelekeo wanakimbilia Huko wanakotoroshea Mali na fedha za umma.

Watanganyika wasipoamka nchi itauzwa na usalama Wa nchi Utakua tegemezi . Hapo ndipo ndoto za Wamarekani kujenga military base pale kigamboni itakapo timia Kwa sababu tu ya mikataba ya kimangungo .

Rwanda itatumika kudhibiti utajiri Wa Kongo na Tanzania kupitia bandari zetu na viwanja vyetu vya ndege.

Tuwekeze kwingine lakini sio bandari iliyopo Mita Chache Toka kwenye Kambi zetu za Majeshi Yetu ya JKT,JWTZ,Magereza na Polisi.
Tusikubaliane na Huu mpango Wa kuiteka nchi na wao wakimbile kuishi Dubai na familia zao. Sisi tunayategemea majeshi Yetu na hatuna pa kukimbilia.

Wao wameshapewa fedha za kuishi popote Duniani penye Amani na Kula bata.
 
Mshauri asiende kutubu CHATO!!!

Leo ni siku mbaya sana kwako, Rudi kwenye thread zako zote kumtusi Magu uombe radhi!!!
Usi generalise hii issue for no reason, Lissu amemzungumzia Magufuli specifically kwenye angle ya kulinda rasilimali za taifa, ndio amemsifia, lakini kama angegusa maeneo mengine, kama utawala bora na haki za binadamu, naamini story ingekuwa tofauti hapa, hata nawe ungekosa chakujitetea.

Tuliza munkari, just be specific.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…