Tundu Lissu: Upinzani tumechanganya sana Watu, tunahitaji kiongozi ambaye akisema neno anaaminika

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Your browser is not able to display this video.
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu akihojiwa na Kituo cha NTV cha Kenya amesema “Upinzani unahitaji kuwa na Uongozi wenye maono makubwa na yasiyokuwa na mawenge tofauti na ilivyokuwa hapo Katikati.”

Aidha, Lissu amezungumza kuhusu nafasi ya kuwania Urais wa Tanzania kupitia CHADEMA baada ya kuulizwa kuwa licha ya yeye kuwa na mpango wa kuwania pia inadaiwa Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe naye ana mpango wa kuwania Urais.
 
Kosa lilianza hapa:-
1. Kumkaribisha Lowasa na kumpa nafasi ya kugombea urais, ili hali Dr. Slaa alikuwa kishaandaliwa.

Ikaonekana chama hakiheshimu hustle za wanachama wake bali hela.

2. Viongozi kushiriki maridhiano bila ya kuruhusiwa na vikao vya chama toka ngazi ya chini ya chama .

Ikaonekana kuwa kumbe chama ni cha viongozi tu.

3. Kutoa matamko yasiyosimamiwa. Mfano huko nyuma chadema ilosema haitashiriki uchaguzi bila kuwa na tume huru. Mara ghalfa chama kikabadili gia angani.
 
Chadema ina wasemaji wanne ;Mzee Mbowe,Lema,Mrema na Mdude .Hapa Lissu ametenda haki kabisa.
 
Nikishasema siku nyingi sana ,chadema haingozwi kwa mikakati bali upepo ,huwezi toboa kamwe kama chama unaendesha kwa kutegemea hali ya hewa😎😎😎
 
chadema wanatamaa sana kila mtu anataka kuwa rais wanasalitiana mno
 
Kuna issues ambazo ni technical, zinahitaji higher level thinking to resolve. sasa kwenye grassroots level unatafuta nini? Kuna mambo ya kuwashirikisha na mambo mengine yanahitaji higher mental faculties to resolve ambapo chini kabisa hawawezi kuwa na maamuzi!
 
kwa bahati mbaya, amesema ukweli wote. mchaga ukimpa uongozi akuona pesa tu akili yote inamhama. walioelewa hapa ni wale wenye A mbili walau.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…