Tundu Lissu: Walionipiga risasi ni Kikosi Kazi cha Ofisi ya Rais chini ya Mkuu wa TISS, Balozi Kipilimba

Hiyo amri ya kuwaua hao uliowataja ilitolewa na nani, lini na wapi?

Unadhani vijiswali vyako uchwara hivi vinauondoa ukweli kuwa mamlaka ilidhamiria rasmi kabisa kumwua huyu bwana?

Kwani hata Jenerali Sabaya hukumsikia akitekeleza operations zile rasmi kabisa kwa maelekezo kutokea wapi?
 
Lissu kapigwa risasi kila mtu anajua na yote yaliyotokea ulimwengu mzima unafahamu mapaka huyo mama samia anafahamu hayo masaibu yaliyompata kiongozi wako, Tumesikitika sana lakini sasa Lissu anasimamia wapi?? hatua tunasema hazikuchukuliwa lakini Lissu sasa anasimamia wapi?? anarudi nchini hivyo hivyo kuendeleza siasa? au kwa sababu hakuna hatua zilizochukuliwa hadi sasa Ataendelea kubaki belgium?

Kwa sababu kama mwanasiasa lazima awe na msimamo thabiti kufa au kupona kama tunavyoona viongozi mbali mbali duniani wa upinzani wanavyo struggle kutoka kwenye dola tawala lakini sio kama hivi anavyofanya anawaparaganya hata hawa watu wake na chama chake,

Leo ukimuuliza msigwa vipi Lissu kaamua kukutana na mama belgium, msigwa atabaki kimya hana jibu mana si jambo walipanga kwenye chama na haikuwa ajenda ya chama, na hata ukimuuliza Heche pia ataganda kutoa majibu lakini hata huyo Lissu mwenyewe aliulizwa hivi karibuni ni kitu gani kilichompata mbowe kutoka jela akakimbilia Ikulu kwanza jibu lake alisema aulizwe mbowe mwenyewe kuna mikanganyiko na giza nene. Haikueleweka je mbowe ame-sarrenda kwa miezi 8 aliyokaa jela ameshindwa vita au kanunuliwa ili atoke jela au kapewa masharti atatolewa lakini abaki kimya kwa jambo hili na hili nk.

Chadema zamani mulikuwa munaamini Kiongozi wa upinzani akienda Ikulu kuonana na Rais mulikuwa mnasema kwa kelele ni msaliti, mara kadhaa maalim seif ameitwa msaliti ni Chadema, lakini leo chadema wenyewe na wao wanaonekana Ikulu.

Mimi ni muumini wa mabadiliko kupitia vyama vya upinzani kuiondoa CCM madarakani lakini mikanganyo imekuwa mingi sana sasa hatuji ni kiongozi gani hasa wa upinzani ni mkweli na hana chembe za usaliti, lakini nashindwa kufahamu misimamo ya viongozi hawa upinzani sasaiv, nilikuwa na matumaini sana na Chadema kwa Tanzania lakini napata shida sasa
 
Akubaliane na mazingira ya sasa. Sifa ya mwanasiasa ni kuwa na busara ya kukubaliana na kitu ambacho waingereza wanaita 'compromise'.

Bahati mbaya sana JPM hakuwa na uwezo wa kufanya suluhu na wanasiasa wenzake, alikuwa na zile hulka za kisukuma za kushindwa kujishusha katika masuala hata ya msingi na madogo tu.

Mama ni mzenji, na anao utayari wa kujishusha ili muafaka uweze kupatikana, Lissu kama mwanasiasa mzoefu kwa sasa anatakiwa awe ameshaiona tofauti ya SSH na JPM na aitumie katika kujijenga upya kisiasa.

Uzuri wa haya maisha siku zote kuna nafasi ya kuanza upya, kuna nafasi ya kufanyia kazi makosa ya siku za nyuma na kuanza ukurasa mpya.
 
Hana haja ya kutomuamini Samia akisema kuwa eti mazingira ya wasiojulikana kwa sasa hayapo. Rais ni bosi wa taasisi zote nchini, huna sababu ya kutomuamini ikiwa ameshaonyesha kutaka ushirikiano na wewe.
 
Kama ni kweli Marehemu alihusika kwa kuwatumia kikosi kazi TISS na wakatimiza mauwaji hayo, basi Mungu atawalipa kwa walichokifanya.....though siko chadema na wala sina mpango wa kuwa chadema.....Nampenda mama na sio ccm....
 
Ohooo! kusha kucha huku

Lakini mbona hao hao TISS ndo walimpa ulinzi kipindi cha uchaguzi

Au ndo yale mambo ya mchawi mpe mwana akulelee
Hukumbuki pia ile orodha ya mafisadi ambapo Lowassa alikuwemo ila mwisho wa siku Lissu huyo huyo akapanda jukwaani kumpigia debe huyo huyo Lowassa kwamba tumchague awe rais wetu?
 
Yeye ndiye aliyekimbilia ubalozini baada kudai amepokea simu 2 za vitisho dhidi ya maisha yake
Wakati huo kwenye kampeni akikuwa anapanda daladala kwenda kununua nyanya kariakoo!

Nakumbuka pia akiwahi kukatalia barabarani hadi saa 4 za usiku wanazozana na polisi eti wamruhusu afanye kampeni usiku.

Kumuelewa Lisu inabidi uwe zuzu

Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile app
 
Cry baby
 
Yeye ndiye aliyekimbilia ubalozini baada kudai amepokea simu 2 za vitisho dhidi ya maisha yake
Kumbukumbu

Msikie hapa👇 akihojiwa
---
Your browser is not able to play this audio.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…