Lissu kapigwa risasi kila mtu anajua na yote yaliyotokea ulimwengu mzima unafahamu mapaka huyo mama samia anafahamu hayo masaibu yaliyompata kiongozi wako, Tumesikitika sana lakini sasa Lissu anasimamia wapi?? hatua tunasema hazikuchukuliwa lakini Lissu sasa anasimamia wapi?? anarudi nchini hivyo hivyo kuendeleza siasa? au kwa sababu hakuna hatua zilizochukuliwa hadi sasa Ataendelea kubaki belgium?
Kwa sababu kama mwanasiasa lazima awe na msimamo thabiti kufa au kupona kama tunavyoona viongozi mbali mbali duniani wa upinzani wanavyo struggle kutoka kwenye dola tawala lakini sio kama hivi anavyofanya anawaparaganya hata hawa watu wake na chama chake,
Leo ukimuuliza msigwa vipi Lissu kaamua kukutana na mama belgium, msigwa atabaki kimya hana jibu mana si jambo walipanga kwenye chama na haikuwa ajenda ya chama, na hata ukimuuliza Heche pia ataganda kutoa majibu lakini hata huyo Lissu mwenyewe aliulizwa hivi karibuni ni kitu gani kilichompata mbowe kutoka jela akakimbilia Ikulu kwanza jibu lake alisema aulizwe mbowe mwenyewe kuna mikanganyiko na giza nene. Haikueleweka je mbowe ame-sarrenda kwa miezi 8 aliyokaa jela ameshindwa vita au kanunuliwa ili atoke jela au kapewa masharti atatolewa lakini abaki kimya kwa jambo hili na hili nk.
Chadema zamani mulikuwa munaamini Kiongozi wa upinzani akienda Ikulu kuonana na Rais mulikuwa mnasema kwa kelele ni msaliti, mara kadhaa maalim seif ameitwa msaliti ni Chadema, lakini leo chadema wenyewe na wao wanaonekana Ikulu.
Mimi ni muumini wa mabadiliko kupitia vyama vya upinzani kuiondoa CCM madarakani lakini mikanganyo imekuwa mingi sana sasa hatuji ni kiongozi gani hasa wa upinzani ni mkweli na hana chembe za usaliti, lakini nashindwa kufahamu misimamo ya viongozi hawa upinzani sasaiv, nilikuwa na matumaini sana na Chadema kwa Tanzania lakini napata shida sasa