Tundu Lissu: Walionipiga risasi ni Kikosi Kazi cha Ofisi ya Rais chini ya Mkuu wa TISS, Balozi Kipilimba

Huyu kipilimba anatajwa katika uovu mwingi sana nchi hii, ni wakati wa nae kushughulikiwa atambue kuwa kila anaeua kwa upanga nae atakufa kwa upanga
Akili yangu inaniambia hivi, kwa nchi yetu watu ambao wanasiamamia maslahi ya wengi wanaitwa waovu na wale ambao wanajua kulambisha watu makombo yao wanaitwa waungwana...Ni hayo tu, but nitumie nafasi hii kuwashukuru wale wachache ambao katu hawajawahi kuchoka kuisimamia nchi yetu na maslahi yake. Hata sasa Mungu aendelee kuwapigania na kuwalinda ili kazi yenu njema ilisimamishe taifa letu imara.
 
Mkuu Mayalla una hoja lakini kupigwa risasi nyingi vile halafu ukae kimya tena ukiwa mwanasiasa sio rahisi.Huo ndio mtaji wake Lissu hadi anaingia kaburini.Ushauri mzuri kwako jitahidi kusoma alama za nyakati wewe ni Mwandishi mkubwa sana.ukitoa makala zako usijaribu tena kuzichangia au kuzitolea ufafanuzi .Vijana watakuabisha siku moja.
 
Wahuni waliotaka kuivuruga nchi!? Itakuwa yule uchwara aliyewahi kupanga pale magogoni na akaondoshwa kabla ya muhula wake kwisha.
 
Who knows...unayumba sana, hizo ramli zako zinatabu sana

Sio ramli ni matamshi yake
 
Subiri utaambiwa
 
Kwa hiyo atakaa uhamishoni mpaka lini? Na bado mtu anadai eti mbona shauri halikupelekwa mahakamani wakati principal witness wewe unayedai shauri lipelekwe mahakamani umeamua kumficha. Na kuna watu waliojitoa ufahamu wanakusapoti kwamba shauri lipelekwe mahakamani hivyo hiyo bila principal witness.
 
..kama unajua dereva yuko ulaya ina maana kwamba hajafichwa.

..na kama serikali inaamini kwamba dereva ni mhalifu inatakiwa itoe taarifa zake Interpol ili aweze kukamatwa huko aliko na kurejeshwa nchini.
very logical argument kwamba aliko dereva inafahamika ni Belgium. Ila fahamu kuwa dereva is simply an important witness, sio mhalifu. Na aliyemuweka huko Belgium ni mdau mkuu katika kesi ya kushambuliwa kwa Lissu. Ukifahamu hayo utajua kwa nini dereva hafuatwi kwa njia ya Interpol as you are suggesting
 
Halafu wewe ndio unawasema wengine hawajui mambo mengi?
 
Rais wetu lazima ajue kwenda na nyakati bado watu wanamachungu na utawala wa mwendazake.
 

..Good observation.

1.katika hatua ya Uchunguzi, mdau mkuu ni Polisi / Jamhuri, siyo Lissu / victim.

Jeshi la Polisi ndilo lenye mamlaka ya kisheria kuchunguza uhalifu.

2. dereva hajajijificha, inajulikana yuko Belgium.

3. kama taratibu za Interpol sio sahihi kumfikia, Je, kuna taratibu nyingine za kuweza kumfikia?

4. Is Tanpol out of options? Miaka minne tangu uchunguzi uanze wamefanya nini? Hakuna hata suspect.

5. Huenda kwa maoni ya Tanpol dereva sio shahidi muhimu na ndio maana jitihada hazijafanyika kutumia Interpol kumrudisha nchini, au kushirikiana na vyombo vya Ubelgiji kumhoji.

6. Huenda pia Lissu si shahidi muhimu ktk hatua ya uchunguzi kwasababu angekuwa muhimu Polisi wangemhoji alipokuwa Nairobi, au alipokuja Tanzania.
 

Angekufa kusingekuwa na hilo shauri?
 
Orodha ya mliowatia ulemavu au kuwaua ni ndefu. mmezoea mkipiga wanakaa kimya mf. Dr Ulimboka. Sasa hii bouster ya Lissu na Mdude hamkuizoea kabisa. Ni kama wametiwa ndimu

Acha moto uwake. wauaji kutajwa unaumia?
Wahuni wamepandisha bei ya maandazi hapa mtaani kisa vita ya wazungu huko Ulaya Mashariki.
 
Kimsingi bado kuna maswali mengi sana katika hili yanayohitaji tafakari na majibu ya kina.
 
Kimsingi bado kuna maswali mengi sana katika hili yanayohitaji tafakari na majibu ya kina.

..kwa maoni yangu linaleta ukakasi mkubwa sana ktk siasa za Tanzania.

..Ningetamani sana Raisi Ssh atende HAKI ktk suala hili.

..Na kwa maoni yangu haki haiwezi kutendeka kwa kuwaachia Polisi jukumu la kuchunguza tukio lile la kikatili.

..Igp Sirro na Rpc wa Dodoma wameonyesha chuki na kutokumjali Tundu Lissu pamoja na kwamba aliumizwa karibia na kufa.

..Kwa msingi huo sioni kama ni watu sahihi kusimamia uchunguzi wa tukio lile la kinyama.

..Ni imani yangu kwamba namna bora ya kulimaliza suala la Lissu ni Raisi kuunda TUME HURU yenye nguvu za kimahakama itakayotafuta ukweli wa kilichotokea.

Cc Nguruvi3
 
Bure kabisa huyu. Wacha Mbowe aendelee kuwa Mwenyekiti wa kudumu!
 
Lazima lisu awe na khofu na maisha yake kwa sababu waliotaka kumuuwa bado wako huru na hakuna uchunguzi wowote uliofanywa. Mbona yule kijana. Wa madini aliyeuliwa na polisi mtwara samia alimuagiza majaliwa kuunda timu kuchunguza polisi ingawa walishafikishwa mahakamani sasa tujiulize nini kinamzuiya Rais samia kuunda tume huru kuchunguza kupotea kwa Ben saanane na jaribio la mauwaji ya tundu lissu.
 
Magufuli na vijana wake walifanya operation ya kijeshi ndani ya taifa lao kama Putin na jeshi lake dhidi ya Ukraine

Ukraina Si taifa la Putin ,taifa lake ni Russia.
Ni Kama Tanganyika anavuotumiwa kuivamia Zanzibar ,siku Hao wanaowatumia wakiugeuza mchezo watakuja hadithi nyengine kabisa ya kuikan dia Tanganyika
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…