Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Wito wa Polisi siyo barua ya kirafiki, Nitaendelea na ratiba yangu ya kikao na mabalozi

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Wito wa Polisi siyo barua ya kirafiki, Nitaendelea na ratiba yangu ya kikao na mabalozi

Kwa ivyo wewe una amini jeshi la polisi linamuogopa Lissu?

Si suala la kuogopana hapa...

Ni suala la kila upande UNAOTUHUMU na UNAOTUHUMIWA kufuata "legal proçedures" kushughulikia jambo lolote la kisheria...!!+
 
Police haya sasa!! Sisi wengine mnatupigaga tanganyika jeki kwamba tundelee weweeeee.....maelezo utayakuta kituoni...

Jeshi la police ndiyo wasimamizi wa sheria zetu...sasa wanapofikia hatua hawafuati taratibu inakuwa shidah!!
 
Tuwekee hapa hiyo sheria
Sec 100(2) of tha CPA inasema

(2) Every summons shall be directed to the person summoned and shall require him to appear at a time and place to be appointed in the summons before a court having jurisdiction to inquire into or try the offence alleged to have been committed and shall state shortly the offence with which the person against whom it is issued is charged.
 
Sasa kama akikataa wito wa Mwenyekiti wa Chama hvo polisi ndy watamkata Lissu? Hivi wewe ukiwa na Kaka yako polisi wakawa wa nakutaka uende hvo njia sahihi ni kumwandikia Kaka yako barua?Na sio wewe?? Hata kama sheria sikusoma sitaenda labda waje kunikamata na Tractor!! Hapa warudi tena shule kusoma!!

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
Barua kaandikiwa Mwenyekiti wake wa Chama, sasa yeye "anachachawa nini" kwa kutoa hadhari barua ya Mwenyekiti wake mitandaoni!? Atulie.
 
Tundu Lissu katika Ukurasa wake wa Twitter, ameweka Barua ya Polisi na kuandika Maneno haya "Wito wa polisi sio barua ya kirafiki, ni amri ya kisheria. Wito huo unatakiwa kueleza kosa la mtuhumiwa. Barua hii haielezi kosa ninaloitiwa na imepelekwa kwa Mwenyekiti wa chama. Huu sio wito wa polisi kwa mujibu wa sheria. Nitaendelea na ratiba yangu ya kikao na mabalozi kesho."

Soma pia: IGP Sirro amtaka Tundu Lissu kuripoti kituo cha polisi Moshi mkoani Kilimanjaro
Sec 100(2) of the CPA ndivyo haswa inavyotaka:-

(2) Every summons shall be directed to the person summoned and shall require him to appear at a time and place to be appointed in the summons before a court having jurisdiction to inquire into or try the offence alleged to have been committed and shall state shortly the offence with which the person against whom it is issued is charged.
 
Lissu anatafuta sababu ya kushindwa, kisheria polisi wanaweza kukuita hata kwa simu, maelezo utayakuta polisi na utapewa haki ya kusikilizwa ukiwa na mwanasheria wako au mtu yoyote.
Tuwekee vifungu vya sheria vinavyosema hata kwa simu ni wito halali acha kuishi kwa kukalili
 
Kwa hivyo wewe ni Rais wa Dunia unaamini ICC iwaogopa polisi?
Ndio maana nika kwambia unaongea upuuzi, kwa mamlaka gani ya dunia ICC inaweza kwenda mkamata mtu? Ebu tupe somo la international law kidogo.
 
Tundu Lissu katika Ukurasa wake wa Twitter, ameweka Barua ya Polisi na kuandika Maneno haya "Wito wa polisi sio barua ya kirafiki, ni amri ya kisheria. Wito huo unatakiwa kueleza kosa la mtuhumiwa. Barua hii haielezi kosa ninaloitiwa na imepelekwa kwa Mwenyekiti wa chama. Huu sio wito wa polisi kwa mujibu wa sheria. Nitaendelea na ratiba yangu ya kikao na mabalozi kesho."

Soma pia: IGP Sirro amtaka Tundu Lissu kuripoti kituo cha polisi Moshi mkoani Kilimanjaro


Ha ha ndio shida kuwa na vilaza ha ha unatumia nguvu nyingi akili kiduchu
 
Soma vizuri barua imeandikwa kwa mwenyekiti wa Chana siyo chama.

Pili kwa akili yako ndogo kama samaki unataka kutushawishi na sisi tuwe mambulula kama wewe kuwa polisi tena policcm wako juu ya sheria?
Lissu ndiye yuko juu ya sheria !!! Kiasi muda huu uko huru kutumia lugha ya "faragha" hadharini!? Mna taabu ninyi...Kha!!
 
Barua kaandikiwa Mwenyekiti wake wa Chama, sasa yeye "anachachawa nini" kwa kutoa hadhari barua ya Mwenyekiti wake mitandaoni!? Atulie.

yule jamaa ni kama kitimoto.

yaabi sielewi anaombaje dhamana ya kuongoza hii nchi kwa kuonyesha usela usela na uhuni namna hii.
 
Tatizo wengi wanaopewa hizi kazi za upolisi ni makada wa CCM na waliofeli darasa la saba na form 4. Na wanapoenda mafunzo wanapewa maneno ya wazee wa chama ndio vitabu vyao . Kila ukiwasifu wazee wa Chama na ukiwaumiza wananchi ndio unapewa cheo zaidi , matokeo yake ndio haya tunayoyaona leo.
Mkuu polisi kwa sasa hivi wamemchoka Magu na ccm,amini nawaambia wengi wako upande Wa Lisu,hebu niambie kwa akili za kawaida MTU kama Wambura ni mpelezi mzoefu Wa polisi,we jiulize hyo barua ya kumwita Lisu polisi baada ya kuandikwa INA maana haikuhakikiwa kama haina makosa kabla haijapelekwa kwa mwenyekiti Mbowe?.

Hapo ndo utakubaliana na Mimi kuwa,aidha wanaweka hayo makosa makusudi kwa kuwa wanashurutishwa na maagizo toka juu,wakijua kuwa kwa makosa hayo bwana yule nguli Wa sheria atapangua kisheria ataendelea kupeta na kampeni zake.
 
Njozi nyingine ni ushuhuda wa jinsi waTZ walivyoharibiwa na utawala wa ukandamizaji. Wanaogopa hata haki zao. Mwaka wa ukombozi
Huoni tu huyo anaitwa magonjwa mtambuka hivyo unabishana na mgonjwa huyo achana nae
 
Si suala la kuogopana hapa...

Ni suala la kila upande UNAOTUHUMU na UNAOTUHUMIWA kufuata "legal proçedures" kushughulikia jambo lolote la kisheria...!!+
Nani anaevunja sheria polisi inaelinda mikutano yake, au yeye anaetaka kufanya campaign bila ya kibali, kuongea na watu usiku wakati mwisho saa 12 jioni na kuanza kutukana watu.

Kanuni zipo wazi omba kibali utapewa ili mikutano isiingiliane na mikutano mwisho saa 12 jioni. Yeye ataki anataka kusimama anapojisikia na kukutana na watu kwenye giza.
 
Hakuna kitu hapo hana cha kukutana na mabalozi wala nini muongo anaenda kuhojiwa tume ya maadili
Wewe ndugu kusoma hujui hata picha huoni.haya wewe ndio umesema anaenda tume
 
NB: Hapo hakuna kesi, ni mbinu tu za kum - distract huyu bwana kujaribu kumtoa kwenye reli. Bahati mbaya kwao ni kuwa, CHADEMA na mgombea wao wako very prepared kuliko wao....!!
Yeye ndiye anajitoa kwenye reli...aendelee na kampeni zake. Mwenyekiti akimuhitaji atamweleza, wasi wasi nini mpaka anatao barua za Mwenyekiti wake mitandaoni!!
 
Makosa hayo ya kiuandishi sio utetezi kabisa kisheria, Tundu anajua hilo na hiyo barua kupelekwa kwa Mwenyekiti wa Chama chake kwake sidhani kama ni utetezi anapaswa atambue kuwa Chama ni Cha mwenyekiti na Chama hicho ndio kimemdhamini yeye kuwa Mgombea wa Urais na hata alipofika Tume aliwasilisha barua ya Utambulisho kutoka kwa Chama ambayo Katibu wa Chama ndio alimtambulisha Tume. Hivyo Polisi kumtaarifu Mwenyekiti juu ya hilo ni sahihi kabisa kuwa mtu wako anahitajika. Na anahitajika kuhojiwa kutokana na matamshi na kauli zake alizozitoa.

Tundu anachofanya ni kuchelewesha tu lakini bado sheria inambana.
Malalamiko yoyote kuhusu uchaguzi sheria inaelekeza yapelekwe mbele ya baraza la maadili, Na sio kumwambia mgombea aripoti kituo cha polisi.
 
Alisema police ni wapumbavu, wamempiga mabomu ila hajabu mkutano alifanya na police wakamsindikiza😂
Polisi hawa ngazi za chini wako upande Wa lisu,wanajua akiingia maslahi yao yatafanyiwa kazi zao,pia hawatapoteza ajira zao hata upinzani ukipita uchaguzi.shida iko kwa hawa ngazi za juu ndo wanaitetea ccm wasipoteze vyeo vyao.
 
Haijalishi sababu.Ni lazima hata polisi anapokukakamata akutamkie kosa lako.Haweza kukwambia Maelezo utakuta Polisi.Hawezi kukupotezea muda.Kama anataka kukuhoji anakufuata wewe mahali ulipo na kukuhoji na iwapo kuna sababu ya kukuweka kizuizini ndo anatafuta kibali cha kukukamata.Watanzania amkeni msiwe kama mbuzi kwenye banda.

Vizuri sana👏👏👌👌

Hivi ndivyo ilivyo, ndivyo inavyopaswa kuwa...

Mfano mwingine ni huu;

Polisi kisheria wana mamlaka ya kumpekua mtu yeyote nyumbani kwake au kazini kwake...

Vivyo hivyo wana mamlaka kisheria kum - arrest mtu yeyote wakati wowote....

Lakini hii haifanyiki kienyeji tu eti kwa sababu tu wao ni polisi, wamevaa magwanda ya polisi...

Ni lazima UPEKUZI na ARREST hiyo ifuate procedures za kisheria isipokuwa ktk mazingira maalumu sana kwa makosa fulani maalumu ndiyo inaweza kufanyika kwa kuruka baadhi ya procedures...!
 
Back
Top Bottom